
Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)
Your email address is safe with us!
CHANZO: Mwananchi
Nadhani sasa kuna umuhimu wa kuangalia kama Spika huyu wa Viwango na Spidi bado anastahili kuendelea na wadhifa wake ambao ni wa nne kitaifa.Natoa hoja hiyo kwa vile kuna kila dalili kuwa Spika Samwel Sitta sasa anaogopa kivuli chake mwenyewe.
Ni hatari kwa kiongozi wa kitaifa kama Spika kutoa madai mazito namna hiyo pasipo kuwa na uthibitisho wowote.Hivi hao mafisadi wanaohatarisha maisha yake ni akina nani?Nauliza hivyo kwa vile kwa mujibu wa maelezo yake inaonyesha anawafahamu hata kwa majina.Sasa tunapokuwa na kiongozi wa kitaifa ambaye pindi maisha yake yanapokuwa hatarini (kama unaamini anachosema) anakimbilia kuomba aongezewe ulinzi hadharani,then hapo kuna mushkeli.
Ni hatari zaidi kumsikia Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,taasisi tukufu yenye jukumu la kutunga sheria za nchi,akiuliza bila aibui wala uoga "Hivi kama kweli nataka kuficha faili la Bunge nani anaweza kunizuia humu ndani?” You can't be serious,Mzee wa Spidi na Viwango!Yaani unatuambia kuwa kwa wadhifa wako unaweza kuficha nyaraka muhimu za Taifa (mfano faili la Bunge) na hakuna mwenye uwezo wa kukuzuia?Nadhani unatafsiri vibaya madaraka yako.Uspika ni nafasi inayoongozwa kwa taratibu na sheria,za nchi na za Bunge unaloongoza.Sasa unapotuambia kuwa hakuna wa kukuzuia ndani ya Bunge kuficha faili (ukijiskia kufanya hivyo) unatuaminisha kuwa aidha huelewi mipaka ya kazi yako,au unadhani Uspika ni kuwa juu ya sheria za nchi na Bunge,au kulewa madaraka.
Tukiwa hapohapo kwenye hoja yako ya "hakuna wa kukuzuia...",na tukiamini kuwa ni kweli hakuna wa kukuzuia,je utalalamika kuwa mafisadi wanakuwinda wakikuzushia zengwe kwamba umeficha nyaraka muhimu zaidi ya faili la Bunge?Sawa utasema wanakuandama lakini ushawapa hoja kwamba "ukitaka kuficha faili la bunge hakuna wa kukuzuia".Well,wao wanaweza kuja na tuhuma kubwa zaidi ya kuficha faili.Laiti busara zingetumika,ungeishia tu kukanusha tuhuma za kwamba una mpango wa kuchoma moto ofisi za bunge,na sio kukurupuka kudai una uwezo wa kuficha faili la bunge pasipo kuwapo wa kukuzuwia.
Ni rahisi kwa Spika kuomba aongezewe ulinzi (kwa kigezo kuwa ulinzi alionao sasa hautoshi) kwa vile gharama za kuongezewa ulinzi zitabebwa na walipa kodi na si kutoka mfukoni mwa Spika.Hoja hii ya Spika Sitta pia inaweza kufanya tujiulize iwapo licha ya nafasi yake ya Uspika,Mheshimiwa Sitta pia ni mtaalam wa mambo ya ulinzi wa viongozi,na review aliyofanya katika protection anayopewa hivi sasa imempelekea kuhitimisha kuwa ulinzi alionao hautoshi.Hii ni sawa na kuwadharau professionals wenye jukumu hilo,ambao naamini wangetambua mapungufu hayo kabla hata ya Spika Sitta kutamka hadharani.
Lakini twende mbali zaidi kwenye hili la "ulinzi alionao Spika hautoshi"Je anaweza kututhibitishia japo tukio moja linaloashiria kutotosha kwa ulinzi alionao hivi sasa?Yaani kutuhumiwa kuwa anataka kuchoma moto ofisi za bunge, na "maadui zake kumwaga fedha jimboni kwake" vimekuwa matishio ya kiusalama yanayotosheleza kufikia uamuzi wa kumuongezea ulinzi?
Kichekesho ni kwamba wakati Spika akimtaka Mbunge wa Cuf (Mheshimiwa Shoka Hamis Juma) afute kauli yake kwa kuwa "ushahidi aliotoa-katika madai kuwa kuna chama flani kinanunua shahada wakati wa chaguzi-ni dhaifu",yeye mwenyewe anafanya kilekile cha kutoa madai dhaifu kuwa nguvu ya mafisadi inahatarisha usalama wake ilhali hajaweza kutoa uthibitisho wowote zaidi ya "kauli za kisiasa" kuwa maadui zake wanapeleka pesa jimboni kwake ili asirejee bungeni.Ana uhakika gani kuwa hao anaowaita maadui zake si wananchi wenye dhamira ya kuleta maendeleo katika jimbo hilo pasipo kuwa na ajenda za kisiasa?Au Spika Sitta anataka kutuambia kuwa ni yeye tu aliye na hatimiliki ya kupeleka misaada katika jimbo hilo?Jamani,yaani hadi maendeleo ya jimbo yanafanywa kuwa mithili ya maamuzi ya mtu binafsi!?
Kuna mengi ya kujadili kuhusu kauli za Spika Sitta,lakini lililo wazi ni kwamba nafasi anayojipachika ya ukinara wa mapambano dhidi ya ufisadi ni sawa na political conmanship.Kwa lipi hasa?Sio Sitta huyu aliyempa "kifungo" Zitto Kabwe kwa "kosa" la kumkalia kooni Karamagi kuhusu Buzwagi?Sio Spika Sitta huyu aliyetishia kumfungulia mashtaka Dkt Wilbroad Slaa pale mbunge huyo wa Karatu aliposhikilia bango kuhusu ishu za ufisadi?Ni lipi alilofanya Samweli Sitta,kama Spika wa Bunge la Jamhuri au Mbunge wa Urambo linaloweza kumjumuisha kwenye kundi la vinara wa mapambano dhidi ya ufisadi?Yaani Watanzania wenzake kutamani jimbo la Urambo imekuwa ufisadi?Au mtu kutamani nafasi ya uspika imekuwa ufisadi?
Lakini kwa vile siasa zetu kwa sasa zinaruhusu mambo ya ajabu kabisa kutokea,kauli hizi za Spika Sitta hazitawahangaisha wenye dhaman ya uchambuzi wa kauli hatari kama hizi na kuchukua hatua za haraka.Ni business as usual,kauli imetolewa,siku imepita,and life goes on!
Na kwa vile magazeti yetu yako bize zaidi kuripoti habari badala ya kuchambua mantiki ya habari husika,yayumkinika tutasikia makubwa zaidi ya kauli hizi za wanasiasa wanaoogopa vivuli vyao wenyewe.Na kwa vile kilio,kicheko,kuchafua hewa na hata kukoroma kwa mwanasiasa kunatosha kuwa leading news kwenye magazeti yetu,basi tutarajia vimbwanga zaidi.
Trust me,tutashuhudia vituko vingi zaidi na zaidi kadri siku zinavyoyoyoma kuelekea uchaguzi mkuu wa 2010.By the way,si ndio tunaelekea kile kipindi cha usanii wa kisiasa ambapo watu wazima hupiga magoti majukwani na wengine kutoa shikamoo hata kwa watoto wadogo alimradi wahakikishiwe kura?
KINACHOKWAMISHA VITA DHIDI YA UFISADI NI HUU MTINDO WA KUENDESHA MAMBO KISHKAJI.UKITAFAKARI KAULI YA CHEYO KUHOFIA KUHUSISHA HABARI ZA UFISADI HUO NA HATUA YA SPIKA KUMTOA NJE YA BUNGE HIVI KARIBUNI UTAGUNDUA KUWA BADALA YA MBUNGE HUYO KUSHUGHULIKIA SUALA HILO KAMA MWENYEKITI WA KAMATI HUSIKA,YEYE ANAJIONA KAMA JOHN MOMOSE CHEYO ALIYETOLEWA NJE NA SAMUEL SITTA,BADALA YA OFISI YA BUNGE ILIYO CHINI YA SPIKA NA WATENDAJI KADHAA.
NA UNAFIKI MWINGINE NI WA HAO WABUNGE WALIONUKULIWA KATIKA HABARI HII AMBAYO HAWATAKI KUTAJWA MAJINA KISA WANAOGOPA KUANDAMWA NA WABUNGE WENZAO.KWANI WALIINGIZWA BUNGENI NA HAO WABUNGE WENZAO WANAOWAOGOPA AU WANANCHI HUKO MAJIMBONI?
WIZI MTUPU!