
Tunaomba radhi kwa picha hizi ambazo ni graphic. Tumejitahidi kuficha sura ya marehemuMwili wa mtu aliyeuawa kutokana na shambulio hilo la bomuMtu mmoja ameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa katika shambulio la bomu karibu na msikiti huko Zanzibar. Kwa mujibu wa polisi, shambulio hilo lilitokea katika eneo la Stone Town kwenye sehemu ya biashara ya Darajani.Mashuhuda wa tukio hilo walieleza kwamba miongoni mwa majeruhi ni waumini waliokuwa wanatoka kuswali katika msikiti ulio jirani na eneo hilo."Tunafanya uchunguzi kutambua aina ya bomu, waliohusika na shambulio hilo na lengo lao. Tunaomba wananchi kutupatia taarifa," alisema afisa mwandami...