SOURCE: The Daily Mail
CHANZO: HabariLeo
* Waziri Sophia Simba asema Mengi kachemsha
*Mkuchika naye asema wanamchunguza
Ramadhan Semtawa na Leon Bahati
MAWAZIRI wawili, Sophia Simba na George Mkuchika jana walimshambulia mfanyabiashara maarufu nchini, Reginald Mengi ambaye wiki iliyopita alitangaza majina ya wafanyabiashara watano wenye asili ya Kiasia, akisema ni mafisadi waliokubuhu.
Simba, ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora) na Mkuchika, Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo walisema mfanyabiashara huyo wa jijini Dar es salaam "amechemsha".
Mengi alitangaza majina ya wafanyabiashara hao Alhamisi iliyopita akisema ni kati ya watu wasiozidi 10 ambao alidai wanaifilisi nchi na kutaka wadhibitiwe mapema kabla hawajaitingisha na kuiyumbisha nchi. Hata hivyo, Mengi, ambaye alidai katika taarifa yake kuwa juhudi za Rais Jakaya Kikwete zinakwamishwa na watu hao, hakueleza jinsi watano hao wanavyoitafuna nchi zaidi ya kusema kuwa wanatorosha fedha wanazozipata 'kifisadi'.
Jana, kwa nyakati tofauti jijini Dar es Salaam mawaziri hao wawili walitoa kauli za kumshambulia mwenyekiti huyo mtendaji wa makampuni ya IPP, kauli ambazo zinadokeza mtazamo wa serikali katika mjadala unaoendelea wa vita dhidi ya ufisadi na vinara wake.
Waziri Simba, ambaye wizara yake pia inawajibika katika vita dhidi ya ufisadi, alisema: "Kakosea... watoto wa mjini wanasema kachemsha." Simba alitoa msimamo huo jijini Dar es Salaam jana muda mfupi baada ya kufungua semina ya wadau wa vyama vya siasa kuhusu namna ya kuiboresha Sheria ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1995.
Simba alisema Mengi hana mamlaka hayo ya kutaja watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi.
Kabla ya kujibu swali kuhusu kitendo cha Mengi, ambaye anamiliki televisheni ya ITV na kituo cha redio cha Radio One Stereo, kutaja majina ya watu hao aliowaita
mafisadi papa, Simba alihoji: " Hapa kuna mtu wa ITV?." Baadaye alisema: "Sikilizeni, kwanza kitendo alichokifanya Mengi si sahihi, kakosea hawezi kuhukumu watu, mamlaka hayo anatoa wapi?"
Simba, huku akionekana kama mtu ambaye alikuwa akitafuta jukwaa kuzungumzia suala hilo, alisema Mengi amekosea kwa kuwa baadhi ya watu aliowataja wana kesi mahakamani."Anahukumu watu," alisema. "Kuna mtu kama Jeetu (Patel) ana kesi mahakamani (EPA), sasa unapokuja kusema ni fisadi wakati mahakama haijathibitisha, unakuwa na maana gani.
"Kwanza kwanini awatuhumu wafanyabiashara wenzake tu, ina maana si ana nia mbaya nao."
Alisema Mengi amechukua uamuzi huo kama vile serikali, wakati serikali ipo siku zote na imekuwa ikifanya kazi zake kwa umakini kwa kufuata misingi ya sheria.
"Serikali ipo na inafanya kazi kwa misingi ya sheria, sasa yeye kukaa na kutangaza watu nasema si sahihi kabisa. Mahakama pekee ndiyo inaweza kumtia mtu hatiani, lakini huwezi kuhukumu watu kama hakuna mamlaka."
Waziri Simba, ambaye pia ni mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT), alisema Mengi hapaswi kutumia vyombo vyake vibaya. "Asitumie vyombo vyake kufanya atakavyo yeye. Huwezi kukaa katika chombo chako na kuanza kuhukumu watu. Kila mtu akifanya hivyo itakuaje," alihoji.
Akiongea na Mwananchi baada ya kupata taarifa za kauli ya Simba, Mengi alisema: "Namuombea kwa Mwenyezi Mungu na kwa maskini wa Tanzania ili wamsamehe kwa sababu hajui anenalo." Mengi hakutaka kuzungumza zaidi kuhusu hatua hiyo ya Mama Simba.
Naye Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, George Mkuchika aliwaambia waandishi wa habari kuwa serikali itamchukulia hatua za kisheria Mengi iwapo itabainika alikiuka taratibu na kanuni za nchi kwa kutangaza majina ya watu anaowatuhumu kwa ufisadi.
Mkuchika alisema jijini Dar es Salaam jana kwa sasa serikali inafanya uchunguzi juu ya suala hilo na itatumia mikanda ya video pamoja na maelezo ya kimaandishi aliyoyatoa Mengi siku alipokutana na waandishi wa habari.
"Tumekusudia kupata ule mkanda wa video, pia tusome maelezo yake ya kimaandishi... tukigundua kuna mahala ambapo sheria haikuzingatiwa, (Mengi) atachukuliwa hatua," alisema Mkuchika.
Mkuchika alisema serikali imepokea malalamiko mengi kutoka kwa watu wengi, wakishutumu hatua iliyochukuliwa na Mengi, ambaye pia anamiliki viwanda vya vinywaji.
Bila kutaka kuwataja majina, Mkuchika alisema miongoni mwa walalamikaji, wapo walioeleza kuwa vyombo vya habari vya mfanyabiashara huyo havikuwatendea haki watuhumiwa waliotajwa kuwa ni mafisadi wakuu.
Alisema ni kutokana na vyombo hivyo kuwataja majina watuhumiwa bila ya kuwapa fursa ya kujibu madai dhidi yao. Waziri Mkuchika alipotakiwa kueleza siku ambayo uchunguzi huo utakamilika, alijibu wananchi wanapaswa kuwa watulivu kwa sababu serikali ikimaliza kuchunguza, itawatangazia yale waliyobaini.
Hii ni mara ya pili katika kipindi cha miezi takribani mitatu kwa Mengi kuingia katika mvutano na serikali baada ya kuvutana mapema mwaka huu na Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha kutokana na kutangaza kuwa kuna mipango ya kumfilisi na kumuua.
Mengi pia amewahi kujikuta katika malumbano na watendaji wa serikali hasa na waziri wa zamani wa nchi, ofisi ya rais (utawala bora), Wilson Masilingi alipotoa tuhuma kuwa suala la utoaji zabuni ya ununuzi wa hoteli ya Kilimanjaro, hivi sasa inajulikana kama Kilimanjaro Kempiski, kulikuwa na kitu alichokiita "mchezo mchafu". Suala hilo liliamsha malumbano makali, lakini liliishia hewani.
Katika tuhuma za wiki iliyopita, Mengi aliwahusisha wafanyabiashara hao watano na kashfa za wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), utoaji zabuni ya ufuaji umeme wa dharura kwa kampuni ya Richmond Development (LLC) na uuzwaji wa jengo la Mfuko wa Hifadhi ya Taifa ya Jamii (NSSF).
Mengi, ambaye kituo chake cha televisheni cha ITV kiliwahi kuendesha mchezo mkubwa wa bahati nasibu ya Jackpot Bingo, pia aliitaja Bahati Nasibu kuwa katika tuhuma hizo, pamoja na mradi wa makaa ya mawe wa Mchuchuma.
na Mwandishi Wetu, Kilombero
KIJIJI cha Namwawala, kilichopo Kata ya Idete, Tarafa ya Ifakara, Wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro, kiko hatarini kuuzwa kwa mwekezaji, huku viongozi wanaosimamia mpango huo wakidai ni agizo kutoka kwa Rais Jakaya Kikwete.
Habari za uhakika ambazo Tanzania Daima imezipata kutoka katika kijiji hicho, zilidai kuwa baadhi ya viongozi wa wilaya na mkoa, wanasimamia uuzaji wa ekari zaidi ya 3,384, sawa na asilimia 95 ya ardhi ya kijiji chote, kwa ajili ya mwekezaji anayetarajia kuanzisha mashamba ya miwa na kiwanda cha sukari.
Hivi sasa, kijiji hicho kimeunda kamati kufuatilia mambo manne ya msingi ambayo ni kuthibitisha kauli ya viongozi wao kwamba Rais Kikwete ameamuakuchukua ardhi hiyo, na kama ardhi inayochukuliwa ni asilimia 95 ya eneo lote la
kijiji.
Mambo mengine ni, Mkurugenzi Mtendaji Kilombero kuanza kuthaminisha mali zao bila taarifa rasmi na kutaka wasomewe waraka unaoelekeza Rais Kikwete kutoa agizo la kuchukua ardhi na kumpa mwekezaji.
Kamati hiyo ambayo inadaiwa kuishi kwa kutishiwa na baadhi ya viongozi wilayani humo, inaundwa na Mwenyekiti Zuberi Kapindijega, Kenani Haule (Katibu), wakati wajumbe ni Johson Msuya na Godfrey Lwema.
Akizungumza na Tanzania Daima kutoka mjini Ifakara jana, Kapindijega, alisema baada ya viongozi wa wilaya na kata kupita kwa wananchi na kuwataka waanze kufanya tathimini ya mali zao na kujiandaa kuhama, walifikisha barua yao kwa Rais Kikwete jijini Dar es Salaam wakitaka ufafanuzi wa mpango huo.
“Januari 31 kwenye mkutano wa mapato na matumizi ya kijiji, iliibuka hoja ya wanakijiji kutaka kujua hatma ya ardhi yetu, ndipo mwenyekiti wa kijiji alitusomea waraka aliodai wa rais, ambao umetumika katika kuchukua asilimi 95 ya ardhi hiyo. Kutokana na mazingira na mfumo uliotumika kufikisha waraka huo wa rais kwetu, tunahisi kuna mchezo
mchafu.
“Kwa hofu hiyo na kwa kuwa kila tunaloliuliza jibu ni moja tu la rais kaamua kuchukua ardhi yake, ndiyo maana tumeamua kuja kuonana na wewe mwenyewe Mheshimiwa Rais,” ilisomeka sehemu ya barua hiyo kwenda kwa rais iliyoandikwa Februari 13 na Tanzania Daima kupata nakala yake.
Hata hivyo, katika majibu ya rais kwa viongozi hao wa tume yalitolewa kwa barua iliyosainiwa na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, F. Mwaipaja, Februari 16, viongozi hao walitakiwa kuwasiliana na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, na Mkuu wa Mkoa na kama hawataridhishwa, wanaweza kuonana na rais.
Kutokana na barua hiyo kutoka kwa rais, viongozi wa tume hiyo walibisha hodi katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero kwa barua waliyoiandika Februari 20 nakufuatiwa na nyingine ya Februari 27, ambazo pia Tanzania Daima nakala zake inazo.
Hata hivyo, ofisi hiyo ya mkuu wa wilaya, ilijibu barua hiyo kupitia kwa Katibu Tawala, E Mmbaga, akidai kuwa ameagizwa na DC Evarist Evarist Ndikilo awajulishe wajumbe hao wa tume kwamba amepokea barua hizo.
“Aidha mnafahamishwa kuwa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya itawasiliana na SUDECO, Bodi ya Sukari Tanzania (SBT), Serikali ya Kijiji (Namwawala) pamoja na ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji (W), wanafanya tathmini ya fidia. Mnaombwa mvute subira kwani matokeo ya mawasiliano hayo, mtajulishwa,” ilisema barua hiyo.
Baada ya majibu hayo, tume hiyo pia ilifika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, na kuwasilisha barua yao Machi 6, mwaka huu kutaka kupata ufafanuzi wa kuuzwa kwa ardhi ya kijiji chao.
Ofisi ya mkoa kupitia kwa Kaimu Katibu Tawala, L. Msuya, iliahidi katika barua yenye kumb namba CD/148/06/87, kwamba italishughulikia suala hili kwa makini.
“Kumbukeni kwamba mmeshafikisha malalamiko yenu kwenye ofisi ya rais na sasa mmerudishwa kwa Mkuu wa Mkoa, kwa hiyo suala hili linatakiwa lishughulikiwe kwa umakini sana.
Mnatakiwa mvute subira wakati mkuu wa mkoa anafanya uchunguzi wa kina ili kupata ufumbuzi wa kudumu,” ilisema barua hiyo.
Hata hivyo, akizungumzia malalamiko ya tume hiyo, DC wa Kilombero, jana alikaririwa na moja ya vyombo vya habari vya kila siku kwamba wajumbe wa tume hiyo ni wachochezi na kutoa amri wakamatwe mara moja.
Uchunguzi wa Tanzania Daima umebaini kuwa, hali ya kijiji hicho si shwari kwani wananchi wanashindwa kuendelea kufanya shughuli za maendeleo kwa hofu ya kuhamishwa, huku baadhi ya viongozi wakitofautiana kuhusu mpango huo unaodaiwa kuendeshwa kiujanja ujanja kwa kutumia jina la rais.
Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)
Your email address is safe with us!
SOURCE: The Daily Mail
CHANZO: HabariLeo
* Waziri Sophia Simba asema Mengi kachemsha
*Mkuchika naye asema wanamchunguza
Ramadhan Semtawa na Leon Bahati
MAWAZIRI wawili, Sophia Simba na George Mkuchika jana walimshambulia mfanyabiashara maarufu nchini, Reginald Mengi ambaye wiki iliyopita alitangaza majina ya wafanyabiashara watano wenye asili ya Kiasia, akisema ni mafisadi waliokubuhu.
Simba, ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora) na Mkuchika, Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo walisema mfanyabiashara huyo wa jijini Dar es salaam "amechemsha".
Mengi alitangaza majina ya wafanyabiashara hao Alhamisi iliyopita akisema ni kati ya watu wasiozidi 10 ambao alidai wanaifilisi nchi na kutaka wadhibitiwe mapema kabla hawajaitingisha na kuiyumbisha nchi. Hata hivyo, Mengi, ambaye alidai katika taarifa yake kuwa juhudi za Rais Jakaya Kikwete zinakwamishwa na watu hao, hakueleza jinsi watano hao wanavyoitafuna nchi zaidi ya kusema kuwa wanatorosha fedha wanazozipata 'kifisadi'.
Jana, kwa nyakati tofauti jijini Dar es Salaam mawaziri hao wawili walitoa kauli za kumshambulia mwenyekiti huyo mtendaji wa makampuni ya IPP, kauli ambazo zinadokeza mtazamo wa serikali katika mjadala unaoendelea wa vita dhidi ya ufisadi na vinara wake.
Waziri Simba, ambaye wizara yake pia inawajibika katika vita dhidi ya ufisadi, alisema: "Kakosea... watoto wa mjini wanasema kachemsha." Simba alitoa msimamo huo jijini Dar es Salaam jana muda mfupi baada ya kufungua semina ya wadau wa vyama vya siasa kuhusu namna ya kuiboresha Sheria ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1995.
Simba alisema Mengi hana mamlaka hayo ya kutaja watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi.
Kabla ya kujibu swali kuhusu kitendo cha Mengi, ambaye anamiliki televisheni ya ITV na kituo cha redio cha Radio One Stereo, kutaja majina ya watu hao aliowaita
mafisadi papa, Simba alihoji: " Hapa kuna mtu wa ITV?." Baadaye alisema: "Sikilizeni, kwanza kitendo alichokifanya Mengi si sahihi, kakosea hawezi kuhukumu watu, mamlaka hayo anatoa wapi?"
Simba, huku akionekana kama mtu ambaye alikuwa akitafuta jukwaa kuzungumzia suala hilo, alisema Mengi amekosea kwa kuwa baadhi ya watu aliowataja wana kesi mahakamani."Anahukumu watu," alisema. "Kuna mtu kama Jeetu (Patel) ana kesi mahakamani (EPA), sasa unapokuja kusema ni fisadi wakati mahakama haijathibitisha, unakuwa na maana gani.
"Kwanza kwanini awatuhumu wafanyabiashara wenzake tu, ina maana si ana nia mbaya nao."
Alisema Mengi amechukua uamuzi huo kama vile serikali, wakati serikali ipo siku zote na imekuwa ikifanya kazi zake kwa umakini kwa kufuata misingi ya sheria.
"Serikali ipo na inafanya kazi kwa misingi ya sheria, sasa yeye kukaa na kutangaza watu nasema si sahihi kabisa. Mahakama pekee ndiyo inaweza kumtia mtu hatiani, lakini huwezi kuhukumu watu kama hakuna mamlaka."
Waziri Simba, ambaye pia ni mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT), alisema Mengi hapaswi kutumia vyombo vyake vibaya. "Asitumie vyombo vyake kufanya atakavyo yeye. Huwezi kukaa katika chombo chako na kuanza kuhukumu watu. Kila mtu akifanya hivyo itakuaje," alihoji.
Akiongea na Mwananchi baada ya kupata taarifa za kauli ya Simba, Mengi alisema: "Namuombea kwa Mwenyezi Mungu na kwa maskini wa Tanzania ili wamsamehe kwa sababu hajui anenalo." Mengi hakutaka kuzungumza zaidi kuhusu hatua hiyo ya Mama Simba.
Naye Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, George Mkuchika aliwaambia waandishi wa habari kuwa serikali itamchukulia hatua za kisheria Mengi iwapo itabainika alikiuka taratibu na kanuni za nchi kwa kutangaza majina ya watu anaowatuhumu kwa ufisadi.
Mkuchika alisema jijini Dar es Salaam jana kwa sasa serikali inafanya uchunguzi juu ya suala hilo na itatumia mikanda ya video pamoja na maelezo ya kimaandishi aliyoyatoa Mengi siku alipokutana na waandishi wa habari.
"Tumekusudia kupata ule mkanda wa video, pia tusome maelezo yake ya kimaandishi... tukigundua kuna mahala ambapo sheria haikuzingatiwa, (Mengi) atachukuliwa hatua," alisema Mkuchika.
Mkuchika alisema serikali imepokea malalamiko mengi kutoka kwa watu wengi, wakishutumu hatua iliyochukuliwa na Mengi, ambaye pia anamiliki viwanda vya vinywaji.
Bila kutaka kuwataja majina, Mkuchika alisema miongoni mwa walalamikaji, wapo walioeleza kuwa vyombo vya habari vya mfanyabiashara huyo havikuwatendea haki watuhumiwa waliotajwa kuwa ni mafisadi wakuu.
Alisema ni kutokana na vyombo hivyo kuwataja majina watuhumiwa bila ya kuwapa fursa ya kujibu madai dhidi yao. Waziri Mkuchika alipotakiwa kueleza siku ambayo uchunguzi huo utakamilika, alijibu wananchi wanapaswa kuwa watulivu kwa sababu serikali ikimaliza kuchunguza, itawatangazia yale waliyobaini.
Hii ni mara ya pili katika kipindi cha miezi takribani mitatu kwa Mengi kuingia katika mvutano na serikali baada ya kuvutana mapema mwaka huu na Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha kutokana na kutangaza kuwa kuna mipango ya kumfilisi na kumuua.
Mengi pia amewahi kujikuta katika malumbano na watendaji wa serikali hasa na waziri wa zamani wa nchi, ofisi ya rais (utawala bora), Wilson Masilingi alipotoa tuhuma kuwa suala la utoaji zabuni ya ununuzi wa hoteli ya Kilimanjaro, hivi sasa inajulikana kama Kilimanjaro Kempiski, kulikuwa na kitu alichokiita "mchezo mchafu". Suala hilo liliamsha malumbano makali, lakini liliishia hewani.
Katika tuhuma za wiki iliyopita, Mengi aliwahusisha wafanyabiashara hao watano na kashfa za wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), utoaji zabuni ya ufuaji umeme wa dharura kwa kampuni ya Richmond Development (LLC) na uuzwaji wa jengo la Mfuko wa Hifadhi ya Taifa ya Jamii (NSSF).
Mengi, ambaye kituo chake cha televisheni cha ITV kiliwahi kuendesha mchezo mkubwa wa bahati nasibu ya Jackpot Bingo, pia aliitaja Bahati Nasibu kuwa katika tuhuma hizo, pamoja na mradi wa makaa ya mawe wa Mchuchuma.
na Mwandishi Wetu, Kilombero
KIJIJI cha Namwawala, kilichopo Kata ya Idete, Tarafa ya Ifakara, Wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro, kiko hatarini kuuzwa kwa mwekezaji, huku viongozi wanaosimamia mpango huo wakidai ni agizo kutoka kwa Rais Jakaya Kikwete.
Habari za uhakika ambazo Tanzania Daima imezipata kutoka katika kijiji hicho, zilidai kuwa baadhi ya viongozi wa wilaya na mkoa, wanasimamia uuzaji wa ekari zaidi ya 3,384, sawa na asilimia 95 ya ardhi ya kijiji chote, kwa ajili ya mwekezaji anayetarajia kuanzisha mashamba ya miwa na kiwanda cha sukari.
Hivi sasa, kijiji hicho kimeunda kamati kufuatilia mambo manne ya msingi ambayo ni kuthibitisha kauli ya viongozi wao kwamba Rais Kikwete ameamuakuchukua ardhi hiyo, na kama ardhi inayochukuliwa ni asilimia 95 ya eneo lote la
kijiji.
Mambo mengine ni, Mkurugenzi Mtendaji Kilombero kuanza kuthaminisha mali zao bila taarifa rasmi na kutaka wasomewe waraka unaoelekeza Rais Kikwete kutoa agizo la kuchukua ardhi na kumpa mwekezaji.
Kamati hiyo ambayo inadaiwa kuishi kwa kutishiwa na baadhi ya viongozi wilayani humo, inaundwa na Mwenyekiti Zuberi Kapindijega, Kenani Haule (Katibu), wakati wajumbe ni Johson Msuya na Godfrey Lwema.
Akizungumza na Tanzania Daima kutoka mjini Ifakara jana, Kapindijega, alisema baada ya viongozi wa wilaya na kata kupita kwa wananchi na kuwataka waanze kufanya tathimini ya mali zao na kujiandaa kuhama, walifikisha barua yao kwa Rais Kikwete jijini Dar es Salaam wakitaka ufafanuzi wa mpango huo.
“Januari 31 kwenye mkutano wa mapato na matumizi ya kijiji, iliibuka hoja ya wanakijiji kutaka kujua hatma ya ardhi yetu, ndipo mwenyekiti wa kijiji alitusomea waraka aliodai wa rais, ambao umetumika katika kuchukua asilimi 95 ya ardhi hiyo. Kutokana na mazingira na mfumo uliotumika kufikisha waraka huo wa rais kwetu, tunahisi kuna mchezo
mchafu.
“Kwa hofu hiyo na kwa kuwa kila tunaloliuliza jibu ni moja tu la rais kaamua kuchukua ardhi yake, ndiyo maana tumeamua kuja kuonana na wewe mwenyewe Mheshimiwa Rais,” ilisomeka sehemu ya barua hiyo kwenda kwa rais iliyoandikwa Februari 13 na Tanzania Daima kupata nakala yake.
Hata hivyo, katika majibu ya rais kwa viongozi hao wa tume yalitolewa kwa barua iliyosainiwa na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, F. Mwaipaja, Februari 16, viongozi hao walitakiwa kuwasiliana na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, na Mkuu wa Mkoa na kama hawataridhishwa, wanaweza kuonana na rais.
Kutokana na barua hiyo kutoka kwa rais, viongozi wa tume hiyo walibisha hodi katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero kwa barua waliyoiandika Februari 20 nakufuatiwa na nyingine ya Februari 27, ambazo pia Tanzania Daima nakala zake inazo.
Hata hivyo, ofisi hiyo ya mkuu wa wilaya, ilijibu barua hiyo kupitia kwa Katibu Tawala, E Mmbaga, akidai kuwa ameagizwa na DC Evarist Evarist Ndikilo awajulishe wajumbe hao wa tume kwamba amepokea barua hizo.
“Aidha mnafahamishwa kuwa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya itawasiliana na SUDECO, Bodi ya Sukari Tanzania (SBT), Serikali ya Kijiji (Namwawala) pamoja na ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji (W), wanafanya tathmini ya fidia. Mnaombwa mvute subira kwani matokeo ya mawasiliano hayo, mtajulishwa,” ilisema barua hiyo.
Baada ya majibu hayo, tume hiyo pia ilifika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, na kuwasilisha barua yao Machi 6, mwaka huu kutaka kupata ufafanuzi wa kuuzwa kwa ardhi ya kijiji chao.
Ofisi ya mkoa kupitia kwa Kaimu Katibu Tawala, L. Msuya, iliahidi katika barua yenye kumb namba CD/148/06/87, kwamba italishughulikia suala hili kwa makini.
“Kumbukeni kwamba mmeshafikisha malalamiko yenu kwenye ofisi ya rais na sasa mmerudishwa kwa Mkuu wa Mkoa, kwa hiyo suala hili linatakiwa lishughulikiwe kwa umakini sana.
Mnatakiwa mvute subira wakati mkuu wa mkoa anafanya uchunguzi wa kina ili kupata ufumbuzi wa kudumu,” ilisema barua hiyo.
Hata hivyo, akizungumzia malalamiko ya tume hiyo, DC wa Kilombero, jana alikaririwa na moja ya vyombo vya habari vya kila siku kwamba wajumbe wa tume hiyo ni wachochezi na kutoa amri wakamatwe mara moja.
Uchunguzi wa Tanzania Daima umebaini kuwa, hali ya kijiji hicho si shwari kwani wananchi wanashindwa kuendelea kufanya shughuli za maendeleo kwa hofu ya kuhamishwa, huku baadhi ya viongozi wakitofautiana kuhusu mpango huo unaodaiwa kuendeshwa kiujanja ujanja kwa kutumia jina la rais.