Featured Posts

Showing posts with label DUNIA INA MAMBO. Show all posts
Showing posts with label DUNIA INA MAMBO. Show all posts

Monday, August 15, 2011

Duniani Kuna Vituko: Jamaa Anamuuza Mama Mkwe Mwenye Gubu BUREE


Nadhani suaskia stori kadhaa kuhusu mama wakwe.Wajuzi wa ndoa wanadaia ukitaka ndoa ivunjike basi mruhusu mkeo amlete mama yake muishi pamoja.Sijui kwanini,lakini mama wakwe ni watu wanaotazamwa kama vyanzo vya matatizo kwenye ndoa.

Sasa leo katika pita pita zangu mtandaoni nimekutana na tangazo huko Gumtree ambapo kuna jamaa ameweka tangazo kuwa "anamtoa mama mkwe wake bure." Kwa Kiingereza chenye lahaja ya Kiskotishi tangazo husika linasomeka hivi:


Free Mother In Law
Glasgow

MOANY, GREETIN' FACED!!!!!! USES YOUR WASHING MACHINE ALL THE TIME FOR NOTHING....... DESPERATE TAE GET RID OF HER!!!!! APPLY A.S.A.P.


Sasa,kama yeye mwenye mkwe yamemshinda,anatarajia nani atakayekubali kupokea mtambo huo wa kuzalisha gubu?

Sunday, June 14, 2009

WATOTO WAKIFUNZWA SANAA YA KUCHEZA NA NYOKA (SNAKE CHARMING)







Yote ni katika kuendeleza mila.Ni katika kabila la wahamaji (nomads) la Vadi katika jimbo la Gujarat nchini India.Kabila hilo lenye takriban watu 600 hivi,lina mila ya kuwapatia watoto mafunzo ya sanaa ya kucheza na nyoka (snake charming).Lakini,hilo sio suala la siku moja,wiki,mwezi au mwaka bali ni muongo mzima (mika 10)!
Watoto huingizwa kwenye mafunzo hayo wanapotimiza miaka miwili tangu wazaliwe.Inatarajiwa kuwa watapofikisha umri wa miaka 12,watoto hao watakuwa wakielewa kila kitu kinachohusiana na nyoka.

Sunday, December 28, 2008

MHH,HIZI PRODUCTS NYINGINE...HII CREAM YA "KUREJESHA BIKRA" ITAWAINGIZA WATU MKENGE

Haya ni maongezi ya ki-utu uzima,kwahiyo under-18s mnaombwa kutosoma post hii.Well,just saying it bcoz I know ishu ya umri katika dunia ya sasa ni more theoretical than practical.Anyway,"kuvunja bikra" ni ndoto ya wanaume wengi,na japo ni suala lisilozungumzika hadharani,wengi wa wanaodai kuwa wameshawahi kupata "bahati" hiyo huwa si wakweli (wanaongopa) na wale ambao kweli walishaangukiwa na "kismati" hicho huwa hawaaminiwi wanapotoa "ushuhuda" wao,na wakati mwingine kutakiwa watoe uthibitisho!How could they?

Na pengine wapo akina dada ambao wangetamani kutopeteza bikra "kabla ya muda mwafaka" lakini mara nyingi tukio hilo (la kupoteza bikra) hutokea kwenye foolish age.Inadaiwa (japo sina uthibitisho katika dai hilo) kwamba kuna something very special kwa "ungo kuvunjwa" na mume usiku wa kwanza baada ya ndoa.Hata hivyo,jamaa yangu mmoja anayeelekea kuwa specialist wa kitu chochote kinachohusiana na jinsia ya kike anadai kuwa suala la kuvunjishwa ungo siku ya ndoa lilitengenezwa tu na walinzi wa maadili ili kuhakikisha amri ya sita haivunjwi (kwa wasiofahamu,amri ya sita ni USIZINI.Na kidini,kuzini ni tendo la ndoa nje ya ndoa).

Well,sasa kuna product ambayo "inarejesha" bikra.Nimeweka inverted commas kwa vile urejeshaji huo ni more technological than biological. Ni mithili ya ku-hack elimu-viumbe ya sehemu nyeti.

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Hot Sonakshi Sinha, Car Price in India