Featured Posts

Friday, April 22, 2011

Makala yangu ktk Raia Mwema Toleo la April 20: "CCM na joka lenye vichwa vitatu!"


Makala yangu katika toleo la wiki hii la jarida mahiri la Raia Mwema inazungumzia suala lililokamata hisia za Watanzania wengi kwa sasa la CCM kujivua magamba.Makala hiyo inachambua chanzo cha magamba hayo na namna inavyomwia vigumu Mwenyekiti wa CCM,Rais Kikwete kufanikisha azma yake ya kukisafisha chama hicho (if at all ana azma hiyo).

Jarida hilo pia limesheni makala nyingine moto moto,sambamba na habari za uhakika ikiwa ni pamoja na zile zinazohusu ufisadi mpya wa "Stimulus Package".Zaidi,BONYEZA HAPA KUSOMA MAKALA HIYO na HAPA kusoma jarida zima.

Ijumaa Kuu Njema.Tukumbuke Kwanini Yesu Aliteswa na Kufa Msalabani


Nina miaka kadhaa sijawahi kwenda kanisani.Sijisifu wala kujisikia vizuri.Kila mara ninapoongea na Baba huwa nalazimika kumdanganya kuwa siku hizi nakwenda kanisani.Ninatoka familia ya kidini hasa,na huenda leo hii ningekuwa padre kama nisingeamini kuwa sina wito.Hata hivyo,familia yetu imemtoa mmoja wetu kwa Bwana,na sasa yeye ni sista.
Mdogo wangu mpendwa,Sista Maria-Solana Chahali

Leo ni Ijumaa Kuu,siku ambayo Bwana wetu Yesu Kristo alikufa msalabani kwa ajili yetu.Nimesema sijatia mguu kanisani kwa miaka kdhaa lakini najitahidi kadri ninavyoweza kuishi kulingana na matakwa ya Bwana.Sio kwenda kanisani au kuimba mapambio kutakompatia mwanadamu uzima wa milele bali matendo.Japo ni muhimu kujumuika na waumimni wenzetu makanisani,la muhimu zaidi ni kuishi kwa mfano wa Bwana Yesu ambaye licha ya upendo wake usiomithilika alikuwa tayari kufa msalabani kwa dhambi zetu ili atuletee ukombozi.

Wakati tovuti hii inakutakia wewe msomaji mpenda Ijumaa Kuu njema,siku hii inaweza kuadhimishwa ipasavyo kwa kutafakari kuhusu upendo wa Bwana,kujitoa kwake kwa jili yetu na upeno kwa ujumla.Kama humpendi jirani yako unayemwona kila siku utakuwa mnafiki kudai unampenda Bwana mbaye hujawahi kumwona.Yesu ni upendo na amani.

Watu 100 Wenye Ushawishi Mkubwa Zaidi Duniani kwa mwaka 2011


Jarida la kimataifa la TIME la nchini Marekani limechapisha orodha yake ya kila mwka ya watu wenye ushawishi mkubwa zaidi duniani (the Time 100 Most Influential People in the World).

Kinarani katika orodha hiyo ni Wael Ghonim,mwanaharakati aliyahamasisha mageuzi ya kidemokrasia nchini Misri kwa kutumia vyombo vya habari vya jamii (social media) na hatimaye kupelekea kuanguka kwa utawala wa kidikteta wa aliyekuwa Rais wa nchi hiyo,Hosni Mubarak.


BONYEZA PICHA IFUATAYO kusoma orodha kamili


Tuesday, April 19, 2011

Jina la kijiji au mitishamba?: Llanfairpwllgwyngyllgogerychwyrndrobwllllantysiliogogogoch


Mara kwa mara nimekuwa ninasumbuliwa na watu wanaodhani jina langu la Evarist lina mahusiano na Mlima Everest.Hata hivyo,kwa upole kabisa,huwa ninawaelimisha kuwa jina hilo ni Kitatoliki na nimelirithi kutoka kwa Mtakatifu Evaristus,aliyekuwa Baba Mtakatifu (Pope) kati ya mwaka 99 hadi 108.

Lakini ukilinganisha jina langu na majina mengine,kwa mfano ya kijiji kimoja huko Wales,hapa Uningereza,basi mie sipaswi hata kunung'unika.Kijiji hicho kinaitwa Llanfairpwllgwyngyllgogerychwyrndrobwllllantysiliogogogoch.Kurahisisha ugumu na urefu wa jina hilo,kijiji hicho pia hujulikana kama Llanfairpwllgwyngyll, au spelled Llanfair Pwllgwyngyll.Kurahisisha zaidi,hujulikana kwa kifupi kama Llanfair PG or Llanfairpwll.

Unaweza kudhani hilo ndio jina refu zaidi duniani.Hapana.Kuna mengine kadhaa,kama ambavyo nimeorodhesha hapa:

Jina kamili:
Taumatawhakatangihangakoauauotamateaturipukakapikimaungahoronukupokaiwhenuakitanatahu (herufi 85)
Kifupisho: Taumatawhakatangihangakoauauotamateapokaiwhenuakitanatahu (herufi 57)
Mahali: North Island, New Zealand
Lugha: Māori
Sehemu hii inashilikia rekodi katika Guinness World Records kama jina la sehemu lililo refu zaidi kuliko yote.

Jina kamili: Llanfairpwllgwyngyllgogerychwyrndrobwllllantysiliogogogoch (herufi 58)
Kifupi: Llanfairpwllgwyngyll (herufi 20)
Mahali: Anglesey, Wales, Uingereza
Lugha: Ki-Welshi

Jina kamili: Chargoggagoggmanchauggagoggchaubunagungamaugg (herufi 45)
Kifupi: Ziwa Chaubunagungamaug (herufi 17)
Mahali: Ziwa huko Massachusetts,Marekani.
Language: Nipmuc

Jina kamili: Tweebuffelsmeteenskootmorsdoodgeskietfontein (herufi 44)
Mahali: Afrika Kusini
Lugha: Afrikaans

Jina kamili: Äteritsiputeritsipuolilautatsijänkä (herufi 35)
Mahali: Lapland, Finland

Jina kamili: Pekwachnamaykoskwaskwaypinwanik (herufi 31)
Mahali: ziwa huko Manitoba na Nunavut,Kanada
LUGHA: Inuktitut

Jina kamili: Venkatanarasimharajuvaripeta (herufi 28)
Mahali: kijiji huko Andhra Pradesh, India

Jina kamili: Mamungkukumpurangkuntjunya (herufi 26)
Mahali: Australia Kusini
Lugha: Pitjantjatjara

Jina kamili: Bullaunancheathrairaluinn (herufi 25)
Mahali: County Galway, Ireland

Jina kamili: Gasselterboerveenschemond (herufi 25)
Mahali: Drenthe, Uholanzi
Lugha: Kidachi

Jina kamili: Kuchistiniwamiskahikan (herufi 22)
Mahali: kisiwa huko Quebec, Canada

Jina kamili: Parangaricutirimicuaro (herufi 22)
Mahali: mji huko Michoacán, Mexico
Lugha: P'urhepecha

Jina kamili: Drehideenglashanatooha (herufi 22 letters)
Mahali: daraja huko County Tipperary, Ireland

Jina kamili: Siemieniakowszczyzna (herufi 20)
Mahali:kijiji huko Hajnówka County, Poland
Lugha: Kipolishi

Jina kamili: Newtownmountkennedy (herufi 19)
Mahali: kijiji huko County Wicklow, Ireland
Lugha: Kiingereza

Jina kamili: Thiruvananthapuram (herufi 18)
Mahali: mji huko Kerala, India
Lugha: Malayalam

Jina kamili: Torreblascopedro (herufi 16)
Mahali: Kijiji huko Andalucía,Hispania.

Jina kamili: Hostotipaquillo (herufi 15)
Mahali: mji huko Jalisco, Mexico
Lugha: Nahuatl

VYANZO: Wikipedia

Monday, April 18, 2011

Ten Places it's (almost) Impossible to Visit


1. Poveglia
Where is it? The Venetian lagoon, Italy
Why can’t I visit?: Because it’s haunted! According to legend it was used to isolate plague victims during Roman times, and then as a giant Black Death grave in the Middle Ages. As if that wasn’t scary enough, it’s also home to spooky abandoned building – complete with bell tower naturally – that was apparently a mental hospital. These days it’s off-limits to visitors unless you bribe a gondolier to take you there.

2. Area 51
Where is it? Nevada, USA
Why can’t I visit?: It’s a top secret military testing base, protected by armed private security teams patrolling in jeeps who are authorised to use deadly force to deal with intruders. Whether or not you believe UFOs have crashed landed there, the ridiculously strict security around the base means you’re never going to find out for sure.

3. Le Cercle Munster
Where is it? Luxembourg
Why can’t I visit?: It’s an exclusive private members club that’s extremely selective about adding new members. Want to join? You must be backed by two sponsors and be approved by a selection committee made up of bigwigs from the finance world. Unless you’re an incredibly rich banker, businessman or equity trader, you’ll never see the sumptuous insides of the club, take part in the ‘Programme culturel’ or eat the delicious food at the in-house restaurant. Damn!

4. Church of Our Lady Mary of Zion
Where is it? Axum, Ethiopia
Why can’t I visit?: Because it’s no ordinary church. According to legend it's home to one of the most important biblical artefacts ever – the Ark of the Covenant (and we thought Indiana Jones left it in a warehouse). Only a specially chosen monk is allowed to guard the ‘Ark’. No-one else is allowed to lay eyes on it or even get close, in case they melt presumably (see Indiana Jones again). Of course, some claim this secrecy means the Ethiopian church is telling porkies…

5. Most of Niihau Island
Where is it? The Hawaiian Islands, USA
Why can’t I visit?: Super-rich family the Robinsons (they’re not Swiss) bought Niihau in 1915 and closed it off to preserve its indigenous culture and wildlife. The 200-or-so natives who live there lead a blissful existence free of electricity, burger joints and, for the most part, tourists. There are very rare helicopter tours to the isle where you can wander along one of the beaches, but getting anywhere near the locals is strictly forbidden; hence its nickname, the, er, ‘Forbidden Island’.

6. Bohemian Grove
Where is it? California, USA
Why can’t I visit?: It’s an extremely secretive men-only club whose members include artists, musicians, businessmen politicians… and the odd president (Nixon was a member). Once a year they all gather for a two-week long festival where (allegedly) rituals such as the ‘Cremation of Care’ - a wicker-man-style faux-pagan rite - and the ‘Grove Play’ - a large-scale musical theatre production - are performed by members. It sounds like fun to us, but somehow I don’t think we’ll get an invite…

7. Lechiguilla Cave
Where is it? New Mexico, USA
Why can’t I visit?: It’s perhaps the most beautiful cave on the planet and frankly, the authorities don’t want you ruining it. Discovered in 1986 by miners, the sprawling underground complex is home to stunning speleothems, gypsum chandeliers and hydromagnesite balloons. We don’t know what any of these are, but they sound impressive. Sadly, unless you’re an extremely experienced caver you’ll never get a permit to see them.

8. Jiangsu National Security Education museum
Where is it? Nanjing, China
Why can’t I visit?: Anyone is allowed in… as long as they are Chinese. There’s a big sign outside the front of this very unusual museum stating that only Chinese citizens are allowed inside. The unusual entry requirements are because the museum documents the history of Chinese espionage, and the state doesn’t want us foreigners finding out their spying secrets.

9. Ilha de Queimada Grande
Where is it? Off the shore of Brazil
Why can’t I visit?: Basically, because it’s full of snakes – hence the nickname: ‘Snake Island’. Local legend states there’s between one and five snakes per square metre on the island. And not just any old snakes, most of ‘em are golden lanceheads – noted for their extremely potent venom. Because of this, understandably, the Brazilian Navy forbids tourists from stepping foot on the island.

10. The peak of Mount Kailash
Where is it? The Himalayas, Tibet
Why can’t I visit?: Because it's home to a Hindu god. Lord Shiva, to be precise, who resides at the summit in a state of perpetual meditation. Sounds like bliss to us, which is appropriate, as Buddhists also believe the peak is home to the Buddha Demchok, who represents supreme bliss. Because of this religious significance the peak was always considered off-limits by most climbers, before this Chinese government issued an official ban in 2001

SOURCE: Yahoo!Travel UK

Mkutano wa Wawekezaji: Wawekeze Wapi,Kwa Faida ya Nani,Watuchome Moto Zaidi?


Mkutano mwingine wa wawekezaji umeanza leo jijini Dar es Salaam.Mkutano huo ni mwendelezo wa mikutano mingine inayopigiwa debe kwa nguvu kuhusiana na umuhimu wa wawekezaji kwa uchumi wetu.

Naamini wengi wet bado tunakumbuka vuguvugu la Mkutano wa Sullivan.Baadaye ukafuatiwa na mkutano mkubwa wa mambo ya uchumi (economic forum).So far,hayo yamebaki kuwa matukio tu ambayo kwa upande mmoja yamewaachia baadhi ya wajanja utajiri wa kutosha baada ya kupewa tenda za chakula,malazi,vifaa,nk huku Watanzania wakiendelea kubaki masikini (na hapo tukiweka kando adha ya usafiri kutokana na barabara kufungwa kwa ajili ya misafara ya waheshimiwa).

Wakati viongozi wetu wakituhadaa na mikutano ya kila mwaka ya wawekezaji,kuna umuhimu wa kufanya uchambuzi wa kina kuhusu suala zima la uwekezaji.Kama uwekezaji mkubwa uliopo hadi sasa hauna manufaa kwa Mtanzania wa kawaida,ni miujiza gani itapelekea wawekezaji wapya walete mabadiliko?

Suala moja la msingi linalopuuzwa na watawala wetu ni ukweli kwamba wawekezaji sio taasisi za hiari za kutuletea maendeleo yetu.Hawa ni wafanyabiashara ambao miaka michache tu iliyopita tuliwaita kila aina ya majina-from watangulizi wa ukoloni to mabeberu.Of course dunian imebadilika,lakini mabadiliko hayo sio yawe at expense of wazawa au wenye nchi.

Tunaingia gharama kubwa kuvutia watu wa aina ya Richmond,Dowans,wezi wa madini huko migodini,na wababaishaji wengine.Wengi wa wanaoitwa wawekezaji wanakuja na briefcase tupu zikiwa na mikataba tupu lakini ikishasainiwa,na baada ya miaka michache wanaondoka wakiwa na mamilioni kwenye akaunti zao-huku wakiacha,kwa upande mmoja, mafisadi wameongeza idadi ya nyumba ndogo zao,mahekalu yao na magari yao ya kifisadi,na upande mwingine walalahoi wakikodolea ardhi yao iliyoachwa mashimo matupu baada ya raslimali yote kuibiwa.

Tunakaribishaje wawekzaji kabla ya kutengeneza sera na sheria mwafaka za kutuwezesha kunufaika na ujio wa wawekezaji hao?Na uwekezaji wa aina ya "kupangisha nyumba kisha mwenye nyumba kulala mtaani" ni uhayawani usiopaswa kuendelea.

Tunafahamishwa wizi unaofanywa na baadhi ya makampuni ya simu ambayo kila baada ya muda flani yanabadili majina ilhali huduma zao mbovu zikiendelea kuwa zile zile za kuchefua.

Tunakaribisha wawekezaji wakati baadhi ya hao waliopo wanapata hadi jeuri ya kuchoma moto wazawa (rejea tukio la Kigamboni)lakini vyombo vya dola vinachelea kuchukua hatua zinazostahili.

Viongozi wetu wanapaswa kuwa makini na kurejea yaliyotokea nchini Afrika Kusini hivi karibuni ambapo wazawa waliamua kuelekeza hasira zao kwa wageni wakiamini kuwa ndio chanzo cha matatizo yao ya kila siku japo ukweli ni kwamba chanzo cha tatizo ni uongozi mbovu wa watawala wa nchi hiyo.

Tumeshuhudia jana baadhi ya wakazi wa Kigamboni wakiamua kupambana na wawekezaji japo kama ilivyo kawaida waliishia kudhibitiwa na polis,na huenda wakafunguliwa mashtaka huku mwekezaji aliyeua akiachwa "anakula kuku kwa mrija".

Nikirejea tukio hilo la Kigamboni,nilifadhaika kusoma tweet ya Mbunge wa jimbo hilo akieleza bila aibu kuwa "maandamano yamekuwa SUPPRESSED na CULPRITS watachukuliwa hatua za kisheria".Huyu ni mwakilishi wa watu haohao waliompoteza mwenzao kwa kuchomwa moto na mwekezaji!

Anyway,ujio wa wawekezaji ni habari njema kwa mafisadi kwani unapanua fursa za kupata teni pasenti na vijizawadi vya likizo huko ughaibuni,huku the so called wawekezaji wakigeuza nchi yetu kuwa shamba la bibi.

Sunday, April 17, 2011

Maswali Magumu ya Ansbert Ngurumo: "Chomoa, chomeka itainusuru CCM?"



Chomoa, chomeka itainusuru CCM?

Ansbert Ngurumo

SAKATA la CCM kujivua gamba limezaa maswali mengi ambayo hayajajibiwa. Na limetusaidia kujua zaidi upeo wa watawala wetu, na uwezo wa kukabiliana na misukosuko ya ndani na nje ya chama tawala.

Na kwa kuwa wanapima upeo wa Watanzania kwa mizani ya upeo wao wenyewe, watawala wetu wamediriki kujitapa kwamba CCM imezaliwa upya. Wengine wanasema CCM imefufuka. Wamekosea!

Ni fursa kwa CCM ya Kikwete kujiuliza au kuulizwa. Kama CCM ya Julius Nyerere, Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa ilionekana imara, ni nani ameidhoofika CCM ya Kikwete?

Mtu mmoja alinieleza miezi mitatu iliyopita, kwamba Rais Jakaya Kikwete alisikika akimweleza rafiki yake mmoja wa Iringa kwamba anavyoona chama kimeanza kumfia mikononi, na hilo ni jambo analoogopa sana. Je, mabadiliko haya ya kuchomoa na kuchomeka sura ndiyo yanaweza kuinusuru CCM inayokufa?

Tumesikia wanajitapa kwamba wameondoa mafisadi kwenye Kamati Kuu, na sasa wanataka waliobaki kwenye Halmashauri Kuu na vyombo vingine vya chama wajiondoe wenyewe, la sivyo watafukuzwa! Jambo jema.

Lakini CCM wameanza lini kukiri kwamba chama chao ni cha mafisadi au kina mafisadi? Si hawa hawa ndio walibeza na kulaani kauli ya wapinzani, iliyotolewa na Dk. Willibrod Slaa Septemba 2007, Mwembeyanga, Dar es Salaam, alipotaja orodha ya mafisadi na kufafanua ufisadi wa kila mmoja wao?

Si ndio hawa waliotishia, na baadaye wakaogopa kumshitaki Dk. Slaa, lakini wakaendelea kuwatumia mawaziri na makada wengine kuzunguka mikoani kushambulia wapinzani kwa kile walichoita ‘uzushi?’

Hoja ya ufisadi si ndiyo ilimfanya Rais Kikwete awabeze na kuwakejeli wapinzani akidai kelele za mlango hazitamzuia mwenye nyumba (yeye) kulala?

CCM hii si ndiyo iliwatuma Yusuph Makamba, Kingunge Ngombale-Mwiru, Jaji Joseph Warioba, Sofia Simba na makada wengine kubeza na kudhihaki wapinzani na vyombo vya habari, wakidai wanaendekeza habari za ufisadi badala ya masuala ya maendeleo?

Kama Rais Kikwete na wenzake wanasema kuwa umefika wakati chama kiondokane na mafisadi, basi wamethibitisha kwamba Dk. Slaa na wenzake walikuwa sahihi. Sasa tuwaamini CCM au akina Dk. Slaa?

Pili, dhana hii ya kujivua gamba bado ni tata hata kwa wenyewe wanaoipigia debe. Mwenyekiti mwenyewe aliyeianzisha alidhani CCM ina gamba moja tu inalopaswa kujivua; na akadhani inatosha tu kuvua gamba. Inasikitisha kwamba yeye anaishia hapo, lakini hata sisi tusio wana CCM tunajua kuwa CCM haikuhitaji kuvua gamba, bali kuwa na moyo mpya.

Lakini wale waliopenda kuendelea kuchambua hoja ya gamba wameshaorodhesha magamba ya CCM. Na wengine wamesisitiza kwamba Rais Kikwete, kwa staili yake ya uongozi, na baada ya kutathimni alikokitoa na alikokifikisha chama, naye ni gamba.

Kwa bahati mbaya, inavyoonekana, hata watawala wenyewe bado hawajajua idadi, na aina ya magamba wanayopaswa kukivua chama chao. Vile vile, hawajajua kwamba hata kama wangefanikiwa kuyatambua na kuyavua mgamba hayo, bado chama chao hakitaweza kuwa kipya.

Tatu, na hili ndilo la msingi kwangu, hivi watawala wanadhani kwamba nyoka anapojivua gamba anabadilika na kuwa mjusi au kinyonga?

Tunaona, na tunasema wazi kwamba CCM ya Kikwete, yenye gamba na isiyo na gamba, ni ile ile. Wanachofanya sasa ni kujaribu (na kufanikiwa kwa sehemu kubwa) kuwafukuza ’wabaya wao’ wa sasa na kuingiza marafiki wapya. Na bahati mbaya, ni sura zile zile tulizozizoea, tunazozifahamu, na ambazo tunapata shida kuzitenganisha na ufisadi uliowakumba kina Yusuph Makamba, Rostam Aziz, Andrew Chenge na wenzao.

Kikubwa zaidi ni mamlaka ya kimaadili yanayotumika kuwafukuza wengine na kuingiza wengine. Maana kama tunaendelea kukuza na kusisitiza hoja ya Mwembeyanga, waliotajwa kwenye orodha ya mafisadi ni hawa hapa:

1. Daudi Balali
2. Andrew Chenge
3. Basil Mramba
4. Gray Mgonja
5. Patrick Rutabanzibwa
6. Nazir Karamagi
7. Nimrod Mkono
8. Rostam Aziz
9. Edward Lowassa
10. Benjamin Mkapa
11. Jakaya Kikwete

Chama kinachojivua gamba, kwa mfano, kitajitapaje kwamba kimeondokana na mafisadi, wakati hata mwenyekiti mwenyewe yumo kwenye orodha?

Si hilo tu. Kwa misingi ya kikatiba, kihistoria na kitamadumi, CCM inaongozwa na mwenyekiti. Na hii ndiyo asili ya kaulimbiu ya siku nyingi ya CCM ya ‘zidumu fikra za mwenyekiti.’

Kwa mantiki hiyo, chama kinapofanikiwa au kinapokwama, mtu wa kwanza ambaye wana CCM wanapaswa kumhoji si katibu mkuu (maana utendaji wake unasimamiwa), bali mwenyekiti.

Sekretariti na Kamati Kuu ni zao la mwenyekiti. Ni mikono ya kazi anayotumia kuendesha chama. Ni kweli, Yusuph Makamba, kwa elimu na upeo wake, alibebeshwa mzigo mzito. Lakini ndiye huyo ambaye mwenyekiti aliridhika naye kwa miaka mitano.

Kwa hiyo, mwenyekiti ndiye aliyepaswa kubeba udhaifu wa katibu na chama kwa ujumla. Maana wana CCM walipohoji na kubeza uteuzi wa Makamba mwaka 2006 kurithi nafasi ya Philip Mangula, mwenyekiti hakujali.

Hata ilipopatikana fursa ya kubadilisha uongozi wa chama hapa katikati, Rais Kikwete aliridhika na utendaji wa Makamba. Huyu huyu hawezi kuibuka leo na kusema Makamba na sekretarieti yake hawajamsaidia kazi.

Nionavyo mimi, yaliyomkuta Makamba na Sekretarieti na Kamati Kuu yake ni sawa na yaliyomkumba Lowassa na Baraza la Mawaziri lililokuwa chini yake mwaka 2008.

Uamuzi wa kuondokana na Lowassa ilikuwa njia pekee ya kumnusuru Kikwete na anguko la kisiasa akiwa madarakani, kwa maana kashfa yenyewe iliyomsomba Lowassa iliwahusu wote.

Na hili la Makamba limeharakishwa na vuguvugu la mapinduzi ya ndani, baada ya mwenyekiti kuletewa taarifa kwamba kuna watu wananadi uenyekiti wake kwa maelezo kuwa ameshindwa kuongoza vema chama. Walitaka (na bado wanataka) abaki na urais, aachie uenyekiti.

Wanajua kuwa kwa utamaduni wao, mwenyekiti ndiye kiongozi wa chama. Anakotaka chama kiende, ndiko kinakokwenda. Na wandhani kuwa wakipata mwenyekiti mzuri watakuwa na chama kizuri.

Katika mazingira haya, njia pekee ya mwenyekiti kujinusuru ilikuwa kuwashughulikia walio chini yake ili ajipange upya, abadili hoja, na apate pa kuning’iniza propaganda za CCM mpya.

Na kwa maana hiyo, kujiuzulu kwa wajumbe wa Kamati Kuu na Sekretarieti (kwa shinikizo la mwenyekiti) ilikuwa faraja kwake binafsi si kwa CCM. Na ndiyo maana sisi wengine tunakataa kukubaliana na propaganda za akina Nape Nnauye eti chama kimezaliwa upya!

Nne, upya wa chama hauletwei na upya wa sura za wajumbe. Kama muono wa chama ni ule ule; itikadi ni ile il; sera zake ni zile zile; i wapi CCM mpya inayozungumzwa?

Bahati nzuri Katibu Mkuu mwenyewe ameshakiri kwamba hana jipya, bali anataka kurejesha na kusimamia misingi ile iliyokiasisi chama. Mwisho wa fikra!

Zaidi ya yote, kama huyu anayeteua, kupendekeza na kufukuza wajumbe wa kamati ndiye aliyesimamia waliopita, amepata wapi njozi mpya za kusimamia wapya kwa ufanisi? Au ni yale yale tuliyozoea kuona kila anapoteua baraza la mawaziri? Kama ndivyo, je, udhaifu wa uteuzi na utendaji tunaoshuhudia serikalini hautaendelezwa kwenye chama?

Kumwondoa Makamba na kumwingiza Mukama ni mabadiliko ya mwelekeo? Kumwondoa John Chiligati na kumwingiza Nape Nnauye ni kukipa chama dira mpya?

Kumwondoa Amosi Makala na kumwingiza Mwigulu Nchemba ni kukipa chama moyo mpya? Kumwondoa Bernard Membe na kumwingiza January Makamba ni kukipa chama katiba mpya? Kurejeshwa kwa Zakia Meghji kunakipa chama itikadi mpya?

Lililo wazi ni kwamba CCM ni chama kinacho kufa. Kina sura zile zile na mawazo yale yale. Na kwa sababu wameishiwa mapya, wamebaki katika siasa za kuwindana na kumalizana. Wanachomoa hawa na kuchomeka wale. Inatosha kuwanusuru?

Udikteta wa CCM Katika Usanii wa Kujivua Magamba


Natambua kuwa CCM ni chama chenye sheria,taratibu na kanuni zake.Nafahamu pia kuwa kama chama huru (hata kama kumekuwa kikiwakumbatia mafisadi kukiendesha) kina mamlaka na uhuru wa kufanya mambo kipendavyo alimradi hakifunji sheria za nchi.

Hata hivyo,mengi ya maamuzi ya CCM-kama si yote-yanamgusa kila Mtanzania kwa vile chama hicho ndio tawala kwa sasa.Na kwa vile mfumo wetu wa siasa umeendelea kuwa wa chama kushika hatamu,kwa maana ya matakwa ya chama ndiyo yanayoiongoza serikali iliyopo madarakani,kila mwananchi mwenye mapenzi mema kwa Tanzania yetu anawajibika kuishauri,kuipongeza na hata kuikosoa CCM pale inapofanya mambo “ndivyo sivyo”.

Majuzi,chama hicho kimetangaza “kujivua magamba”.Nimeshaliongelea hilo kwa mapana,na makala yangu ya Jumatano ijayo kwenye jarida la Raia Mwema inajadili suala hilo kwa undani zaidi.Kwahiyo hapa sintingia kwa undani kuhusu uamuzi huo wa chama tawala uliopelekea vigogo wake kadhaa kuvuliwa madaraka (japo kwa kuwaheshimu,kilichofanyika ni kuvunja kamati kuu na kuingiza sura mpya kwenye nafasi mbalimbali).

Wasiwasi wangu mkubwa ni tendencies za kidikteta zinazoelekea kushamiri ndani ya CCM.Sijawahi kuwa shabiki wa Edward Lowasa,Rostam Aziz au Andrew Chenge,sio kwa vile siwapendi bali naamini kuwa matendo yao yanaikwaza sana Tanzania kupiga hatua kimaendeleo huku mamilioni ya wananchi wakigubikwa na umasikini wa kutupa.Hata hivyo,kutokuwa shabiki wao hakumaanishi kutoangalia namna walivyotendwa na CCM.

Haihitaji kuwa na uelewa wa uchambuzi wa siasa kumaizi kuwa by kujivua magamba CCM imemaanisha kuondokana na baadhi ya viongozi wake ambao kwa namna moja au nyingine wamekuwa wakihusishwa na ufisadi.Kwa lugha nyingine,magamba ni ufisadi,na ilichofanya CCM ni kujivua joho la ufisadi.

Wengi wetu tunafahamu kuwa uhasama mkubwa kati ya CCM na Dokta Wilbroad Slaa na Chadema kwa ujumla ni suala la ufisadi.Na kwa upande mwingine,umaarufu wa Slaa na Chadema umetokana zaidi na harakati zao katika kupambana na ufisadi.

Ndio maana katika majadiliano yangu ya kistaarabu huko Twitter na msanii wa Bongofleva mwenye mwamko mkubwa wa kisiasa,Hamisi Mwinjuma a.k.a Mwanafalsafaau MwanaFA,nimekuwa nimkumbusha mara kwa mara kuwa mie si mwanachama wa chama chochote kile cha siasa,achilia mbali Chadema.Kinachonifanya niafkiane na Chadema ni mtizamo,misimamo na harakati zao katika kupinga na kupambana na ufisadi.Kadhalika,sina chuki binafsi na Rais Jakaya Kikwete,serikali yake au CCM kwa ujumla bali “ugomvi” wangu nao ni jinsi wanavyokumbatia ufisadi na kupuuza vilio vya wanyonge wa Kitanzania kuhusu suala hilo.

Tunalazimika kuamini kuwa magamba yaliyovuliwa na CCM ni Lowassa,Rostam na Chenge kwa sababu kuu mbili.Kwanza,ni kwa vile kutoswa kwao kama vigogo wenye nguvu ndani ya chama hicho kumeendana na CCM kutangaza kuwa imejivua magamba.Ni wazi kuwa kama umevuliwa madaraka kisha aliyekuvua madaraka akitangaza kuwa ameondokana na uozo basi lazima utatafsiri kuwa uozo huo ni wewe uliyevuliwa madaraka.Pili,hata kabla ya CCM kuchukua uamuzi huo,wanasiasa hao wamekuwa wakituhumiwa kuhusika na ufisadi,japo mara kwa mara CCM iliwatetea huku ikidai kuwa tuhuma dhidi yao zinaweza tu kuthibitishwa na mahakama na si vinginevyo.

Na hilo la pili ndilo lililonisukuma kuandika makala hii.Si Kikwete,CCM au Kamati/Halmashauri Kuu yake wenye mamlaka ya kumtia mtu hatiani,hususan hatia yenyewe inapokuwa kubwa kama tuhuma za ufisadi.Hivi kwa mfano,Lowassa,Rostam na Chenge wakiamua kwenda mahakamani wakiituhumu CCM kwa kuwachafua kwenye jamii chama hicho kitasemaje?

Unaweza kudhani kuwa itakuwa rahisi kwa CCM kuweka hadharani ushahidi wa kusapoti tuhuma zake dhidi ya wanasiasa hao.Lakini hilo sio rahisi kwa vile,kwanza,tangu mwaka 2005 CCM hiyohiyo imekuwa ikipita huku na kule kudai kuwa tuhuma za ufisadi dhidi ya wanasiasa mbalimbali wa chama hicho (including Lowassa,Rostam na Chenge) ni porojo tu zisizo na ukweli wowote.Actaully,Mwenyekiti wa chama hicho,Rais Kikwete,ameshanukuliwa mara kadhaa akidai kuwa “kelele za mlango hazimnyimi usingizi mwenye nyumba”,akimaanisha kuwa tuhuma za ufisadi dhidi ya chama hicho na baadhi ya viongozi wake ni kelele tu  zisizopaswa kuendekezwa au kuamsha tafakuri ya Watanzania.

Kana kwamba hiyo haitoshi,miezi machache iliyopita,wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana,Rais Kikwete alisimama katika jukwaa jimboni Monduli kumpigia debe Lowassa,na akasimama kwenye jukwaa jimboni Igunga kumpigia debe Rostma,na akaenda jimboni kwa Cheyo kumpigia kampeni mwanasiasa huyo.Kadhalika,siku moja kabla ya Uchaguzi mkuu,Kikwete alizungumza na waandishi wa habari na kuwatetea tena watuhumiwa wa ufisadi na kudai kuwa ni watuhumiwa tu kwa vile hawajatiwa hatiani.

Sasa kama kilichofanyika Dodoma si udikteta ni kitu gani?Kwa sababu haiingia kabisa akilini kwamba viongozi waliosfifiwa na kutetewa mwezi Oktoba mwaka jana kuwa ni wasafi na wanaopaswa kuchaguliwa tena,waonekane hawafai miezi 6 baadaye.Of course,lolote linaweza kutokea katika kipindi cha miezi 6 lakini sote tunafahamu kuwa tuhuma za ufisadi wa Lowassa,Rostam na Change hazijatokea katika kipindi hiki cha miezi 6.

Kama maovu yao yalivumiliwa huko nyuma,na wakasafishwa hadharani na Rais Kikwete,iweje basi leo wanasiasa hao wabebeshwe tuhuma hizohizo ambazo walishasafishwa nazo?Ndio maana nimesema kuwa laiti wanasiasa hao wakiamua kufungua kesi ya kudhalilishwa mbele ya jamii,CCM itakuwa na kazi kubwa sana kujinasua.

Na sio hivyo tu bali wengi wetu tunafahamu kuwa ni vigumu mno kuwatuhumu watu kama Lowassa na Rostam kwa ufisadi pasipo kumhusisha Kikwete mwenyewe.Kama Lowassa ndiye aliyesababisha na kumwezesha utapeli wa Richmond,mwenye maamuzi ya mwisho kabisa alikuwa Kikwete mwenyewe ambaye aliidhinisha matakwa ya Lowassa kupitia vikao vya Baraza la Mawaziri ambavyo Kikwete ndio mwenyekiti wake.

Kama Rostam anahusishwa na suala la EPA,Kagoda na Dowans,again Kikwete alibariki yote hayo katika wadhifa wake kama Rais wa Tanzania.Anaweza kujiteteea kuwa hakufahamu ufisadi huo wakati unatokea.Hiyo inaweza kumfanya akaishi kwa muda wa kuazima lakini baadaye atalazimika kutueleza alichukua maamuzi gani baada ya kubaini kuwa ufisadi huo ulisababishwa na swahiba wake.

Lakini kuna suala jingine kubwa zaidi ambalo ni uhusika wa watu wasio na nyadhifa ndani ya CCM.Kwa mfano,ni watu gani ndani ya Idara ya Usalama wa Taifa waliwezesha kufanikiwa kwa wizi wa EPA na Kagoda,na ujambazi wa Richmond na Kagoda?Kwanini hawajachukuliwa hatua hadi leo?Je nao si magamba?Kam jibu ni ndiyo,je ni CCM au serikali yake itakayowapa siku 90 za kuwajibika?Na watawajibikaje?Wajipeleke wenyewe mahakamani?
Vipi kuhusu Mwanasheria Mkuu Mstaafu wa Serikali Johnston Mwanyika?Vipi kuhusuMkurugenzi Mkuu wa Takukuru Edward Hosea?Je hawa nao si magamba yanayopaswa kuvuliwa?Wangekuwa ndani ya CCM wangeweza kupewa notisi ya siku 90 lakini hawa sio wanasiasa,hivyo haitowezekana kuwawajibi9sha katika namna ya akina Lowassa na Rostam.
Vipi kuhusu Rais Mstaafu Benjamin Mkapa?Kwa wadhifa wake bado ni kiongozi wa CCM.Kwanini basi iwe Lowassa,Rostma na Chenge pekee na sio rais huyo Mstaafu,sambamba na akina Mangula,Sumaye,Malecela,Mwinyi au hata Zakia Meghji,Mkuchika na Chiligati?

Na kama kujivua magamba kuna maana yoyote,kwanini basi Waziri Membe aendelee kuwa Waziri ilhali kuondolewa kwake kwenye madaraka aliyokuwa nayo kunaweza kutafsiriwa kuwa ni hatua dhidi ya mafisadi?Vipi kuhusu akian Lawrence Marsha,Daniel Yona na Basil Mramba ambao kwa sasa hawapo madarakani?Na vipi kuhusu watu kama William Ngeleja na Naibu wake Malima ambao wizara yao,kwa namna moja au nyingine,imewezesha ujambazi wa Richmond na Dowans?Vipi kuhusu watendaji kama Dr Idris Rashid na Mgonja?

Narejea tena.Siwatetei Lowassa,Rostam au Chenge wala sipingani na hatua yoyote iliyo,inayo na itakayochukuliwa dhidi yao.Lakini kama lengo la Kikwete na CCM yake ni kupambana na ufisadi kwa vitendo basi ni lazima zoezi hilo litanuliwe kwa mapana zaidi.Lakini sote tunajua kuwa sio rahisi kwa Kikwete kwenda mbali zaidi kwa vile anatambua kuwa anakalia kuti kavu.Najua fika kuwa washirika wake wanaweza kabisa kumwaga uozo wote hadharani katika staili ya “bora tufe wote”.

Jingine,na hili lina umuhimu wa ikipekee,Kikwete anatambua kuwa vyovyote iwavyo,lazima mwakani apitishwe na kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa CCM mpaka atakapomaliza muda wake.Na sio kupitishwa na kuchaguliwa tu,bali pia anapaswa kupata ushindi wa kishindo wa asilimia tisini na kitu.Sasa kwa vile anafahamu fika kuwa asipokuwa makini, “magamba” aliyoyavua yanaweza kabisa sio tu kumpunguzia kura hapo mwakani bali pia,in worst case scenario, kumuingiza kwenye vitabu vya historia kama mwenyekiti wa kwanza wa CCM kushindwa kurejea kwenye wadhifa wake huku akiwa bado madarakani,hawezi kwenda mbali zaidi ya alivyokwishafanya sasa.

Lililo wazi ni kwamba tutashuhudia mengi.Na tayari tumeshaanza kushuhudia baadhi ya vituko.Kwa mfano,mara baada ya “CCM kujivua magamba”,magazeti yanayomilikiwa na Rostam Aziz yameanza kuonekana yakiinanga CCM na serikali ya Kikwete.Tusisahau uwezo wa “magamba” hayo kifedha na influence kubwa waliyanayo ndani ya CCM na kwenye jamii.It is a bad influence lakini still ni influence.

All in all,matarajio ya Watanzania ni kuona nchi yao ikiondokana na nira ya ufisadi.Anayedhani “CCM kujivua magamba” ni sehemu ya process hiyo basi ni vema aamke kwenye lindi la usingizi aliomo.Kinachofanyika ndani ya chama hicho ni revelation ya msemo wa Kiswahili kuwa ushirika wa wachawi haudumu.Ni vita ya kimaslahi zaidi kuliko ya maslahi kwa jamii.Na ndio maana inasemekana hata maamuzi ya Kikwete kuvunja kamati kuu na kuwatosa maswahiba zake ni baada ya kutambua walikuwa wamedhamiria kwa dhati kumwondoa yeye mwenyewe kwa kuanzia na ajenda ya kutenganisha urais na uenyekiti wa CCM taifa.

Sihitaji kukwambia nani anayeweza kutuongoza kufikia ukombozi wa kweli wa Tanzania.Matendo hukidhi haja maridhwa kuliko maneno.Na kwa kila Mtanzania mwenye uzalendo na mapenzi ya kweli kwa nchi yetu anafahamu ni nani na chama kipi kinaweza kutufikisha tunakostahili kuwepo na kuwateketeza mafisadi wote.

Saturday, April 16, 2011

Breaking News: Chadema Wataja Orodha Mpya ya Mafisadi.Wamo Malecela,Magufuli


Kama ilivyoripotiwa na vyombo mbalimbali vya habari,Chama cha Demokrasia Na Maendeleo (Chadema) leo kimefanya mkutano wake wa hadhara mjini Tabora na kutaja orodha mpya mafisadi ikiwa ni ziada ya wale waliotajwa kwenye List Of Shame,Mwembeyanga.

Kwa mujibu wa habari zilizokwishapatikana hadi muda huu,mafisadi wapya ni pamoja na mwanasiasa mkongwe John Malecela na Waziri wa Ujenzi na Miundombinu John Pombe Magufuli.

Kwa habari kamili fuatilia HAPA

Friday, April 15, 2011

OMBI MAALUM: Aliyechomwa Moto na Mdosi Kigamboni Anaomba Msaada wa Kisheria


Ndugu wa Bwana Lilah Hussein ambaye anadaiwa kuchomwa moto na walinzi na Meneja/Mmiliki wa Hotel ya South Beach wameomba wapatiwe mwanga wa kisheria jinsi ya kudai haki kwa ndugu yao aliyechomwa moto.

Akiongea nami mmoja wa jamaa wa Lilah amesema kuwa mpaka sasa wako gizani hawajui pakuanzia kutokana na kutojua mambo ya kisheria.

Labda kwa anayeweza kutoa msaada au muongozo wowote wa kisheria anaweza kuwasiliana na mmoja wa ndugu hao kupitia 0655362785

Kwa sasa Lilah bado amelazwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Hot Sonakshi Sinha, Car Price in India