Featured Posts

Monday, August 15, 2011

Duniani Kuna Vituko: Jamaa Anamuuza Mama Mkwe Mwenye Gubu BUREE


Nadhani suaskia stori kadhaa kuhusu mama wakwe.Wajuzi wa ndoa wanadaia ukitaka ndoa ivunjike basi mruhusu mkeo amlete mama yake muishi pamoja.Sijui kwanini,lakini mama wakwe ni watu wanaotazamwa kama vyanzo vya matatizo kwenye ndoa.

Sasa leo katika pita pita zangu mtandaoni nimekutana na tangazo huko Gumtree ambapo kuna jamaa ameweka tangazo kuwa "anamtoa mama mkwe wake bure." Kwa Kiingereza chenye lahaja ya Kiskotishi tangazo husika linasomeka hivi:


Free Mother In Law
Glasgow

MOANY, GREETIN' FACED!!!!!! USES YOUR WASHING MACHINE ALL THE TIME FOR NOTHING....... DESPERATE TAE GET RID OF HER!!!!! APPLY A.S.A.P.


Sasa,kama yeye mwenye mkwe yamemshinda,anatarajia nani atakayekubali kupokea mtambo huo wa kuzalisha gubu?

0 comments:

Post a Comment

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Hot Sonakshi Sinha, Car Price in India