Featured Posts

Sunday, April 06, 2008

PICHA ZAIDI KUTOKA BONGO

Pata burudani ya picha zaidi kutoka Bongo
Lounge ya hoteli ya Kempinski

Kempinski kwa ndani,kwa hakika wanastahili pongezi kwa namna palivyoboreshwa.
Msikiti wa Kichangani Magomeni.Jirani na msikiti huuu,kuna makutano ya barabara za Morogoro na Kawawa.Eneo hilo ni maarufu sana kwa vibaka wababe wanaopora madereva.Ni zaidi ya kosa la jinai kusimamisha gari eneo hilo huku kioo kikiwa chini au nusu.
Makutano ya barabara za Morogoro na Bibi Titi.
Kasi ya majengo mapya ni kubwa katika maeneo mengi ya Dar.Hata hivyo,wananchi wengi wanalalamika kuwa hali ya maisha inazidi kuwa ngumu.
Sehemu hii inapendeza.Kwa muda nilijiskia kama niko Scotland vile.Hapa ni Kilimanjaro Hotel Kempinski.

Kempinski

Hakuna sheria muhimu ya uendeshaji gari mitaa ya Kariakoo zaidi ya ubabe.Ukifuata taratibu za usalama barabarani utaishia kugongwa,kuporwa au kulala hapohapo.
Mbinde za driving mitaa ya Kariakoo
Leo ni Jumapili na foleni katika barabara nyingi ni pungufu
I wish kila siku barabara zingekuwa nyeupe namna hii.
Msikiti wa Kichangani Magomeni
Millennium Towers.Eneo hili kuna internet cafe ambayo ni kimbilio la wengi wanaotegemea wireless connection.Pia ni mahala unapoweza kugongana na jamaa mbalimbali mliopoteana kutokana na kwenda nje kusaka hili au lile
Hii joint inaitwa "SAMAKI SAMAKI".The name tells it all...it's all about fish,fish and even more fish...Jana tulipewa ofa ya bure ya dagaa wa kukaanga.Yaani.... ndio mambo ya home sweet home hayo!However,dont let these nice pics fool you,mapambano ya maisha hapa yanataka ujasiri...na ukiwa jijini hapa inaweza kuwa rahisi kufahamu kwanini UFISADI unashamiri.The going seems to be getting tougher and tougher,forcing some folks to try to make the tough get going.
Barabara nyeupe
Barabara nyeupe pyee
Mitaa ya Kariakoo







Wakati unasubiri batch nyingine ya picha kutoka hapa,hebu pata burudani kutoka kwa Common featuring Dwelle katika track ya The People

Saturday, April 05, 2008

PICHA ZAIDI ZA BONGO

Zoezi la kuleta picha za Bongo linaendelea.I'm not trying to become a photoblogger of some sort,hiyo wanaiweza magwiji WA FANI kama rafiki yangu HAKI.Hapa chini kuna kiji-collection kidogo ca picha nilizodhani zinaweza kukupendeza wewe msomaji. Zote zimepigwa kwa kutumia Samsung Armani,na naamini quality ya picha inaridhisha.If not,let me know,plz!















Foleni za magari bado ni tatizo sugu kama Ufisadi.Hapa ni junction ya maeneo ya Namanga.Halafu jana kulikuwa na mvua si utani.Breaking news niliyopata jana mchana ni kuwa maji yalikuwa yanalazimisha kuingia ndani ya "mansion yetu" huko Ifakara (well,kwa level ya kijiji chetu,nyumba ikipigwa lipu nje,na vikorombwezo flani na geti la kizushi basi inapata hadhi ya kuitwa "mansion")

















Hapa ni HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI.Jana nayo ilikuwa imeelemewa na maji.Tatizo la Hospitali hii ni kwamba mazingira ya nje hayaridhishi,ya ndani ni ya kusikitisha na huduma ndani ni za kuvunja moyo. It's like a hospital from hell.



















Niliamua kuwanasa kwa picha hawa wageni waliokuwa wanafanya nini sijui hapo Mbuyuni,barabara ya Ali Hassan Mwinyi.Lilikuwa sio kundi kubwa as such lakini kama ujuavyo Bongo hakuna jambo dogo,muda si muda kukawa na lundo la watu wanawashangaa hao jamaa...I could swear I saw someone cancelling his trip to work just ku-join the party ya kushangaa... More pics hapo chini




















STAY TUNED FOR MORE PICS.

Wednesday, April 02, 2008

PICHA ZA BONGO

Dar kuna tatizo kubwa sana la foleni.Na kwa kasi magari yanayoingizwa kila siku jijini hapa,nadhani kimeo cha foleni kitaebndelea kwa muda mrefu sana.Na inavyoonekana,hakuna mipango ya kuboresha barabara ili ziweze kumudu wingi wa magari.Sijui quality ya picha hizi ikoje.Ni majaribio ya Samsung Armani kwenye poor light (mida ya saa 12).Location ni Millennium Towers.Will keep on bringing more pics for you guys.





Monday, March 31, 2008

SAMAHANI NYIIINGI

KWA MUDA SASA BLOGU HII IMEKUWA KIMYA.HIYO NI KUTOKANA NA SAFARI YA KUJA HAPA NYUMBANI BONGO.LIBENEKE LITAENDELEA PINDI MAMBO YAKISHATULIA.WILL DO MY BEST TO KEEP YOU GUYS POSTED ABOUT WHAT'S HAPPENING KIPANDE HII

Sunday, March 23, 2008

MTU-TEMBO (ELEPHANT MAN) HAJAKATA TAMAA YA KUPATA KIMWANA

Wakati tunasherehekea sikukuu ya Pasaka ni vema tukifanya tafakuri ya mambo ambayo machoni yanaweza kuonekana madogo lakini yenye uzito mkubwa katika hali halisi.Ni muhimu kumshukuru Mungu kwa mengi au machache aliyo/anayotujalia.Hivi kuna zawadi kubwa kutoka kwa Mungu zaidi ya UHAI?Sambamba na uhai ni uzima/ukamili wa miili yetu.Tuliozaliwa tukiwa kamili (yaani bila ulemavu) tunaweza kujisahau kuuliza maswali magumu kama "ingekuwa vipi kama ningezaliwa nina mkono nusu,au pua iliyozama ndani,au hata jicho lililokaa kisogoni" hadi pale tunapowaona wenzetu kama huyu mtu-tembo (elephant man-sio yule wa dancehall),ambaye stori yake inapatikana HAPA

Saturday, March 22, 2008

HERI NA BARAKA YA PASAKA

NAWATAKIENI NYOTE HERI NA BARAKA ZA SIKUKUU YA PASAKA.UFUFUKO WA BWANA YESU KRISTO ULETE AMANI,UPENDO,AFYA NJEMA NA MAFANIKIO KWA KILA MMOJA WETU.PAMOJA NA SALAMU HIZI NI SHUKRANI ZANGU ZA DHATI KWENU NYOTE MNAOTEMBELEA BLOGU HII NA KUSOMA MAKALA ZINAZOTOKA KATIKA BAADHI YA MAGAZETI YA NYUMBANI.BWANA AWABARIKI SANA,AMEEN.

FOXNEWS WAUMBUANA LIVE ON AIR

Jana nilishuhudia kituko cha mwaka.Mwanzoni nilidhani ni porojo tu lakini asubuhi hii nimeona tukio hilo limekuwa gumzo mtandaoni.Ilikuwa takriban saa 6 mchana za hapa (hapa saa zitabadilika mwishoni mwa mwezi huu),nikaamua kupoteza muda kwa kuangalia kipindi cha Fox&Friends.Nasema kupoteza muda kwa vile waendesha kipindi hicho huwa wananikera sana kutokana na kauli zao za upendeleo wa wazi kwa wahafidhina na upinzani wao mkubwa dhidi ya Democrats na liberals.Sikujutia uamuzi wa "kupoteza muda" kwani huku watangazaji Steve Doocy na Gretchen Carlson wakishikia bango kauli ya Obama kwamba grandmom wake ni like typical White person,mwenzao Brian Kilmeade aliamua kuondoka kwa muda studioni kutokana na kukerwa na namna wenzie walivyokuwa wakimsakama Obama.Kama hiyo haitoshi,muda mfupi baadaye,mtangazaji mwandamizi wa kituo hicho,Chris Wallace,alionekana hewani wakati Fox&Friends inaendelea ambapo alielezea waziwazi kwamba alikuwa akiangalia kipindi hicho na hakupendezwa na namna kauli ya Obama kuhusu bibi yake ilivyokuwa ikipotoshwa.Wallace alieleza wazi kwamba yeye si msemaji wa kambi ya Obama lakini angependa kuona kipindi hicho kinazungumzia suala hilo ndani ya context,na kwenda mbali zaidi kwa kuwashauri wana-Fox&Friends kuangalia pia habari nyingine za muhimu kuhusu Obama kama vile endorsement ya Bill Richardson na hotuba zake mbili kuhusu uchumi na vita ya Irak.




Wednesday, March 19, 2008

WATANZANIA WANAFURAHIA UFISADI? (MAKALA NDANI YA GAZETI LA RAIA MWEMA)

Makala yangu katika toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema inajaribu kudadisi chanzo cha ufisadi huko nyumbani.Je tatizo ni mfumo unaozaa na kulea ufisadi au tatizo ni watu wanaosabaisha ufisadi na kuishia kutengeneza mfumo haramu wa maovu?Lakini kabla ya kuingia kwenye mjadala huo,makala hiyo imeanza kwa discussion fupi kuhusu kipindi cha BET cha Hip-Hop vs America.Binafsi,nimetafsiri dhima ya kipindi hicho kuwa ni jamii ya Black Americans kujiuliza adui yao halisi ni nani: wao wenyewe au mfumo dhalimu uliotawaliwa na ubaguzi na nguvu za Corporate America.Basi,pamoja na habari na makala nyingine zilizokwenda shule,bingirika na makala hiyo kwa KUBONYEZA HAPA.

Tuesday, March 18, 2008

P.DIDDY AKANUSHA KUHUSIKA NA MAUAJI YA TUPAC

Gazeti la Los Angeles Times lina habari kwamba rapa tajiri na maarufu,Sean "P.Diddy" Combs alikuwa na taarifa za ndani kuhusu mpango wa mauaji ya Tupac Shakur aliyepigwa risasi na hatimaye kufariki Novemba mwaka 1994.
Kwa mujibu wa taarifa za kiuchunguzi za gazeti hilo,watu mbalimbali wamethibitisha tuhuma hizo ambazo zimekanushwa vikali na P.Diddy.Itakumbukwa kwamba kifo cha Tupac kinahusishwa pia na mauaji ya rapa mwingine maarufu Christopher Wallace a.k.a. Notorious B.IG. ambacho kinadhaniwa kuwa ni kisasi cha washirika wa Tupac.


                
              Uchunguzi huo wa L.A.Times unadai kwamba sababu kubwa iliyopelekea kuuawa kwa Tupac ni "adhabu" kwa nguli huyo wa rap kukataa kuwa mshirika wa kibiashara wa lebo ya Bad Boy inayomilikiwa na P.Diddy.

Kwa habari zaidi soma habari hiyo ya kusisimua kwa KUBONYEZA HAPA.Hapo chini ni clip ya B.I.G katika track Mo Money Mo Problems akimshirikisha Puff Daddy na Mase


Pia waweza kuangalia track hii hapo chini ya Tupac  f/t The Outlawz (Caution: Very Explicit Lyrics) Hit Em Up ambapo rapa huyo na vijana wake wanatupa "madongo" makali kwa P.Diddy (enzi hizo akijulikana kama Puff Daddy),B.I.G,Lil' Kim,Lil' Cease,Mobb Deep na lebo nzima ya Bad Boy.Ni dhahiri kuwa track hii ilichangia sana kukuza beef kati ya mahasimu hao wa Pwani ya Mashariki na ya Magharibi huko Marekani.


Monday, March 17, 2008

DOUBLE STANDARDS OR OPEN RACISM?

Hebu toa hukumu mwenyewe katika MAKALA HII

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Hot Sonakshi Sinha, Car Price in India