Featured Posts

Showing posts with label MSIBA. Show all posts
Showing posts with label MSIBA. Show all posts

Monday, June 10, 2013

Rest in Peace Mama Mzazi wa Bloga mwenzangu na dada yangu Lilly Melody


Bloga mwenzangu Lilly Melody amefiwa na mama yake. Bado sina taarifa za kutosha kuhusu tukio hili la kuhudhunisha mno.Kwa wakti huu ninawaomba wasomaji wa blogu tuungane kumwombea marehemu na kumfariji mfiwa.

Pumziko la milele, umpe ee Bwana na Mwanga wa milele umwangazie apumzike kwa amani Amen.

Pole sana Lilly

Saturday, April 27, 2013

Tangazo la Msiba wa Mtanzania mwenzetu nchini Marekani



Watanzania wanaoishi New Jersey na New York City. Wanasikitika kutangaza kifo cha mtanzania mwenzao Adolph aka Brian aka Thadeo Lwakajende kilichotokea tarehe 24 mwezi wa 4, 2011 hapa New Jersey, USA. Mipango ya kusafirisha mwili wa marehemu inaendelea huko New Jersey. Ili kufanikisha mipango hiyo wanawaomba watanzania wote popote pale walipo wajiunge nao kusaidia kuchangisha hela za shughuli hiyo. Unaweza kutuma hela kwa kutumia paypal adolffuneralcost@gmail.com au katika site hii ya Adolf sending home fund http://dt.tl/adolfsendhomecost.
Kwa mawasiliano ya shughuli hizi wasiliana na 

Peter Luangisa (917) 681-6971

Rashidi Kamugisha (973) 703-4596

Bernard Kivugo (973) 580-7166

William Vedasto (973) 551-2916

Tunatanguliza shukurani zetu za dhati. 

--
Thanks
--
******************************
Sara (Admin/Writer/ Editor)
http://www.tanzanianblogawards.com
Skype Id: Bongoblogawards
Twitter Id: Bongoblogawards
******************************


Thursday, February 07, 2013

MSIBA MZITO: Askofu Thomas Laizer wa KKKT Afariki



Habari zilizotufikia hivio punde kutoka Jijini Arusha zinaarifu kuwa Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini Kati, Ask Thomas Laizer amefariki dunia.

Taarifa hizo zinadai kuwa Ask. Laizer amefikwa na umauti alasiri ya leo katika Hospitali ya Rufaa ya Selelian ya Mjini Arusha.


Jana Februari 6, 2013 Waziri Mkuu Mizengo Pinda, alimtembelea  na kumjulia hali Askofu Thomas Laizer wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kaskazini Kati.

Taarifa zilipasha kuwa Askofu Laizer alilazwa Hospitalini hapo kwa zaidi ya mwezi mmoja, na hakuna daktari wala ndugu aliye tayari kusema ugonjwa unaomsibu.

Pinda alikwenda hospitalini hapo jana saa 9 alasiri na kukaa zaidi ya nusu saa, huku waandishi wa habari wakizuiwa kuingia katika chumba alimolazwa cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu.

Hata hivyo, baada ya kutoka katika chumba hicho kama ilivyo ada ya viongozi kuzungumzia hali ya mgonjwa, Pinda hakuzungumza na waandishi wa habari na kulikuwa na ulinzi mkali ambapo pia waandishi wa habari walizuiwa kuzungumza naye.

Awali ilisemekana kuwa Askofu Laizer amehamishiwa katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC ya Moshi mkoani Kilimanjaro, baada ya watu wengi kumiminika Selian kutaka kumwona, lakini jana ilidhihirika kuwa, amelazwa hospitalini hapo.

 FK Blog inatoa pole kwa Waumini na washarika wote wa KKKT nchini kote kufuatia msiba huo mzito ulilolikumba Kanisa la Kilutheri hasa wakati huu ambao kuna mgongano kati ya waumini na Viongozi wa Dayosisi ya Kaskazini Kati.


Sunday, July 15, 2012

Mazishiya Mtanzania Aliyefariki ghafla huko Boston,Massachusetts, Marekani (PICHA)
































Marehemu Patrin Kibelloh aliefariki ghafla siku ya Jumanne July10,2012. alizikwa Ijumaa july13 huka kwenye makaburi ya Gardner, West Roxbury ,Massachusset. Nchini Marekani 



  
Baadhi ya ndugu na marafiki waliohudhuria katia msiba huko nyumbani kwake Saugus, Boston Massachusset.


Marehemu Patrin Kibelloh amepata mafunzo katika Institute proffesional & Restaurant mjini Boario nchini ITALY alizaliwa April 25,1963 huko Tanzania ameacha mke wa Watoto wawili akiwa na umri wa miaka 49. (Picha zote na swahilivilla.blogspot.com)

         Mwenyezi Mungu ailaze roho ya Marehemu Mahali Pema Peponi!

Wednesday, April 11, 2012

Taswira za Safari ya Mwisho ya Kanumba (PICHA ZOTE KWA HISANI YA MXCARTER)



IMG_1316

IMG_1315
IMG_1317

IMG_1330

IMG_1331
IMG_1324
IMG_1323
IMG_1325
IMG_1631

IMG_1630

IMG_1371
IMG_1363

IMG_1358

IMG_1350

IMG_1348
IMG_1640
IMG_1345
IMG_1344
IMG_1343
IMG_1334

IMG_1333

IMG_1332

Wednesday, January 18, 2012

Picha za Mazishi ya Marehemu REGIA MTEMA huko Ifakara













Picha zote kwa hisani ya Jamii Forums

Saturday, January 14, 2012

Taarifa Zaidi kutoka Chadema Kuhusu Msiba wa Mheshimiwa Regia Mtema



TANZIA


Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepatwa na majonzi makubwa na kinasikitika sana kwa kifo cha Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Taifa, Mheshimiwa Regia Mtema ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum na Waziri Kivuli wa Kazi na Ajira. Mheshimiwa Regia Mtema amefariki leo tarehe 14 Januari 2011 kwa ajali ya gari katika eneo la Ruvu darajani.
 


Katika uhai wake marehemu Regia Mtema amefanya kazi mbalimbali za kisiasa na kijamii katika taifa. Marehemu Regia Mtema amezaliwa tarehe 21 mwezi Aprili mwaka 1980 na kusoma shule za sekondari kidato cha kwanza mpaka cha sita katika shule ya sekondari ya Forodhani na Shule ya Wasichana ya Sekondari ya Machame. Marehemu Regia Mtema alipata shahada yake ya kwanza (Bsc Home Economics and Human Nutrition) katika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine. 



Mara baada ya kuhitimu masomo yake marehemu Regia Mtema alifanya kazi katika taasisi mbalimbali kabla ya kujiunga na CHADEMA na kuteuliwa kuwa Afisa Mwandamizi katika Kurugenzi ya Vijana ya CHADEMA na baadaye kuteuliwa kuwa Afisa Mwandamizi katika Kurugenzi ya Mafunzo ya CHADEMA nafasi ambayo aliishikilia hadi mwaka 2010 alipoteuliwa kuwa mbunge wa viti maalum. 



Viongozi wakuu wa CHADEMA wakiongozwa na Mwenyekiti Freeman Mbowe ambaye pia ni kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani bungeni, Katibu Mkuu Dr. Wilbroad Slaa, wajumbe wa kamati kuu, wakurugenzi wa chama makao makuu na wabunge wamejumuika hivi sasa na familia ya marehemu katika kipindi hiki kigumu. 



CHADEMA inatoa pole kwa familia ya marehemu Regia Mtema, wananchi wa Mkoa wa Morogoro hususani wa Jimbo la Kilombero, wanachama wote wa CHADEMA, jamii ya watu wenye ulemavuTanzania na Watanzania wote kwa ujumla, kutokana na msiba huu wa ghafla katika wakati ambapo mchango wake ukihitajika kwa chama na kwa taifa. 



Taarifa zaidi kuhusu taratibu za maziko, itatolewa mara baada ya kukamilisha majadiliano baina ya familia ya marehemu, chama na Ofisi ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 


Mipango ya mazishi ya marehemu inapangwa nyumbani kwa Baba wa Marehemu Regia Mtema, Ndugu Estelatus Mtema, Tabata Chang'ombe. Ratiba ya maziko itatolewa baada ya kukamilika kwa taratibu zinazopangwa na familia ya marehemu, Ofisi ya Bunge na chama. 


Mungu ailaze roho ya Marehemu Regia Mtema, mahali pema peponi. Amina.



Imetolewa na: 

John Mnyika(Mb)
Mkurugenzi wa Habari na Uenezi

Picha kwa Hisani ya Jamii Forums

Breaking News: Mbunge Regia Mtema afariki kwa ajali ya gari



Habari za kusikitisha zilizopatikana kwenye mtandao wa jamii wa Twitter na ukumbi wa mijadala ya mtandaoni wa Jamii Forums zinaeleza kuwa Mbunge wa Viti Maalum kwa tiketi ya Chadema,Regia Mtema,amefariki kwa ajali ya gari iliyotokea daraja la mto Ruvu.

Licha ya kifo cha Regia kuwa pigo na pengo kubwa kwa Chadema pia ni msiba mkubwa kwa sie wazawa wa wilaya ya Kilombero,mahali alipozaliwa marehemu na ambapo alipatumikia kwa nguvu zake zote.

Tutawaletea taarifa zaidi kadri zinavyopatikana.

Bwana Ametoa Bwana Ametwaa,Jina lake lihimidiwe Milele.Amen.

Wednesday, November 02, 2011

Pole sana Sophia Mwanauta kwa Kufiwa na mdogo wako mpendwa


KWA NIABA YANGU BINAFSI NA  WASOMAJI WA BLOGU NINATOA SALAMA NYINGI ZA POLE KWA PRODUCER WA SPORAH SHOWSOPHIA MWANAUTA, KWA MSIBA MKUBWA WA KUONDOKEWA NA MDOGO WAKE MPENDWA.

HAKUNA MANENO MWAFAKA TUNAYOWEZA KUKUPA KATIKA KIPINDI HIKI KIGUMU LAKINI MAANDIKO YANATUFUNDISHA KUWA SOTE NI WAJA WA MUUMBA NA HUTUCHUKUA KATIKA MUDA NA WAKATI ATAKAO YEYE.LAKINI KWA VILE MWENYEZI MUGNU NI MWINGI WA HURUMA NA UPENDO BASI SIO TU ATAWALIWAZA WAFIWA KATIKA KIPINDI HIKI KIGUMU LAKINI PIA ATAMJAALIA MAREHEMU PUMZIKO LA AMANI

YEYE NDIYE MUUMBA,ANAPOMCHUKUA MMOJA WETU NI KWA VILE LICHA YA KUWA TULIMPENDA MAREHEMU LAKINI MOLA ALIMPENDA ZAIDI NA KUAMUA KUMCHUKUA.

POLE SANA SANA SOPHIA.MOLA AKUJAALIE WEWE BINAFSI NA FAMILIA,NDUGU NA JAMAA NGUVU NA MOYO WA KUSTAHILIMILI MAJONZI MLIYONAYO

INNA LILLAHI WA INNA ILAYHI RAJI'UN

من المؤكد أننا ننتمي إلى الله وإنا إليه راجعون يجب

SURELY WE BELONG TO ALLAH AND TO HIM SHALL WE RETURN


Wednesday, October 12, 2011

Tangazo la Msiba wa Mtanzania Mwenzetu

MSIBA WA MTANZANIA MWENZETU MZEE SAID MUHAMMAD SIKAMKONO

Tunaskitika kuwataarifu kuhusu kifo cha Mtanzania mwenzetu Mzee Said Muhammad Sikamkono kilichotokea jana tarehe 11/10/2011 mchana katika hospitali ya Queen Elizabeth, Woolwich, London.
Mipango ya mazishi inaendelea na mtaendelea kujulishwa. Kwa wakati huu ambao tutakuwa tunasubiri kupata taarifa ya mazishi, mwenye kuweza kuchangia chochote au mwenye kuhitaji kujua zaidi kuhusu msiba huu, tunaomba awasiliane na;
Sheikh Ayub kwa namba; 07944930708
AU
 Said Surur kwa namba; 07538063536
AU
Mr. Haruna Mbeyu kwa namba; 07813539025.

“MWENYEZI MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU SAID MUHAMMAD SIKAMKONO MAHALI PEMA.  MUNGU AMETOA NA MUNGU AMETWAA, JINA LAKE LIBARIKIWE”

Monday, July 07, 2008

RAMBIRAMBI KUTOKA KWA JONGWE

Jamaa yangu mmoja mkazi wa Kwa Jongwe (Zimbabwe) kanitumia fedha hii kama rambirambi rambi yake kwa msiba ulionikumba hivi karibuni.

Tuesday, June 03, 2008

TANGAZO LA MSIBA

NINASIKITIKA KUWATANGAZIA KIFO CHA MAMA YANGU MZAZI ADELINA MAPANGO KILICHOTOKEA IFAKARA MOROGORO TAREHE 29/05/2008 NA MAZISHI YALIKUWA JANA TAREHE 02/06/2008 KATIKA MAKABURI YA UKOO WA CHAHALI HAPA IFAKARA.NAWASHUKURU NYOTE AMBAO KWA NAMNA MOJA AU NYINGINE MLIUNGANA NAMI KATIKA KUMUOMBEA MAMA APONE LAKINI BWANA AMEMPENDA ZAIDI NA HATIMAYE KUMREJESHA KWAKE.UKOO WA CHAHALI NA MAPANGO UNAWASHUKURU SANA KWA USHIRIKIANO WENU.BWANA AMETOA BWANA AMETWAA,JINA LA BWANA LIHIMIDIWE MILELE.

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Hot Sonakshi Sinha, Car Price in India