Featured Posts

Wednesday, November 28, 2007

KAZI NA DAWA

KILA MUDA UNAPORUHUSU,NAPENDELEA KUTEMBELEA KIJI-LIBRARY CHANGU CHA DVDs






COLLECTION INAKUA,200+ DVDs SI HABA.


KUSOMA NOVELS ZA SYDNEY SHELDON na JOHN GRISHAM NI MITHILI YA KUANGALIA DVDs



POLISHING LANGUAGE SKILLS AND EMPOWERING MYSELF SPIRITUALLY







KAULIMBIU YA KUHAMASISHA ZOEZI LA KUPIMA UKIMWI KWA HIARI ILIKUWA "TANZANIA BILA UKIMWI INAWEZEKANA".TAFADHALI UNGANA NAMI KWENYE "TAKE" YANGU KUHUSU UWEZEKANO HUO,KATIKA MAKALA YANGU YA WIKI HII NDANI YA GAZETI LA RAIA MWEMA






---------------------------------------------------------------------------------------------------------------
CHECK OUT THIS CLIP.DEFINITELY,A LOW-BUDGET VIDEO BUT I LIKE THE VIBE,DO YOU?


Monday, November 26, 2007

MAKALA MBILI KWA MPIGO

MTANZANIA UGHAIBUNI-4

Miongoni mwa matatizo yanayowakabili wageni na wahamiaji katika nchi mbalimbali ni suala la ubaguzi.Ubaguzi wa aina yoyote ni mbaya,uwe wa rangi,dini,jinsia au maumbile.Ubaguzi unaosumbua zaidi barani Ulaya na nchi nyingine za Magharibi ni ubaguzi wa rangi,na waathirika wakubwa ni sie wenye ngozi nyeusi.Na ubaguzi wa rangi dhidi ya watu weusi unavuka mipaka ya uenyeji wa huyo anayebaguliwa kwani hata Weusi ambao wamezaliwa katika nchi husika nao hukumbana na vitendo vya ubaguzi kama vile tunavyokumbana navyo sie wageni.

Kuna rafiki yangu mmoja Mwamerika Mweusi aliwahi kuniuliza kuhusu tatizo la ubaguzi kwa hapa Scotland.Nikawa mkweli kwake kwa kumfahamisha kwamba ubaguzi upo japo sio wa wazi sana,na kuna nyakati sio rahisi kubaini kwamba umebaguliwa hadi uchunguze kwa makini.Akanipa “matumaini” kwa kuniambia kuwa nisijali sana hasa kwa vile mie ni mgeni hapa,na kwamba hata yeye huwa anakumbana na ubaguzi huko Marekani,nchi aliyozaliwa na kukulia yeye na vizazi vyake kadhaa vilivyomtangulia.Alikwenda mbali zaidi na kunijulisha kwamba yeye binafsi huwa anakumbana na “ubaguzi wa aina nyingine” pia.Rafiki yangu huyo ni mzaliwa na jimbo la South Carolina liloko kusini mwa Marekani.Kwa maelezo yake mwenyewe,lafidhi ya Wamarekani wenya asili ya kusini mwa nchi hiyo ni tofauti na wale wanaotaka maeneo mengine.Alieleza kuwa kuna wakati huwa anagundua kwamba baadhi ya watu anaoongea nao “wanamsanifu” kutokana na lafidhi yake.Lakini kama hiyo hazitoshi,rafiki yangu huyo ni mfupi (kwa maana halisi ya neno hilo,japo sio “mbilikimo”).Alidai kuwa kuna nyakati huwa anakutana na watu wanaoelekea kufanya ufupi wake kama kichekesho flani.

Kwa hapa barani Ulaya,ubaguzi wa rangi unaweza kuonekana unaongezeka kwa kasi kutokana na kukua kwa siasa za mrengo mkali wa kulia (far-right politics) hasa kuanzia miaka ya 90.Baadhi ya wachambuzi wa siasa wanasema kwamba kukua kwa siasa hizo ni matokeo ya kushindwa kwa serikali zilizoundwa na vyama vya mrengo wa kushoto (au kati) kukidhi matarajio ya wanaoongozwa (wananchi).Linapotokea suala la ukosefu wa ajira, “majeruhi” wa kwanza kulaumiwa watakuwa wageni/wahamiaji,kuongezeka kwa uhalifu nako kunahusishwa na wageni hata pale ambapo takwimu za uhalifu hazionyeshi hivyo,na ukosefu wa makazi pia huhusishwa na wingi wa wageni katika miji husika licha ya ukweli kwamba sera nyingi za makazi hutoa kipaumbele kwa wazawa kuliko wageni.Yayumkinika kusema kuwa wageni wamegeuzwa kuwa jalala la lawama kwa takriban kila baya linalotokea katika nchi hizi.

Kwa haraka haraka,kuna takriban vyama vya siasa 11 ambavyo kwa kiasi kikubwa vimekuwa vichochezi vikubwa vya ubaguzi wa rangi barani Ulaya.Vyama hivyo ni pamoja na BNP (British National Party) cha Uingereza,ambacho japo hakijawa na mafanikio makubwa ya kisiasa,kinaendelea na jitihada za kukusanya wafuasi.Vyama vingine ni Freedom Party (FPO) cha Austria ambacho kina wafuasi wengi kusini mwa nchi hiyo,Flemish Block (VB) cha Ubelgiji chenye viti 15 katika bunge dogo la nchi hiyo,na huko Denmark ni chama cha DPP (Danish People’s Party) ambacho pamoja na mambo mengine kimekuwa kikiishinikiza serikali ya mseto ya nchi hiyo kupunguza misaada kwa nchi masikini.Pamoja na kutopata matokeo mazuri kwenye uchaguzi uliopita nchini Ufaransa,Jean-Marie Le Pen na chama chake cha National Front (FN) ameendelea kuwa miongoni mwa vielelezo rahisi vya namna siasa za mrengo mkali wa kulia zinavyoshamiri barani Ulaya.Le Pen aliwashangaza wapenzi wengi wa soka duniani wakati wa michuano iliyopita ya kombe la dunia pale alipodai kuwa ni vema timu ya taifa ya soka ya nchi hiyo ikatolewa mapema kwani haiwakilishi Ufaransa kwa vile imejaa wachezaji weusi.Vyama vingine “hatari” ni pamoja na LPF cha Uholanzi,Progress Party cha Norway,Popular Party cha Ureno,na Swiss People’s Party (SVP) chenye uwakilishi mkubwa zaidi bungeni na ambacho kimetamka bayana kuwa watu weusi wanapaswa kutimuliwa nchini humo eti kwa vile “wao ndio chanzo cha uhalifu”.Huko Ujerumani,vyama vya Republican Party (REP),German People’s Union (DVU),na National Democratic Party (NPD) vimekuwa kama mwendelezo wa siasa za ki-Nazi ambapo wanachama wake wanasifika zaidi kwa uhuni,vurugu na chuki yao ya wazi dhidi ya wageni na wahamiaji.Lakini matatizo nchini Ujerumani hayaishii kwenye vyama hivyo vya ki-Nazi pekee kwani kwa mujibu wa kituo cha televisheni cha Foxnews cha Marekani,asilimia 25 ya Wajerumani wote (wengi wao wakiwa wenye umri wa miaka 60 na zaidi) wana mtizamo chanya (positive view) kuhusu sera za kibaguzi za ki-Nazi,na wanauona unyama wa Hitler ulikuwa sahihi.

Kama ilivyo nchini Ujerumani ambako vyama vya mrengo mkali wa kulia vinaelekea kurithi siasa za kinyama za ki-Nazi,nchini Italia nako vyama “hatari” vya National Alliance na Northern League vina sera za ajabu kabisa ikiwa ni pamoja na wazo lao la kuanzishwa kwa kikosi cha askari wa majini (coast guard) kitachokuwa na jukumu la kuwapiga risasi wageni wote wanaoingiza nchini humo kwa kuzamia.Pia vyama hivyo vyenye mrengo wa kifashisti vinapinga kwa nguvu Muungano wa nchi za Ulaya (EU) huku madai yao yakiwa eti EU inaongozwa na wanaopenda kufanya ngono na watoto (pedophiles).Angalau kidogo nchini Uholanzi,chama cha Pim Fortuyn’s List (PFL),licha ya msimamo wake mkali dhidi ya wahamiaji na wageni,kimekuwa na viongozi wanaotoka katika makundi ya kijamii ambayo kimsingi ni “maadui wa asili” wa siasa za mrengo wa kulia,kwa mfano watu weusi,mashoga,nk.Mwanzilishi wa chama hicho,Pim Fortuyn alikuwa shoga asiyejificha (openly gay) na naibu wake Joao Varela alikuwa Mholanzi mhamiaji Mweusi.Fortuyn ambaye aliuawa kwa kupigwa risasi alianzisha PFL baada ya kutimuliwa kwenye chama kingine cha mrengo wa kulia nchini humo cha Liveable Netherlands kutokana na upinzani wake mkali dhidi ya wageni na wahamiaji.

Hivyo ndivyo siasa za ubaguzi zinavyoshika kasi huku ughaibuni.Ninapoichambua hali hii najikuta nashindwa kujizuia kujadili “sekeseke” linalotengenezwa huko nyumbani kuhusu suala la uanzishwaji wa mahakama ya Kadhi.Nikiwa kama mwanafunzi ninayefanya utafiti ambao kwa namna flani unahusu mahusiano kati ya siasa na dini kwa huko nyumbani,naomba kusema kuwa pamoja na mazuri yote ambayo jamii inanufaika kutokana na dini,kuna tatizo moja la msingi ambalo pia linaweza kusababishwa na dini ambalo ni ubaguzi.Pengine ni vema kukumbusha pia kwamba kukua kwa siasa za ubaguzi katika nchi mbalimbali kumeambatana na baadhi ya “wazawa” kuwaangalia waumini wa dini nyingine,hususan zile za wageni na wahamiaji,kuwa “hazifai”.Tunaweza kukubaliana kuhusu kitu kimoja kwamba mara nyingi msingi wa imani wa dini moja ni kuwa dini hiyo iko bora zaidi ya dini nyingine,au pengine Mungu wa dini hiyo ndio Mungu halisi kuliko wa dini nyingine.

Mjadala kuhusu suala la mahakama ya kadhi unapaswa kufanywa kwa umakini sana hasa kwa vile ni suala nyeti na linalogusa hisia za kidini.Nadhani kuna mambo mawili matatu yanayopaswa kufanyiwa kazi mapema.Kwa upande mmoja ni kwa mamlaka husika kulishughulikia suala hili kwa uwazi na kwa kuzingatia maslahi ya pande zote husika.Nadhani badala ya kukaa kimya au kuendeleza ahadi kwamba “suala hili linashughulikiwa na litapatiwa ufumbuzi hivi karibuni” ni vema maamuzi kuhusu suala hilo yakatolewa mapema ili pamoja na mambo mengine kuzuia uwezekano wa kuzuka chokochoko za hapa na pale kutoka kwa makundi mbalimbali katika jamii.Kama maamuzi hayo yanaweza kutolewa na watengeneza sera pekee basi na yafanywe mapema lakini kwa umakini,na kama maamuzi yatapaswa kutolewa kwa njia ya maoni ya wananchi basi na iitishwe kura ya maoni mapema kadri iwezekanavyo.Kwa upande mwingine ni subira inayohitajika miongoni mwa makundi mbalimbali katika jamii.Izingatiwe kwamba katika masuala yanayogusa imani ya mtu,kauli zinazoonekana za kawaida tu lakini zenye maana tofauti kwa waumini wa dini tofauti na ya mtoa kauli hizo,zinaweza kupelekea uvunjifu wa amani na hata kuitumbukiza nchi kwenye machafuko ya kidini.Ni jukumu letu sote kukubushana kwamba wakati inachukua miongo kadhaa,kama sio karne,kujenga amani,kuipoteza ni suala la wiki chache tu,kama sio siku kadhaa.Tusiruhusu tofauti zetu za mitazamo ziwe chanzo cha kutupiana makonde,na kwa hakika tunaweza kabisa kupingana ki-hoja pasipo kutishiana amani.

IFUATAYO NI MAKALA NYINGINE

KULIKONI UGHAIBUNI-86


Asalam aleykum,

Moja ya mambo nayopendelea kufanya pindi muda unaporuhusu ni kuangalia runinga.Lakini naweza kusema kwa kujiamini kabisa kwamba mahaba yangu kwa runinga yamekuwa ni sawa na mithili ya kuingia darasani kwani ni nadra kwangu kupitisha siku nzima pasipo kujifunza kitu kipya kwenye runinga.Hiyo haimaanishi kwamba kila kipindi nachoangalia kina jambo jipya au la maana,bali najitahidi kuwa makini katika uchaguzi wa kile nachoangalia.Halafu nimejenga desturi ya kuangalia runinga huku laptop yangu ikiwa pembeni.Hiyo huwa inanirahisishia kufanya “reference” ya kitu nachokiona kwenye runinga lakini pengine hakijafafanuliwa vizuri.Inapotokea hivyo basi huwa naingiza neno husika kwenye mtambo wa kusaka habari kwenye mtandao ujulikanao kama “Google” au nakimbilia kwenye tovuti nyingine maarufu kwa maelezo ya watu na vitu ijulikanayo kama “Wikipedia”.

Kitu kimoja nilichojifunza kuhusu vipindi vya televisheni hapa Uingereza ni namna mashindano ya kupata watazamaji yalivyo juu.Kutokana na mashindano hayo,vituo vya televisheni hujitahidi kuja na ubunifu wa kila namna,wa maana na wa kipuuzi.Na miongoni mwa ubunifu huo ni hivi vipindi vinavyojulikana kama “reality tv” ambavyo kwa tafsiri isiyo rasmi ni vipindi vinavyoonyesha maisha katika uhalisi wake.Sintoingia kwa undani sana kuelezea maana ya vipindi vya namna hiyo kwani nilishawahi kuviongelea katika makala yangu moja huko nyuma.Ila kwa kukumbushia tu,katika makala hiyo nilizungumzia mbinde iliyojitokeza kwenye kipindi cha “celebrity big brother”,yaani “Big Brother” kama hiyo aloshinda Richard lakini wahusika wake wanakuwa “watu wenye majina” (celebrities).Hiyo ni “version” (aina) tofauti ya “Big Brother” ya kawaida ambayo kwa mwaka huu iliweka historia ya kupata mshindi Mweusi,Brian,Mwingereza mwenye asili ya Nigeria.Katika “Celebrity Big Brother” iliyopita kulizuka migogoro wa ubaguzi wa rangi dhidi ya stta wa filamu za Kihindi,Shilpa Shetty,ambapo washiriki watatu wakiongozwa na mshindi wa zamani wa “Big Brother” (ya kawaida) Jade Goody,walitoa matamshi kadhaa yaliyoashiria ubaguzi wa rangi.Zilipigwa kelele nyingi sana na nusura mashindano hayo yavunjike kabla ya muda wake,lakini yalifanikiwa kumalizika salama ambapo Shilpa aliibuka mshindi.Sokomoko hilo lilifika hadi bungeni na wakati flani Gordon Brown (Waziri Mkuu wa sasa) akiwa ziarani nchini India alilazimika “kuwaomba radhi” Wahindi kwamba yaliyomkuta Shilpa katika jumba la “Big Brother” sio taswira halisi ya jamii ya Waingereza.

Sokomoko la ubaguzi wa rangi katika kipindi hicho lilipelekea baadhi ya watu kuhoji umuhimu wa vipindi vya namna hiyo na faida yake kwa jamii.Lakini pia lilizua swali moja la msingi,je panapojitokeza vipindi vya kipuuzi namna hiyo wa kulaumiwa ni nani?Waandaaji au watazamaji?Kwamba kama waandaaji watakuwa makini basi ni dhahiri hakutakuwa na upuuzi katika vipindi wanavyoandaa.Lakini pia iwapo kipindi kitaonekana cha kipuuzi basi watazamaji wanaweza kukisusia hivyo kuwalazimisha waandaaji kukirekebisha au kukiondoa kabisa hewani.Ikumbukwe kwamba kwa nchi za Magharibi,vyombo vya habari vinahangaika sana kupata “ratings” nzuri,yaani idadi kubwa ya watazamaji au wasomaji.Wapo wanaodhani kuwa “ratings” zimekuwa zikichochea sana vyombo vya habari kukurupuka na habari zenye utata au za kusababisha mgongano kwani sote twafahamu kuwa “mbwa kung’ata mtu sio habari lakini mtu kung’ata mbwa ni zaidi ya habari”.Yaani kwa kifupi,utata “unalipa sana” kwenye habari.

Nije kwenye “Big Brother” ya akina Richard.Binafsi sikuwa nafuatilia kwa karibu japo ilipokuwa inaelekea ukiongoni nilijikuta natamani Mtanzania mwenzetu Richard ashinde.Lakini tukiwa wakweli na waadilifu,tunaweza kweli kujibu kwa uhakika nini cha msingi tulichojifunza kutokana na mashindano hayo?Hivi kuna lolote la maana la kujifunza pale mshiriki mmoja anapolewa chakari na kuishia kufanya tendo la ndoa huku anafahamu bayana kuwa kamera zinarekodi tukio hilo laivu?Naamini kuna wenzangu wengi tu ambao “Big Brother” kwao ina umuhimu mdogo kuliko hata vichekesho vya kikundi cha “Ze Comedy” ambavyo kwa kiasi flani vinafikisha ujumbe muhimu katika namna ya kuvunja mbavu.Sina tatizo na ushindi wa Richard,ila tatizo langu ni mantiki nzima ya “Big Brother”.

Lakini kama nilivyosema awali kuwa “mtu akimng’ata mbwa inakuwa zaidi ya habari”.Pengine laiti “Big Brother” ikiondoa “manjonjo” ya ngono za hadharani na uchafu mwingine inaweza kupoteza umaarufu na si ajabu ikafutiliwa mbali baada ya muda mfupi.Nadhani vimbwanga vinavofanyika kwenye jumba hilo vinachangia sana kuongeza umaarufu wa kipindi hicho.Kwa bahati mbaya,vimbwanga hivyo havina umuhimu wowote,sio kwa washiriki pekee bali hata kwa watazamaji.Pia nadhani ngono ndani ya jumba la “Big Brother” inaweza kufunua unafiki wa namna flani wa wenye majukumu ya kulinda maadili ya jamii yetu.Nilisoma mahala flani habari kwamba video ya wimbo “Simama Tucheze” wa Q-Chief imepigwa stop kuonyeshwa katika vituo vya runinga kwa vile imejaa vitendo vya ngono.Japo siungi mkono video zenye kuonyesha vitendo vya ngono lakini kinachonifanya niwatolee mimacho “askari wetu wa maadili” ni namna wanavyoweza kufumbia macho matendo ya ngono kwenye jumba la “Big Brother” lakini wanadiriki kumkalia kooni Q-Chief.Na si hapo tu,kama msomaji mpendwa utakuwa msikilizaji wa vipindi vya miziki (hususan vile vya mchana) nadhani utakuwa umeshasikia baadhi ya tungo za muziki wa kufokafoka (hasa wa Marekani) ambazo “hazijachujwa” na hivyo kujumuisha maneno yasiyofaa katika maadili ya jamii yetu.Kwa kawaida na kwa kuzingatia ujumbe uliomo,nyimbo za kufokafoka hutolewa katika “versions” mbalimbali lakini nazozungumzia hapa ni “radio version” (ambapo “maneno machafu” huwa yamefutwa,yamehaririwa-edited-au yameminywa) na “dirty version” (ambapo kila neno linasikika bila kujali “makali” yake).Inawezekana watangazaji wanaopiga “dirty versions” radioni huwa hawajui kinachoongelewa katika nyimbo hizo au wanajua lakini hawajali kwa vile “askari wa maadili” hawana muda wa kufuatilia.

Kabla ya kuandika makala hii nilisoma Sera ya Taifa ya Utamaduni ambayo inaharamisha waziwazi burudani zinazoendana kinyume na maadili ya jamii yetu.Lakini nadhani ufuatiliaji ni mdogo kwani hata video za baadhi ya nyimbo za wakongomani (Wazaire) ni “chafu” mno kuzionyesha kwenye runinga.Na kama unadhani hiyo ni ndogo basi nenda kajionee “ubunifu” wa bendi zetu katika suala zima la unenguaji.Amin nakuambia,namna baadhi ya wanenguaji wanavyocheza ni mithili ya kuangalia filamu ya “X”.Ukilogwa kwenda na mama mkwe kwenye shughuli kama hizo basi unaweza kujikuta unamtaka radhi kwa namna wanenguaji “wanavyojituma”.

“Askari wa maadili” wanakabiliwa na changamoto nyingine kubwa ya kudhibiti watazamaji wenye umri mdogo kwenye shughuli “za watu wazima”.Kwa hapa Uingereza,ili kijana aweze kuingia kwenye ukumbi wa disko ni lazima awe na kitambulisho kinachoonyesha kuwa umri wake unamruhusu kuingia humo.Na hilo ni hata kwenye kununua pombe na sigara.Sheria iko wazi na inasomeka kwenye kila duka kwamba ili mteja anayeonekana kuwa na umri mdogo aweze kuuziwa bidhaa anapaswa kuthibitisha umri wake.Lakini kwa huko nyumbani ni suala la kawaida kumwona mtoto mdogo kabisa akiwa na “michupa kadhaa ya bia” akielekea grosari au baa kwenda kununua bia.Hivi lile zoezi la kuanzisha vitambulisho vya taifa limefikia wapi?Je vitambulisho hivyo vitaonyesha umri wa mwenye kitambulisho?Nadhani mpango huo utakapokamilika basi inaweza kuwa rahisi kwa “askari wa maadili” kuanza kudhibiti watoto na vijana wenye umri mdogo wasiruhusiwe kuingia sehemu zinazoweza “kuwazibua akili” au kuwabana kununua bidhaa kama bia au sigara.

Pengine kabla sijamalizia makala hii utakuwa unajiuliza tangu lini jeshi la polisi limekuwa na kitengo cha “askari wa maadili”.Well, “askari wa maadili” ni pamoja na mamlaka zinahusika na kuhakikisha maadili ya jamii hayavunjwi,kuupuuzwa au kupindwa.Wahusika wengine ni wazazi,kaka,dada,mabaunsa wanaoruhusu watu kuingia disko,wauza maduka na baa,bila kusahau mimi na wewe.

Alamsiki

Sunday, November 18, 2007

KULIKONI UGHAIBUNI-86


 CHEKI MAKALA YANGU YA  WIKI HII NDANI TOLEO LA WIKI HII LA GAZETI MAHIRI NA LINALOTAMBA HUKO NYUMBANI LA RAIA MWEMA
=========================================================================================================================
Soma makala nyingine MBILI za "KULIKONI UGHAIBUNI hapa

Asalam aleykum,

Moja ya mambo nayopendelea kufanya pindi muda unaporuhusu ni kuangalia runinga.Lakini naweza kusema kwa kujiamini kabisa kwamba mahaba yangu kwa runinga yamekuwa ni sawa na mithili ya kuingia darasani kwani ni nadra kwangu kupitisha siku nzima pasipo kujifunza kitu kipya kwenye runinga.Hiyo haimaanishi kwamba kila kipindi nachoangalia kina jambo jipya au la maana,bali najitahidi kuwa makini katika uchaguzi wa kile nachoangalia.Halafu nimejenga desturi ya kuangalia runinga huku laptop yangu ikiwa pembeni.Hiyo huwa inanirahisishia kufanya “reference” ya kitu nachokiona kwenye runinga lakini pengine hakijafafanuliwa vizuri.Inapotokea hivyo basi huwa naingiza neno husika kwenye mtambo wa kusaka habari kwenye mtandao ujulikanao kama “Google” au nakimbilia kwenye tovuti nyingine maarufu kwa maelezo ya watu na vitu ijulikanayo kama “Wikipedia”.

Kitu kimoja nilichojifunza kuhusu vipindi vya televisheni hapa Uingereza ni namna mashindano ya kupata watazamaji yalivyo juu.Kutokana na mashindano hayo,vituo vya televisheni hujitahidi kuja na ubunifu wa kila namna,wa maana na wa kipuuzi.Na miongoni mwa ubunifu huo ni hivi vipindi vinavyojulikana kama “reality tv” ambavyo kwa tafsiri isiyo rasmi ni vipindi vinavyoonyesha maisha katika uhalisi wake.Sintoingia kwa undani sana kuelezea maana ya vipindi vya namna hiyo kwani nilishawahi kuviongelea katika makala yangu moja huko nyuma.Ila kwa kukumbushia tu,katika makala hiyo nilizungumzia mbinde iliyojitokeza kwenye kipindi cha “celebrity big brother”,yaani “Big Brother” kama hiyo aloshinda Richard lakini wahusika wake wanakuwa “watu wenye majina” (celebrities).Hiyo ni “version” (aina) tofauti ya “Big Brother” ya kawaida ambayo kwa mwaka huu iliweka historia ya kupata mshindi Mweusi,Brian,Mwingereza mwenye asili ya Nigeria.Katika “Celebrity Big Brother” iliyopita kulizuka migogoro wa ubaguzi wa rangi dhidi ya stta wa filamu za Kihindi,Shilpa Shetty,ambapo washiriki watatu wakiongozwa na mshindi wa zamani wa “Big Brother” (ya kawaida) Jade Goody,walitoa matamshi kadhaa yaliyoashiria ubaguzi wa rangi.Zilipigwa kelele nyingi sana na nusura mashindano hayo yavunjike kabla ya muda wake,lakini yalifanikiwa kumalizika salama ambapo Shilpa aliibuka mshindi.Sokomoko hilo lilifika hadi bungeni na wakati flani Gordon Brown (Waziri Mkuu wa sasa) akiwa ziarani nchini India alilazimika “kuwaomba radhi” Wahindi kwamba yaliyomkuta Shilpa katika jumba la “Big Brother” sio taswira halisi ya jamii ya Waingereza.

Sokomoko la ubaguzi wa rangi katika kipindi hicho lilipelekea baadhi ya watu kuhoji umuhimu wa vipindi vya namna hiyo na faida yake kwa jamii.Lakini pia lilizua swali moja la msingi,je panapojitokeza vipindi vya kipuuzi namna hiyo wa kulaumiwa ni nani?Waandaaji au watazamaji?Kwamba kama waandaaji watakuwa makini basi ni dhahiri hakutakuwa na upuuzi katika vipindi wanavyoandaa.Lakini pia iwapo kipindi kitaonekana cha kipuuzi basi watazamaji wanaweza kukisusia hivyo kuwalazimisha waandaaji kukirekebisha au kukiondoa kabisa hewani.Ikumbukwe kwamba kwa nchi za Magharibi,vyombo vya habari vinahangaika sana kupata “ratings” nzuri,yaani idadi kubwa ya watazamaji au wasomaji.Wapo wanaodhani kuwa “ratings” zimekuwa zikichochea sana vyombo vya habari kukurupuka na habari zenye utata au za kusababisha mgongano kwani sote twafahamu kuwa “mbwa kung’ata mtu sio habari lakini mtu kung’ata mbwa ni zaidi ya habari”.Yaani kwa kifupi,utata “unalipa sana” kwenye habari.

Nije kwenye “Big Brother” ya akina Richard.Binafsi sikuwa nafuatilia kwa karibu japo ilipokuwa inaelekea ukiongoni nilijikuta natamani Mtanzania mwenzetu Richard ashinde.Lakini tukiwa wakweli na waadilifu,tunaweza kweli kujibu kwa uhakika nini cha msingi tulichojifunza kutokana na mashindano hayo?Hivi kuna lolote la maana la kujifunza pale mshiriki mmoja anapolewa chakari na kuishia kufanya tendo la ndoa huku anafahamu bayana kuwa kamera zinarekodi tukio hilo laivu?Naamini kuna wenzangu wengi tu ambao “Big Brother” kwao ina umuhimu mdogo kuliko hata vichekesho vya kikundi cha “Ze Comedy” ambavyo kwa kiasi flani vinafikisha ujumbe muhimu katika namna ya kuvunja mbavu.Sina tatizo na ushindi wa Richard,ila tatizo langu ni mantiki nzima ya “Big Brother”.

Lakini kama nilivyosema awali kuwa “mtu akimng’ata mbwa inakuwa zaidi ya habari”.Pengine laiti “Big Brother” ikiondoa “manjonjo” ya ngono za hadharani na uchafu mwingine inaweza kupoteza umaarufu na si ajabu ikafutiliwa mbali baada ya muda mfupi.Nadhani vimbwanga vinavofanyika kwenye jumba hilo vinachangia sana kuongeza umaarufu wa kipindi hicho.Kwa bahati mbaya,vimbwanga hivyo havina umuhimu wowote,sio kwa washiriki pekee bali hata kwa watazamaji.Pia nadhani ngono ndani ya jumba la “Big Brother” inaweza kufunua unafiki wa namna flani wa wenye majukumu ya kulinda maadili ya jamii yetu.Nilisoma mahala flani habari kwamba video ya wimbo “Simama Tucheze” wa Q-Chief imepigwa stop kuonyeshwa katika vituo vya runinga kwa vile imejaa vitendo vya ngono.Japo siungi mkono video zenye kuonyesha vitendo vya ngono lakini kinachonifanya niwatolee mimacho “askari wetu wa maadili” ni namna wanavyoweza kufumbia macho matendo ya ngono kwenye jumba la “Big Brother” lakini wanadiriki kumkalia kooni Q-Chief.Na si hapo tu,kama msomaji mpendwa utakuwa msikilizaji wa vipindi vya miziki (hususan vile vya mchana) nadhani utakuwa umeshasikia baadhi ya tungo za muziki wa kufokafoka (hasa wa Marekani) ambazo “hazijachujwa” na hivyo kujumuisha maneno yasiyofaa katika maadili ya jamii yetu.Kwa kawaida na kwa kuzingatia ujumbe uliomo,nyimbo za kufokafoka hutolewa katika “versions” mbalimbali lakini nazozungumzia hapa ni “radio version” (ambapo “maneno machafu” huwa yamefutwa,yamehaririwa-edited-au yameminywa) na “dirty version” (ambapo kila neno linasikika bila kujali “makali” yake).Inawezekana watangazaji wanaopiga “dirty versions” radioni huwa hawajui kinachoongelewa katika nyimbo hizo au wanajua lakini hawajali kwa vile “askari wa maadili” hawana muda wa kufuatilia.

Kabla ya kuandika makala hii nilisoma Sera ya Taifa ya Utamaduni ambayo inaharamisha waziwazi burudani zinazoendana kinyume na maadili ya jamii yetu.Lakini nadhani ufuatiliaji ni mdogo kwani hata video za baadhi ya nyimbo za wakongomani (Wazaire) ni “chafu” mno kuzionyesha kwenye runinga.Na kama unadhani hiyo ni ndogo basi nenda kajionee “ubunifu” wa bendi zetu katika suala zima la unenguaji.Amin nakuambia,namna baadhi ya wanenguaji wanavyocheza ni mithili ya kuangalia filamu ya “X”.Ukilogwa kwenda na mama mkwe kwenye shughuli kama hizo basi unaweza kujikuta unamtaka radhi kwa namna wanenguaji “wanavyojituma”.

“Askari wa maadili” wanakabiliwa na changamoto nyingine kubwa ya kudhibiti watazamaji wenye umri mdogo kwenye shughuli “za watu wazima”.Kwa hapa Uingereza,ili kijana aweze kuingia kwenye ukumbi wa disko ni lazima awe na kitambulisho kinachoonyesha kuwa umri wake unamruhusu kuingia humo.Na hilo ni hata kwenye kununua pombe na sigara.Sheria iko wazi na inasomeka kwenye kila duka kwamba ili mteja anayeonekana kuwa na umri mdogo aweze kuuziwa bidhaa anapaswa kuthibitisha umri wake.Lakini kwa huko nyumbani ni suala la kawaida kumwona mtoto mdogo kabisa akiwa na “michupa kadhaa ya bia” akielekea grosari au baa kwenda kununua bia.Hivi lile zoezi la kuanzisha vitambulisho vya taifa limefikia wapi?Je vitambulisho hivyo vitaonyesha umri wa mwenye kitambulisho?Nadhani mpango huo utakapokamilika basi inaweza kuwa rahisi kwa “askari wa maadili” kuanza kudhibiti watoto na vijana wenye umri mdogo wasiruhusiwe kuingia sehemu zinazoweza “kuwazibua akili” au kuwabana kununua bidhaa kama bia au sigara.

Pengine kabla sijamalizia makala hii utakuwa unajiuliza tangu lini jeshi la polisi limekuwa na kitengo cha “askari wa maadili”.Well, “askari wa maadili” ni pamoja na mamlaka zinahusika na kuhakikisha maadili ya jamii hayavunjwi,kuupuuzwa au kupindwa.Wahusika wengine ni wazazi,kaka,dada,mabaunsa wanaoruhusu watu kuingia disko,wauza maduka na baa,bila kusahau mimi na wewe.

Alamsiki

MAKALA NYINGINE MBILI


KULIKONI UGHAIBUNI-85


Asalam aleykum,

Katika makala yangu moja huko nyuma niliwahi kuzungumzia jinsi tofauti katika misimamo ya kisiasa zinavyowagawanya Wamarekani.Nilielezea kwamba tofauti kati ya wenye mtizamo wa kihafidhina (“conservatives”) na wale wenye mtizamo wa kiliberali (“liberals”) zinavyowafanya baadhi ya Wamarekani waangaliane kama maadui.Nakumbuka siku moja nilimsikia mtangazaji maarufu wa runinga katika kituo cha Foxnews,Billy O’Reilly akimwelezea tajiri anayemwaga mamilioni kwa vikundi vya kiliberali,George Soros,kuwa ni mtu hatari zaidi katika nchi hiyo kwa vile tu anavisapoti vikundi vya kiliberali.Nilitamani kumuuliza hivi ni nani wa hatari zaidi kwa nchi hiyo kati ya Soros na Osama bin Laden.Baadhi ya wachambuzi wa siasa za ndani za Marekani wanadai kwamba miaka minane ya Rais Joji Bushi katika Ikulu ya Marekani itakumbukwa zaidi sio kwa vita ya Irak bali kushindwa kwake kujenga daraja la kuwaunganisha waliberali na wahafidhina.

Pengine unaweza kujiuliza ni nyenzo gani zinazotumiwa na makundi hayo mawili kuendeleza propaganda zao.Jibu ni jepesi.Wakati wahafidhina wanatumia zaidi watu wanaojulikana kama “radio talk show hosts” (yaani kwa mifano ya huko nyumbani ni watu kama Jenerali Ulimwengu na kipindi chake cha Jenerali on Monday-japo sijui kama bado kipo hewani,au kile cha Hamza Kassongo,au Makwaiya Kuhenga-ambavyo navyo sina uhakika kama bado vipo hewani) waliberali wanatumia zaidi nguvu mpya ya mtandao ambapo tovuti kama Media Matters,the Daily Kos,the Huffington Post,na kadhalika zimekuwa zikijitahidi ipasavyo kupambana na ajenda za talk show hosts wahafidhina kama O’Reilly,Sean Hannity,Rush Limbaugh na wengineo ni sauti muhimu katika kuzifanya ajenda za wahafidhina zisikike na kufikisha ujumbe kwa wale ambao hawako katika kundi lolote (neutrals”).

Kitu ambacho kinawatenganisha zaidi wahafidhina na waliberali ni namna ya kuifanya Marekani iwe salama zaidi hasa baada ya mashambulizi ya kigaidi yaliyofanywa tarehe Septemba 11,2001.Wakati wahafidhina wanasisitiza umuhimu wa kuwa na sheria kali kabisa ambazo zitakuwa juu ya uhuru na haki za binadamu,waliberali wanapinga kabisa hatua zozote za kupuuza haki za msingi za raia kwa kisingizio cha usalama wa nchi.Kwa mfano,wakati wahafidhina wanaoona kwamba sheria (iliyotungwa mara baada ya mashambulizi ya kigaidi ya Septemba 11) ya “kuiunganisha na kuiimarisha Marekani kwa kuipatia nyenzo mwafaka zinazohitajika kuzuia ugaidi” (the Patriot Act of 2001) inahitaji kupanuliwa zaidi bila kujali kama itaingilia uhuru wa watu binafsi,au kuwanyanyasa watu wenye asili flani (kwa mfano Waarabu),waliberali wamekuwa wakipinga sana sheria hiyo ambayo wanaoona kuwa ni ya kibaguzi,inayoingilia maisha ya watu binafsi na inayotumiwa na wahafidhina kuwadhibiti watu wasiowataka (kwa mfano wahamiaji).

Jambo jingine “linaloyagombanisha” makundi haya ni vita vya Irak.Katika hili mgawanyiko unapata mkanganyiko zaidi kwani hata miongoni mwa wahafidhina zipo sauti kadhaa ambazo aidha hazikuafiki wazo la vita tangu mwanzo au zile ambazo kwa sasa zinaamini kuwa vita hiyo haina mwelekeo na hakutakuwa na ushindi bali fedheha tu.Kwahiyo,licha ya vita hivyo kuwagawa Wamarekani kwa ujumla,pia imewagawa wahafidhina kimtazamo.Waliberali wengi waliipinga vita hiyo tangu mwanzo lakini idadi ya wapinzani wa vita hiyo,bila kujali uhafidhina au uliberali wao,imekuwa ikiongezeka siku hadi siku kutokana na mwenendo usioridhisha kwenye vita hiyo.

Pamoja na tofauti hizo kati ya makundi hayo mawili,yayumkinika kusema kuwa sio vigumu kutambua kuwa wote wanasukumwa na kitu kimoja:mapenzi kwa nchi yao,lakini wanatofautiana tu katika namna ya “kuhaisha” (keeping alive) mapenzi hayo kwa kuhakikisha kuwa taifa hilo kubwa linabaki kuwa “nchi ya ahadi” kwa kila raia.Wakati wahafidhina wanaamini kuwa ili “ndoto ya Kiamerika” (the American Dream) idumu kwa wale walokwishaifikia au iwafikie wale ambao hawajaipata,ni muhimu kuhakikisha kuwa nchi hiyo inakuwa salama kabisa,na namna pekee ya kuhakikisha usalama huo ni kwa kuweka sheria kali kabisa,waliberali wanataka kila mtu aliyepata au anayetafuta “the American Dream” awe huru pasipo kuminywa uhuru wake kwa visingizio vya kumfanya mtu huyo awe salama kabisa.

Napoiangalia “picha” ya wahafidhina na maliberali wa Marekani,najikuta nikijaribu kuichomeka kwenye jamii yetu huko nyumbani hasa pale panapojichomoza mgawanyiko katika jamii.Ni dhahiri kuwa nasi pia tuna makundi,na yaliyo bayana zaidi ni yale ya “walionazo” na “wasionazo”.Hapo nazungumzia mambo ya fedha.Na ndani ya kundi ya walionazo,kuna wale walifanikuwa “kuwa nazo” kwa njia halali,na wale ambao “wanazo” kwa njia za kisanii (hapa ndio tunakutana na mafisadi,wala rushwa,matapeli,wauza unga,watu wa noti feki,wahujumu uchumi,na wanaharamu wengine).Katika kundi la “wasio nazo” ambalo yayumkinika kusema ndio lenye kujumuisha watu wengi zaidi (kwani laiti “walio nazo” wangekuwa wengi basi nchi yetu isingekuwa maskini kiasi hiki) kuna wale ambao angalau wanapata kidogo lakini mbinde inakuja katika kukipanga bajeti kidogo hicho wanachopata,na wale ambao hawana hata hicho kidogo cha kupangia bajeti,yaani kwa Kindamba wanasema “migwala kwahela”,au kwa lugha ya zamani hizooo walikuwa wanasema “apeche alolo”,yaani ni hohehahe,hawana kitu,hawajui asubuhi itapitaje mchana utakuwaje jioni itaishaje na usiku watalala vipi.

Makundi haya mawili yanakuwa na mitizamo tofauti kutokana na nafasi zao katika jamii.Ni dhahiri kwamba kutakuwa na tofauti ya mawazo na mtizamo kati ya mtu aliyeshiba na yule mwenye njaa,kama ilivyo kwa yule aliyelala kwenye chumba chenye kiyoyozi na yule aliyelala kibarazani Kariakoo akipigwa na mbu huku akijaribu kuwa makini “asifanyiziwe” na watoto wa kihuni.Ni dhahiri pia kwamba kuna tofauti kati ya mtu aliyelewa bia ghali kama Heinkein na yule aliyelewa mataputapu uwanja wa fisi,ambapo wakati mmoja wao anakunywa bia kuustarehesha ubongo,huyo mwingine anakunywa kuzuia ubongo usifikirie kesho itakuwaje.

Habari njema kuhusu makundi haya,ya “walionazo” na “wasionazo”,ni kwamba wote ni Watanzania.Na hapo ndio napotaka kupigilia msumari wa pointi yangu.Kwa vile sote ni Watanzania,basi hatuna budi,licha ya tofauti zetu kiuchumi,kusaidiana kufanikisha ndoto ya “Tanzania yenye neema inayoundwa na Watanzania wenye neema”.Hapa simaanishi watu wakatwe mishahara yao ili kuwasaidia wale wasio na kitu,bali walengwa wangu wakuu hapa ni wale ambao kwa tamaa zao binafsi wanakwamisha jitihada za kujenga jamii ambayo,japo sio yenye usawa wa asilimia 100 (hakuna jamii kama hiyo duniani),tofauti kati ya wenye nacho na wasio nacho ni ndogo kuliko ilivyo hivi sasa.Kwa wenye jukumu la kuhakikisha kuwa kodi inalipwa katika wakati stahili na kwa kiwango sahihi,kwa wale wenye kuhakikisha wala rushwa wanafikishwa mbele ya vyombo vya sheria na kupewa adhabu wanayostahili (sheria sio tu ichukue mkondo wake bali pia ionekane imechukua mkondo wake) na kwa wale wanaojua bayana kuwa wanachosaini kwenye mikataba kina mapungufu lakini wanaendelea kuisaini kwa sababu wanazojua wenyewe,au wanasiasa wanaoweka maslahi ya chama mbele badala ya ustawi wa taifa,mnaweza kabisa kuisaidia Tanzania yetu kuwa ya neema zaidi ya hapa ilipo iwapo kila mmoja ataweka mbele maslahi ya taifa badala ya maslahi ya tumbo lake au nyumba ndogo yake.Tumkumbuke Mwalimu Nyerere,na kumzawadia kwa kujitahidi kutimiza ndoto yake aliyoihangaikia muda mrefu ya kujenga jamii yenye usawa.Narudia kusema,haihitajiki watu kuchangia fedha zao (halali au za kisanii),kinachohitajika ni kuwajibika kwa kuweka mbele maslahi ya taifa na kuacha ubinafsi.

Mwisho,napenda kuelezea masikitiko yangu kuhusu namna uhuru wa habari unavyotumiwa ndivyo sivyo.Kuna mwandishi mmoja wa huko nyumbani (sintomtaja jina hapa) ambaye amebobea sana kwenye picha za utupu kiasi kwamba ameamua kufungua blogu yake inayohusu picha za ngono pekee.Kutaja jina la blogu hiyo itakuwa ni sawa na kuwashawishi watu wakaone uchafu uliomo humo.Naamini kwamba kama mie nisie na ujuzi wa kutosha katika fani ya kompyuta nimeweza kumtambua mmiliki wa blogu hiyo,naamini kabisa mamlaka zenye wataalam (wanaolipwa mishahara kutokana na utaalam huo) watamdhibiti paparazzi huyo mwenye shetani wa picha za ngono.Wito wangu kwa mwanaharamu huyu ni kwamba asidhani kila mtu ana mtindio wa akili kama yeye,namshauri aache upuuzi huo kabla hajaumbuka.

Alamsiki

-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------

KULIKONI UGHAIBUNI-84


Asalam aleykum,

Leo nianze na swali.Hivi demokrasia ni kitu cha aina moja duniani kote (“universal”) au ni kila nchi inaweza kutafsiri demokrasia kwa mtazamo unaendana na mazingira ya nchi husika?Watu kadhaa wamehoji uhalali wa nchi kama Marekani kudai ni kinara wa demokrasia ilhali mfumo wake wa uchaguzi unaweza kutafsiriwa na wengine kuwa ni dhaifu kuliko tulionao huko nyumbani.Au Uingereza ina demkrasia ya kweli huku taasisi kama bunge la mabwanyenye (“House of Lords”) linalojumuisha vingunge ambao hawapigiwi kura lakini wana nguvu kubwa katika kutunga na kurekebisha sheria zinazotawala nchi hii?Na hapo hatujagusia nafasi ya familia ya kifalme katika maana nzima ya demokrasia ya Uingereza,au pale Tony Blair alipoamua kuwapuuza asilimia kubwa ya Waingereza waliompinga asimuunge mkono Joji Bush kupeleka majeshi ya Uingereza huko Irak.

Pengine ugumu wa kuelewa maana na matumizi ya demokrasia unachapata mkanganyiko zaidi tunapoangalia mabadiliko ya kutoka mfumo wa chama kimoja kwenda vyama vingi barani Afrika.Baada ya mageuzi hayo ya kisiasa,tumeshuhudia baadhi ya nchi zikiwa na vyama vya siasa lukuki lakini wingi huo haujawa na manufaa makubwa kwa wananchi.Sanasana baadhi ya vyama hivyo vimeishia kuwa kama enzi zile ambapo Simba na Yanga zilikuwa na timu za pili (yaani Simba-B au Yanga-B) ambapo tunaona kitu kama “chama tawala-A”, “chama tawala-B”, “chama tawala-C”,na kadhalika.Na tofauti na mataifa ambayo yamekuwa na mfumo wa vyama vingi kwa muda mrefu ambapo baadhi ya watu wamezaliwa wakiwa kwenye vyama flani,kwenye “demokrasia changa” hakuna namna zaidi (“alternative”) ya vyama vipya kutotegemea viongozi na wanachama kutoka kwenye chama tawala.Yayumkinika kusema kuwa ni vigumu kubaini iwapo kweli viongozi na wanachama hawa wanapohama chama tawala na kwenda chama kingine wanakuwa wamefuta kabisa “mahaba” yao kwa chama chao cha awali.

Kuna matukio mawili yaliyojiri hivi karibuni hapa Uingereza ambayo kwa namna flani yanaleta changamoto ya namna flani kwenye mjadala huu usioisha kuhusu suala la demokrasia.Kwanza ni ujio wa mfalme wa Saudi Arabia.Ziara hiyo ilizua upinzani mkali kutoka kwa baadhi ya makundi katika jamii ambayo yalidai kuwa si sahihi kwa nchi kama Uingereza inayojigamba kuwa inathamini sana demokrasia na haki za binadamu kumkaribisha kiongozi wa Saudi Arabia ambayo (kwa viwango vya nchi za Magharibi) haijali demokrasia wala haki za binadamu.Ilifikia hatua kiongozi wa chama cha upinzani chas Liberal Democrats alisusia ziara ya mfalme huyo akipinga namna nchi hiyo inavyokandamiza haki za binadamu na demokrasia.Pengine alikuwa sahihi lakini Uingereza ina kila sababu za kuikumbatia Saudi Arabia hasa kwa vile Saudi ni mteja mkuu wa zana za kijeshi zinazotengenezwa Uingereza.Kwa namna flani, “uhai” wa kampuni ya BAE Systems (najua hapa utakuwa umekumbuka habari za rada) unategemea sana mahitaji ya zana za kijeshi ya Saudi.Na hapa najikuta nakumbuka “darasa” langu la moja katika mwaka wangu wa kwanza pale Mlimani ambapo ulijitokeza mjadala kuhusu uchumi na siasa.Swali lilikuwa “je uchumi ndio unatengeneza siasa ya nchi au siasa ya nchi ndio inatengeneza mfumo wa uchumi”.Hadi leo naposomea “uzamivu kwenye siasa” sina jibu la uhakika kwenye swali hilo.

Wapo waliosema sio haki kwa Uingereza kuibana Zimbabwe lakini inaikumbatia nchi kama Saudi Arabia.Wengine wanasema Saudi inakumbatiwa kwa sababu za kiuchumi (mauzo ya zana za kijeshi na mafuta) lakini Zimbabwe inabanwa kwa sababu za kisiasa tu.Na hao wanakwenda mbali zaidi kwa kudai kuwa hata vita ya Irak haikuwa ya kumng’oa Saddam bali tamaa ya mafuta na ndio maana sababu zilizopelekea uvamizi wa Irak hazitumiki kwenda kurekebisha mambo katika nchi kama Sudan,Somalia au DRC.


Jingine ni hukumu iliyotolewa dhidi ya Metropolitan Police (tuliite jeshi la polisi la Uingereza,kufupisha maelezo) kutokana na kifo cha M-Brazil Jean de-Menezes.Baada ya hukumu hiyo iliyowaona polisi wana hatia,kumesikika vilio vinavyomtaka “mkuu” wa polisi hao Sir Ian Blair (hana undugu na Tony Blair) ajiuzulu.Inaweza kuitwa demokrasia ya kweli kwani huyo aliyeuawa wala hakuwa Mwingereza (na kulikuwa na madai kuwa hata hati yake ya kuishi hapa ilikuwa imesha-“expire”).Lakini kwa hawa wenzetu,suala la “kulindana” linakabiliwa na ugumu mkubwa kutoka na uwazi unaotawala taasisi zao.Nakumbuka kuna mkulima aliyeuawa wilayani Kilombero wakati anafukuzwa na polisi na mwingine ambaye aliyefia kituo cha polisi hukohuko wilayani Kilombero lakini hadi leo sijaskia kilichoendelea.Kwa kuwahukumu polisi waliojikuta wakiua raia asiye na hatia wakati wanahangaika kuzuia matukio ya kigaidi jijini London,yayumkinika kusema kuwa hiyo ndio demokrasia,kujali haki ya kila binadamu kuishi na uwazi unaotakiwa kufuatwa popote pale ulimwenguni.Lakini kama ishu ni hiyo,vipi kuhusu kukumbatia wale wanaodaiwa kutojali haki za binadamu kama Saudi Arabia?

Tuachane na hayo ya demokrasia kwani ni mjadala mrefu ambao sio wa kuisha leo au kesho.Niangalie huko nyumbani.Hivi karibuni kumekuwa na mtikisiko ulioletwa na kile kiitwacho “orodha ya mafisadi”.Pamoja na kuwa nimeshalisikia neno “fisadi” mara kadhaa lakini majuzi nilishindwa kumjibu rafiki yangu mmoja aliyeniuliza “hivi neno fisadi linamaanisha nini”.Nachofahamu ni kuwa maana ya neno hilo haiko mbali na maneno kama mwizi,jambazi,mhujumu uchumi,mbadhirifu,na kadhalika.Sitaki kujadili kama waliotoa madai hayo wako sahihi au la,au labda waliotuhumiwa ni mafisadi kweli au la,nachotaka kukizungumzia hapa ni namna ya baadhi ya waliotuhumiwa walivyo-“react”.Kuna waliosema watakwenda mahakamani kuhakikisha hao waliowatuhumu wanathibitisha madai hayo.Hilo lilikuwa wazo zuri kwa sababu kama mtu anakuita mwizi huhitaji kubishana nae bali mpeleke mahakamani akathibitishe madai yake.Cha kushangaza ni kwamba takriban waliotishia kwenda mahakamani vitisho hivyo vimebaki kuwa hadithi.Kwa upeo wangu mdogo wa masuala ya sheria nafahamu kuwa kesi ya madai inaweza kufunguliwa muda wowote ndani ya miezi 12 tangu yatolewe madai husika (naomba nikosolewe kama nimekosea hapo) lakini “mkwara” wa kwenda mahakamani ungekuwa na uzito zaidi kama ungetolewa baada ya kufungua kesi dhidi ya watoa tuhuma au ungeambatana na utekeleezaji wa vitisho hivyo kuliko hali ilivyo sasa ambapo watu wengi wanajiuliza “kulikoni”?

Kuna walioamua kuyapuuza madai hayo,pengine kwa hekima kwamba kuzijibu tetesi ni sawa na kuzimwagia petroli.Au pengine wameamua kuziacha tuhuma hizo kama zilivyo kwa minajili ya kuwaachia wananchi wachambue pumba na mchele,yaani kujua ukweli ni upi na uzushi ni upi.Kwa mtizamo wangu,hao wamefanya vema zaidi kwani hatotokea wa kuwauliza “ee bwana vipi kuhusu ile ahadi yako ya kumpeleka flani mahakamani akathibitishe tuhuma dhidi yako?Au ndio unaafikiana na alichokisema?” Nakumbuka kuna sehemu flani kwenye Biblia Takatifu ambapo Yesu alimwomba Mungu awasemehe wale waliokuwa wanahoji na kubeza u-masiya wake,na alisema “Bwana naomba uwasamehe hawa kwani hawajui walitendalo”.Je waliotishia kwenda mahakamani kudai haki zao lakini hawajafanya hivyo hadi leo nao wameamua kuwasamehe waliowatuhumu “kwa vile waliotoa tuhuma hizo hawakujua watendalo”,au bado wanakusanya ushahidi? Miongoni mwa madhara yanayoweza kujitokeza kwa waliotuhumiwa kuendelea kukaa kimya ilhali walishatamka kuwa wanawaburuza “wagomvi wao” mahakamani ni kuenea kwa hisia miongoni mwa wananchi kuwa labda wameogopa kwenda mahakamani kwa vile yaliyosemwa dhidi yao ni ya kweli (binafsi nadhani mahakama ndio yenye nafasi nzuri zaidi ya kuthibitisha “ukweli” au “uongo” wa tuhuma hizo).

Mwisho,napenda kuwapongeza wana-CCM wote walioshinda kwenye uchaguzi mkuu wa chama hicho.Waingereza wana msemo “when you get something how you got it is immaterial” yaani ukishapata kitu,namna ulivyokipata sio muhimu sana.Ushindi wenu (kwa namna yoyote ulivyopatikana) una maana kubwa sio kwa kwenu na CCM pekee bali kwa Watanzania wote kwa ujumla kwani mnategemewa kuwa mtampatia sapoti ya kutosha JK kuendeleza dhamira yake ya kufanya maisha bora kwa kila Mtanzania yawezekane.Napenda kuamini kuwa kila aliyegombea na kushinda alikuwa na dhamira moja kuu ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya neema kwa kila mmoja wetu,na hilo linawezekana kabisa.

Alamsiki

KULIKONI UGHAIBUNI-86

Soma makala nyingine mbili hapa

Asalam aleykum,

Moja ya mambo nayopendelea kufanya pindi muda unaporuhusu ni kuangalia runinga.Lakini naweza kusema kwa kujiamini kabisa kwamba mahaba yangu kwa runinga yamekuwa ni sawa na mithili ya kuingia darasani kwani ni nadra kwangu kupitisha siku nzima pasipo kujifunza kitu kipya kwenye runinga.Hiyo haimaanishi kwamba kila kipindi nachoangalia kina jambo jipya au la maana,bali najitahidi kuwa makini katika uchaguzi wa kile nachoangalia.Halafu nimejenga desturi ya kuangalia runinga huku laptop yangu ikiwa pembeni.Hiyo huwa inanirahisishia kufanya “reference” ya kitu nachokiona kwenye runinga lakini pengine hakijafafanuliwa vizuri.Inapotokea hivyo basi huwa naingiza neno husika kwenye mtambo wa kusaka habari kwenye mtandao ujulikanao kama “Google” au nakimbilia kwenye tovuti nyingine maarufu kwa maelezo ya watu na vitu ijulikanayo kama “Wikipedia”.

Kitu kimoja nilichojifunza kuhusu vipindi vya televisheni hapa Uingereza ni namna mashindano ya kupata watazamaji yalivyo juu.Kutokana na mashindano hayo,vituo vya televisheni hujitahidi kuja na ubunifu wa kila namna,wa maana na wa kipuuzi.Na miongoni mwa ubunifu huo ni hivi vipindi vinavyojulikana kama “reality tv” ambavyo kwa tafsiri isiyo rasmi ni vipindi vinavyoonyesha maisha katika uhalisi wake.Sintoingia kwa undani sana kuelezea maana ya vipindi vya namna hiyo kwani nilishawahi kuviongelea katika makala yangu moja huko nyuma.Ila kwa kukumbushia tu,katika makala hiyo nilizungumzia mbinde iliyojitokeza kwenye kipindi cha “celebrity big brother”,yaani “Big Brother” kama hiyo aloshinda Richard lakini wahusika wake wanakuwa “watu wenye majina” (celebrities).Hiyo ni “version” (aina) tofauti ya “Big Brother” ya kawaida ambayo kwa mwaka huu iliweka historia ya kupata mshindi Mweusi,Brian,Mwingereza mwenye asili ya Nigeria.Katika “Celebrity Big Brother” iliyopita kulizuka migogoro wa ubaguzi wa rangi dhidi ya stta wa filamu za Kihindi,Shilpa Shetty,ambapo washiriki watatu wakiongozwa na mshindi wa zamani wa “Big Brother” (ya kawaida) Jade Goody,walitoa matamshi kadhaa yaliyoashiria ubaguzi wa rangi.Zilipigwa kelele nyingi sana na nusura mashindano hayo yavunjike kabla ya muda wake,lakini yalifanikiwa kumalizika salama ambapo Shilpa aliibuka mshindi.Sokomoko hilo lilifika hadi bungeni na wakati flani Gordon Brown (Waziri Mkuu wa sasa) akiwa ziarani nchini India alilazimika “kuwaomba radhi” Wahindi kwamba yaliyomkuta Shilpa katika jumba la “Big Brother” sio taswira halisi ya jamii ya Waingereza.

Sokomoko la ubaguzi wa rangi katika kipindi hicho lilipelekea baadhi ya watu kuhoji umuhimu wa vipindi vya namna hiyo na faida yake kwa jamii.Lakini pia lilizua swali moja la msingi,je panapojitokeza vipindi vya kipuuzi namna hiyo wa kulaumiwa ni nani?Waandaaji au watazamaji?Kwamba kama waandaaji watakuwa makini basi ni dhahiri hakutakuwa na upuuzi katika vipindi wanavyoandaa.Lakini pia iwapo kipindi kitaonekana cha kipuuzi basi watazamaji wanaweza kukisusia hivyo kuwalazimisha waandaaji kukirekebisha au kukiondoa kabisa hewani.Ikumbukwe kwamba kwa nchi za Magharibi,vyombo vya habari vinahangaika sana kupata “ratings” nzuri,yaani idadi kubwa ya watazamaji au wasomaji.Wapo wanaodhani kuwa “ratings” zimekuwa zikichochea sana vyombo vya habari kukurupuka na habari zenye utata au za kusababisha mgongano kwani sote twafahamu kuwa “mbwa kung’ata mtu sio habari lakini mtu kung’ata mbwa ni zaidi ya habari”.Yaani kwa kifupi,utata “unalipa sana” kwenye habari.

Nije kwenye “Big Brother” ya akina Richard.Binafsi sikuwa nafuatilia kwa karibu japo ilipokuwa inaelekea ukiongoni nilijikuta natamani Mtanzania mwenzetu Richard ashinde.Lakini tukiwa wakweli na waadilifu,tunaweza kweli kujibu kwa uhakika nini cha msingi tulichojifunza kutokana na mashindano hayo?Hivi kuna lolote la maana la kujifunza pale mshiriki mmoja anapolewa chakari na kuishia kufanya tendo la ndoa huku anafahamu bayana kuwa kamera zinarekodi tukio hilo laivu?Naamini kuna wenzangu wengi tu ambao “Big Brother” kwao ina umuhimu mdogo kuliko hata vichekesho vya kikundi cha “Ze Comedy” ambavyo kwa kiasi flani vinafikisha ujumbe muhimu katika namna ya kuvunja mbavu.Sina tatizo na ushindi wa Richard,ila tatizo langu ni mantiki nzima ya “Big Brother”.

Lakini kama nilivyosema awali kuwa “mtu akimng’ata mbwa inakuwa zaidi ya habari”.Pengine laiti “Big Brother” ikiondoa “manjonjo” ya ngono za hadharani na uchafu mwingine inaweza kupoteza umaarufu na si ajabu ikafutiliwa mbali baada ya muda mfupi.Nadhani vimbwanga vinavofanyika kwenye jumba hilo vinachangia sana kuongeza umaarufu wa kipindi hicho.Kwa bahati mbaya,vimbwanga hivyo havina umuhimu wowote,sio kwa washiriki pekee bali hata kwa watazamaji.Pia nadhani ngono ndani ya jumba la “Big Brother” inaweza kufunua unafiki wa namna flani wa wenye majukumu ya kulinda maadili ya jamii yetu.Nilisoma mahala flani habari kwamba video ya wimbo “Simama Tucheze” wa Q-Chief imepigwa stop kuonyeshwa katika vituo vya runinga kwa vile imejaa vitendo vya ngono.Japo siungi mkono video zenye kuonyesha vitendo vya ngono lakini kinachonifanya niwatolee mimacho “askari wetu wa maadili” ni namna wanavyoweza kufumbia macho matendo ya ngono kwenye jumba la “Big Brother” lakini wanadiriki kumkalia kooni Q-Chief.Na si hapo tu,kama msomaji mpendwa utakuwa msikilizaji wa vipindi vya miziki (hususan vile vya mchana) nadhani utakuwa umeshasikia baadhi ya tungo za muziki wa kufokafoka (hasa wa Marekani) ambazo “hazijachujwa” na hivyo kujumuisha maneno yasiyofaa katika maadili ya jamii yetu.Kwa kawaida na kwa kuzingatia ujumbe uliomo,nyimbo za kufokafoka hutolewa katika “versions” mbalimbali lakini nazozungumzia hapa ni “radio version” (ambapo “maneno machafu” huwa yamefutwa,yamehaririwa-edited-au yameminywa) na “dirty version” (ambapo kila neno linasikika bila kujali “makali” yake).Inawezekana watangazaji wanaopiga “dirty versions” radioni huwa hawajui kinachoongelewa katika nyimbo hizo au wanajua lakini hawajali kwa vile “askari wa maadili” hawana muda wa kufuatilia.

Kabla ya kuandika makala hii nilisoma Sera ya Taifa ya Utamaduni ambayo inaharamisha waziwazi burudani zinazoendana kinyume na maadili ya jamii yetu.Lakini nadhani ufuatiliaji ni mdogo kwani hata video za baadhi ya nyimbo za wakongomani (Wazaire) ni “chafu” mno kuzionyesha kwenye runinga.Na kama unadhani hiyo ni ndogo basi nenda kajionee “ubunifu” wa bendi zetu katika suala zima la unenguaji.Amin nakuambia,namna baadhi ya wanenguaji wanavyocheza ni mithili ya kuangalia filamu ya “X”.Ukilogwa kwenda na mama mkwe kwenye shughuli kama hizo basi unaweza kujikuta unamtaka radhi kwa namna wanenguaji “wanavyojituma”.

“Askari wa maadili” wanakabiliwa na changamoto nyingine kubwa ya kudhibiti watazamaji wenye umri mdogo kwenye shughuli “za watu wazima”.Kwa hapa Uingereza,ili kijana aweze kuingia kwenye ukumbi wa disko ni lazima awe na kitambulisho kinachoonyesha kuwa umri wake unamruhusu kuingia humo.Na hilo ni hata kwenye kununua pombe na sigara.Sheria iko wazi na inasomeka kwenye kila duka kwamba ili mteja anayeonekana kuwa na umri mdogo aweze kuuziwa bidhaa anapaswa kuthibitisha umri wake.Lakini kwa huko nyumbani ni suala la kawaida kumwona mtoto mdogo kabisa akiwa na “michupa kadhaa ya bia” akielekea grosari au baa kwenda kununua bia.Hivi lile zoezi la kuanzisha vitambulisho vya taifa limefikia wapi?Je vitambulisho hivyo vitaonyesha umri wa mwenye kitambulisho?Nadhani mpango huo utakapokamilika basi inaweza kuwa rahisi kwa “askari wa maadili” kuanza kudhibiti watoto na vijana wenye umri mdogo wasiruhusiwe kuingia sehemu zinazoweza “kuwazibua akili” au kuwabana kununua bidhaa kama bia au sigara.

Pengine kabla sijamalizia makala hii utakuwa unajiuliza tangu lini jeshi la polisi limekuwa na kitengo cha “askari wa maadili”.Well, “askari wa maadili” ni pamoja na mamlaka zinahusika na kuhakikisha maadili ya jamii hayavunjwi,kuupuuzwa au kupindwa.Wahusika wengine ni wazazi,kaka,dada,mabaunsa wanaoruhusu watu kuingia disko,wauza maduka na baa,bila kusahau mimi na wewe.

Alamsiki



Friday, November 09, 2007

MAKALA NDANI YA GAZETI LA RAIA MWEMA

Ukurasa wa mbele wa gazeti la RAIA MWEMA



Makala kamili bonyeza hapa
----------------------------------------------------------------------------------------------------------------
SHUGHULI YA 50 CENT NDANI YA ABERDEEN

Jana kulikuwa na burudani ya aina yake hapa Aberdeen.Rapa mahiri kutoka USA,50 Cent alifanya concert "la kufa mtu" katika ukumbi wa AECC ambapo maelfu ya mashabiki walijitokeza.Baada ya kupelekeshana na shule yangu,niliona ni wazo zuri kwenda kupumzisha akili maeneo hayo,pamoja na kupata picha mbili tatu za ku-share nanyi wasomaji wa blogu hii.

Baada ya kusota kwenye foleni ndeeefu,hatimaye nilitia mguu ndani ya ukumbi.Kwa bahati mbaya mie ni mzembe flani linapokuja suala la "namba" (hesabati) na hivyo nashindwa hata kukadiria idadi ya watu waliojazana ukumbini humo.Lakini nadhani kulikuwa na makumi ya maelfu ya watu,may be 10,000 may be 50,000.Labda nituie "njia za uswahilini" kuelezea urefu wa foleni ili kukupa idea ya watu waliojitokeza .Nilipofika eneo hilo kulikuwa na "mnyororo wa watu" kwa umbali sawa na kuanzia kituo cha basi cha Morocco hadi Mkwajuni (kwa makadirio ya chini).Kwa bahati mbaya sikubahatika kupata picha ya foleni hiyo.

Warming up ya ukumbi ilifanywa na DJ maarufu WHOO KID,


ZAIDI KUHUSU DJ WHOO KID CHEKI HAPA

Concert lilifunguliwa na rapa mwingine mahiri FABOLOUS.Roho yangu ilisuuzika vilivyo pale rapa huyo alipopiga kibao ambacho nimekisevu kwenye collection yangu katika Palm Treo yangu (bado natumia Treo 650-chuma cha pua hicho).Kibao hicho kinaitwa Breathe.Nilikirekodi lakini memory kwenye simu yangu ikanifanyia uhuni,ikajaa kabla wimbo haujaisha.



Baada ya burudani nzito ya FABOLOUS,ilifuatia zamu ya 50 CENT akishirikiana na LOYYD BANKS.Nachosikitika ni kwamba nilifanya uzembe wa kutosoma manual ya kiji-Casio Exilim EX-Z75 changu kabla sijaondoka maskani kwangu.Nikiri kuwa jana nilikuwa naitumia kamera hiyo kwa mara ya kwanza,na baada ya memory ya simu kujaa,nilitaraji ningerekodi sehemu kubwa ya concert hiyo kwa kutumia kamera hiyo.Ah wapi,kila nikibonyeza hiki inakuwa vile,basi mwishowe nikaamua kupiga picha tu badala ya kurekodi video.Picha zenyewe ndio hizo (nilifanya uzembe mwingine wa kutotumia anti-shake setting ya kamera ndio maana picha zenyewe haziko clear sana.Anyway,wakati mwingine tunajifunza kutokana na makosa).Hebu ngoja niache picha hizo zizungumze zenyewe.


SHUGHULI INAANZA KUCHUKUA KASI

BURUDANI

50 CENT NA LOYYD BANKS

KWENYE HUO MSITU WA HAWA WHITES NI VIGUMU KUDHANI NA SIE WENGINE TULIKUWEPO

MIKONO JUU....

NI MAPENZI KWA 50 CENT AU KUKUBALIKA KWA HIP-HOP BEYOND HIMAYA YA BLACKS?

PEOPLE WERE ASKING WHERE IS YOUNG BUCK?WHERE'S TONY YAYO?

WASKOTISHI WALICHENGUKA SI MCHEZO

MATAA

50 CENT NA LOYYD BANKS

LOYYD BANKS AKIWAKILISHA

50 CENT AKIRUSHA SNEAKERS ZAKE ZA G-UNIT KAMA KUMBUKUMBU KWA MASHABIKI

50 CENT AKIJIANDAA KURUSHA T-SHIRT YAKE YA G-UNIT KWA MASHABIKI

MAMBO YA MEGA SCREEN HAYO
VINNI VIDDI VICCI

Nimalizie kwa burudani hii ya 50 CENT katika video ya Piggy Bank (huyu jamaa hajambo kwa "kuponda") na hii ya FABOLOUS ya So Into You (I hope you take note of my favourite video vixen KD Aubert).Talkin of Video Vixens,I can't stop looking at the way these ladies dance in the background,and so is huyu vixen aliye kati katika in most scences.Kwa kumalizia,ni huyu innocent looking vixen na message ya Skinnyman katika soundtrack ya movie Kidulthood.

Friday, November 02, 2007

MTANZANIA UGHAIBUNI-3

Ama kweli ni rahisi kupanga sera na kutegemea ifanikiwe lakini ni habari nyingine kwa mpanga sera kuwa sehemu ya utekelezaji huo.Hilo limejihidhirisha katika taarifa kutoka nchini Marekani ambapo maafisa wa mambo ya nje wa nchi hiyo wamefahamishwa kwamba watakuwa wakipelekwa nchini Irak kama sehemu ya utekelezaji wa majukumu yao ya kazi.Pamoja na kukumbushwa kwamba wakati wanakubali ajira waliapa kufanya kazi mahala popote watakapopangiwa na mwajiri wao,maofisa hao wameonekana kutoafikiana na pango huo ambapo baadhi yao wamefikia hatua ya kuuita “mpango wa kujipeleka kwenye hukumu ya kifo” hasa kwa vile “ziara” za aina hiyo tayari zimeshagharimu maisha ya maofisa watatu tangu kuanza kwa vita ya Irak.Maofisa wanaokaidi agizo hilo wanakabiliwa na hatari ya kuchukuliwa hatua kali ikiwa ni pamoja na kufukuzwa kazi.Nadhani pamoja na hatari inayoweza kuwakabili maofisa wanaopelekwa huko,nadhani utekelezaji wa agizo hilo utawasaidia kufahamu namna hali halisi ilivyo kwenye uwanja wa mapambano ni ambayo ni ngumu zaidi kuliko urahisi wa kuandaa sera,mikakati na mipango mizuri.



Kwa hapa UK,moja ya masuala ambayo kwa siku kadhaa sasa yametawala duru za habari ni kuhusu “Muungano” wa Uingereza (the United Kingdom of Great Britain and Northern Ireland). Kumekuwa na mjadala wa muda mrefu kuhusu mambo makuu mawili: kwa upande mmoja ni umuhimu wa Muungano huo (miongoni mwa wale wanaopendelea kuona unadumu milele) na upande mwingine ni hoja kwamba muungano huo unazipunja baadhi ya sehemu zinazounda nchi hii.Katika uchaguzi mkuu uliopita,chama tawala cha Labour kilibwagwa na chama cha SNP (Scottish National Party) kwa upande wa Scotland.Hofu ya awali kwa Labour na “wapenda Muungano” baada ya ushindi wa SNP ilikuwa kwenye ukweli kwamba miongoni mwa malengo ya muda mrefu ya SNP ni kuiona Scotland ikiwa nchi huru inayojiendesha pasipo kuelekezwa na “serikali” ya London.Na katika manifesto yao ya uchaguzi,SNP hawakuogopa kutamka bayana matamanio yao uhuru wa Scotland.Chama hicho kilikuwa kinaelewa bayana kwamba sera hiyo ingeweza kuwapatia ushindi au kushindwa kwenye uchaguzi huo,kwani suala la uhuru wa Scotland ni miongoni mwa mambo yanayowagawa sana watu hawa.Kura mbalimbali za maoni kuhusu suala hilo zimekuwa na matokeo yanayothibitisha mgawanyiko huo,ambapo takriban nusu ya Waskotishi wanadhani uhuru ni wazo zuri huku takriban nusu nyingine wakipinga wazo hilo.Jeuri ya madai ya uhuru inachangiwa na kile Waskotishi wengi wanachokiona kama utajiri katika eneo hili (mafuta) ambao wanadhani unapaswa kuwanufaisha zaidi wao sambamba na kuwa na maamuzi ya namna ya kutumia utajiri huo badala ya kusubiri maelekezo kutoka England.Lakini wapo wanaoonya kwamba Scotland haiwezi kujimudu yenyewe kwa kutegemea tu utajiri wa mafuta,na baadhi ya wachumi wamekwenda mbali zaidi kwa kuonyesha pengo la bajeti litakaloikumba Scotland pindi ikijitoa kwenye Muungano huu.

Mjadala bado unaendelea na ni vigumu kusema bayana iwapo uhuru utapatikana au Muungano utaendelea.Majuzi,kiongozi wa chama pinzani cha Conservatives,David Cameron amewasha tena moto kuhusu suala hilo baada ya kutamka kwamba ana nia ya kusukuma sheria itakayowabana wabunge wa Scotland waliopo kwenye bunge la jumla la Uingereza (yaani linalojumuisha wabunge wa England,Wales,Scotland na Northern Ireland) wasipige kura kwenye masuala yanayoihusu England pekee.Hili ni suala linalujulikana kama “the West Lothian Question” (jina linalotokana na swali lililoulizwa mwaka 1977 na mbunge wa jimbo la Scotland la West Lothian,Tam Dalyell,wakati wa mjadala wa bunge kuhusu kuanzisha serikali-devolved governments-za Scotland na Wales).Swali hilo lilihusu uhalali wa wabunge wa “nchi” hizo mbili kushiriki katika mijadala na maamuzi yanayowahusu watu wa England pekee,ilhali wabunge wa England hawana nafasi kama hiyo kwa vile hawaingii kwenye mabunge ya sehemu hizo.Chama cha Labour kimemshutumu Cameron kwa kile walichokiita sera za kuvunja Muungano lakini kwa vyovyote vile hoja hiyo ni habari njema kwa Alec Salmond (First Minister wa Scotland) na chama chake cha SNP pamoja na wale wote wanaotaka uhuru.

Na kuna mambo yanayoshangaza kuhusu Muungano huu.Kwa mfano,wakati noti zinazotolewa na benki ya England (English Pounds) zinatumika nchi nzima,na zinakubalika mahala popote duniani kama sarafu halali ya nchi hii,noti zinazotolewa na mabenki ya Scotland (ambazo zina thamani sawa na English pounds) zinakataliwa katika baadhi ya maeneo ya England.Nilipokuja huko nyumbani mwaka jana,nilishindwa kabisa kubadilisha Scottish pounds na ilinilazimu nizitume huku ili zibadilishwe kuwa English pounds.Sheria za elimu ya juu na huduma za afya pia zinatofautiana kwa namna flani,ambapo kwa Scotland huduma nyingi zinatolewa bure ilhali kwa England zinaendelea kulipiwa.Scotland pia imekuwa ikilalamikia suala la uhamiaji ambapo sheria zinazotawala ni zile za nchi nzima ilhali mahitaji ya “nguvu-kazi” kutoka nje (kupitia uhamiaji wa wageni) unaathiriwa na sheria “kali” zinazotawala nchi zote zilizopo kwenye Muungano huu. Wakati Scotland imekuwa ikiendesha program kadhaa za kuvutia wageni,ikiwa ni pamoja na kuwashawishi wale walio hapa waifanye “nchi” hii kuwa makazi ya pili (second home) au makazi ya kudumu,kelele za wanasiasa huko England ni kwamba wageni wamezidi na lazima serikali idhibiti zaidi wahamiaji.

Masuala ya muungano ni nyeti na yamekuwa chanzo cha matatizo katika sehemu mbalimbali duniani.Lakini tofauti na wenzetu hawa ambao wanadiriki kutoa mawazo yao hadharani na kukaribisha mijadala kuhusu suala hilo,huko nyumbani kuzungumzia kuhusu Muungano inaelekea kuwa sio wazo la busara sana kwa mwanasiasa anayotaka mafanikio.Kuna kile kinachoitwa “jinamizi la Mwalimu kwa atakayetaka kuvunja Muungano” ambacho kimsingi nakiona ni kama kikwazo kwa wale wote wanaodhani kwamba ni muhimu kuwa na mjadala kuhusu hatima ya Muungano wetu.Tukiendelea kuogopa kuujadili,yayumkinika kusema kwamba tunautengenezea mazingira mazuri ya kuuharibu.Sio siri kwamba wenzetu wa Visiwani wamekuwa wakipiga kelele sana kwamba Muungano unawaumiza,lakini hofu yangu kubwa ni pale wenzao wa Bara nao “watakaposhikilia bango” hoja hiyo ya kuumizwa na mzigo wa Muungano.Na “the West Lothian Question” ya Uingereza “ina-fit” kabisa mazingira yalivyo huko nyumbani ambapo wabunge kutoka Zanzibar wamekuwa wakishiriki (katika bunge la Muungano) katika kujadili na kutoa maamuzi katika baadhi ya mambo ambayo yanayowahusu Wabara pekee ilhali wabunge wa Bara hawana nafasi hiyo kwani hawaingii kwenye Baraza la Wawakilishi huko Zanzibar.

Nafahamu kuwa kuna kitu kama “tume” au “kamati” iliyoundwa kujadili kero za Muungano,lakini japo sijui imefikia hatua gani katika majadiliano yao,yayumkinika kusema kwamba kasi nzima ya kulitafutia ufumbuzi wa kudumu suala hilo sio ya kuridhisha.Pengine katika kuepuka maamuzi yanayotoka juu kwenda chini (yaani kutoka kwa viongozi kwenda kwa wananchi) japo waathirika au wafaidika wakubwa ni hao wa chini,sio wazo baya kufikiria kuitisha kura ya maoni ili kupata mawazo ya wadau wakubwa wa Muungano huo (wananchi).Ashakum si matusi,lakini ni vema Muungano ukavunjika kwa ridhaa kuliko ukadumu kwa manung’uniko,kwani manung’uniko hayo yasipopatiwa tiba yanaweza kabisa kuuvunja Muungano huo pasipo kusubiri ridhaa ya wadau.Kikubwa nilichojifunza katika mjadala wa Muungano wa Uingereza ni namna ambavyo unavyoendeshwa kwa uwazi na upana zaidi kiasi kwamba sauti zote,zinazopinga na kukubali suala hilo,zinasikika waziwazi.Ukiniuliza iwapo Muungano wetu ni muhimu,jibu nitakalokupa hata niwapo usingizini ni “ndio”.Hata hivyo,umuhimu wa Muungano huo hauondoi haja ya kuufanya uwe bora zaidi,wa manufaa kwa pande zote mbili na wenye mazingira yatakayoufanya udumu daima dumu.Tusipoziba ufa leo,kesho tutajenga ukuta.

Mwisho, napenda kutoa pongezi kwa kizazi kipya cha vijana wabunifu. Hivi karibuni, mchora katuni na mtangazaji maarufu Masudi “Kipanya” alizindua duka la nguo za lebo yake ya “KP Wear”. Na msanii wa bongoflava AY nae anaelekea kufuata mkondo huo. Hawa na wengineo wenye mawazo kama hayo wanatumia vizuri umaarufu walionao kwenye jamii na wanastahili sapoti yetu. Wito wangu kwao ni kwamba wanapomiminiwa sifa kwa jitihada zao, wazitumie sifa hizo kuwa chemchem ya kusaka mafanikio zaidi. Pia wanaweza kwenda mbali zaidi kwa kutumia mianya ya biashara ya kimataifa kama vile katika e-Bay ili kuwawezesha Watanzania popote walipo duniani kunufaika na ubunifu wao. Kwa lugha ya mtaani, mie “nawapa tano”.Tanzania ya “masupastaa” wanaovuma kwa ubunifu wao,na sio kwa skendo,inawezekana.

Alamsiki

Sunday, October 28, 2007

KULIKONI UGHAIBUNI-83

Asalam aleykum,

Kwanza nianze kwa salamu za rambirambi kwa familia,ndugu,jamaa na marafiki wa marehemu Salome Mbatia,aliyetutoka hivi majuzi kutokana na ajali ya gari.Sote ni wasafiri,mwenzetu ametutangulia tu,Bwana ametoa Bwana ametwaa,jina lake lihimidiwe milele.Baada ya rambirambi hizo naomba kuzungumzia suala moja ambalo kwa naona kwa namna flani linaathiri umoja wetu wa kitaifa.Jambo hilo ni kuendekeza itikadi za chama kwenye matukio ambayo kimsingi ni ya kitaifa zaidi kuliko kichama.Katika picha mbalimbali kuhusu msiba wa marehemu Mbatia nimeona “makada” lukuki wa chama tawala wakiwa katika magwanda yao ya kijani na nyeusi.Nikabaki najiuliza,hivi waungwana hao wangevaa mavazi yao ya kawaida wangeonekana hawana majonzi ya msiba huo?Au walivaa mavazi hayo kwa maagizo ya kiongozi flani?Kama ni maagizo kutoka ngazi za juu,mbona viongozi wakuu wa chama hicho walikuwa kwenye mavazi yao ya kawaida tu (hasa suti nyeusi)?JK,Malecela,Karume,Makamba,nk wote walikuwa wamevalia suti nyeusi na wala sio magwanda ya kijani na nyeusi,pengine kwa sababu msiba huo ulikuwa wa kitaifa,na hata jeneza la marehemu halikuvikwa bendera ya CCM bali ya Taifa.

Nafahamu marehemu Mbatia alikuwa mwanachama,kada na kiongozi wa chama dume,lakini marehemu pia alikuwa naibu waziri wa serikali ambayo japo inaongozwa na CCM lakini inawatumikia Watanzania wote bila kujali itikadi zao.Katika utekelezaji wa majukumu yake ya unaibu waziri,marehemu Mbatia alikuwa akigusa maisha ya kila Mtanzania,awe mwanachama wa CUF,TLP,Chadema,au kama sie tusio memba wa chama chochote.Nafahamu waliovaa magwanda ya CCM watasema kuwa walitinga mavazi hayo kutokana na nafasi ya marehemu katika chama,lakini sote tunafahamu kuwa alama za chama (mfano bendera,vipeperushi,mavazi,nk) zina tabia ya kuvuta hisia hasi katika mikusanyiko ya isiyo ya kichama.Nafahamu pia kwamba kila mwombolezaji alikuwa na haki ya kuvaa vyovyote atakavyo lakini pia naamini wengi wetu tunapojiandaa kwenda kwenye misiba huwa tunatafakari nini cha kuvaa,na kuepuka mavazi ambayo yanaweza kuleta hisia tofauti.

Hakuna dhambi kuweka maslahi ya chama mbele ya chama kingine lakini ni dhambi kubwa kuweka maslahi ya chama mbele ya maslahi ya taifa.Chama cha siasa kinaweza kufa lakini taifa lazima liendelee kuwa hai.Mtu anaweza kuamua kuhama chama kimoja na kuingia kingine kadri apendavyo,lakini ni mbinde kwelikweli kuhama utaifa wako na kuchukua mwingine kirahisi namna hiyo.Nafahamu kuna watakaopingana nami,lakini binafsi naamini kwamba kuna wenzetu wamekuwa wakituletea “politiki” hata pale pasipostahili.Yaani matukio kadhaa ya kitaifa yamekuwa yakiporwa na hao wanaotaka kutuonyesha namna gani walivyo wakereketwa kwenye siasa.Na katika hili sio wanachama wa kawaida tu bali hata baadhi ya viongozi wenye nyadhifa serikalini.Kuweka kando mambo ya chama na kuzungumzia masuala ya kitaifa hakumfanyi kiongozi wa serikali kukosa sifa za uongozi.Kuna vikao na mikutano ya chama,na huko ndiko mahala pa kupiga propaganda za vyama.

Kwa kawaida huwa naanza makala zangu na habari za ughaibuni lakini niliona ni vema katika makala hii nikaanza na mada hiyo ya msiba wa marehemu Mbatia,na “kuwananga” wale walioleta mambo ya siasa kwenye msiba huo wa kitaifa.Huku ughaibuni,duru za kisiasa zinaelekea zaidi eneo la Ghuba ambapo kwa upande mmoja hali ya usalama ni ya wasiwasi huko kaskazini mwa Irak kwani majeshi ya Uturuki yameripotiwa kufanya mashambulizi kadhaa dhidi ya Wakurd.Waturuki wanadai kuwa lengo la mashambulizi hayo ni kuwadhibiti wapiganaji wa kikundi cha PKK kinachipigania kuunda kwa taifa huru la Wakurd.Kwa upande mwingine,kuna dalili kwamba Marekani inajiandaa kuivamia Iran.Majuzi,Marekani ilitangaza vikwazo kadhaa dhidi ya Iran,lakini zaidi ya hapo kuna taarifa kwamba jeshi la anga (US air force) limeomba fedha za dharura dola milioni 88 kwa ajili ya kufanya marekebisho kwenye ndege za kivita ziitwazo B2 ili ziweze kuhimili uzito wa mabomu yanayojulikana kama “Big Blu” au “the Mother of All Bombs” (mama wa mabomu yote).Mabomu hayo yana uzito wa takriban tani 13 kila moja,na yana uwezo mkubwa zaidi wa kupenya vizuizi (ardhi,miamba,nk).Inasemekana kuwa majengo ya kituo cha nyuklia cha Iran huko Natanz yapo futi 75 chini ya ardhi,Inaelezwa pia kwamba tayari Marekani imeshatambua “targets” 1000 nchini Iran ambazo zitakuwa za kwanza kushambuliwa pindi mambo yatapokuwa mambo.

Mahesabu ya kisiasa yanaashira pia kwamba wazo la mkutano kati ya Israel na Palestina utakaofanyika hivi karibuni huko Annapolis,Marekani (ambao unatarajiwa “kuzaa” taifa la Palestina) ni miongoni mwa dalili za Marekani kujipanga kuivamia Iran.Yaani mantiki hapo ni kwamba kwa kuunda taifa la Palestina,kelele za mataifa ya Waarabu wa Sunni kama Saudi Arabia na Misri zitakuwa sio kubwa sana pindi Iran itakaposhambuliwa na Marekani.Hata hivyo,wazo la kuishambulia Iran linaangaliwa kwa wasiwasi na baadhi ya wajuzi wa siasa za kimataifa na diplomasia.Kuna wanaodhani kwamba ni vema Marekani ikamaliza kibarua ilichojipachika huko Irak na Afghanistan kabla ya kukimbilia kuivamia Iran.Pia wanaonya kwamba uvamizi dhidi ya Iran unaweza kuzua wimbi kubwa la ugaidi wa kimataifa (pengine kutokana na madai kwamba Iran imekuwa ikivisaidia baadhi ya vikundi vinavyodaiwa kuwa vya kigaidi,mfano Hizbollah),kukongoroa kabisa hali ya usalama nchini Irak na pengine kusababisha bei ya mafuta kupanda zaidi ya dola 100 kwa pipa.

Sababu zinazotolewa na Marekani kuhusu umuhimu wa kuidhibiti Iran ni pamoja na kwamba dunia itakuwa mahala salama zaidi iwapo Iran haitakuwa na uwezo wa kutengeneza au kumiliki silaha za nyuklia (ilishasemwa huko nyuma kuwa dunia itakuwa salama zaidi pindi Saddam Hussein atapong’olewa madarakani).Ukweli ni kwamba Iran yenye uwezo wa kinyuklia ni tishio kwa swahiba mkuu wa Marekani,Israel.Pia kuna wanaotaka Bush aingie kwenye vitabu vya historia kwa “kuiadhibu na kuidhibiti Iran na hivyo kuepusha madhara yanayoweza kutokea pindi nchi hiyo ikiweza kutengeneza na kumiliki silaha za maangamizi”.Waumini wa mawazo haya wanatambua kuwa Bush amebakiwa na muda mchache kabla hajafungasha virago vyake kutoka jengo lilipo namba 1600 Pennsylvania Avenue (makazi ya rais,White House),na wanadhani kwamba asipotumia muda huu kuishikisha adabu Iran,basi inaweza kuwa vigumu mno kufanya hivyo mbeleni hususan iwapo mgombea yoyote wa chama cha Democrats atamrithi Bush.

Nirejee tena huko nyumbani.Hapa nina mawili.Kwanza,katika kikao kilichopita cha Bunge tulisikia namna baadhi ya watendaji katika Wizara ya Maliasili na Utalii wanavyoendeleza ufisadi.Waziri alieleza kuwa ameshakabidhi orodha ya wahusika mahala panapostahili,na akaahidi kuendelea kuwabana mafisadi katika wizara hiyo.Tukio la hivi karibuni ambapo magogo kadhaa yalikamatwa yakiwa tayari kusafirishwa nje,limezuia “mchezo wa kuigiza” ambapo wakati Waziri anasema hivi baadhi ya watendaji wake wanadiriki kumpinga hadharani kwa kusema vinginevyo.Hivi hawa wanaompinga Waziri wanapata jeuri hiyo wapi?Nimeona kwenye gazeti la “Habari Leo” ambapo Waziri Maghembe alieleza kwamba amejipanga vizuri kukabiliana na matatizo yote ndani ya wizara yake,ikiwa ni pamoja na tatizo la ufisadi.Yayumkinika kutabiri kuwa dhamira yake nzuri inaweza isifanikiwe kutokana na kiburi kilichojengwa na baadhi ya anaowaongoza katika wizara hiyo ambapo bila kujali protokali au nidhamu wanadiriki kupinga hadharani na kauli halali ya serikali (kupitia waziri wake).Hivi jeuri,kiburi na kujiamini kwa “wazalendo” hao inatoka wapi?

Mwisho,ni ushindi wa Simba dhidi ya Yanga.Mwenye kununa na anune,lakini ndio hivyo tena,milioni 50 hazikufanikiwa kumaliza uteja wa watani wetu wa mtaa wa Jangwani.Nilishatabiri katika makala za nyuma kuwa atakaefungwa kwenye mapambano wa watani wa jadi ataingia kwenye mgogoro.Mie nadhani kufungwa huko ni sehemu ndogo tu ya tatizo linaloikabili Yanga.Ukiangalia maelezo aliyotoa Mwenyekiti wa klabu hiyo pale mfadhili wao alipojitoa (kwa muda!?) ambapo alieleza kwa undani na kwa kuzingatia vipengele vya sheria kuhusu utata uliopo kwenye suala zima la klabu hiyo kugeuzwa kampuni.He!!muda si mrefu Mwenyekiti huyohuyo alisikika tena akipita huku na kule kuomba radhi.Je ina maana yale maelezo aliyotoa awali hayakuwa sahihi?Mie naamini yalikuwa,bado yako na yataendelea kuwa sahihi kama kweli Yanga (na Simba pia) wanataka wafike sehemu wakajiendesha wenyewe kwa mafanikio na kuachana na utegemezi.Yote yanawekana iwapo kila mmoja atatimiza wajibu wake.

Alamsiki

Thursday, October 18, 2007

LEO MAKALA MBILI KWA MPIGO

Nadhani sio wazo baya kuja na makala mbili kwa mpigo.Usichoke kusoma,au kama namna gani vipi soma moja halafu nyingine iweke kiporo uisome baadae.

KULIKONI UGHAIBUNI-82

Asalam aleykum,

Siasa za kimataifa zina vituko vyake,na pengine hakuna mahala pazuri vya kushuhudia vituko hivyo zaidi ya kuangalia baadhi ya siasa za nadani na za nje za Marekani.Hivi karibuni kumeibuka mgawanyiko baina ya pande mbili za siasa za nchi hiyo,yaani chama cha Democrats na kile cha Republicans,kuhusu unyama uliofanywa na Uturuki kwa Waarmenia mwaka 1915 ambapo inakadiriwa zaidi ya watu milioni moja walipoteza maisha.Democrats wanataka Marekani itamke bayana kuwa unyama huo uliosababisha maafa makubwa ni sawa na “genocide”,yaani mauaji ya halaiki kama yale ya Rwanda au yale ya Manazi dhidi ya Wayahudi.Lakini Republicans wanasema kuwa kwa kufanya hivyo Marekani itajiweka pabaya katika vita yake dhidi ya ugaidi ambapo Uturuki ni mshirika wake wa karibu.Democrats wanaoona kwamba siasa za kuwapendeza marafiki walioshiriki kwenye vitendo vya kukiuka haki za binadamu sio wazo la busara pengine kwa imani kwamba pasipo Marekani kuweka bayana msimamo wake katika suala hilo itapelekea kuchafua taswira yake kama taifa linalopigania usawa katika kila kona ya dunia (kwa mujibu wa imani ya nchi hiyo).Tayari Uturuki imeanza kutunisha misuli yake kwa kumtaka balozi wake huko Marekani kurejea nchini kwake “kwa majadiliano” (hiyo ni lugha ya kidiplomasia ya kuonyesha kutoridhishwa na mambo flani) na pia kumekuwa na maandamano ya kulaani jitihada zinazoendelea nchini Marekani kuutangaza unyama huo kuwa ni “genocide”.

Kimsingi,Marekani inategemea sana maelewano yake na Uturuki hasa kwa vile nchi hiyo inaweza kuvamia kaskazini mwa Iraki wakati wowote ule kuwadhibiti Wakurd ambao kwa Uturuki wanaonekana kama magaidi wa namna flani.Ni dhahiri kwamba kwa namna hali ya usalama nchini Iraki ilivyo legelege,uvamizi wa Uturuki kwa Wakurd utaleta mparaganyiko mkubwa zaidi ya uliopo sasa.Pia Uturuki inafuatilia kwa karibu sana mwenendo wa mambo huko Irak hasa inapojitokeza hoja ya kuwa sera ya majimbo (yaani Wakurd kaskazini,na waumini wa madhehebu ya Sunni na Shia katika maeneo yaliyosailia). Wapo wanaodhani suluhu ya kudumu nchini Irak itapatikana tu pale nchi hiyo itapogawanywa kwa misingi ya kidini/ukabila,pengine kwa vile jitihada za kuwaunganisha Wairak zinaelekea kuwa ngumu kuliko kuchanganya maji na mafuta.Hofu ya Uturuki ni kwamba iwapo Wakurd watapata “uhuru” wa namna hiyo basi kuna uwezekano wakajaribu kuvuruga amani nchini Uturuki.Hivi sasa nchi hiyo inasubiri idhini ya bunge la nchi hiyo kabla haijaanza “kuwashughulikia” inaowaita magaidi wa Kikurd kaskazini mwa Irak.Uhasama kati ya Waturuki na Wakurd ni wa muda mrefu sana,na kuelezea kwa undani kutahitaji makala nzima.Pamoja na vurugu zinazoendelea nchini Irak,eneo la kaskazini mwa nchi hiyo linalokaliwa na Wakurd limetulia kwa kiasi kikubwa,na iwapo Uturuki itavamia eneo hilo basi ni dhahiri kwamba jiographia nzima ya vita ya Irak itabadilika.

Hebu tuangalie mambo huko nyumbani kwenye anga za soka,hususan ubabaishaji usioisha wa wakongwe wetu wa soka Simba na Yanga.Hivi ni lini vilabu hivi vitatambua kwamba ni rahisi zaidi kupata damu kutoka kwenye jiwe kuliko kupata kocha mahiri wa kigeni kuingia mkataba wa muda mrefu na vilabu hivyo?Nionavyo mie,suala la makocha wa kigeni limekuwa ni la ushabiki zaidi kuliko mantiki.Utasikia moja ya vilabu hivyo ikidai kuwa na orodha ya makocha kadhaa wa kimataifa ambao wameonyesha nia ya kuja kufundisha.Well,sisemi kwamba hilo haliwezekani lakini cha msingi hapa sio kuwa na makocha kadhaa “wachovu” bali wataaluma wa soka ambao wataleta mapinduzi ya kweli kwenye vilabu hivyo.Hivi kuna mtu mwenye busara yake ambaye yuko tayari kuacha shughuli zake huko aliko na kwenda kubahatisha maisha nchi nyingine kwenye timu ambazo uhai wa uongozi ulio madarakani ni wa kusuasua kuliko wa joto la mgonjwa wenye homa ya vipindi.

Na japo nafahamu kuwa sio dhambi kutafuta makocha ya nje ya nchi,swali la msingi wanalopaswa kuulizwa Simba na Yanga ni hili:kama mara kadhaa wanashindwa kumudu gharama za makocha wa ndani ambao wanalipwa kwa sarafu ya Tanzania,watawezaje kumudu mshahara unaopaswa kulipwa kwa dola ya Kimarekani.Kocha yeyote mzuri hawezi kuvumilia ubabaishaji unaopelekea kocha huyo aonekane hafai.Ni kama Jose Maurinho alivyoamua kuachana na klabu ya Chelsea baada ya kutofautiana na bilionea mmiliki wa timu hiyo Abrahmovic.Ili timu ifanye vizuri inahitaji uongozi imara,uongozi ambao utamudu kutekeleza matakwa ya kocha ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kwamba programu yake ya maendeleo ya timu inafuatwa vizuri,uongozi ambao hautakuwa “ukimsomesha” kila kukicha kocha kuhusu stahili zake.Kigumu zaidi kwa wakongwe hawa wa soka kumudu kuleta makocha wa kigeni ni huo utegemezi wao kwa wafadhili.

Kuna wakati huwa najiuliza iwapo baadhi ya viongozi wa vilabu hawa wanafahamu kuwa timu zao ziko Tanzania,na sio katika nchi ya Magharibi ambako kuna siku mabilionea huwa “wanawashwa” na utajiri wao na kuamua kumwaga fedha kana kwamba wamepagawa.Lakini hata mabilionea hao huwa hawapati “kichaa” hicho kwa mwaka mzima,na kwa maana hiyo wanakuwa makini sana na fedha wanazotoa kama msaada.Sasa nani anatarajia tajiri mmoja awe anamwaga fedha zake kwa klabu ambayo si ajabu wakati mwenendo wake kwenye ligi unasuasua huku wachezaji wakilalama njaa (japo mfadhili anatoa fedha za mishahara),viongozi wanazidi kunawiri.Kwenye somo la sosholojia kuna “kanuni ya kupeana” (exchange theory) ambapo inaaminika kwamba kila anayetoa kitu anategemea kupata kitu flani.Mfano mwepesi ni pale unapotoa senti zako kwa ombaomba barabarani.Iwapo atanyoosha mikono juu kukuombea dua kwa ulichompatia basi kuna uwezekano kesho yake utampatia tena msaada kwa vile siku iliyopita alikurudishia fadhila kwa njia ya “dua” (kuonyesha shukrani zake).Kadhalika,mfadhili anapojitokeza kudhamini timu anatarajia kupata kitu flani,kama sio faida kwa kuitangaza kampuni au bidhaa zake basi angalau matokeo ya timu husika yawe ya kuridhisha (hapo anachorudishiwa ni liwazo la moyo,au tuite “kutarazika” kwa Kiswahili cha pwani).Hata kama atajitokeza tajiri ambaye anageuza mchanga kuwa fedha ni dhahiri atachemsha tu akijiingiza kwenye udhamini wa vilabu hivi kwani mara nyingi harufu ya fedha kwa waungwana hawa ni kama nuksi inayosababishwa na bahati ya utajiri wa raslimali katika baadhi ya nchi za dunia ya tatu.

Zamani nikuwa nafuatilia ratiba ya ligi kujua lini itakuwa siku ya siku ya mtanange kati ya watani wa jadi.Siku hizi sina muda mbovu namna hiyo kwani raha ya enzi hizo ilikuwa kushinda mechi zote,na droo ilikuwa ni sawa na kupoteza mechi.Sasa hata Simba wakiifunga Yanga ilhali wameshatandikwa na Coastal Union na Prisons,na pengine kuishia kuukosa ubingwa,huo ushindi dhidi ya watani wao unakuwa na maana gani.Niite “Sultani njozi” lakini kwangu umuhimu pekee wa mechi ya watani hao wa jadi ni kwamba yeyote atakayefungwa atakuwa amefungulia kifuniko kinachozuia (kwa muda) migogoro ambayo kwa muda mrefu sasa imekuwa inanyemelea klabu zote mbili.Mie sio muumini wa kulaumu pasipo kutoa ushauri lakini pia yayumkinika kusema kwamba kuzishauri Simba na Yanga zifanye mambo yake katika namna inavyopaswa kuwa ni sawa na kujaribu kumtafuta paka mweusi kwenye chumba chenye giza ilhali paka huyo hayupo kabisa chumbani humo.Ni kupoteza muda.

Alamsiki
$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$$

KULIKONI UGHAIBUNI-81

Asalam aleykum,

Kwanza inabidi niwatake radhi wasomaji wapendwa wa safu hii baada ya kupotea kwangu wiki mbili zilizopita.Haikuwa nia yangu kutojumuika nanyi katika safu hii bali ni kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wangu.Napenda kuwahakikishia kuwa nitakuwa nanyi kama hapo awali.

Miongoni mwa matukio ya muhimu yanayojiri hapa Uingereza kwa sasa ni pamoja na kesi inayoendelea dhidi ya polisi kuhusiana na kifo cha raia wa Brazil (aliyekuwa na makazi jijini London) Jean Charles de Menezes,aliyeuawa kwa kupigwa risasi na polisi waliomfananisha na gaidi waliyekuwa wakimwinda.Tukio hilo lilitokea mwaka juzi siku chache baada ya mashambulizi ya kigaidi kwenye mfumo wa usafiri wa jiji la London ambapo vijana watatu walijilipua mabomu ya kujitoa mhanga kwenye treni za chini ya ardhi na mmoja alijilipua kwenye “daladala”,mashambulizi yaliyochukua uhai wa zaidi ya watu 50 huku wengine kadhaa wakiachwa na majeraha ikiwa ni pamoja na ulemavu wa kudumu.M-Brazil huyo alikumbana na mauti yake katika namna ya kusikitisha.Polisi walikuwa wakimwinda gaidi flani aliyekuwa akaishi kwenye ghorofa moja na alilokuwa akaishi de Menezes,na kwa mujibu wa maelezo yaliyopatikana baadaye,polisi hao walishasisitizwa kwamba gaidi huyo “adhibitiwe kwa gharama yoyote ile”.Kwa bahati mbaya au pengine kwa uzembe (mahakama ndio itaamua) de Menezes alipotoka kwenye makazi yake,alidhaniwa kuwa ndie huyo gaidi aliyekuwa akiwindwa,na polisi walimfuatilia hadi alipoingia kwenye treni kabla ya kumdhibiti na hatimaye kummwagia risasi kadhaa zilizochukua uhai wake hapohapo.Haikuchukua muda mrefu kubainika kuwa aliyeuawa alikuwa raia asiye na hatia,lakini hiyo sio kabla ya baadhi ya magazeti kuibuka na stori kuwa “big boss” wa mashambulizi ya kigaidi ameuawa,wakidhania kuwa M-Brazil huyo alikuwa ndiye hasa anayesakwa na polisi.

Kwa kawaida ya hapa,pindi polisi wakiua,kamisheni huru inayofuatilia utendaji wa polisi (IPCC) hujitosa mara moja kuendesha uchunguzi wake.Na hivyo ndivyo ilivyokuwa baada ya kifo cha M-Brazil huyo.Matokeo ya uchunguzi wa IPCC yalionyesha kuwa polisi walikuwa na makosa yaliyosababishwa na mkanganyiko baina ya viongozi wa mkakati wa kumnasa gaidi aliyekuwa akiwindwa,askari waliokuwa wakimfuatilia gaidi huyo na askari wa kitengo cha SO19 ambacho ni wataalamu wa silaha.Hata hivyo,IPCC haikupendekeza hatua zozote za kisheria dhidi ya wahusika kwa madai kwamba lengo la operesheni hiyo lilikuwa ni kwa ajili ya maslahi ya usalama wa umma lakini uzembe uliojitokeza ulipekea kifo cha mtu asiye na hatia.Badala yake,suala hilo lilielekezwa kuwa kinyume na sheria ya Afya na Usalama (health and safety act),ambapo kimsingi ilipunguza uzito wa kosa zima.Kwahiyo,hivi sasa kesi hiyo inaendelea kuunguruma huku mashahidi mbalimbali wakielezea namna de Menezes alivyokutana na mauti yake.Pamoja na kukiri makosa yao,polisi wameendelea na msimamo kuwa nia yao ilikuwa nzuri,yaani kumdhibiti gadi waliyekuwa wakimfuatilia,na mkanganyiko wa kumfananisha de Menezes na gaidi huyo inaweza kuwa matokeo ya presha iliyokuwa ikivikabili vyombo vya usalama katika kipindi hicho cha mashambulizi ya ugaidi jijini London.

Kimsingi,utendaji kazi wa polisi (na vyombo vingine vya usalama) hapa Uingereza ni kama mtihani wa namna flani.Kwa upande mmoja wanategemewa kuhakikisha raia wako salama muda wote,lakini kwa upande mwingine wanatakiwa wasiminye haki za raia kwa kisingizio cha kuwalinda raia hao.Na hapo ndipo siasa za ndani za Uingereza zinapokinzana sana na za Marekani.Baada ya mashambulizi ya kigaidi ya Septemba 11,2001,usalama wa raia nchini Marekani ulichukua umuhimu wa juu zaidi kuliko haki za kiraia,tofauti na hapa ambapo watengeneza sheria wameendelea kusisitiza kwamba kusalimisha uhuru wa raia (civil liberty) katika jina la kuilinda jamii dhidi ya magaidi ni sawa na kuwazawadia magaidi hao ushindi wa mezani.

Mamlaka husika zinajitahidi kuwaandaa polisi wafanye kazi kwa ufanisi lakini bila kunyanyasa raia.Japokuwa polisi wamekuwa wakilaumiwa sana kwa ubaguzi (yaani namna wanavyodili na raia weupe na wale wasio weupe) ukweli unabaki kwamba mamlaka husika zinajitahidi ipasavyo katika kutekeleza wajibu wake.Lakini hata baada ya kutekeleza wajibu huo kwa kuweka wazi taratibu zinazotakiwa kufuatwa na polisi,kuwapo kwa taasisi huru kama IPCC kunasaidia kuwafanya polisi wawajibike ipasavyo zaidi.Yayumkinika kusema kwamba askari polisi hapa hufikiria kwa makini sana kabla hajafikia uamuzi wa kutumia nguvu ya ziada au silaha aliyonayo.

Nimeona habari moja ya kusikitisha kwenye gazeti flani la huko nyumbani ambapo inadaiwa kwamba mkazi mmoja wa Wilaya ya Kilombero aliuawa kutokana na mateso aliyopewa na polisi.Kwa mujibu wa habari hiyo,marehemu alikutana na mauti yake baada ya kifikishwa “Kalvari” ya polisi hao (Kalvari ni mahala aliposulubiwa Yesu Kristo).Hili limekuja miezi michache baada ya kifo cha mfugaji mmoja wilayani humo ambaye kifo chake kilizua maswali kutokana na tofauti za maelezo kati ya polisi wilayani Kilombero (yaliyoungwa mkono na daktari mmoja wa hospitali ya Mtakatifu Francis ya Ifakara) na matokeo ya uchunguzi wa maiti katika hospitali ya taifa ya Muhimbili.Binafsi sijasikia matokeo ya uchunguzi wa kifo cha mfugaji,lakini naamini sheria itachukua mkondo wake.Siongelei matukio ya wilayani Kilombero kwa vile ni maeneo ya nyumbani,bali nashawishika kutoa changamoto kwa polisi wetu kutambua uhumimu wa usawa katika utekelezaji wa majukumu yao na haki za kiraia walizonazo wananchi wa kawaida.

Nadhani wapo watakubaliana nami kwamba kumekuwa na malalamiko ya mara kwa mara kuhusu utendaji wa polisi wetu hususan linapokuja suala la kuthamini haki za raia.Utakuta askari trafiki anasimamisha daladala pengine kwa nia nzuri tu lakini pasipo kujali kuwa kuna abiria wanaowahi shughuli zao mbalimbali.Katika mazingira kama hayo,namna pekee ya kuonyesha kujali haki za abiria hao ni kumpatia dereva maelekezo mafupi (kwa mfano kujisalimisha mwenyewe kituo cha polisi baada ya kukamilisha ruti yake) au kuwasihi abiria watafute usafiri mwingine badala ya kuwagandisha muda mrefu katika mazingira yanayoweza kuzusha hisia kwamba trafiki “anadai kitu kidogo”.Kuna wakati flani nilijikuta nikiwa “mwenyeji” kwenye kituo flani cha polisi wilayani Kinondoni baada ya kuingizwa mjini na vibaka walionikwapulia kiselula changu.Ziara zangu za mara kwa mara kituoni hapo zilinipa picha ambayo sio ya kupendeza sana.Ifahamike kuwa sio kila anayekamatwa na polisi ana makosa,huyo ni mtuhumiwa,na ni mahakama pekee yenye mamlaka ya kuthibitisha (au kukanusha) tuhuma dhidi ya mtuhumiwa.Yayumkinika kusema kuwa baadhi ya polisi wanajiona kama wako juu ya sheria na maneno “haki za binadamu” au “uhuru wa raia” ni mithili ya misamiati mipya vichwani mwao.Ifahamike kuwa silizungumzii jeshi zima la polisi bali baadhi ya watendaji wa jeshi hilo ambao licha ya kuchafua jina la taasisi hiyo muhimu,wanaikwamisha pia katika utendaji kazi wake hasa katika maeneo ya “uswahilini” ,wilayani na vijijini ambako baadhi ya polisi hugeuka Miungu-watu.Na watu wanawaogopa kweli hasa kwa vile wanafahamu kuwa wanaweza kumzulia mtu kesi na kama hana uwezo wa kupata wakili mzuri basi ataozea jela.

Nafahamu kuwa kuna kitu kinachoitwa tume ya haki za binadamu na utawala bora (sina uhakika sana na jina hilo,pengine kwa vile taasisi hiyo haisikiki sana) lakini yayumkinika kusema kwamba kuwa na taasisi pekee haimaanishi kwamba mambo yatakwenda vema bali kuwa na taasisi ambazo zinaonekana zinatekeleza majukumu yake ipasavyo.Iwapo polisi huwa wanasihi wananchi mara kwa mara kuepuka kujichukulia sheria mikononi (mob justice) je wananchi wajifunze nini pindi mtuhumiwa anapofia mikononi mwa polisi (“police justice”?!!!).Huku nikiamini kuwa tukio hilo la mauaji ya “Kalvari” wilayani Kilombero litafanyiwa kazi,nimefarijika kusikia agizo la serikali kupiga marufuku kuwaweka watuhumiwa kituo cha polisi zaidi ya masaa 24 (japo hayo masaa 24 ni mithili ya karne nzima kutokana na mazingira ya kutisha kwenye selo hizo).

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Hot Sonakshi Sinha, Car Price in India