Featured Posts

Showing posts with label MKULO. Show all posts
Showing posts with label MKULO. Show all posts

Thursday, October 13, 2011

KIKWETE UPO??? Zitto Kabwe Amlipua Mkulo,Ataka Apishe Uchunguzi wa CHC.





Kabwe ZuberiZitto, Mb



WaziriKivuli wa Fedha na Uchumi



TAARIFA KWAVYOMBO VYA HABARI



Waziri wa Fedha ndugu Mustafa Mkulo akae pembeni kupishauchunguzi dhidi yake kuhusu Shirika la CHC.

Katika Mkutano wa Nne wa Bunge la Kumi kulitokea malumbano makali kati ya Serikali na Wabunge wajumbe wa Kamati yaHesabu za Mashirika ya Umma kuhusu kuongezwa muda wa Shirika la CHC. WakatiWaziri wa Fedha alileta Azimio la kulivunja Shirika hili lenye taarifa nyingina nyeti kuhusu zoezi la Ubinafsishaji, Kamati ya Bunge ya POAC kutokana nauzoefu wake wa kukagua mahesabu ya Mashirika ya Umma na kufuatilia zoezi laUbinafsishaji wa Mashirika ya Umma, ilipinga hatua hii na kulitaka Bungekukataa Azimio la Serikali na kulifanyia marekebisho makubwa.

Hatimaye Bunge liliridhia kufanya mabadiliko makubwa katika Azimio la CHC, kwa kuamuru Shirikalipewe uhai wa miaka 3 na kuagiza uchunguzi wa namna bora ya kuendesha shughuliza Shirika la Consolidated Holdings. Mapendekezo ya Kamati ya POAC ni kulifanyaShirika hili kuwa la kudumu na kulipa jukumu la kumiliki na kusimamia uwekezajiwa Serikali kwenye kampuni binafsi (National Investment Agency) kama ilivyo Shirikala Tamasek ya Singapore na Shirika la Khazana ya Malaysia. Kwa sasa Uwekezajiwa Serikali katika Kampuni binafsi unasimamiwa na Hazina na usimamizi wake nimbovu na hauleti tija kwa Taifa.

Kitendo cha kushindwa kwahoja Bungeni kiliifedhesha Serikali na hivyo kwa kupitia Wizara ya Fedha kuamuakulihujumu Shirika kwa kumsimamisha Mkurugenzi wake Mkuu kwa makosa ya kimajungumajunguna kwa kuzusha kwamba CHC iliwahonga wabunge ili kuitetea. Waziri wa Fedha ndugu Mustafa Mkulo alilitaarifuBunge kuwa Bodi ya CHC imeomba ukaguzi maalumu kuhusu tuhuma za ubadhirifundani ya Shirika hilo. Niliitaka Serikali ichunguze pia tuhuma kwamba Kamati yaPOAC ilihongwa na kuahidi kuahidi kujiuzulu nyadhifa zangu zote ikithibitika.

Katika Uchunguzi wakeMdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Heabu za Serikali kwa kupitia Kampuni ya Ernest andYoung walitaka kufanya mahojiano na Waziri wa Fedha juu ya tuhuma mbalimbalizinazomkabili ndani ya CHC. Waziri Mkulo alikataa kuhojiwa na wakaguzi nabadala yake akaandika barua (kumb TYC/B/70/2/03 ya Oktoba 8, 2011) yenye kujibutuhuma moja, tena kwa juu juu, kuhusu yeye kuliamuru Shirika kuuza kiwanja cha Shirikabila kufuata taratibu za sheria.

Wakati Waziri anakanusha kuliagiza Shirikakuuza kiwanja kwa mtu aliyemtaka yeye, mimi nina ushahidi tosha wa Nyarakakutoka Hazina, kwa mfano barua TYC/A/290/13/4 ya Machi 9, 2011 ambayo inawagizaCHC kutekeleza agizo la Waziri la Fedha kuhusu kiwanja na. 10 barabara yaNyerere. Vilevile, nina ushahidi wa mkutano uliofanyika huko Morogoro Hotelkati ya Waziri wa Fedha na Mwenyekiti wa Bodi ya CHC kuhusu jambo hilo.

Siku mbili baada yakumjibu CAG, Waziri wa Fedha ndugu Mustafa Mkulo aliamua kutengua uamuzi wakewa kuongeza muda wa Bodi ya Shirika la CHC mpaka mwezi Disemba 2011 na hivyokuivunja. Uamuzi huu wa Waziri una lengo la kuficha ukweli kwani CHC bila Bodiya Wakurugenzi inaendeshwa na Hazina na hivyo taarifa ya ukaguzi itabidiipelekwe Hazina ambayo Waziri wake ni mtuhumiwa.

Uchunguzi wa kina
Ninapendekeza uchunguzi wakina ufanyike kwa kutumia vyombo vya dola na hasa TAKUKURU kuhusu tuhuma hizidhidi ya Waziri wa Fedha na alazimishwe kisheria kujibu maswali ya wakaguzi (Auditors) kuhusu tuhuma dhidi yake.

Wakati uchunguziunaendelea ndugu Mustafa Mkuloasimamishwe kazi ya Uwaziri wa Fedha hadi hapo uchunguzi utakapokamilika.Kitendo chake cha kuiamuru Bodi kumsimamisha kazi aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu kwatuhuma za kutunga na majungu na baadaye kuvunja Bodi ya CHC wakati inasubiritaarifa ya uchunguzi kutoka kwa CAG ni kuingilia uchunguzi na pia ni matumizimabaya ya Ofisi ya Umma ili kulinda maslahi binafsi. Ni dhahiri akiendelea kuwaWaziri wa Fedha ataharibu uchunguzi.Vilevile, Rais wa Jamhuriya Muungano wa Tanzania ndugu Jakaya Kikwete aangalie kama anaitendea haki nchina Uchumi wa nchi kwa kuwa na Waziri wa Fedha ambaye anasema uwongo Bungenibila kuogopa na mwenye kutumia Ofisi yake vibaya kwa kuchukua maamuziyanayoingilia uchunguzi unaomhusu ili kujilinda.

Taarifa ya Uchunguzi ikabidhiwe kwa Spika
Kutokana na ukweli kwambasuala la CHC lilianzia Bungeni na hata Waziri mwenyewe kukiri kuwa taarifa yauchunguzi inapaswa kuwekwa wazi. Kutokana na matokeo ya sasa ambapo Waziri waFedha mwenyewe ana tuhuma za kujibu na kwamba hivi sasa hakuna Bodi yaWakurugenzi ya Shirika na hata itakayoundwa itateuliwa na Waziri mtuhumiwaninashauri kuwa taarifa ya uchunguzi wa Shirika la CHC sasa ipelekwe kwa Spikawa Bunge kwa hatua zaidi.

KZZ
Dar es Salaam, 13 Oktoba,2011.


Nadhani unaweza kuhoji kwanini kichwa cha habari kimeanza na "KIKWETE UPO..." Well,kama tunavyoelewa,utamaduni wa kijiuzulu ni msamiati wa kigeni kwa viongozi wetu.Kutaraji kuwa Waziri Mkulo atatekeleza ushauri wa Zitto ni ndoto ya mchana.Kinachopaswa kufanyika ni kwa Rais Jakaya Kikwete kumpumzisha Mkulo hadi uchunguzi wa suala hili utakapomalizika.By the way,hatuwezi kuruhusu uwepo wa Waziri wa Fedha anayeandamwa na tuhuma za ufisadi.MTIHANI MWINGINE KWA KIKWETE.Let's wait and see!

Sunday, February 13, 2011

Watanzania Wana Haki ya Kujua Hali ya Uchumi wa Taifa lao


Kumekuwa na tetesi za muda mrefu kuwa hali ya uchumi wa Tanzania ni mbaya.Hata hivyo,kama ilivyozoeleka,wahusika serikalini wameendelea kuwanyima Watanzania haki yao ya msingi ya kufahamishwa hali ya uchumi wa taifa lao. 

Hivi karibuni Gavana wa Benki Kuu,Profesa Benno Ndulu,alizungumza na waandishi wa habari kuhusu ubora wa noti mpya.Licha ya kuonekana kufahamu kuwa wananchi hawaridhishwi na kiwango duni cha noti hizo,Gavana Ndulu alizitetea kwa nguvu zote.Akemee ili ifahamike kuwa 'zimechakachuliwa'?

Akiichambua hali ya uchumi, gavana huyo alisema kwa sasa hali ya uchumi ni nzuri na kwamba nchi ina uwezo wa kulipa huduma kwa miezi sita bila kutegemea sehemu yoyote.Lakini katika kile kinachoweza kiashirikia kiwa kauli hiyo ilikuwa ya kisiasa zaidi kuliko ya kitaalamu,Gavana alidai kuwa mwenye dhamana ya kueleza athari za mgao wa umeme kwa uchumi ni Waziri wa Nishati na Madini.Huku sio tu kukwepa majukumu bali mwendelezo wa danadana za kibabaishaji zinazoeleka kuunda mfumo wa utendaji wa viongozi wengi wa taasisi za umma.Na kwa vile 'Mteuzi Mkuu' Serikalini,yaani Rais,anaonekana kama yupo usingizini kubaini mapungufu ya baadhi ya watendaji aliowateua,ni dhahiri utendaji kwa mfumo wa 'bora liende' utaendelea kuwepo kwa muda mrefu.

Kwa hapa Uingereza,Benki Kuu imekuwa ikitoa taarifa kuhusu viwango vya riba kila mwezi.Taarifa hiyo huambatana na maelezo ya kutosha kuhusu mwenendo wa uchumi wa nchi hii.Na kila baada ya miezi michache,ofisi ya takwimu nayo hutoa taarifa yenye takwimu zinzoashiria kupanda,kutuama au kushuka kwa uchumi.Kadhalika,vielekezo muhimu kuhusu uchumi wa nchi kama vile idadi ya wasio na ajira,mfumuko wa bei,wastani wa thamani ya sarafu,nk vimekuwa vikiwekwa wazi kwa umma.

Na huko nchini Marekani,Serikali ya Rais Barack Obama,imekuwa ikitoa taarifa za hali ya uchumi wa nchi hiyo mara kwa mara,hata kama kufanya hivyo kufanya hivyo kunaathiri namna wananchi wanavyoridhishwa au kutoridhishwa na serikali hiyo.Huku sio tu kutambua haki ya wananchi kuhabarishwa bali pia kuelewa kuwa kuficha ukweli kuhusu hali ya uchumi hakuwezi kuufanya uchumi husika kuboreka.

Na ndio maana licha ya kuwaficha Watanzania kuhusu hali ya uchumi wa nchi yao,sambamba na kauli mbalimbali za kisiasa kuwa 'hali cha uchumi ni poa' gazeti la Mwananchi katika toleo lake la leo linaripoti kuwa Serikali imelazimika kufumua bajeti yake ya mwaka wa fedha 2010/11 kwa kupunguza matumizi ya Wizara ili kufidia upungufu wa Sh670.4 bilioni zilizotegemewa kupatikana kutokana na makusanyo ya kodi katika mwaka huu wa fedha.

Hata hivyo,gazeti hilo lilipomtaka Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustaffa Mkullo, kuihusina na hali hiyo alisema taarifa ya hali ya uchumi wa nchi alishaitoa hivi karibuni kwenye chombo kimoja nchini, hivyo hahitaji kuitoa tena."Nilitoa taarifa kwa wenzenu wa gazeti (sio Mwananchi) sasa siwezi tena kuirudia," alisema.Ni dhahiri kuwa laiti hali ingekuwa nzuri,Mkulo asingefanya dharau hiyo hasa kwa vile viongozi dhaifu huwa wepesi sana kumwaga hadharani habari njema wakiamini zitawaletea sifa.

Wakati Watanzania wanasubiri 'waletewe' Katiba mpya,ni muhimu kuangalia tatizo hili la ukandamizwaji wa makusudi wa haki ya kuhabarishwa.Nchi mbalimbali zina sheria zinazoilazimisha Serikali na taasisi za umma kutoa au kuruhusu upatikanaji wa taarifa.Japo tunafahamu kuwa taarifa nyingi nchini 'zinachakachuliwa' kwa minajli ya kufisadi,kudanganya wapiga kura,kughilibu wafadhili,au sehemu tu ya utamaduni wa kutowajibika,uwepo wa sheria ya Haki ya Habari (Freedom of Information act) utakomesha tabia kama hiyo ya dharau Waziri Mkulo kupuuza kuwaeleza Watanzania kuhusu hali ya uchumi wa nchi yao

Wednesday, December 29, 2010

Waziri Wa Fedha Anapokuwa Mfuja Fedha.



Waziri Mkulo afanya kufuru
•  Akodi ndege kwenda Dodoma, aagiza shangingi toka Dar

na Bakari Kimwanga

WAKATI serikali ikisisitiza kutaka kupunguza gharama za matumizi kwa kuacha kuendelea kununua magari ya kifahari 'mashangingi', baadhi ya matumizi ya mawaziri yanatisha na kuwa mzigo kwa serikali.
Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima Jumatano kwa muda mrefu sasa, umebaini kuwa wapo mawaziri na watendaji wengine wa serikali, wanaofanya ziara mikoani na kusafiri kwa ndege za kukodi, lakini hulazimika kuyaagiza mashangingi yao aina ya G8 kutoka Dar es Salaam hadi katika mikoa wanayokwenda kufanya ziara hata kama yatatumika kwa siku moja.

Mmoja wa mawaziri hao ni Waziri wa Uchumi na Fedha, Mustafa Mkulo, ambaye wiki iliyopita alikodi ndege kwa fedha za serikali kwenda kuhudhuria mahafari ya Chuo cha Mipango mjini Dodoma, lakini bado aliliagiza gari lake la uwaziri limfuate kutoka jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kulitumia katika mji huo wakati Wizara ya Fedha na Uchumi, ina ofisi na magari mjini Dodoma.

Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima Jumatano, ulibaini kuwa Desemba 17, mwaka huu, Waziri Mkulo mwenye dhamana ya fedha nchini, alikodi ndege ya Shirika la Tanzania Air, yenye namba za usajili 5HTZC na kuwasili katika uwanja wa ndege wa mjini Dodoma, majira ya saa nane mchana.

Wakati Waziri Mkulo akipasua anga la Dodoma kwa ndege ya kukodi, siku hiyo hiyo, dereva wake alilazimika kujaza mafuta shangingi la waziri huyo na kuweka kibindoni posho yake kumfuata bosi wake mjini Dodoma.

Kwa mujibu wa habari hizo, ndege hiyo ilikodishwa kwa dola za Kimarekani 5,000, sawa na sh milioni 7.5.

'Mimi niko hazina, hivi sasa serikali haina fedha, kuna madeni mengi, kuna walimu zaidi ya 500,000 waliomaliza vyuo vya elimu ya juu tangu Mei mwaka huu wanasubiri ajira kutokana na ukosefu wa fedha, lakini hazina inafanya matumizi mabaya kila siku. Huku ni kulifilisi taifa bila sababu,' alisema mtoa habari wetu ambaye jina lake limehifadhiwa.

Akizungumza na Tanzania Daima Jumatano kuhusina na kashfa hiyo, Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, John Haule, alikiri kuwa Desemba 17, mwaka huu, wizara yake ilikodi ndege kwa ajili ya kumuwahisha Waziri Mkulo kuwahi mahafali ya Chuo cha Mipango ambapo alikuwa mgeni rasmi.

Haule ambaye alikuwa na wakati mgumu kutoa ufafanuzi huo, alisema walilazimika kufanya hivyo kutokana na umuhimu wa kazi alizokuwa nazo Waziri Mkulo siku hiyo kabla ya kuondoka kwenda Dodoma na kusisitiza kuwa ukodishwaji wa ndege ni jambo la kawaida kwa watendaji wa wizara hiyo.

'Hili ni suala la kawaida kabisa katika utendaji wa wizara yetu; siku hiyo ilikuwa lazima waziri aende Dodoma katika mahafali na kuzindua bodi ya chuo cha mipango, sasa kwa hili tulishirikiana na chuo chenyewe kulipia gharama za ndege kwa waziri,' alisema Haule bila kufafanua chuo kililipia kiasi gani na wizara kiasi gani.

Alisema gharama za kukodisha ndege hiyo ilikuwa dola za Kimarekani 350,000, sawa na sh milioni 5.2 na kusisitiza kuwa kiasi hicho kimelipwa na wizara kwa kushirikiana na Chuo cha Mipango.

Alipoulizwa sababu ya wizara kulituma shangingi la waziri huyo kutoka Dar es Salaam wakati Dodoma kuna magari ya wizara hiyo yenye hadhi ya waziri, Haule alisema walilazimika kufanya hivyo ili Waziri Mkulo aende na kurudi kuwahi majukumu mengine jijini Dar es Salaam.

Mwanzoni mwa mwaka huu, Naibu Waziri wa wizara nyeti inayochangia sehemu kubwa ya pato la taifa (jina lake limehifadhiwa), ambayo iliwahi kuwa katika wakati mgumu kutokana na kugubikwa na hoja ya ufisadi, alikumbwa na kashfa ya aina hiyo ya matumizi mabaya ya fedha za serikali.

Waziri huyo akiambatana na msaidizi wake, alifanya ziara mkoani Kilimanjaro kwa kutumia usafiri wa ndege ya kampuni ya Precision, lakini alilitanguliza gari lake la uwaziri kutoka jijini Dar es Salaam hadi mkoani humo siku mbili kabla ambapo alilitumia kwa takriban saa sita tu na jioni alirejea Dar es Salaam kwa ndege hiyo na kuliacha gari lake likirudi na dereva pekee.

Gari hilo lilifika mkoani humo siku moja kabla ya waziri huyo na msaidizi wake kufika na mara alipotua katika Uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), majira ya saa 2.30 asubuhi, tayari dereva wa gari lake alikuwa akimsubiri na kumpeleka katika ofisi ya wizara hiyo mkoani humo kwa ajili ya kuanza ziara ya kikazi.

Ilipofika majira ya saa 12 jioni siku hiyo hiyo, Naibu Waziri huyo ambaye ni mmoja wa mawaziri vijana na mara yake ya kwanza kuwa waziri baada ya Rais Kikwete kufanya mabadiliko madogo ya baraza lake, aliwasili tena KIA na msaidizi wake kwa ajili ya safari ya kurudi jijini Dar es Salaam kwa ndege na kuliacha shangingi lake lililorudi siku iliyofuata.

Kwa hali hiyo, serikali ililazimika kulipa posho ya siku tatu kwa dereva huyo na gharama za mafuta yaliyotumika kuliwezesha gari hilo kusafiri kwenda na kurudi mkoani Kilimanjaro.

Malalamiko ya matukio kama hayo, yaliwahi kutolewa bungeni na Mbunge wa Viti Maalum, Halima Mdee (CHADEMA) wakati akichangia hoja ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwamba kigogo mmoja mkoani Kigoma, alialikwa kwenye semina iliyofanyika mjini Bagamoyo na kusafiri kwa ndege, lakini alilitanguliza shangingi lake wiki moja kabla ya yeye kuwasili.

Halima ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Kawe (CHADEMA), alisema gari hilo lilitumika kumpokea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam na mwisho wa semina, alilitumia kumfikisha katika uwanja huo wa ndege na gari hilo lilisafari kurudi Kigoma baada ya kigogo huyo kuondoka.

Mbunge huyo alilalamikia kuwa hali hiyo imekuwa ikitumiwa na viongozi wengi wa serikali na kumtaka Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuwa makini kudhibiti matumizi ya aina hiyo kwa watendaji wake.

Mawaziri hao pia wamekuwa wakilalamikiwa kwa matumizi binafsi ya magari ya serikali kama vile kuyatumia kuwapeleka watoto wao shule katika safari nyingine binafsi ambazo hutumia mafuta ya serikali.

Wakati yakitumika kwa shughuli hizo binafsi, magari hayo hung'olewa namba za uwaziri na kubandikwa zingine, jambo ambalo linaelezwa na duru za kisiasa kama ni aina nyingine ya ufisadi.

Chanzo: Tanzania Daima

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Hot Sonakshi Sinha, Car Price in India