Featured Posts

Showing posts with label MIZENGO PINDA. Show all posts
Showing posts with label MIZENGO PINDA. Show all posts

Friday, August 02, 2013

Baada ya rekodi ya kuwa Waziri Mkuu wa Kwanza wa TZ kulia Bungeni, Pinda aweka rekodi nyingine, aburuzwa mahakamani


HATIMAYE PINDA KUWA WA KWANZA KUBURUZWA MAHAKAMANI ...
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimemfungulia mashtaka Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kutokana na kauli yake aliyoitoa bungeni hivi karibuni kwamba wanaokaidi maagizo ya dola wapigwe.

Hatua hiyo ya LHRC imepingwa vikali na Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP), Dk Elieza Feleshi akisema hakuna uhalali wa mashtaka yoyote dhidi ya kiongozi huyo sababu kauli ya Pinda kuwa pigeni haikuwa piga ua.

Mkurugenzi wa LHRC, Dk Hellen Kijo Bisimba alifungua mashtaka hayo katika Mahakama Kuu jana akisema kuwa wanamshtaki Waziri Mkuu kwa maelezo kuwa amekiuka kifungu cha Katiba Ibara 13 (1). Pinda ametajwa kuwa ni mdaiwa wa kwanza katika kesi hiyo namba 24.

Mkurugenzi wa Maboresho na Utetezi wa LHRC, Harold Sungusia alisema jana kwamba, mwingine aliyeunganishwa katika kesi hiyo ya kikatiba iliyofunguliwa na LHRC na Chama cha Wanasheria Tanzania (TLS) ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema.

Alisema katika kesi hiyo, kuna jopo la mawakili wasiopungua 20 na kwamba wamepata saini za wananchi 2,029 wanaopinga kauli hiyo ya Pinda na kuunga mkono kufunguliwa kwa kesi hiyo.

Mjumbe wa Bodi ya LHRC, Wakili Dk Ringo Tenga alisema katika kesi hiyo wameangalia zaidi sheria na hasa haki za msingi za binadamu na kwamba kauli hiyo ya Waziri Mkuu Pinda inahatarisha haki hizo.

Kauli yenyewe

Wakati wa Kipindi cha Maswali ya Papo kwa Papo kwa Waziri Mkuu bungeni, Juni 19, mwaka huu, Waziri Mkuu akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Kilwa Kaskazini (CCM), Murtaza Mangungu aliyeuliza: “Serikali ipo tayari kiasi gani kubainisha na kuchukua hatua stahiki, badala ya kusakama makundi fulani, tujue chanzo halisi cha vurugu hizi na matatizo haya na jinsi gani vyombo vya dola vinavyoshughulikia kwa sababu yapo malalamiko katika baadhi ya maeneo kama Mtwara kwamba wananchi wanapigwa na vyombo vya dola?”

Waziri Mkuu alijibu: “Ni lilelile nililosema... mwishowe unaona anasema vyombo vya dola vinapiga watu. Ukifanya fujo, umeambiwa usifanye hiki, ukaamua kukaidi, utapigwa tu... hamna namna nyingine, maana wote tukubaliane kwamba nchi hii tunaiendesha kwa misingi ya kisheria.

“Sasa kama wewe umekaidi, hutaki unaona kwamba ni imara zaidi... wewe ndiyo jeuri zaidi watakupiga tu.... Mimi nasema muwapige tu, kwa sababu hakuna namna nyingine... maana tumechoka.” Kesi hiyo itakayosikilizwa na majaji watatu, haina uhusiano na kesi nyingine ambazo wajibu maombi hupewa siku 90 kujibu hoja zilizowasilishwa. Kesi hiyo imefunguliwa kwa mujibu wa Katiba Sura ya Tatu.

Akizungumza juzi kwenye Viwanja vya Bunge mjini Dodoma baada ya kufungwa kwa Warsha ya Wapelelezi na Waendesha Mashtaka wa Serikali ngazi ya mikoa, Dk Feleshi alisema hakuna uhalali wa mashtaka hayo kwa sababu kauli ya Pinda kuwa pigeni haikuwa piga ua.

“Hii haikuwa kuchochea apige watu, alichosema ni kupiga wale wasiotaka kutekeleza amri halali na zaidi alisema piga lakini si kupiga na kuua,” alisema.

Mkutano huo uliendeshwa chini ya ulinzi mkali huku kukiwa na udhibiti wa kuvuja siri kwa kiwango cha juu. Pamoja na mambo mengine, ulikuwa ukijadili mbinu za kisasa katika kuendesha kesi pamoja na kujiuliza sababu za Serikali kushindwa katika kesi nyingi.

“Kwa sababu lile neno kupiga ni lazima lipewe maana pana huwezi kumpiga tu mtu hivihivi ambaye hakuvunja sheria lakini nilivyoelewa, ilikuwa ni hivyo, ni sawa na mtu ambaye anamshambulia askari,” alisema Dk Feleshi.

Alisema kuna sheria ya kutumia nguvu pale ambako kuna mkusanyiko usiokuwa wa halali pindi raia wanapokaidi kutawanyika kwa hiari hivyo hakuna shaka kauli ya Waziri Mkuu ililenga hivyo.

Hata hivyo, alisema hajapata taarifa za LHRC kumshtaki Waziri Mkuu kimaandishi na kwamba akizipata atatoa ufafanuzi baada ya kuona lengo la mashtaka.

Msimamo

Akizungumza baada ya kufungua mashtaka hayo, Dk Bisimba alisema Waziri Mkuu anaweza kushtakiwa kwa kuwa alizungumza kwa nafasi yake ya Waziri Mkuu na si mbunge na kusisitiza kwamba hakuna aliye juu ya sheria na kudai kwamba kauli hiyo ni kinyume cha Katiba.

Alisema kuwa kila anayevunja Katiba lazima ashughulikiwe kisheria na kwamba mahali pake ni mahakamani tu. Alisema kwa mujibu wa hati hiyo ya madai, kauli na amri kama hizo zinapotolewa na kiongozi mwenye hadhi kama ya mdaiwa wa kwanza (Waziri Mkuu) huchukuliwa kama sheria inayopaswa kutekelezwa na wakala wa utekelezaji wa sheria kama vile polisi. Wadai hao wanadai kuwa kwa ufahamu wao polisi wanaweza kuchukulia kauli hiyo kama amri halali kutoka kwa mkubwa wao na hivyo kuwapiga na kuwatesa watu wasio na hatia, kinyume cha Katiba.

Pia wanadai wanatambua kuwa Ibara ya 100 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatoa kinga kwa wabunge na uhuru wa maoni bungeni. Hata hivyo, wanatambua kuwa Ibara ya 100 (2) ya Katiba hiyo inawawajibisha wabunge wote chini ya masharti ya Katiba na kwamba kauli aliyoitoa Waziri Mkuu Pinda inakiuka Ibara ya 12(12).

Hivyo wanaiomba Mahakama hiyo itamke kuwa kauli na amri hiyo aliyoitoa Pinda inavunja Katiba.

Mkurugenzi wa taasisi inayofuatilia Mwenendo wa Bunge (Watch), Marcos Albania alidai kwamba wamegundua kuwa kauli hiyo ya Pinda ni moja kati ya matamko makubwa yanayovunja Katiba.

Alisema mbali na shtaka hilo, kuna la pili dhidi ya Waziri Mkuu Pinda, ambalo hawajalifikisha mahakamani ambalo pia linatokana na kauli hiyo aliyoitoa bungeni kwamba: “Sasa wamechoka.”


Wednesday, July 24, 2013

Mtoto wa Mkulima PINDA Hovyooo!!! Rais Kikwete Amuumbua



Naam, Tanzania yetu imewahi kuwa na viongozi mbalimbali wabovu, lakini linapokuja suala la mawaziri wakuu, basi Mizengo Kayanda Pinda, anaweza kabisa kuingia kwenye kumbukumbu kama WAZIRI MKUU MBOVU KULIKO WOTE KATIKA HISTORIA YA NCHI YETU.

Ndio, Kuna Edward Lowassa, aliyeng'oka kwa kashfa ya Richmond, lakini angalau yeye hakuwa m-babaishaji katika kauli zake. N apengine kilichmosaidia Lowassa ni kutambua busara kuwa mdomo sharti ushirikiane na ubongo kabla ya kutoa kauli yoyote ile.

Pinda, anayeitwa Mtoto wa Mkulima, amekuwa maarufu zaidi kwa kauli zake za kipuuzi kuliko utendaji kazi.Mbabaishaji huyo aliwahi kuzua sokomoko huko nyuma alipohalalisha MAUAJI: kwa uzembe tu wa kufikiri, Pinda alidai kuwa anaguswa sana na mauaji ya maalbino,kwahiyo ni ruksa kwa wananchi kuwauwa WATUHUMIWA wa mauaji hayo. Japo kitaaluma  mwanasheria, lakini Pinda hakuona tatizo katika kauli yake hiyo ambayo kimsingi ilikuwa inahamisha nguvu za polisi na mahakama na kuzikabidhi kwa umma.Kwa lugha nyingine, mzembe huyo alikuwa anahalalisha mob justice.

Badala ya ku-behave kama mtu mzima, Pinda akenda bungeni na kujitetea kwa KULIA KAMA MTOTO.Lakini kwa bahati nzuri, wengi wa wabunge wetu wapo bize zaidi na posho zao kuliko kuwatendea haki wananchi wanaowawakilisha, na machozi hayo ya kinafiki ya Pinda yakamnusuru.


Katika kuonyesha kuwa Tanzania kwa sasa ni kama haina Waziri Mkuu kwani Pinda anayeshikilia nafasi hiyo ni so useless kiasi kwamba uwepo au kutokuwepo kwake hakuna tofauti, majuzi akakurupuka tena na kauli nyingine ya kibabaishaji.Akatangaza kuwa ni ruksa kwa polisi kupiga raia ZAIDI...Yaani kana kwamba unyanyasaji unaofanywa na polisi hautoshi, na sasa wanahamasishwa kutoa vipigo zaidi.

Watu tumesema weee kuhusu kauli hiyo ya kihuni lakini kwa vile aliyemteua Pinda kushika nafasi hiyo hana tofauti sana na Pinda, Waziri Mkuu huyo bado yupo madarakani hadi dakika hii.

Na uwepo wake huo umepelekea ujinga mwingine. Majuzi kumezuka sokomoko la kodi mpya ya SIM kadi.Badala ya kusikia kilio cha mamilioni ya Watanzania wanaopinga kodi hiyo, mropokaji Pinda akadai eti "wanaopinga kodi hiyo hawaitakii mema nchi yetu..." COMPLETELY USELESS!

Bahati nzuri, safari hii Rais Kikwete kaamua kutumia busara, na kwa namna flani, amemudu KUMUUMBUA PINDA. Rais amezitaka mamlaka husika kukaa pamoja kutafuta ufumbuzi wa haraka kuhusu kodi hiyo inayolalamikiwa na wananchi wengi. Rais aliyasema hayo alipokutana na viongozi wa Wizara ya Fedha, na wale wa Wizara ya Sayansi na Teknolojia, na Mamlaka ya Mawasiliano TCRA.

SIJUI MTOTO WA MKULIMA ANAJISIKIAJE MUDA HUU....ONE THING FOR SURE, PINDA AMETHIBITISHA KWA MARA NYINGINE KUWA YEYE NI MTU MZIMA OVYO ASIYEFAA HATA KUONGOZA DARASA KAMA KIRANJA, ACHILIA MBALI HUO UWAZIRI MKUU.NI WABABSIAHJI KAMA PINDA WANAOIFANYA SIASA KUWA MCHEZO MCHAFU ZAIDI YA UCHAFU WA SIASA.

CAN'T WAIT TO SEE HIM GONE COME 2015, OR EVEN EARLIER...GOOD RIDDANCE.

Monday, July 01, 2013

#UjioWaObama: Gazeti la USA TODAY lazungumzia Pinda kuruhusu polisi wapige raia, mabomu,ufisadi... na furaha kuhusu Obama

obama_tanzania

DAR ES SALAAM, Tanzania — Vendors carrying trinkets and snacks usually weave in and out of the dense traffic of this bustling East African capital, their hawking adding to the cacophony of horns and chatter that are the soundtrack to everyday life here.
But not today.
An eerie silence and empty streets cleared for security reasons herald the arrival of President Obama on his first visit to this usually overlooked country Monday, a visit that overjoyed locals hope results in change and progress.
"My country is crazy at the moment about Obama's visit and I am, too," said Asteria Benedicto, 32, a student at the Institute of Social Work in Dar es Salaam. "If I get a chance, I will ask him to see to it that there's an equal distribution of resources, fair elections and trustworthy security force in my country."
Tanzania is President Obama's last stop on a week-long trip to Africa – a continent some Africans accuse Obama of neglecting during his presidency. His visit to the East African nation was a surprise choice but one the White House said was made because of its strong and vibrant democracy as well as its importance as a partner on a range of security issues.
While Obama is being feted on this visit — one main artery of the capital, Ocean Road is being renamed Obama Avenue during his visit — some Tanzanians want to use this opportunity to speak out about problems such as poverty and corruption they say plague the country.
"I have been struggling to make a living and facing a lot of challenges," said Sylvester Pius, a 34-year-old farmer who lives in Iringa, a small town 400 miles south of Dar es Salaam.
He says one of the biggest problems is corruption. He recalls how this problem caused tragedy for his family when his wife gave birth to their fourth child in 2011.
"The nurse who was attending her wanted a bribe to help her deliver on time but I didn't have any money," he said. "Several days after delivery, my wife died because she didn't receive this help and bled out. The child survived but the challenge was now how could I manage to raise him?"
But Pius's story is common in a country where the average monthly income is less than $50 and corruption is out of control, according to locals. They say the situation is not inevitable.
"Considering the peace and potential prosperity of Tanzania, there should be a way," said Alfred Kinge, 54, an entrepreneur in Dar es Salaam. "But of course there are the chronic poor in every country. Still, can't something be done?"
Tanzania has undertaken economic reforms in a bid to lift the country out of such stark poverty, and it has made efforts to improve its infrastructure and also develop its tourism sector but analysts say there is still a long way to go.
"Serious problems remain in mining, education and agriculture — all are key to national progress," said Emanuel Sulle, a Tanzanian researcher at the Institute for Poverty, Land and Agrarian Studies at the University of the Western Cape in South Africa.
"The failures in most of these sectors are the result of poor reforms in education, constitution and, of course, lack of good governance."
Tanzania has also experienced recent terrorist attacks: On June 15, a bomb that went off at a political rally in Arusha, 500 miles north of Dar es Salaam, organized by the opposition Democracy and Development Party, left three people dead and 60 injured.
The attack followed another bomb a month earlier that killed another three during a Catholic Church service in Arusha as Archbishop Francisco Montecillo Padilla inaugurated the local parish.
It is the first time since Tanzania became independent in 1961 that it has witnessed such attacks and many point fingers at the government and its ruling Chama Cha Mapinduzi (Party of the Revolution or CCM) party, an allegation both the government and the party deny.
Regardless, no one has claimed responsibility for the attacks.
However, Tanzanian Prime Minister Mizengo Pinda has been accused of endorsing the use of violence by police against dissidents and the opposition, and has been criticized by human rights groups such as the country's Legal and Human Rights Center, who say some recent statements by Pinda violate the country's constitutional protections.
"Once you reject obeying (the law) and cause trouble, or fail to respect the laws of the country, you will be beaten, and I say such people should be beaten…we (the government) are tired," said Pinda following the blasts on June 21, in one such statement.
As a result, some Tanzanians are losing hope and trust in the government as it fails to properly investigate and address intimidation and violence.
"Lack of good governance and weak leadership both contribute to poverty we face today even as we (Tanzanians) should be a champion economically in the region," said Deodatus Kazinja, who works in the penal system in Dar es Salaam, adding that Obama should not ignore the human rights abuses being carried out in the country.
Many are hoping that Obama will share his experiences with leaders in the East African country and build even stronger relations with Tanzania to help them tackle their ongoing problems.
"Our relationship with America is a continuation and cementation of our friendship since President Kennedy's period when the father of our nation Julius Nyerere paid a visit to the U.S.," said Salaam Mecky Sadick, governor of Dar es Salaam. "Since then the U.S. has supported us in many areas like education, agriculture and health."
But others say they know Obama is coming for "American interests."
"One thing I would like to note is that there has been a scramble for Tanzania's resources, like gas and gold, and there's an obvious competition between the U.S. and China," said retired teacher Jesca Mbelwa, 65.
"But I want to see Africans benefit from their resources first and second the Americans or the Chinese."

CHANZO: http://goo.gl/srxVl 

Sunday, April 14, 2013

Waziri Mkuu Pinda 'Alikoroga'



WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda anaweza kujikuta katika wakati mgumu, baada ya kuumbuliwa na ripoti ya tume ya uchunguzi wa matokeo mabaya ya mwaka 2010, inayodaiwa hakuifanyia kazi na badala yake akakimbilia kuunda tume nyingine.


Ripoti hiyo ambayo imesambazwa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii, ikiwamo ule wa Jamii Forums, imekuja siku moja baada ya Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu kuwashawishi wabunge wampigie kura Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ya kutokuwa na imani naye, kutokana na kushindwa kumwajibisha Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa 



Katika ripoti hiyo ya mwaka 2011, iliyosambazwa kwenye mtandao wa Jamii Forum, na gazeti hili kuipata inabainisha upungufu wa wazi hasa kwa Serikali kwamba, uteuzi unaofanywa kwa viongozi mbalimbali wa kisiasa katika sekta ya elimu hauzingatii uzoefu, utaalamu, uwezo, uadilifu na uwajibikaji. 



Gazeti hili limebaini kuwa tume iliyokuja na ripoti hiyo iliongozwa na Profesa Sefue Mchome na utafiti wake ulifanywa kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali wa sekta ya elimu.



Hata hivyo, Serikali imeshutumiwa kwa kushindwa kuiweka wazi na namna hatua ilizochukua baada ya kupokea ripoti hiyo.



Baadhi ya watu waliotoa maoni yao walionyesha kushangazwa na hatua ya Pinda kuunda Tume kuchunguza kushuka kwa ufaulu kwa matokeo ya mwaka jana, ili hali tayari kulikuwa na ripoti nyingine ambayo ilikuwa haijafanyiwa kazi.



Kitendo hicho kimetafsiriwa kuwa kilikuwa na lengo la kuwahadaa wananchi ili kuwaonyesha kuwa anauchungu na anataka kulifanyia kazi suala hilo kumbe sivyo.



Ripoti hiyo ambayo ilijikita katika kufanya utafiti wa kushuka kwa elimu nchini, ulifanywa kwa ushirikiano kati ya TAMISEMI na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi (WEMU), ikihusisha Taasisi ya Elimu Tanzania na Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA).



Moja kati ya mambo ambayo yamebainika katika utafiti huo ni pamoja na sababu za kushuka kwa kiwango cha ufaulu wa Mtihani wa Taifa wa Kidato cha 4 mwaka 2010, ambazo ni masuala ya kimfumo ikiwemo upungufu katika usimamizi na uendeshaji wa elimu nchini. 



Maeneo mengine ni katika kujenga uwezo wa wasimamizi na watekelezaji wa mitaala, kuhakikisha upatikanaji wa vifaa bora na vya kutosha vya kufundishia, kujifunzia na uboreshaji wa majengo na miundombinu ambayo yanahitaji nguvu ya pamoja kati ya Serikali na wabia wake.



Katika moja ya mapendekezo yake Utafiti huo uliitaka Serikali 



kuona umuhimu wa kushirikiana na washirika na wadau wa elimu nchini, ili kuweza kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika sekta ya elimu.



Itakumbukwa kuwa hivi karibuni, Waziri Mkuu Pinda aliunda Tume kuchunguza kushuka kwa ufaulu kwa matokeo ya kidato cha nne, kitendo ambacho kilipingwa na baadhi ya wadau waliosema kuwa hakukuwa na haja ya kufanya hivyo, kwa sababu kila kitu kipo wazi.

Saturday, April 21, 2012

Familia ya PINDA Yahamia CHADEMA? (PICHA)

A PICTURE COULD TELL A MILLION WORDS: Dogo anaonekana akitoa alama ya V (for victory over mafisadi) huku Mtoto wa Mkulima akionekana kupigwa na bumbuwazi!

Friday, April 20, 2012

Kilio Kumwokoa tena Pinda?Anyway,yeye na Mawaziri Wake ni Dalili tu,Chanzo ni Kikwete

Waziri Mkuu Pinda akifanya usanii wa kulia bungeni katika sakata la maalbino.Je hatorejea tena mbinu hii?

Tusiume maneno.Tanzania hivi sasa inayomba kwa vile Rais tuliye nae,Jakaya Kikwete,ni mithili ya mtu asiyejua kwanini Watanzania walimpa dhamana ya kuongoza nchi yetu-moja ya nchi masikini kabisa duniani licha ya utajiri luluki ilionao.

Kikwete alifanya uzembe kwa kuteua rundo la mawaziri (ambapo ukubwa tu wa Kabineti yake ni mzigo mzito kwa nchi yetu masikini) lakini kana kwamba hiyo haitoshi,akajaza wababaishaji kibao ambao aidha ni maswahiba wake au kwa busara zinazomtosha yeye pekee aliwaona wababaishaji hao kama sehemu muhimu ya timu yake ya kuwaletea Watanzania MAISHA BORA.

Hivi Rais mwenye busara angeweza kumkabidhi Mustafa Mkulo Uwaziri wa Fedha ilhali historia yake huko nyuma inafahamika vyema?Well,Kikwete hakumpa Mkulo nafasi hiyo kimakosa bali kwa sababu maalum.Teuzi za Mawaziri wa Fedha Barani Afrika huzingatia sana ushkaji kati ya Rais na mteuliwa.Kimsingi,wengi wa mawaziri wa fedha wa Afrika ni kama wahasibu binafsi wa Rais.

Si kwamba Kikwete hajui ufisadi wa Mkulo na mawaziri wengine.HAPANA.Anafahamu fika ila hawezi kuchukua hatua kwa vile Mkulo hafanyi hivyo pasipo uelewa wa bosi wake.Hapa ninamaanisha kuwa kwa kiasi kikubwa,kinacholalamikiwa kuhusu Mkulo kina baraka za Kikwete.

Sijui Tanzania itakuwa katika hali gani wakati huyu mtu anamaliza muda wake hapo 2015!Cha kusikitisha zaidi,wakati nchi inazidi kuangamia yeye yuko bize kushindana na Christopher Columbus kwenye 'safari za uvumbuzi.'

Majuzi kapewa ripoti ya ukaguzi wa fedha za serikali na CAG Ludovick Utouh.Kana kwamba kilichomo kwenye ripoti hiyo ni salamu za hepi bethdei,siku chache baadaye Kikwete huyooo safarini Brazil.Hana habari kuwa nchi inaangamia.Yey na safari,safari na yeye.Basi bora amwondoe Waziri wa Mambo ya Nje,Bernard Membe,kisha yeye Kikwete ajiongezee wadhifa wa uwaziri huo ili akisafiri hata kila wiki tujue moja.

Back to the point ya kumwajibisha Pinda na/au mawaziri,well,kama wabunge watafanikiwa kutekeleza hilo itakuwa vema.Waiwasi wangu mkubwa ni unafiki wa wengi wa wabunge wa CCM.Japo Tanzania yetu inaanza kuonyesha dalili za watu kuchoka kuiona nchi ikigeuzwa shamba la bibi,napatwa na wasiwasi kama wabunge wa CCM watakauwa tayari kumtosa Pinda au kushinikiza mawaziri mafisadi wajiuzulu.Pinda ni msanii anayeweza kuwahadaa wabunge wa chama chake kwa kulia tena hadharani....nao wakalainika.

Lakini,hata kama Pinda na mawaziri mafisadi waking'olewa,bado tutaendelea kuwa na tatizo hapo juu kabisa-yaani Kikwete na urais wake wa sandakalawe (wa kubahatisha).Ameshauthibitishia umma wa Watanzania kuwa sio tu yeye ni dhaifu wa uongozi bali pia hana nia ya kurekebisha chochote dhidi ya kansa inayoitafuna nchi yetu.

Anyway,kama kura ya kutokuwa na imani na Pinda itafanikiwa nadhani hatua itakayofuata ni kura ya kutokuwa na imani na Kikwete mwenyewe.Actually,ni kwa sababu tu ya hizi taratibu za kirasimu za kupiga kura.Sidhani kama kuna Mtanzania yeyote mwenye akili timamu ana imani na Kikwete-hasa baada ya kushindwa kutekeleza hata ahadi alizojiwekea mwenyewe pasipo shinikizo lolote lile.Kitu pekee ambacho amefanikiwa kukitekeleza kwa ufanisi mkubwa ni mashidano yake dhidi ya Vasco da Gama na Christopher Columbus.

MUNGU INUSURU TANZANIA (kwa namna yoyote ile...hata kama ni kwa majonzi) 

Pinda Kumfuata Lowassa?


Pinda kumfuata Lowassa

• HATMA YA MAWAZIRI WATANO MIKONONI MWA JK

na Mwandishi wetu

WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda, sasa yuko katika hatari ya kuondolewa madarakani kwa kupigiwa kura ya kutokuwa na imani naye kufuatia tuhuma nzito za ubadhirifu wa fedha za umma unaodaiwa kuwahusisha mawaziri watano wakiongozwa na Waziri wa Fedha Mustafa Mkulo.

Akiwasilisha majumuisho ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, mwenyekiti wa kamati hiyo, Zitto Kabwe, aliliambia Bunge kuwa kuanzia leo wataanza kukusanya saini za wabunge wenye nia ya kupiga kura hiyo na kwamba uamuzi wake utawasilishwa bungeni Jumatatu wiki ijayo.

Mwenyekiti huyo alisema ikiwa mawaziri hao ambao hata hivyo hakuwataja majina mmoja baada ya mwingine hawatakuwa wamejiuzulu wenyewe hadi kufikia siku hiyo, basi wabunge watamwondoa Pinda madarakani kwa kumpigia kura ya kutokuwa na imani naye.

Kwa hali hiyo, Zitto alisema kuwa itakuwa ni jukumu la mawaziri hao kabla ya Jumatatu wiki ijayo kuamua wenyewe kujiuzulu au kumwacha waziri mkuu atimuliwe.

Hatua hiyo ya Zitto ilitokana na hoja iliyokuwa imetolewa mapema na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA), ambaye aliwataka wenyeviti wa kamati za Bunge wakati watakapokuwa wanajumuisha hoja zao kupendekeza kupiga kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu Pinda ikiwa mawaziri wake hawatakuwa wamejiuzulu wenyewe.

Lissu alisema wakati wa kupiga kelele umekwisha, na sasa wanachotakiwa ni kuchukua hatua, kwani mamlaka hiyo wanayo kwa mujibu wa Katiba.

“Waziri Mkuu wajibika kwa madudu ya serikali. Nitaomba wenyeviti wa kamati hizi wanapomalizia mjadala huu kupendekeza kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu kwa kujenga mfumo wa siasa wa udokozi. Tukifanya hivyo wananchi watatuamini. Ninyi chama tawala ndio mnaosababisha haya kama mtatumia wingi wenu sawasawa tutafanikiwa, sisi tupo wachache.

“Badala ya kupiga makofi, chukua hatua kwa uozo huu. Mkifanya hivyo mtaheshimika na msipofanya hivyo mtaingia kwenye vitabu vya historia,” alisema.

Alisema masuala ya ufisadi yamekuwa yakizungumzwa na zaidi ya miaka 10 sasa, lakini hawajawahi kuona serikali ikichukua hatua.

“Wakati kila mwaka CAG anatuletea taarifa za wizi, hatujawahi kuona serikali ikichukua hatua dhidi ya wahusika. Hatujawahi kuona mtendaji amechukuliwa hatua wala waziri kuwajibika katika hili. Watu wanapata kupata nafasi za uwaziri ili kuhujumu nchi,” alisema na kuongeza mfumo uliopo ni wa kulinda wezi.

Tanzania sio ya CCM

Akichangia mjadala huo, asubuhi na pia jioni, Mbunge wa Ludewa Deo Filikunjombe (CCM) aliwafyatua mawaziri kadhaa akisema kuwa wanaongoza kwa kutafuna pesa za Watanzania na kumtaja Waziri wa Fedha Mustafa Mkullo kuwa kinara wa wizi huo.

Mbunge huyo alisema baadhi ya mawaziri wamegeuka kuwa mchwa wanaotafuta fedha za Watanzania bila woga na kuongeza kuwa sasa umefika wakati kwa wabunge kuweka tofauti za kisiasa pembeni na kuzungumza kwa umoja masuala yanayoliangamiza taifa, na katika hilo akadai kuwa hatakuwa tayari kuwaachia mawaziri wachache waangamize nchi.

“Mheshimiwa Naibu Spika, inashangaza na kusikitisha kuwa nchi inatafunwa. Wanaofanya haya ni mawaziri wetu. Nchi inakufa na tuelewe kuwa Tanzania sio mali ya CCM, ni ya Watanzania wote.

“Mawaziri wetu wamekuwa mchwa, wanaangamiza nchi na leo nitamtaja waziri anayeongoza kwa kutafuta fedha za Watanzania. Ni Waziri wetu wa Fedha, Mustafa Mkulo. Ameuza viwanja, amelidanganya Bunge baada ya kuivunja CHC,” alisema mbunge huyo.

Awali Filikunjombe alisema Waziri wa Viwanda na Biashara, Cyril Chami, alikuwa amelidanganya Bunge kwa kudai amefuata maagizo yote ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC).

Alisema kuwa ana ushahidi wa kutosha jinsi mawaziri hao wanavyoitafuna nchi na kuhoji Bunge linachukua hatua gani inapobainika mawaziri wamelidanganya Bunge.

“Waziri Chami amedai kuwa ametekeleza agizo la kamati kuhusu uchunguzi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS). Uchunguzi ulifanywa wakati mkurugenzi alikuwa akiendelea na kazi, wakati kamati ilishauri wakati wa uchunguzi mkurugenzi huyo awekwe pembeni,” alisema.

Kutokana na kauli hiyo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, ambaye pia ni mnadhimu mkuu wa shughuli za serikali bungeni, alimtaka kuthibitisha madai kuwa mawaziri wote ni wezi kwa kukabidhi ushahidi na kama hana uhakika na anachozungumza afute kauli hiyo. Hata hivyo, mbunge huyo alisisitiza kuwa alichosema ni kwamba mawaziri wengi ni wezi na si wote.

Mbunge wa Kasulu, Moses Machari, alisema wabunge wanaotaka mawaziri na wabadhirifu kunyongwa wanafanya hivyo wakiwa na akili timamu kwa sababu wamechoshwa na wizi wa waziwazi unaofanywa na mawaziri na baadhi ya viongozi wa serikali bila kuchukuliwa hatua yoyote.

Kwa upande wake, Mbunge wa Musoma Mjini, Vicent Nyerere (CHADEMA), alitaja waziwazi majina ya vigogo wanaomiliki kampuni za ukaguzi wa magari ambazo zilitajwa bungeni kama ni za nje, hali iliyolifanya Bunge kuzizima kwa muda.

Nyerere alisema kuwa makampuni hayo yalilipwa mamilioni ya dola za Kimarekani kwa udanganyifu, na kibaya zaidi waziri mhusika akalidanganya Bunge akidai kuwa taarifa hizo zilikuwa za uongo. Alionyesha kushangazwa kwake na nguvu kubwa ya kumlinda Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Nchini (TBS) wakati ukweli wa mambo uko wazi.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Cyril Chami, alisema kuwa dhana iliyojengeka kuwa wizara hiyo inaibena TBS na mkurugenzi wake, haina ukweli, kwani taarifa ya kamati ndogo ya uchunguzi wa shirika hilo aliipata jana na ameshaiagiza bodi ya shirika hilo kuifanyia kazi.

Hata hivyo, alisema yuko tayari kuweka rehani uwaziri wake iwapo mbunge huyo atathibitisha kuwa kuna kampuni hewa zinazokagua magari nje ya nchi na iwapo kampuni hizo zina uswahiba naye.

“Nimekosea wapi? Kila nilichoagizwa nimetekeleza. Wizara halindi uozo. Tukilazimishwa kufanya maamuzi bila kufuata taratibu tutakuwa tunakiuka sheria,” alisema.

Ujasiri huo hata hivyo, uliyeyuka kama nta jioni, baada ya Nyerere kumuumbua kwa kutaja majina ya wamiliki wa kampuni hizo, hali iliyompa wakati mgumu waziri huyo.

Mbunge wa Nkasi, Ali Kessy (CCM), alishauri Rais Kikwete kuacha upole na kuwashughulia wote wanaotafuna mali za umma.

“Mawaziri walioshindwa kazi waondolewe na wawekwe wengine. Hakuna aliyesomea uwaziri kila mtu anaweza kuwa waziri. Unakuta kiongozi anatembea na msafara wa magari 40 unamtisha nani. Wakati watu hawana dawa wala chakula,” alisema.

Alisema kutokana na ubadhirifu huo, hata watendaji wa chini wa halmashauri wanakuwa na fedha nyingi kuliko halmashauri yenyewe, hali inayochangia kuiendesha serikali.

“Mafisadi wote tuwanyonge. Tukishanyonga 10 wataogopa. Leteni muswada mtu yeyote mwizi wa mali za umma anyongwe na mali itaifishwe. Tutaokoa nchi yetu. Wabunge tuwe wakali, lisiwe Bunge la mchezo mchezo,” alisema.

Mbunge wa Kigoma Mjini, Peter Serukamba, alisema kila wizara kuna mambo ya hivyo na kusema kinachoonekana mawziri hawajali suala hilo.

“Wabunge wa CCM twende kwenye Party Cacus tukafanye kazi tuliyotumwa. Kama kuna mtu atatulaumu basi, tuondoe waziri asiyefaa. Mbilinyi, Iddi Simba na Ngasongwa waliondolewa humu ndani. Tufanye kazi ya kibunge jamani. Nawaomba wabunge tufanye jukumu letu na tukifanya hakuna waziri atakayefanya mchezo,” alisema.

Wabunge waridhia vikao bila posho

Kutokana na uzito wa suala hilo, wabunge wameunga mkono hoja ya kuendelea na mjadala huo kwa kuongeza siku mbili zaidi hata kama vikao hivyo havitakuwa na posho.

Hoja hiyo ilitolewa na mbunge wa Buchosa, Dk. Charles Tizeba (CCM), ambaye alisema siku zilizotengwa kwa ajili ya kuchangia mjadala huo ni chache, hivyo wabunge wote walioomba kuchangia wanaweza wasipate nafasi.

“Mjadala huu ni muhimu sana, tunaomba kuongezewa siku mbili au tatu za kujadili suala hili hata kama hakuna posho tutafanya hivyo,” alisema Tizeba na hoja hiyo kuungwa mkono na nusu ya wabunge waliokuwapo ukumbini hapo.

Naibu Spika, Job Ndugai, alieleza kuwa hajawahi kuona hoja iliyoungwa mkono kama hiyo na kusema suala hilo atalifikisha kwa Spika, Anne Makinda, ambaye naye atajadiliana nayo na kamati ya uongozi na ndipo atakapotoa majibu kuhusiana na hoja hiyo.

Kwa upande wake, Mbunge wa Viti Maalum, Christowaja Mtinda (CHADEMA), alisema suala la mishahara hewa limekuwa sugu katika elimu ya juu na kwamba imefikia hatua jina lake limetumika katika suala hilo.

“Pale Open University kuna mtumishi anaitwa Christowanja Mtinda. Sijawahi kuomba kazi hapo wala kufanya kazi hata siku moja,” alisema.

Aidha, alisema makatibu wakuu hawakai katika nyumba zao zilizoko Dodoma na kusema kuwa wanazitumia wakati wa bikao vya Bunge na kuhoji kwa nini nyumba hizo wasipewe wabunge ambao wanapokuwa wanahudhuria vikao vya Bunge wanapata shida kupata nyumba za kuishi.

Naye Mbunge wa Kibiti, Abdul Marombwa, alishauri wabunge wapitishe sheria ya kuwapo kwa kamati kwa ajili mawaziri wanaoshindwa kuwajibika.

“Wenzetu wa Kenya wameanzisha sheria kwa ajili ya mawaziri wanaotoa ahadi zisizotekelezeka. Baada ya miezi miwili anaulizwa ametekeleza ahadi kwa kiwango gani, akishindwa anatimuliwa. Kenya wameshafukuza mawaziri. Tukianzisha hiyo mawaziri watahakikisha ahadi zao zinatekelezeka. Ni lazima tuwe na mahali pa kuanzia,” alisema.

Aidha, alihoji wizara kutumia fedha nyingi katika maonesho mbalimbali kama Sabasaba, Nanenane na utumishi na kuhoji yameleta manufaa gani nchini. Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, imetumia sh bilioni 1.9 kwa ajili ya maonesho kama hayo katika kipindi cha mwaka 2009/2010.

Mapema asubuhi, Zitto alikuwa ameliomba Bunge kutoa kumbukumbu za mwaka jana kutokana na Waziri Aggrey Mwanri kuendelea kutoa ahadi bila kuwapo kwa utekelezaji.

“Ukichukua ‘hansard’ ya mwaka jana ukasoma maelezo ya majibu ya hoja hayana tofauti na haya anayotaka kutuaminisha leo. Mheshimiwa Naibu Spika naomba kupata mwongozo wako tupate hansard ya mwaka jana ya maelezo ya Mheshimiwa Waziri ili tulinganishe na maelezo ya sasa na aliyotolewa mwaka jana na tuone kama ametekeleza,” alisema Zitto.

Zitto alitoa kauli hiyo, baada ya Waziri Mwanri kueleza serikali imekuwa ikiingilia kati maeneo ambayo yanaona hayaendi na kusema kuwa watakapoanza kushughulikia masuala yanayolalamikiwa na wabunge wasianze kushikwa mikono.

“Tunaomba wabunge tusaidiane; tuseme hakuna kumhamisha mtumishi yeyote aliyekwenda kinyume na tutamchukulia hatua hapo hapo,” alisema.

Aidha, alisema baraza la madiwani limepewa nguvu kushughulikia matatizo yote ya halmashauri husika na kuongeza kwamba hiyo ni vita iliyopangwa na isiyopangwa.

“Hilo rungu tumeshapewa. Tuachieni. Mrema naomba tuamini. Tukitoka hapa kazi ni moja kashi kashi tu...lugha hii inatokana na mazungumzo ya hapa ndani. Halmashauri zilizopata hati chafu, zimeshakabidhiwa barua, haiwezekani sh bilioni 6 zinaondoka halafu mkurugenzi anaendelea kuwapo,” alisema.

Hatma ya mawaziri kwa JK

HATMA ya mawaziri watano wanaotuhumiwa kwa ubadhirifu wa mali ya umma sasa iko mikononi mwa Rais Jakaya Kikwete, kufuatia hatua ya wabunge wa Chama cha Mapinduzi kutaka watendaji hao wajiuzulu.

Habari za kuaminika kutoka ndani ya kikao cha wabunge wa CCM kilichofanyika jana mchana mjini hapa zimesema kuwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, ameamua kulifikisha suala hilo mikononi mwa Rais Kikwete kwa uamuzi zaidi.

Chanzo chetu cha kuaminika kutoka ndani ya kikao hicho, kimewataja wabunge wanaotakiwa kujiuzulu kuwa ni pamoja na waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo, Waziri wa Viwanda na Biashara, Cyril Chami, na Naibu wake, Lazaro Nyalandu, Waziri wa Fedha, Waziri Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi),George Mkuchika, Waziri wa Uchukuzi, Omar Nundu na Waziri wa Afya, Dk. Haji Mponda.

Katika kikao hicho cha dharura kilichokuwa chini ya uenyekiti wa Waziri Mkuu Pinda, wabunge hao walisema mawaziri hao wameiaibisha serikali kwa kiwango kikubwa, hali iliyosababisha wananchi kukosa imani na serikali yao na kuichukia.

Kikao hicho kilichoanza saa 7 mchana na kumalizika saa 11 jioni kilikuwa na mvutano mkali kati ya wabunge hao na mawaziri.

Tuesday, January 31, 2012

EXCLUSIVE TO KULIKONI UGHAIBUNI: Rais Kikwete Azungumzia Kauli ya Pinda Kuhusu Posho za Wabunge


Rais Jakaya Kikwete amekiri kuwepo kwa mkanganyiko uliojitokeza kufuatia kauli ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuwa Rais ameridhiria nyongeza ya posho za Wabunge.Rais alisema hayo katika majadiliano kati yangu na yeye kupitia mtandao wa Twitter kama inavyoonyesha picha hapa juu na hapa chini


Awali,Rais Kikwete alifafanua kuwa ni kweli alitoa maelekezo kuhusu suala la posho hizo lakini maelekezo hayo hayakuwa kuridhia jambo hilo.Kadhalika,Rais alibainisha kwamba alikubali haja ya kuangalia upya posho za wabunge na aliwataka wabunge kutumia hekima na busara katika kutafakari.Vilevile aliwataka wabunge kutumia Kikao cha Februari cha Bunge kulizungumzia upya suala hili,na kusistiza ni muhimu.Picha ifuatayo inaonyesha maelezo hayo ya Rais Kikwete kwenye mtandao wa Twitter.


Jana,gazeti la Mwananchi lilikuwa na habari iliyobeba kichwa 'JK ABARIKI POSHO MPYA ZA WABUNGE' ambapo pamoja na mambo mengine habari hiyo ilieleza kuwa Waziri Mkuu Pinda amesema kuwa tayari Rais Kikwete amesaini kuridhia ongezeko la posho za vikao (sitting alllowances) kwa wabunge kutoka shilingi 70,000 hadi shilingi 200,000 kwa siku.Picha ifuatayo inaonyesha sehemu ya habari hiyo:


Hata hivyo,mapema leo Kurugenzi ya Mawasiliano ya Ikulu ilitoa taarifa ya maandishi kukanusha habari hizo, kama inavyosomeka hapa chini

Taarifa Ya Ikulu

Blogu hii inaendelea kufatilia kwa karibu kuhusu suala hilo.

Friday, September 02, 2011

Tafakuri ya Nova Kambota: Pinda Kubali Kufa Ili Uione Pepo


Na Nova Kambota,
Namkumbuka mwanamuziki wa kizazi kipya Seleman Msindi maarufu kama Afande sele na kile kibao chake cha “Darubini kali” anapohoji “kama unapenda pepo kwanini uogope kifo?”
Tungo hii kwa namna ya pekee inamgusa waziri mkuu wa Tanzania Mh Mizengo Pinda maarufu kama “mtoto wa mkulima” ndiyo namuuliza Pinda ataonaje pepo pasipo kufa kwanza?
Tangu kuteuliwa kwake mara baada ya Edward Lowassa kujiuzulu, Kwa wale wanaomjua Pinda walishasema kuwa “Pinda atapwaya sana”, sasa ikiwa ni takribani miaka mitatu na nusu tayari mambo hadharani kuwa Pinda “kashindwa kazi”
Kwa wasiomjua Mizengo Pinda tafuteni ukweli mtamjua tu, ni Mizengo Pinda huyu amebaki kuwa mshauri wa Kikwete badala ya waziri mkuu kufikia hatua ya kutamka bungeni kuwa hana mamlaka, ni Pinda huyu asiye na makundi lakini anakubali kumezwa na mitandao na makundi ya CCM na bosi wake Kikwete na sasa nimeanza kusikia watu wakimwita ni “mtoto wa mkulima anayeishi kibilionea”
Hakuna ubishi kuwa hata watetezi wachache wa Pinda waliobaki sasa wamefadhaishwa na udhaifu wake kama sio uwoga wa kupindukia, “jeuri” ya Luhanjo na sakata la Jairo limemwaka njia panda Mizengo Pinda, amebaki kujiumauma na kutapatapa tu, kadhalilishwa lakini hataki kuchukua hatua, katukanwa lakini anachekelea! Huyu ndiye Mizengo Pinda.
Waziri mkuu Pinda akiongelea sakata la Jairo akajiapiza kuwa angekuwa na mamlaka angemfukuza kazi Jairo kwa maana nyingine Pinda amekiri kuwa Jairo anastahili adhabu na serikali haikutaka kumwangusha waziri mkuu “ikamtwanga likizo ya malipo” Bw Jairo lakini ghafla katibu mkuu kiongozi anaibuka na kumdhalilisha waziri mkuu eti Jairo hana kosa arudi kazini, wakati Pinda akisita kuchukua hatua wabunge kwa umoja wao wameamua kumtetea waziri mkuu kwa kudhalilishwa sasa Bunge limeunda kamati.
Hivi katika mduara huu wa “kudhalilishana na kushushiana heshima” ipi nafasi ya Pinda? Yapi maamuzi ya Pinda? Kichekesho ni kuwa Pinda “yupoyupo tu” hajachukua uamuzi na dalili zinaonyesha kuwa kwa mara nyingine tena Pinda amekubali kupiga magoti na kujishusha sehemu aliyotakiwa apigiwe  magoti yeye huyu ndiye Pinda ambaye bilashaka hata “ukimpiga ngumi” yeye wakati wa kukurudishia lazima atavaa gloves ili asikuumize.
Pinda anataka pepo? Anataka watanzania tumkumbuke kuwa ni kiongozi jasiri? Basi hana budi kufa ili aione hiyo pepo! Naam amedhalilishwa sana, ameshushiwa hadhi yake, na sasa ni wakati wayeye kufikiria kujiuzulu.
Haiwezekani Luhanjo na Pinda waendelee kuitumikia serikali moja, hiki kitakuwa ni kiinimacho , ni lazima mmoja wao atoke, na kwa vile wote tunakubaliana Pinda anaitamani pepo, anataka kukumbukwa mioyoni mwa watanzania, lazima aachane na serikali hii ya akina Luhanjo na Jairo, hana budi kumwachia Kikwete ateue waziri mkuu mwingine ambaye atakubali kuvunjiwa heshima, Naam! Pepo haiji hivihivi, ni lazima Pinda afe leo ili aione pepo kesho!

Nova Kambota Mwanaharakati,
+255717 709618
Tanzania, East Africa,
Alhamisi, September 1, 2011.

Friday, June 24, 2011

Pinda Apata Mrithi: Jaji Aangua Kilio Baraza Maadili,Ashindwa Kujitetea

Waziri Mkuu Pinda akimwaga machozi Bungeni mwaka 2009
Kwa kifupi tu,Jaji mtajwa katika habari ifuatayo hastahili kuendelea na wadhifa wake.Hili ndio tatizo la kuteua majaji weeeengi mpaka wababaishaji kama hawa wanapata fursa.Pia habari hii imenikumbusha lile tukio la Waziri Mkuu Mizengo Pinda kulia Bungeni alipobanwa kuhusu kauli yake kuhusu wauaji wa maalbino (aliropoka kuwa wauaji hao nawe wauawe)

Jaji aangua kilio akijitetea
Thursday, 23 June 2011 21:49

Hadija Jumanne
JAJI Atuganile Flora Ngwale wa Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam kitengo cha Ardhi, jana alishindwa kujitetea kuhusu kushindwa kwake kujaza fomu zinazohusu mali na madeni yake, kwa mujibu wa sheria ya maadili ya viongozi wa umma.

Jaji huyo alishindwa kufanya hivyo mbele ya Baraza la Maadili ambako aliangua kilio na hivyo kusababisha wanasheria kushindwa kumhoji.

Hali hiyo ililazimisha baraza kusitisha usikilizaji wa shauri hilo.Wakati akiangua kilio, jaji huyo alilieleza baraza kwamba alishindwa kujaza fomu hizo na kuomba msamaha.Wakati akiangua kilio, jaji huo alisema "sina mali yoyote, kazi ndio maisha yangu, watoto wangu wanategemea kazi hii siwezi kudharau mtu, naomba mnisamehe, nimejifunza Mungu wangu,"alisema jaji huyo.

Jaji Ngwale alisimama katika baraza hilo ili kuanza kujitetea, lakini ghafla aliangua kilio kwa sauti ya juu huku akiomba baraza hilo limuonee huruma kwa kutojaza fomu."Ni kweli sijajaza fomu na kama kuna mtu aliniona nimejaza fomu hizi ajitokeze ndani ya baraza hili la maadili," alisema.

"Kazi hii ndio maisha yangu, kazi hii ndio faraja ya watoto wangu hivyo naitegemea sana sina mali zozote za kunitesa na kuniita katika Baraza la Maadili,"alisema Ngwale huku akimwaga machozi.

Baada ya Barazakuona Jaji Ngwale ameshindwa kujitetea kwa njia ya mdomo, lilimtaka atoe utetezi wake kwa njia ya maandishi na kulazimika kusitisha kuendelea na shauri hilo.Mbali na baraza hilo kusitisha kuendelea kusikiliza shauri hilo, pia wanasheria wa sekretarieti ya maadili na hawakupata nafasi ya kumhoji Jaji Ngwale kutoka na hali hiyo.

Baada ya baraza hilo kusitisha kuendelea kusikiliza shauri hilo walimuomba jaji huyo aondoke mbele ya baraza hilo, lakini jaji huyo alikaidi agizo la wanasheria hao na badala yake aliendelea kulia mpaka baraza hilo lilipomuomba mmoja wa wanasheria ambembeleze na baada ya kubembelezwa alikubali kwenda kutoa maelezo yake kwa njia ya maandishi na baadaye aliruhusiwa kuondoka.

Baraza hilo litaendelea leo kwa ajili ya kuhoji watu wanne ambao hawakujaza fomu hizo za maadili ya umma mwaka jana, miongoni mwa watu hao watakaohojiwa ni pamoja na Diwani wa Kata ya Kanazi Mathias Bisoma Mgatta, Mkurugenzi wa Shirika la Hifadhi ya Jamii la Taifa (NSSF), Crecencius Magori.

Wengine ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Tafiki Mwanza, Francis Bayona Katunzi na Diwani wa Mpanda mjini Ally Juma Nsokolo.

CHANZO: Mwananchi

Saturday, June 18, 2011

Mtoto wa Mkulima Ovyoo: Kila jambo SIJUI,SIJUI...Anajua Nini?




Pinda: SIJUI Waziri Nahodha anaishi hotelini

na Martin Malera, Dodoma

WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda, amesema hajui kama Waziri wa Mambo ya Ndani, Shamsi Vuai Nahodha, anaishi hotelini.

Kauli hiyo aliitoa jana bungeni baada ya kuulizwa swali na mbunge wa Chambani, Salim Hemed Khamis (CUF), alihoji dhamira ya serikali kupunguza matumizi.

Mbunge huyo alihoji kwa nini Waziri Nahodha anakaa hotelini wakati serikali ina nia ya kupunguza matumizi yasiyo ya lazima.

“Kuna mawaziri wanaishi hotelini tangu walipoteuliwa hadi sasa, serikali haioni kama hali hiyo ni kikwazo kwa mafanikio ya Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano tulioupitisha hivi karibuni Bungenin?” alihoji mbunge huyo.

Akijibu swali hilo, Waziri Mkuu Pinda kwanza alionekana kushangazwa na taarifa hiyo na baadaye alimtaka mbunge huyo ataje majina ya mawaziri anaowajua wanaioshi hotelini hadi sasa tangu walipoteuliwa.

Mbunge huyo alitaja jina la Waziri Nahodha.

Huku akiwa haamini na kumkazia macho Waziri Nahodha, Pinda alijibu kwa kifupi tu: “Basi nimesikia.”

Katika hatua nyingine, Spika Anna Makinda, alimzuia Waziri Mkuu Pinda kujibu maswali ya Mbunge wa Singida Vijijini, Tundu Lisu, na Esther Matiku wote CHADEMA, yaliyohusu mauaji ya raia katika mgodi wa kampuni ya Barrick, Tarime mkoani Mara

CHANZO: Tanzania Daima
Katuni kwa hisani ya Kipanya 

Sunday, May 22, 2011

Mahojiano kati ya Waziri Mkuu Pinda na Urban Pulse (PICHA)



URBAN PULSE CREATIVE Ilipata fursa ya kufanya mahojiano maalum na MH Waziri Mkuu Mizengo Pinda alipokuja katika Ziara yake hapa nchini Uingereza siku chache zilizopita. Mahojiano hayo maalum yalilenga zaidi kuelemisha jamii yetu ya kitanzania, vile vile kutoa Msimamo kutoka katika serikali yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusiana na mambo mbalimbali yanayomhusu Mtanzania .

Mahojiano hayo yaligusa maeneo tofauti yakiwepo majukumu pamoja na changamoto anazokumbana nazo Mh waziri mkuu, Suala la katiba, Uchumi, Rushwa na Ufisadi, Miundo Mbinu, Maendeleo, Chakula, Nishati, Jumuiya ya Africa mashariki pamoja na mambo mengine mengi.Mahojiano yalifanywa na Baraka Baraka Kutoka URBAN PULSE CREATIVE MEDIA na yatarushwa hewani mda sio mrefu.

MUNGU IBARIKI AFRICA, MUNGU IBARIKI TANZANIA

Asanteni,

URBAN PULSE CREATIVE MEDIA

Saturday, April 09, 2011

Tanzania Karne ya 21: Afya Mikononi mwa Babu Loliondo na Ambulance za bajaji

Waziri Mkuu Mizengo Pinda akikodolea macho ambulance ya bajaji.Labda macho yangu tu lakini naona kama Pinda hana hakika kama tupo karne ya 21 au tunarejea Zama za Mawe!
Na mwenye dhamana ya afya ya Watanzania kwa sasa ni Babu wa Loliondo.

HII NDIO TANZANIA ZAIDI YA UNAVYOIJUA

Monday, February 22, 2010

Pinda Ambeba Rostam

WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amewashauri wananchi wa Jimbo la Igunga mkoani Tabora wasimkatae Mbunge wao Rostam Aziz wakati wa uchaguzi mkuu ujao kwa kusikia maneno yanayosemwa bungeni, badala yake wazingatie kile alichowafanyia.

Wakati Pinda anampigia debe Mbunge huyo jana kwenye mkutano wa hadhara katika uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine, baadhi ya wananchi wa jimbo hilo walimwomba Waziri Mkuu amshinikize Mbunge wao abaki jimboni humo, kwa madai kuwa haonekani.

Wananchi hao walitoa ombi hilo ili waweze kupata fursa ya kumweleza kero zao na awaeleze yanayosemwa bungeni kuhusu yeye (Rostam)...ENDELEA


Thursday, April 30, 2009

PINDA: MISHAHARA YA WABUNGE (MILIONI 7 KWA MWEZI) HAITOSHI


na Ratifa Baranyikwa, Dodoma

WAKATI Bunge zima likimwandama Mbunge wa Karatu, Dk. Wilibrod Slaa (CHADEMA), kutokana na msimamo wake kuwa posho za wabunge ni kubwa na kutaka zipunguzwe, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ameungana na wabunge wengine kwa kusema kuwa posho hizo ni ndogo na kutaka ziongezwe.

Ingawa hakutaja jina, lakini kauli hiyo ya Waziri Mkuu imeonekana dhahiri kumjibu Dk. Slaa anayetaka mishahara na posho za wabunge zipunguzwe, kwamba ni kubwa mno ukilinganisha na watumishi wengine wa umma.

Pinda aliyasema hayo jana mjini hapa wakati akizindua mpango mkakati wa Bunge wa miaka mitano, wenye nia ya kulifikisha Bunge katika kiwango cha juu cha ufanisi.

Katika uzinduzi huo uliofanyika katika Ukumbi wa Pius Msekwa mjini hapa, Pinda alitumia mwanya huo kuchomeka suala la posho za wabunge, ambalo limekuwa agenda kubwa katika mkutano wa 15 wa Bunge unaomalizika leo.

Akielezea hatua ambazo serikali imekuwa ikizifanya kwa upande wa Bunge, Pinda ambaye aliorodhesha hatua kadhaa za kuboresha maslahi ya Bunge, alisema lengo la serikali ni kuboresha maslahi na posho za wabunge ambazo kwa sasa bado ni ndogo.

“Lengo la serikali kwa Bunge ni kuboresha maslahi na posho za wabunge ambazo kwa kweli kwa sasa hazifikii stahiki, lengo ni kuhakikisha Bunge linaboreshewa maslahi ili liweze kufanya kazi yake stahiki na kwa kiwango cha kuridhisha,” alisema Pinda.

Awali, akizungumzia malengo makubwa saba ya mpango mkakati huo, alisema moja ya malengo hayo ni kuboresha maslahi na stahiki za wabunge ili kuliwezesha Bunge kutekeleza majukumu yake ya kikatiba ipasavyo.

Mbali na malengo hayo, mengine ya mkakati huo ni kuboresha muundo na utendaji wa ofisi za Bunge ili kuongeza ufanisi na uwajibikaji, pia kuboresha mazingira ya utendaji kazi ya sekretarieti ya Bunge.

Limo pia suala la kukuza na kuimarisha ushiriki wa Bunge kuwafikia wadau mbalimbali kupitia mikutano, machapisho, vyombo vya habari na njia nyingine ya mawasiliano, pamoja na kukuza na kuinua vipaji vya wabunge.

Kwa upande wa serikali, mbali na malengo ya kuboresha maslahi na posho za wabunge kwa kuzingatia mazingira ya utendaji wao wa kazi, na hali ya uchumi, Pinda pia aliyataja malengo mengine kuwa ni kuwezesha Bunge kuwa na ukumbi mzuri wa kisasa unaotosheleza mahitaji, lengo ambalo kwa sasa tayari limekwishatekelezwa.

Kwa mujibu wa Pinda, lengo lingine ni kuanzishwa kwa mfuko maalumu wa Bunge ambao ulianza kutumika mwaka 2007/08, kuwashirikisha katika ziara za nje za viongozi wa kitaifa, lakini pia kuharakisha ujenzi wa ofisi za wabunge katika majimbo yao.

Tangu alipotoa kauli hiyo akiwa kwenye moja ya mikutano ya chama chake cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Slaa ambaye pia ni Katibu Mkuu wa chama hicho, amekuwa akiandamwa na wabunge wenzake katika mkutano huu wa 15, wakipinga hoja hiyo kwa madai kuwa inawachonganisha wabunge na jamii.

Hali hiyo ilisababisha Dk. Slaa afikie hatua ya kuzomewa mara kadhaa kila jina lake linapotajwa kwenye vikao vya ndani na nje.

Mbunge huyo, hata hivyo, alisisitiza kwamba anasimama katika hoja zake, ikiwamo ya posho za wabunge kutaka kutazamwa upya.

Alisema ataendelea kuisimamia hoja hiyo kwa sababu anataka kuwapo kwa uwazi katika mishahara wanayolipwa viongozi mbalimbali wakiwamo wabunge.


Friday, January 30, 2009

MACHOZI YA PINDA BUNGENI YALAINISHA HOJA YA KUMTAKA AJIUZULU

Zaidi,SOMA HAPA.

Sunday, January 25, 2009

"JINO KWA JINO",KUFUTA LESENI ZA SANGOMA KUTAKOMESHA MAUAJI YA MAALBINO?


Hatimaye katika kukabiliana na wimbi la mauaji ya albino,Waziri Mkuu Mizengo Pinda ameagiza leseni za waganga wa jadi wote zifutwe.Majuzi,Pinda alikaririwa akiagiza wananchi kuchukua sheria mkononi kwa kuwaua "wauaji wa maalbino".Hatua zote mbili zinaweza kutofanikiwa kwa vile inaelekea kana kwamba zimechukuliwa pasipo kufanyiwa utafiti wa kina.


Kuruhusu wananchi wafanye "jino kwa jino" dhidi ya wanaoua maalbino kunaweza kulipeleka Taifa mahala pabaya.Taasisi pekee yenye mamlaka ya kuhukumu ni mahakama zetu,na hizo ndio zinazoweza kuhakiki makosa halasi tofauti na majungu,chuki,visasi,nk na haki inatarajiwa kuwa imetendeka pindi hukumu itapokuwa ya kifo au mshtakiwa kuachiwa huru kulingana na ushahidi uliowasilishwa mahakamani.Hilo haliwezekani katika "mahakama za jino kwa jino mitaani".Si ajabu watu waliokosana kwa sababu zao binafsi wakishia kupigana mapanga kwa kisingizio cha "kudhibiti mauaji ya maalbino".Ikumbukwe kuwa ni rahisi kuruhusu uvunjifu wa sheria lakini ni zaidi ya vigumu kurejesha heshima na utiifu kwa sheria.


Tuje kwa hili la kufuta leseni za waganga wa jadi.Je amri hii inamaanisha ni marufuku kwa mtu yeyote kujihusisha na uganga wa jadi au...?Sijaelewa vizuri hapo lakini nahisi inamaanisha hivyo kwani katika hali ya kawaida,kufanya shughuli inayohitaji leseni pasipo kuwa na leseni husika ni uvunjifu wa sheria.Swali la kwanza,hivi ni waganga wa jadi wangapi wenye leseni (tukiachana na hao Maprofesa wanaojitangaza kwenye magazeti kuwa wanatibu ukimwi,wanawezesha kufaulu pasipo kusoma,na miujiza mingine)?Nauliza hivyo kwani haitaleta mnaana yoyote kumfutia mtu leseni ambayo hajawahi kuwa nayo hata siku moja.Swali la pili,je utekelezaji wa amri hiyo utasimamiwa vipi?Polisi watazungukia mganga mmoja hadi mwingine nchi nzima kuhakikisha kuwa hafanyi uganga?
Swali la tatu,je tumefikia hatua ya kufanya maamuzi kwa kigezo cha "samaki mmoja akioza basi wote wameoza"?Nauliza hivyo kwani tafsiri ya moja kwa moja ya kuwafutia leseni masangoma ni kwamba wao ndio wahusika muhimu katika suala la mauaji ya maalbino.Hii "overgeneralization" inatoka wapi?Mbona wale wazembe wa Muhimbili walipompasua kichwa mgonjwa wa goti na wa goti akapasuliwa kichwa walioadhibiwa ni madaktari husika tu na sio kada nzima ya madaktari hapo Muhimbili au nchi nzima?Au mbona ilipobainika kwamba kuna uhuni umefanyika pale BoT kwenye ishu ya EPA,aliyefukuzwa kazi ni Ballali pekee na wengine wameendelea kuwa madarakani hadi leo?Au mbona aliyekuwa balozi wetu huko Italy alipokumbwa na tuhuma za ubadhirifu wa fedha za umma haikupelekea kutimua mabalozi wote?Sasa iweje "uhuni" wa baadhi ya waganga wa jadi upelekee hukumu kwa wote wanaohusika kwenye taaluma hiyo (na yayumkinika kusema kuwa wengi wao-hususan vijijini-ni waadilifu katika kazi yao)?


Naomba nisisitize kwamba hapa simaanishi two wrongs make a right.Hapana,najaribu kuangalia approaches za nyuma katika kukabiliana na matatizo mbalimbali na namna zinavyokinzanna na hii ya ku-revoke leseni za waganga wa jadi.


Kwa wanaofahamu umuhimu wa tiba asili katika jamii husasan katika kipindi hiki cha uchangiaji wa gharama kwenye public health facilities,ni dhahiri hatua ya kuwafutia leseni waganga wote wa jadi itaathiri Watanzania wengi wanaotegemea huduma hizo (aidha kutokana na imani,nature ya maradhi yao au uwezo duni katika kumudu gharama za huduma za afya hospitalini).


Japo ni muhimu sana kutafuta ufumbuzi wa haraka kukomesha mauaji dhidi ya maalbino,ni muhimu zaidi kutumia common sense and viable approaches kuliko hatua ambazo pamoja na nia zake nzuri zinaweza kutuletea matatizo zaidi.Tukirihusu sheria zivunjwe kwa kuruhusu kuua wanaoua maalbino (badala ya kuwafikisha kwenye vyombo vya dola) basi tusishangae pindi baadhi ya wananchi watakapoamua kuchukua sheria mkononi dhidi ya mafisadi,kwa mfano,badala ya kusubiri kesi zilizoko mahakamani,ripoti za tume,nk

Friday, January 23, 2009

PINDA ATAKA JINO KWA JINO DHIDI YA WANAOUWA ALBINO


KATIKA hali ya isiyo ya kawaida, Waziri Mkuu Mizengo Pinda jana aliwaambia wananchi kuwa wanaoua watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) pamoja vikongwe ni hawana budi kuuawa kwa kuwa wakisubiri mahakama kuwahukumu, watakuwa wanakosea.

Waziri Pinda, ambaye ameanza ziara katika mikoa ya Kanda ya Ziwa yenye lengo la kuhamasisha vita dhidi ya mauaji ya vikongwe na albino, aliutaka Umoja wa Vijana wa CCM kuongoza vita hiyo, akisema lina jeshi zuri. Mauaji ya albino yamekuwa ni tatizo kubwa nchini na hasa katika mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Pamoja na serikali kutangaza hatua kadhaa za kupambana na wauaji hao, bado matukio ya kuuawa kwa watu hao wenye ulemavu wa ngozi yamekuwa yakiendelea kuripotiwa,
lakini Waziri Pinda ameenda mbali zaidi katika kukabiliana na tatizo hilo alipotaka wauaji hao wauawe badala ya kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria.


Kauli ya Pinda, ambayo inaweka maswali katika suala la utawala bora, imekuja wakati ambao wananchi wamekuwa wakijichukulia sheria mkononi na kuua vikongwe kutokana na imani za uchawi. Akihutubia wakati wa kufungua mkutano wa 16 wa Shirikisho la Vyama vya Kuweka na Kukopa (SCCULT) kwenye ukumbi wa Chuo cha Utumishi Umma mkoani hapa, Waziri Pinda alisema iwapo wananchi wataendelea kuwahurumia wauaji hao ambao wanatafuta viungo vya albino wakitegemea mahakama itatenda haki huku nao wakiongeza kasi ya mauaji kwa Watanzania, watakuwa wanakosea.


Hivyo alisema kwamba kuanzia sasa mtu yeyote atakayemuona mtu amemkata shingo au mkono mweziwe basi naye auawe papo hapo hii itakuwa ndiyo dawa kwani vingozi wote tumechoka na mauji hayo.


"
Mkimuona mtu akamkata mwingine shingo naye muueni kwani sasa viongozi wote tumechoka... no more, I can't tolerate anymore (imetosha, siwezi kuvumilia tena)," alisema Pinda huku akiwaacha watu midomo wazi.


Aliviomba vyama vya siasa kushirikiana na wananchi kuhakikisha suala hili la mauji linakwisha kwani wauji "tunaishi nao na ni rahisi kulimaliza iwapo tutakuwa kitu kimoja katika kuondoa kashifa hii ambayo imekuwa mbaya kwa nchi yetu".


Aliuagiza Umoja wa Vijana wa CCM kuhakikisha mauaji hayo yanatokomezwa kabisa, akisema kuwa ni jeshi zuri ambalo likiamua kutokomeza kabisa mauaji ya vikongwe na ndugu zetu maalbino inawezekana.


"Umoja wa vijana mna jeshi zuri ambalo naamini mkiamua mnaweza kutokomeza mauaji ya wazee wetu pmoja na ndugu zetu maalbno na kazi hiyo nawaagiza muanze leo msisubri auawe mwingine tena
," alisema waziri mkuu.


Baada ya kumalizika kwa mkutano huo, baadhi ya watu wanaoonekana kuwa ni wa "serikali" waliwafuata baadhi ya waandishi wa habari, akisihi suala hilo lisiripotiwe magazetini kwa madai kuwa kauli hiyo ya Waziri Pinda inaweza kusababisha matatizo.



Rais Jakaya Kikwete, ambaye pia amekuwa mstari wa mbele kupiga vita mauaji hayo, alitofautiana na Waziri Pinda katika moja ya hotuba zake aliposema kuwa adhabu ya kuua haitofautishi muuaji wa albino na muuaji mwingine na kwamba watakaopatikana na hatia ya kuua albino, atakabiliana na adhabu ya kifo kama ilivyo kwa muuaji mwingine.


Waziri Pinda alionekana kukerwa na mauaji ya albino wakati alipopata taarifa kwamba kuna mama mwingine aliuawa usiku wa kuamkia juzi.


"Nimeambiwa kuwa juzi wilayani Sengerema kuna mama mmoja ambaye ni mlemavu wa ngozi amekatwa mkono na wauaji wakaondoka na mkono huo na tayari mama huyo amekufa," alisema Pinda na kusisitiza kushughulikia wauaji hao. Akitoa takwimu za mauaji ya vikongwe na malbino alisema mwaka 2003 waliuwawa vikongwe 517, mwaka 2004 waliuawa vikongwe 444, mwaka 2005 (494), 2006 (vikongwe 386), mwaka 2007 (vikongwe 526) na albino sita na mwaka 2008 (vikongwe 526 na albino 28). Alisema tayari mwaka huu wameuawa albino watatu hivyo kufanya albino na vikongwe waliouawa kufikia kuwa jumla 2,900.


Waziri mkuu ameanza ziara ya siku nne kutembelea mikoa ya Shinyanga, Tabora na Mwanza ili kuhamasisha wananchi watokomeze vitendo vya mauaji ya vikongwe na watu weye ulemavu wa ngozi.


CHANZO: Mwananchi

WHILE NOT CONDONING THE EVIL DEEDS BY THOSE WHO KILL THE ALBINOS ,I JUST DON'T SEE HOW THIS "AN-EYE-FOR-AN-EYE STYLE OF RULE OF LAW" COULD BE EFFECTIVE IN ELIMINATING THIS PROBLEM!I'M EVEN MORE SCARED OF A POSSIBILITY THAT UVCCM MIGHT TURN THIS THING INTO A POLITICAL CRUSADE...CLAIMING CHADEMA ARE BEHIND THE ALBINO KILLINGS,FOR INSTANCE...WE ALL KNOW HOW DIRTY OUR POLITICS GETS WHEN THE YOUTH WINGS OF OUR PARTIES ARE MOBILIZED TO EXHAUST WHATEVER MEANS THEY HAVE TO ADDRESS SOME SENSITIVE ISSUES IN OUR SOCIETY...

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Hot Sonakshi Sinha, Car Price in India