Featured Posts

Showing posts with label MWAKYEMBE. Show all posts
Showing posts with label MWAKYEMBE. Show all posts

Sunday, October 16, 2011

Afisa Usalama wa Taifa Ahusishwa na Njama za Kumdhuru Mwakyembe




Tuhuma za kuuawa kwa Mwakyembe na wenzake kwa IGP na Mwandishi wetu FEBRUARI 8, mwaka huu, Dk. Mwakyembe alizungumza na baadhi ya viongozi waandamizi wa Jeshi la Polisi makao makuu ya jeshi hilo jijini Dar es Salaam. 

Baada ya maelezo hayo, polisi walimtaka aweke madai yake kwenye maandishi na siku moja baadaye Dk. Mwakyembe aliwasilisha taarifa yake ya maandishi. 

Dk. Mwakyembe amesema kwenye barua hiyo, “Pamoja na kwamba taarifa hii ni mpya yenye matukio ya takriban mwezi moja tu, naamini kwa dhati kuwa msingi wake (kwa maana ya wahusika na maudhui) hautofautiani na ule wa matukio mengine ya awali ambayo baadhi yake yalisharipotiwa polisi na vyombo vingine vya usalama kwa lengo la kuchunguzwa. 

Maelezo ya Barua ya Mwakyembe “Bado nina imani kubwa na Jeshi letu la Polisi kwamba litaifanyia kazi taarifa hii bila kujali nguvu ya ukwasi na ya kisiasa ya watuhumiwa na kwa kuzingatia misingi ya haki na ukweli. 

“Msingi wa mimi kushtuka na kuamua kulivalia njuga suala hili kwa kuwataarifu watu mbalimbali wenye uelewa na kuvitaarifu vyombo vya dola, ni taarifa nilizozipata kutoka Songea Januari 22, 2011 kuhusu kundi la watu saba lililoingia mjini humo usiku wa Januari 21, 2011 kwa gari iliyodaiwa kuwa ya wizara yangu (Ujenzi) aina ya Land Cruiser yenye usajili nambari STK 68… (ambayo kipindi fulani katika safari hiyo ilibadilishwa namba yake kuwa STK 68…). 

Gari hiyo iliwateremsha “abiria” hao saba sehemu iitwayo Madaba na baadaye kuchukuliwa na gari nyingine (Hardtop Land Cruiser yenye namba za usajili T7…BDU) hadi Top Inn ya mjini Songea. “Majina ya baadhi ya watu hao saba ni Wasomali wawili Hafidh na Faraj; kijana wa Kichagga kwa jina Mustafa a.k.a “Master”; Mkusa, jamaa ambaye wenzake wanaamini kuwa yuko Usalama wa Taifa; na mtu mwingine (jina tunalo) kutoka Tanga anayedaiwa kuwa na utaalamu mkubwa wa kukaba watu. 

“Mwenyeji aliyewapokea Songea watu hao saba ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya (kaitaja) akiongozana na mtu aitwaye Manya. Kilichowafanya baadhi ya watu waanze kulidadisi kundi hili ni dhamira ya safari yao. Tetesi zilisema walikuwa wanaelekea Mbunde kwa mganga maarufu wa kienyeji kwa jina (linahifadhiwa). Hivyo, udadisi ukaongezeka kujua nani anakwenda “kulogwa” safari hii. 

Tetesi zikarejea na jina langu na msululu wa majina mengine: Dk. Slaa (Willibrod), Anne Kilango - Malecela, Reginald Mengi, Profesa Mwandosya na Benard Membe. “Pamoja na kwamba sina imani na ushirikina au nguvu za giza, kutajwa kwa jina langu na fursa ya pekee niliyokuwa nayo ya kujua kilichokuwa kinafanyika, kukanipa ari, nguvu na shauku ya aina yake kutaka kulielewa zaidi suala hili ili ikibidi, niwataarifu wenzangu nao waelewe. 

“Usiku wa Jumamosi Januari 22, 2011 kundi hilo lilielekea Mbunde, wilayani Namtumbo, (kwa gari aina ya Defender STK 26…, likiendeshwa na (jina tunalo) kukutana na ‘mganga’ …ambaye anaishi ndani ya Selous Game Reserve With Impunity. Defender hiyo iligeuza kurejea Songea siku mbili baadaye na kuwaacha ‘wageni’ hao kwa mganga ambako walikaa siku saba ‘wakitengenezwa’. Walirejea Songea Januari 29, 2011 na kesho yake Januari 30, 2011 wakaanza safari ya kurejea Dar es Salaam. 

“Kutoka Songea hadi Mafinga walitumia ile Hard Top iliyowatoa Madaba hadi Top Inn ya Songea (T7… BDU). Walifika Mafinga milango ya saa mbili usiku na kukuta gari mbili zikiwasubiri: Hilux Mayai ya (kampuni moja) na Defender iliyowaongoza hadi Morogoro. Walipokewa Morogoro na askari (jina tunalo). 

Hapo kundi likagawanyika: watu wanne wakiwemo wale Wasomali wawili wakaingia kwenye Nissan Patrol (T8… ADH) mali ya (kampuni jina tunalo) na wengine wakabaki Morogoro. “Kufuatana na ‘mganga’ mwenyewe, ambaye wapelelezi wako wanaweza kuongea naye kama walivyofanya walionipa taarifa hizi, aliwapa masharti ya kutotumia silaha za moto ila njia nyingine kumuua kwanza Mwakyembe, baadaye Slaa, n.k., n.k, n.k. kwa zamu; alitengeneza dawa ya kuwapooza wale wengine (wanaosubiri) kwenye orodha ya kuuawa (Dk. Slaa, Anne Kilango, Mengi, Mwandosya na Membe) wasitaharuki na kupiga kelele za nguvu hata kuamsha hasira za wananchi mauaji yakitokea; aliwazindika vilivyo wasiweze kudhuriwa na tendo la kuua na alitengeneza dawa ya kuwapumbaza “waliohukumiwa kifo” (wawe mfano wa mbwa mbele ya chatu). 

“Jijini Dar es Salaam ‘wahitimu’ hao walifikia Kiwalani karibu na kiwanda cha Mohamed Enterprises. Jirani na kiwanda hicho kuna jengo la ghorofa: Februari 5, 2011, wageni wawili zaidi waliwasili kwa ndege kutoka Uganda; mwanaume mmoja (aliyechanganya rangi) na mwanamke mmoja (mweusi vilivyo). Walipokewa na gari mbili: moja ya polisi (PT 02…) na ya pili yenye namba za kibalozi (aina ya RAV 4). 

Ushiriki wa Al Shabaab “Jioni wakawa na mazungumzo ya kina na Wasomali wawili niliowaelezea awali ambao inadaiwa ni wapiganaji wa Harakat al-Shabaab al- Mujahideen (kwa kifupi Al- Shabaab). “Niliweza kupata picha pana zaidi kwa nini wapiganaji wa kikundi hicho (kinachopambana na wanaodhaniwa kuwa maadui wa Uislamu) wameingizwa nchini. 

Nimeweza kukusanya taarifa zinazodai kuwa awali walifikiriwa kuletwa wapiganaji kutoka Rwanda, lakini wazo hili lilikataliwa na wafadhili wa mpango huu ambao walitaka ‘wanaharakati’ wa aina hiyo watoke Somalia. Ndipo kikundi hicho kikashawishiwa kwamba Tanzania kuna tatizo la udini la Uislamu kutishiwa. 

Mimi na wenzangu hao watano tumejengewa hoja kuwa maadui wa Uislamu tunaotumiwa na makanisa, hivyo hatuna budi kukatishwa maisha yetu. “Niliweza vilevile kupata picha kuwa wafadhili wa kundi hili, wana mahusiano ya karibu na Sheikh …(jina tunalo) ambaye baadhi ya utabiri wake unatokana na agenda za wafadhili hao. 

Inadaiwa kuwa utabiri wa sheikh … mwaka jana ulimlenga Dk. Slaa ambaye alidaiwa kubebwa na makanisa. “Utabiri” huo haukutimia kwa kuogopa kuiingiza nchi kwenye machafuko makubwa ya kisiasa/kidini ambayo yangewaweka pabaya hata wafadhili wa mpango huo. “Inadaiwa kuwa Sheikh … ameombwa tena kutoa utabiri wa mwanasiasa na kiongozi mmoja kupoteza maisha mwezi huu (Fabruari). 

Inadaiwa kuwa mwanasiasa huyo anayetembea na kifo ni mimi na tayari maandalizi ya ‘hukumu yangu’ yamefanywa: “(a) Kijana mmoja kwa jina la Hassan alitumwa kutoka Dar es Salaam kwenda Dodoma siku ya Jumamosi Februari 5, 2011 kwa “maandalizi” hayo (mahali pa kufikia kikosi hicho cha mauaji, utambuzi wa nyumba ya kuishi niliyopangiwa na kumtafuta mhudumu mmoja wa Bunge ili ile ‘portion’ ya mganga ya kunipumbaza kabla ya hukumu, iweze kunyunyizwa kwenye kiti changu Bungeni); “(b) Kesho yake (Jumapili) Februari 6, mnamo saa nne usiku, kikosi hicho cha mauaji kikiwa na watu watano kiliondoka Dar es Salaam kwenda Dodoma kwa gari aina ya Land Cruiser nyeupe ya mkongo (T3… AKU) na kimejichimbia Dodoma mpaka leo (Februari 9). 

“Waliomo kwenye kikosi hicho ni Wasomali wale wawili, mgeni moja (wa kiume) kutoka Uganda, Mustafa a.k.a “Master” na kijana mmoja ambaye Januari 19, 2011 aliwabeba Wasomali hao kutoka Morogoro hadi Ununio kupitia Kibaha na Baobab kwa gari aina ya VX Land Cruiser (T6…APF). Kijana huyo ana shepu ya Kitutsi na anaongea Kifaransa. 

“Utabiri atakaoufanya Sheikh … (pengine aamue kuachana nao sasa baada ya kubaini kuwa tunaujua) utakuwa na lengo la kuwapumbaza wananchi waelekeze macho na masikio yao zaidi kwenye utabiri wake kuliko kwenye njama za kundi hilo za muda mrefu za mauaji. “Kila siku ya Mungu napata taarifa za ziada kutoka kwa raia wema kuhusu suala hili. 

Naziingiza kwenye taarifa hii ili ziwasaidie katika upelelezi: “Inadaiwa kuwa Wasomali hao waliingia nchini kutokea Kenya na wakaja kwa barabara hadi Dodoma. Walitumia gari aina ya RAV4 (new model – T8… AQS) Januari 8, 2011 na kusafirishwa hadi Morogoro ambako walipokewa na askari niliyemtaja awali… wa polisi Morogoro. “Mjini Morogoro, walikaa hoteli mbili tofauti: Hilux Hotel Morogoro na Top Life. 

Aliyewafanyia Wasomali hao booking hapo Top Life ni mmiliki wa hoteli ya….(jina la hoteli na mmiliki tunalo). “Magari waliyotumia wakiwa Morogoro ni RAV4 T8… AQS, VX Land Cruiser STK 1…, Mercedes Benz (Station Wagon) T8… BDT, Toyota Mark II GX100 nyeupe T2… BKR na wakiwa Dar es Salaam wametumia magari VX Land Cruiser T6… APF, Nissan Patrol T8… ADH.” 

“Naomba nihitimishe maelezo haya kuwa nimekuwa muwazi kwa asimilia 100 na hata vyanzo vyangu vya habari ni miongoni mwa watu hao niliowataja katika taarifa hii ambao naamini utachukua hatua ya kuwahoji kulipatia ufumbuzi suala hili. 

“Suala la msingi hapa, si uhai wangu, kwani iko siku lazima nitakufa kama ambavyo hao mafisadi wanaodhani wanaweza kufadhili vifo vya wenzao watakavyokufa hata wao hatimaye, watake wasitake, hakika ni suala la muda tu. Suala la msingi hapa ni mustakabali wa taifa letu, taifa aliloliasisi Mwalimu Nyerere na kulilea kwa misingi ya usawa, haki, umoja, amani na utulivu. 

“Nimejieleza awali kuwa nina imani kubwa na Jeshi letu la Polisi kwamba litaifanyia kazi taarifa hii bila kujali nguvu ya ukwasi na ya kisiasa ya watuhumiwa na kwa kuzingatia misingi ya haki na ukweli. 

“Hata hivyo nalazimika kusema nitasikitika sana ikiwa taswira ya ‘ukorofi’ niliyopewa kwenye kesi moja ya awali (2009) itapewa nafasi kwenye suala hili, hivyo kuninyima fursa ya kusikilizwa vizuri na ulinzi ninaostahili kama raia Kikatiba na kisheria. Niko tayari wakati wowote na mahali popote kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi litakaponihitaji.”

CHANZO: Jamii Forums

Saturday, May 30, 2009

BAADA YA MWAKYEMBE,KIMARO NAE AJALINI


MHH,AJALI ZINAZOWAANDAMA WABUNGE "WA AINA MOJA" ZINAWEZA KUZUA MASWALI YA NAMNA FLANI JAPO YAWEZEKANA KABISA KUWA NI AJALI KAMA NYINGINEZO.HEBU SOMA KWANZA HABARI IFUATAYO,KISHA TUJIULIZE MASWALI MAWILI MATATU:

Ally Sonda na Rehema Matowo, Mwanga

MBUNGE wa Jimbo la Vunjo, Aloyce Kimaro amenusurika kufa baada ya gari lake alilokuwa akisafiria kuparamia mawe yaliyopangwa barabarani na kupata ajali usiku wa kuamkia jana. Habari zilizolifikia gazeti hili jana na kuthibitishwa na Kimaro na polisi zinasema kuwa, ajali hiyo ilitokea katika kijiji cha Mikongeni kata ya Lembeni wilayani Mwanga, Kilimanjaro kwenye barabara kuu ya Moshi-Tanga, akiwa safarini kutoka Dar es Salaam kwenda jimboni kwake.

Kwa mujibu wa habari hizo, wakati ajali hiyo inatokea, Kimaro alikuwa na rafiki yake Joseph Temu ambaye ndiye aliyekuwa anaendesha gari hilo aina ya Mercedes Benz akiwa na mkewe na watoto wake watatu. Katika ajali hiyo hakuna aliyejeruhiwa.

Kimaro alisema baada ya ajali hiyo mfanyabiashara wa Mwanga, Shafii Hasanal alitoa msaada wa kulivuta gari hilo hadi kwenye kituo cha mafuta Kisangara.

Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, Lucas Ng’hoboko alisema kuwa ajali hiyo ilitokea saa 2:30 usiku, chanzo kikiwa ni mawe makubwa na matofali yaliyokuwa yamepangwa barabarani katika eneo lenye kona na mlima.

Kamanda Ng’hoboko alisema kuwa watu wanaosadikiwa kuwa ni wezi, walipanga mawe hayo barabarani kwa lengo la kusababisha ajali ili kuwaibia abiria.

“Gari ya mbunge huyo ilipofika katika eneo hilo likiwa katika mwendo wa kawaida na mbele yao kukiwa na lori ambalo liliweza kuyapita mawe hayo bila tatizo, wao walipojaribu kuyapita tairi la mbele upande wa kulia na ‘sampo’ ya gari hilo vilipasuka wakashindwa kuendelea na safari,” alisema Ng’hoboko.

Kamanda huyo alisema kuwa miaka ya nyuma eneo hilo lilikuwa na matukio mengi ya aina hiyo ambayo yameanza kujitokeza upya, kwa kuwa awali wananchi wa eneo hilo kwa kushirikiana na polisi walikuwa wameyamaliza. Alibainisha kuwa polisi wanafanya operesheni ili kuwadhibiti wezi hao na kuwasaka waliohusika na tukio hilo ili wafikishwe mbele ya sheria.


Kimaro ni miongoni mwa wabunge waliojitokeza hadharani kupambana na vitendo vya ufisadi. Mwaka jana aliibua hoja bungeni kutaka, Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa ashitakiwe kwa kutumia madaraka vibaya ya kufanya biashara akiwa ikulu.

Hii ni ajali ya pili inayohusisha wabunge kutokea ndani ya wiki mbili baada ya ajali iliyomhusisha mbunge wa Kyela, Dk Harrison Mwakyembe iliyotokea eneo la Ihemi, Ifunda mkoani Iringa. Dk Mwakyembe, alinusurika kifo baada ya gari alilokuwa akisafiria kutoka Kyela kwenda Dar es Salaam kuacha njia na kupinduka.

Ripoti ya polisi iliyotolewa wiki hii ilieleza kwamba ajali hiyo ilitokana na uzembe wa dereva, lakini mbunge huyo ameiponda na kuifananisha na ripoti ya mpiga ramli kwa vile haikuzingatia vigezo na utaalamu katika uchunguzi.


CHANZO: Mwananchi
NAAMINI WENGI WETU TUNAKUMBUKA AJALI ILIYOMHUSISHA MHESHIMIWA CHEYO a.k.a "Mzee wa Vijisenti" AMBAYO ILIPELEKEA VIFO VYA WATU WAWILI.TOFAUTI KATI YA AJALI YA CHENGE NA HIZI ZA MWAKYEMBE NA KIMARO NI REACTION YA POLISI.BAADA YA GARI LA CHENGE KUUA,SIKUWAHI KUSIKIA RPC AU RTC AKIKURUPUKA KUELEZA CHANZO CHA AJALI HUSIKA (JAPO KATIKA MAZINGIRA YA KAWAIDA,NI RAHISI KUIHUSISHA AJALI YA SAA 10 ALFAJIRI NA STIMU ZA KILEVI).BADALA YAKE ILIUNDWA TUME AMBAYO HADI LEO HAIJATUELEZA MATOKEO YA UCHUNGUZI WAKE (IF AT ALL ILIFANYA UCHUNGUZI).WORSE STILL,INAELEZWA KUWA WAKATI AJALI HIYO INATOKEA GARI LA CHENGE LILIKUWA NA BIMA ILIYOISHA MUDA WAKE.


ALIPOPATA AJALI MWAKYEMBE,RPC AKAKURUPUKA NA KUDAI KWAMBA CHANZO CHA AJALI NI MWENDO MKALI NA SHIMO LILILOKUWA BARABARANAI.BAADAYE TUME YA KAMANDA KOMBE IKAZIDI KUCHANGANYA MADAWA KWA KUTOA FINDINGS AMBAZO SI TU ZIMEINGILIA KAZI YA MAHAKAMA KWA KUWAHUKUMU MWAKYEMBE (kuwa alikuwa amelala wakati wa ajali) NA DEREVA WAKE (kwa uzembe) LAKINI PIA HAZIKUHUSISHA MAELEZO YA MWAKYEMBE KWA VILE HAKUHOJIWA NA TUME HIYO!


KINGINE CHA KUSHANGAZA NI KWAMBA WHILE KWENYE AJALI YA CHENGE,DEREVA WA BAJAJI NA MMILIKI WAKE WALIAMRIWA KUJISALIMISHA POLISI MARA MOJA,HATUJASIKIA KAULI YOYOTE KUTOKA KWA POLISI KUHUSU DEREVA WA LORI LILIOHUSIKA KWENYE AJALI YA MWAKYEMBE!


NA SASA KATIKA AJALI YA KIMARO TUNAELEZWA KUWA MAWE HAYO YALIPANGWA NA WEZI.HOW DID THE POLICE KNOW KUWA WALIOFANYA HIVYO NI WEZI NA SIO WATU WALIOKUWA WANAWINDA UHAI WA MHESHIMIWA KIMARO?KWANINI(ANGALAU KWA KUTUZUGA) ISIUNDWE TUME KAMA ILE YA AJALI YA CHENGE AMBAPO HAKUKUWA HATA HAJA YA KUFANYA SPECULATION LET ALONE KUUNDA TUME?


CALL ME A CONSPIRACY THEORIST,LAKINI NADHANI AJALI HIZI ZINA TAFSIRI KUBWA ZAIDI YA TUNACHOSIKIA AU KUONA KWA MACHO YETU.LET'S WAIT AND SEE!


Thursday, April 02, 2009

TUHUMA ZA UFISADI: MKURUGENZI TAKUKURU "AUMUKA",MBOWE NA DR SLAA NAO WALONGA



Gazeti la Mwananchi linaandika:


MKURUGENZI wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hosea jana alikuwa kwenye wakati mgumu baada ya wabunge kumhoji uhalali wake wa kuiongoza taasisi hiyo wakati akikabiliwa na tuhuma za kusafisha kashfa ya zabuni ya mitambo ya kuzalisha umeme wa dharura.

Mkurugenzi huyo, ambaye alitajwa kwenye taarifa ya tume teule ya bunge iliyochunguza kashfa hiyo na serikali kutakiwa kumchukulia hatua, alikumbwa na mtafaruku huo katika semina ya Miundombinu ya Uadilifu iliyoandaliwa na Takukuru na Chama cha Wabunge wa Afrika (APNAC) na kufanyika kwenye hoteli ya Whitesands jijini Dar es salaam.

Ilifikia wakati Dk Hosea alionekana kukerwa sana na maswali kiasi cha kulazimika kuwaonya kuwa anao uwezo wa kuwachafua kama wakiendelea kufanya mambo yanayoonekana kumvua nguo.

Mbunge wa Busega, Raphael Chegeni ndiye aliyeanzisha kizaazaa hicho baada ya kumhoji Dk Hosea akisema ilikuwaje taasisi yake iliisafisha kampuni tata ya kuzalisha umeme wa dharura Richmond Development (LLC) iliyokuwa inakabiliwa na kashfa ya kushinda zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura wakati kamati teule ya Bunge iliyoundwa kuchunguza mkataba wake, iligundua kuwepo kwa mazingira ya rushwa.

“Inakuwaje wakati wa mjadala wa Richmond, wewe mkururugenzi wa Takukuru ulikanusha kuwapo rushwa na uchunguzi wa kamati ya bunge ulibaini kuwepo rushwa ndani ya kampuni hiyo? Je ni nani mwenye dhamana ya kukuadhibu wewe na taasisi yako kuhusu rushwa’’ aliuliza Chageni.

Swali hilo halikutegemewa na Dk Hosea na lilionekana kumuudhi na kulazimika kuchukua kipaza sauti na kusitisha maswali na kuanza kujibu kwa ghadhabu.

“Hapa siyo jukwaani hivyo tusilete siasa. Nipo hapa kwa ajili ya kufundisha na kama ni suala la Richmond waziri mkuu alishaliongelea na ndiyo mwenye dhamana ya kujibu hilo. Mimi sina jibu kwa hilo na kama mtu hapendi kuvuliwa nguo kwanini umvue mwenzako,” alisema Dk Hosea.

"Mjadala huu aachiwe Waziri Mkuu Mizengo Pinda na aliyeuliza swali hilo hanitendei haki kwani hakuna hoja nyingine ya maendeleo kwa jamii ambalo inaweza kujadiliwa... mbona mnang’ang’ania kujibu hilo pekee.

“Najua kuna watu wanatumiwa ili niongee halafu nibabaike katika kujibu nanishindwe kufanya kazi yangu. Mbona mnang’ang’ania jambo hilo tu wakati kuna hoja nyingine za maendeleo kwa jamii. Kuhusu suala la Richmond sijibu ng’o.”.



Nalo Tanzania Daima linaripoti:


MKURUGENZI wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU), Edward Hosea, jana aliwashambulia wabunge katika semina ya kukabiliana na rushwa iliyoandaliwa na taasisi yake na kuwashirikisha wabunge wa Chama cha Kupambana na Rushwa (APNAC).

Akitoa mada katika semina hiyo, Dk. Hosea aliwashambulia wabunge hao hadharani, kwamba wamekuwa wakichangamkia posho za semina wakati hakuna uwajibikaji.

Katika mada hiyo iliyoonekana dhahiri kuwakera wabunge hao, Dk. Hosea alisema baadhi yao wamekuwa wakihudhuria na kusaini posho zaidi ya tatu katika semina tofauti kwa siku moja, huku wakishindwa kuwajibika, jambo ambalo alisema ni aina mojawapo ya rushwa.

“Wapo wabunge wanaohudhuria semina zaidi ya tatu kwa siku moja na kusaini posho, lakini hata baada ya kuwezeshwa kwa posho hizo, hakuna uwajibikaji. Kwa kweli kuna mambo mengi yanayotokea, lakini tunayafumbia macho,” alisema Dk. Hosea.

Mbali na kusaini posho kwenye semina tatu kwa siku, Dk. Hosea pia alisema wapo wabunge ambao wanatumia vibaya ubunge wao kwa kutokaa kwenye foleni wawapo sehemu za huduma kama benki.

Pia aliwapasha wabunge kuwa hivi sasa siri nyeti za serikali ziko wazi, na kwamba inatokana na ukosefu wa maadili miongoni mwao.

Hata hivyo, baada ya kumaliza kutoa mada hiyo, baadhi ya wabunge walionekana dhahiri kukerwa na mada hiyo na kutaka kujibu mapigo kwa kuhoji utendaji wa taasisi hiyo na mafanikio yake tangu ilipoanzishwa.

Mbunge wa kwanza kutoa dukuduku lake, alikuwa Dk, Raphael Chegeni (Busega-CCM) ambaye alihoji utendaji wa TAKUKURU na kueleza kutoridhishwa kwake.

Dk. Chegeni alianza kujibu mapigo kwa kuhoji uwajibikaji wa Dk. Hosea na taasisi yake kuwa, iliwahi kuchunguza kashfa ya zabuni ya kampuni ya kufua umeme wa dharura, Richmond, na kuitangazia jamii kwamba hakukuwa na rushwa katika zabuni hiyo.

Kama hiyo haitoshi, Dk. Chegeni alisema TAKUKURU pia ilishindwa kuchunguza kashfa ya minara pacha ya majengo ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na badala yake Kampuni ya nje ya Ernest & Young ilibua ufisadi mkubwa na hatimaye leo baadhi ya watuhumiwa wamefikishwa mahakamani.

Huku akishangiliwa na baadhi ya wabunge, Dk. Chegeni alihoji ujenzi wa gharama wa ofisi za TAKUKURU nchini pamoja na magari ya kifahari wanayotumia wakati haiwajibiki ipasavyo katika kukabiliana na rushwa.

“TAKUKURU mnawajibika nini? Mlisema kwenye Richmond hakuna rushwa, lakini baadaye Bunge lilibaini kuwapo kwa rushwa, kwenye ujenzi wa minara pacha ya BoT mmeshindwa kuchunguza hadi kampuni ya nje ndiyo iliyokuja kuibua kashfa hiyo,” alisema Dk. Chegeni.

Kutokana na hoja hiyo, Dk. Hosea alikuja juu na kuwataka wabunge hao kuacha kuhoji mambo hayo, kwani wakianza kuchambuana, hakuna atakayebaki salama.

“Hapa hatukuja kulumbana, tumekuja kwenye semina, si mahala pake, lakini nyie wabunge ndio mlioamua kupitia Kamati Teule ya Bunge na mapendekezo yenu yapo, kwa hiyo iulizeni serikali, lakini hatuko hapa kushambuliana,” alisema Dk. Hosea.

Hata hivyo, baada ya malumbano hayo makali, wabunge na maofisa wa TAKUKURU, waliendelea na semina yao inayofanyika katika ofisi ndogo za Bunge jijini Dar es Salaam, inayotarajia kumalizika leo.



Wakati huo huo viongozi wawili wakuu wa Chadema,

Freeman Mbowe na Dr Wilbroad Slaa wametoa matamshi mazito kuhusiana na ishu ya Dowans.Gazeti la Mwananchi linaripoti




KATIBU mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa amesema kitendo cha Rais Jakaya Kikwete kumtetea mkurugenzi wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) Dk Idris Rashid kinamtia wasiwasi na kuhoji uhalali wa kufunga mjadala wa Dowans.

Dk Slaa alikuwa mmoja wa watu waliohojiwa na Mwananchi kuhusu maoni yao juu ya hotuba ya kila mwezi ya Rais Kikwete aliyotoa juzi kuzungumzia mambo mbalimbali, likiwemo suala la mpango uliokwama wa serikali kununua mitambo ya kuzalisha umeme wa dharura ya kampuni ya Dowans Tanzania Limited.

Ingawa Dk Rashid alionekana kushutumu wabunge waliopinga kutekelezwa kwa azma hiyo wakati akitangaza uamuzi wa Tanesco kuachana na mpango wa kununua mtambo huo, Rais Kikwete aliipongeza Tanesco kwa uamuzi huo huku akionekana kutaka malumbano juu ya suala hilo yaishe.

Lakini Dk Slaa anaona kauli hizo zinalenga kumlinda Dk Rashid, gavana wa zamani wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

"Tuna mashaka naye Kikwete kwa kauli yake ya kumtetea Dk Idris ambaye pia sisi tuna mashaka naye kuwa alihusika katikasakata la ununuzi wa rada," alisema Dk Slaa.

"Kikwete hawezi kueleweka kwa kumtetea mtu aliyedaiwa kuhusika na kampuni ya nchini Uingereza, akidai inatuhumiwa kupokea fedha kupitia akaunti inayodaiwa kuwa ya mwanasheria wa zamani."

Dk Slaa alisema hofu yake inakuwa kubwa zaidi kutokana na kile alichodai kuwa wakati sakata la Tanesco na ununuzi wa mitambo ya Dowans likipamba moto, Kikwete alikwenda nje ya nchi na aliporejea alitoa kauli kumtetea mkurugenzi huyo.

Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini iliishauri serikali isinunue mitambo hiyo ya Dowans kwa kuwa kufanya hivyo ni kukiuka Sheria ya Manunuzi ya Umma, ambayo inazuia kununuliwa kwa vitu vilivyotumika.

Hata hivyo, Tanesco na serikali hawakuridhika na ushauri huo wa Bunge na badala yake wakazunguka na kuliwasilisha suala hilo kwenye Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma, ambayo ilishindwa kutoa maamuzi hasa baada ya bunge kueleza kuwa maoni ya kamati ya awali ndio msimamo wa chombo hicho cha kutunga sheria.

Kukwama kwa mpango huo kulimfanya Dk Rashid kuitisha kikao na waandishi na kulaumu wabunge, akidai kuwa waligeuza suala hilo kuwa la kisiasa na kudai asilaumiwe iwapo nchi itaingia gizani.

Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, ambaye aliunga mkono mpango wa serikali kununua mitambo hiyo akitaka watu waangalie kwa umakini tatizo lililo mbele, hakuwa na maoni yoyote alipotafutwa na Mwananchi.

"Sina maoni yoyote," alisema Zitto ambaye mkoa wake wa Kigoma uko kwenye matatizo makubwa ya umeme na ambao Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja aliahidi bungeni kuwa utakuwa umefungiwa mtambo wa megawati 6 ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.

Naye kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni, Hamad Rashid alisema tatizo la umeme nchini limetokana na serikali kushindwa kufanyia kazi maeneo 15 ambayo iliyaainisha ili kukabiliana nalo na ndiyo inayostahili kubeba mzigo wa lawama.

Alisema serikali inapaswa kulaumiwa kwa tatizo la umeme kwa kuwa imeshindwa kufanyia kazi suala hilo tangu mwaka 2006 na kwamba iwapo maeneo hayo yangefanyiwa kazi, kero ya umeme ingemalizika na wala mjadala kuhusu mitambo ya Dowans usingekuwepo.

“2005/2006 tulikumbwa na tatizo kubwa la ukame na kusababisha mgao mkubwa wa umeme. Katika juhudi za kutafuta njia mbadala, serikali iliainisha maeneo 15 ya kuyafanyia kazi ili kuondoa tatizo hilo,” alisema Rashid.

Alisema moja ya maeneo hayo ni ununuzi wa mitambo ya kufua umeme wa dharura, ambalo ndilo lililosababisha mjadala mkubwa wa kitaifa kutokana na Tanesco kutaka kununua mitambo ya Dowans, ambayo ilirithishwa mkataba wa kampuni ya Richmond Development (LLC) iliyoshinda katika mazingira ya utata zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura.

“Maeneo hayo yapo katika hansard (vitabu maalum vya kuhifadhia kumbukumbu za bunge) na nitayatoa kwa waandishi katika mkutano wangu nao kesho au keshokutwa," alisema Rashid.

Alisema anaunga mkono hotuba ya Kikwete kwa kuwa alichozungumza ndicho alichotaka kukieleza kwa wananchi akiongeza kwamba mkutano wake na waandishi hautakuwa tena wa kutoa msimamo wa kambi ya upinzani kama alivyodhamiria awali bali kuikumbusha serikali kuyafanyia kazi maeneo hayo.

Hata hivyo alisema hotuba hiyo ya Kikwete inathibitisha kuwa serikali iliridhia uamuzi wa bunge juu ya mjadala wa ununuzi
wa mitambo ya kampuni ya Dowans.

Alisema bunge lilitoa maamuzi yake kuishauri Tanesco isinunue mitambo hiyo kutokana na utata uliopo kati ya uhusiano wa Dowans na kampuni ya Richmond na kwamba iwapo haikuridhia ingerudi bungeni na kuliomba bunge libadilishe maamuzi yake.

“Hotuba ya rais ni ushahidi kuwa serikali imeridhia maamuzi halali ya bunge na ndio maana rais akamaliza mjadala wa Dowans na kuwapongeza Tanesco kwa kuachana na nia ya kununua mitambo hiyo,” alisema Rashid.

Lakini Dk Slaa hakukubaliana na kauli ya Rais Kikwete kutaka malumbano kuhusu ununuzi wa mitambo ya Dowans yaachwe.

"Ametumia udikteta kufunga mjadala," alisema Dk Slaa ambaye ni mwanasheria. "Wananchi hawakumpa mamlaka hayo ya kuwazuia kujadili rasilimali zao na nchi yao.

"Siku zote nasema Kikwete asituamulie... wananchi wanazungumza juu ya rasilimali na nchi yao, wanasiasa ni wadau katika maslahi ya nchi, asituamulie juu ya rasilimali zetu.

"Hakupewa mamlaka ya kutuamlia nini cha kujadili. Hatuwezi kukubali... kwa sababu gani analazimisha kufunga mjadala? Lazima kuna kitu."


Nalo Tanzania Daima linaandika:


MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amemtaka Rais Jakaya Kikwete, kutofunga mjadala wa suala la mitambo ya kampuni ya kuzalisha umeme wa dharura, Dowans, bila kuwaeleza wananchi ukweli kuhusu wamiliki wake na mahala walipo.

Mbowe aliyasema hayo jana katika mahojiano maalum na Tanzania Daima, akitoa maoni yake kuhusu baadhi ya masuala aliyoyazungumza Rais Kikwete juzi usiku, wakati akilihutubia taifa kwa njia ya
redio na televisheni.

Alisema hatua ya Rais Kikwete kutangaza kufunga mjadala wa Dowans ni ya kuungwa mkono kwa kuwa mjadala huo si jibu la matatizo ya umeme nchini, lakini alimtaka kwanza awaeleze Watanzania ukweli wote kuhusu Kampuni ya Dowans, ndipo aufunge mjadala huo vizuri.

“Tunakubaliana na ushauri wake wa kutaka mjadala wa Dowans uishe. Tunakubaliana naye kwa sababu Dowans si jibu la matatizo ya msingi ya sekta ya nishati nchini. Hata hivyo, Kikwete asikimbilie kufunga mjadala bila kuwaeleza wananchi, Dowans ni nani. Watoe tamko, waueleze umma wa Watanzania, wamiliki wa Dowans ni nani, wako wapi, wanafanya nini, wataje watu wote wanaonufaika na Dowans, kisha ndipo atufungie mjadala huo vizuri. Kikwete anataka kuficha ukweli,” alisema Mbowe.

Akizungumzia tatizo la uhaba wa umeme nchini, alisema si mara ya kwanza kwa Rais Kikwete kuahidi kumaliza tatizo la umeme, kwani wakati wa sakata la kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond, alishaahidi kuwa tatizo la umeme lingekuwa historia.

“Si mara ya kwanza rais kuahidi kwamba nchi haitakuwa gizani. Ameshaahidi hivyo wakati wa vuta nikuvute ya Richmond, ameshasema hivyo karibu mara tatu. Alishasema kwamba matatizo ya umeme yatakuwa historia, lakini hadi leo nchi haina umeme wa uhakika. Rais anaendelea kutoa maneno matamu, hatuwezi kupata umeme kwa maneno yake….”

“Asitazame tu uchaguzi wa 2010, na kuwapa watu maneno matamu, atazame mbele. Tunahitaji mkakati wa muda mrefu na mfupi. Na si mkakati tu, tunahitaji mpango wa utekelezaji, maana sera ya nishati imeainisha yote hayo, lakini tatizo utekelezaji. Serikali inapaswa kuwa na uhakika wa kulipatia taifa umeme hata kwa miaka zaidi ya 50 ijayo,” alisema Mbowe.

Alisema kwa kiasi kikubwa sekta ya umeme nchini inaathiriwa na wafanyabiashara wakubwa ambao ni maswahiba wa Rais Kikwete na Chama Cha Mapinduzi (CCM), wanaoigeuza sekta hiyo kuwa chanzo chao cha mapato, kwa kuanzisha kampuni za kufua umeme wa dharura na kuiuzia TANESCO kwa gharama kubwa.

Alisisitiza kuwa, msingi wa tatizo la nishati ya umeme nchini ni kutokuwapo kwa sera endelevu na mikakati yakinifu na inayotekelezeka, ya muda mrefu na mfupi, ya kuzalisha na kusambaza umeme.

Alisema pamoja na uhaba wa umeme unaozalishwa, bado sehemu kubwa ya umeme huo imekuwa ikiibwa na kusababisha wananchi wengi kukosa haki ya kupata umeme.

“Na tatizo hapa si uhaba wa umeme unaozalishwa tu. Bado kuna umeme mwingi sana unaibwa, lakini serikali halizungumzii hili,” alisema Mbowe.

Alisema tatizo jingine ni umeme unaozalishwa kuwa wa gharama kubwa kiasi cha wananchi wengi kushindwa kuupata na kuutumia.

“Tuna network (mtandao) kubwa sana ya umeme. Maeneo mengi nyaya za umeme zinapita jirani na nyumba za watu, lakini wenye uwezo wa kuunganisha umeme huo kwenye nyumba zao ni wachache sana. Gharama za kufunga umeme majumbani ni kubwa mno kwa Mtanzania maskini kumudu. Gharama za kuutumia, kulipa ankara pia ni kubwa.

“Kwa hiyo Rais Kikwete na serikali yake, wasiishie tu kuzungumzia uzalishaji, lakini pia lazima waeleze ni jinsi gani watapunguza gharama za umeme ili Watanzania maskini nao waweze kuutumia,” alisema Mbowe.

Akizungumzia tahadhari ya Rais Kikwete, kwamba kwenye baadhi ya mikoa kuna uwezekano wa kutokea tatizo la chakula kwa sababu ya kuchelewa kwa mvua za masika, Mbowe alisema ni aibu na fedheha kubwa kwa nchi yenye maji mengi yanayotiririka kama Tanzania, kutangaza njaa ndani ya msimu mmoja wa matatizo ya mvua.

“Sikio la kufa halisikii dawa. Tatizo la chakula ni tatizo la kujitakia. Kukosa mvua msimu mmoja, halafu rais anatangaza njaa, ni jambo la kutia aibu sana. Tuna maji mengi sana yanatiririka, tuna mito na maziwa, ardhi yenye rutuba nzuri sana. Tuna kila kitu, tatizo ni ukosefu wa sera nzuri na uongozi bora,” alisema Mbowe.

Alisema Rais Kikwete anapaswa kumfukuza mara moja Waziri wake wa Kilimo na Chakula kwa kushindwa kusimamia programu za kilimo cha uwagiliaji nchini.

“Walipoingia madarakani walikutana na tatizo la chakula. Kikwete na Lowassa waligawa chakula na kuahidi kwamba njaa ile isingetokea tena, sasa leo wanatuambia nini? Wamefanya nini? Na hii ndiyo kawaida yake, anaahidi halafu anasahau. Nchi hii ikipata viongozi wazuri serikalini, kilimo cha umwagiliaji kinaweza kabisa kumaliza tatizo la njaa za mara kwa mara,” alisema Mbowe.

Alisema serikali inapaswa kuwa na mpango wa makusudi wa muda mrefu wa kuzalisha na kuhifadhi chakula kwa wingi, ili kiwe kinaingia katika mtandao wa matumizi ya wananchi, pindi kunapokuwa na uhaba wa chakula.

Katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi uliopita, Rais Kikwete pamoja na mambo mengine, alitaka mjadala wa kununua au kutonunua mitambo ya Dowans, ufungwe baada ya wahusika (TANESCO), kutangaza kuachana na uamuzi wa kutaka kuinunua.

Alisema anashangazwa na malumbano ya baadhi ya viongozi wa siasa kuhusu jambo hilo.

Mjadala wa Dowans, hivi karibuni uliwaingiza katika malumbano makali, Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe na Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, wote wa CCM





PENGINE DR HOSEA ANA HAKI YA KUWA MKALI KWANI YEYE HAKUJITEUA KATIKA WADHIFA HUO BALI ALITEULIWA...NA PIA KWA VILE KWA MUJIBU WA "UTAMADUNI WETU" KUJIUZULU NI MITHILI YA KUMKOSEA ADABU ALIYEKUTEUA BASI HUENDA KUMSAKAMA DR HOSEA NI KUMWONEA KWANI YAELEKEA ALIYEMTEAU KARIDHIKA NAE.AMA KWA HAKIKA TANZANIA BILA UFISADI INAWEZEKANA!!!

Friday, March 27, 2009

DR SLAA: MITAMBO YA DOWANS ITAIFISHWE NA SIO KUNUNULIWA


KWA MTU YEYOTE MWENYE AKILI TIMAMU,HATA AKIAMSHWA USINGIZINI AU AKIWA BWII KWA ULEVI,HAIINGII KICHWANI KUSIKIA HOJA ZA KIFISADI ZA KUNUNUA MITAMBO ILIYONGIZWA NCHI KITAPELI NA MAJAMBAZI WA RICHMOND NA HATIMAYE KURITHISHWA KISANII KWA WENZAO WA DOWANS.TUKIRUHUSU HILI LITOKEE,KUNA MAHALA ITAFIKA NCHI YETU NAYO ITAUZWA NA KISHA TUTATAKIWA KUINUNUA BACK....


Tausi Mbowe na Elias Msuya

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Dk Wilbroad Slaa ameitaka serikali kuitaifisha mitambo ya Kampuni ya kuzalisha umeme ya Dowans badala ya kujadili manunuzi yake.

Dk Slaa aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam baada yakutopa taarifa ya kamati kuu kilichokutana kwaajili ya kuandaa mkutano wa baraza kuu.

Alisema kuwa mitambo ya Dowans ilirithiwa kutoka kwenye kampuni ya Richmond ambayo ilibainika bungeni kuwa ni ya kifisadi kwahiyo hakuna haja ya kuinunua tena bali kuitaifisha.

“Msimamo wangu siku zote ni kutaifishwa kwa mitambo ile na siyo kuinunua. Naishangaa serikali, kutaka kuinunua mitambo ya Dowans wakati mitambo ile ilishabainishwa Bungeni kuwa ni ya kifisadi. Kama mtu umekamata kitu chako cha wizi utakinunua tena?" alihoji

Akizungumzia malumbano kati ya Mbunge wa Kyela Dk Harrison Mwakyembe na Mbunge wa Igunga Rostam Aziz, Dk Slaa alisema,

“Mradi wa kuzalisha umeme nimeushughulikia kwa miezi minane. Nilikwenda hadi kijiji cha Kisesida mkoni Singida ambako ndiko kampuni mbili za Power Pool East Africa ya Dk Mwakyembe na wenzake na Wind East Africa ya Rostam Aziz zimewekeza.

Kampuni ya Power Pool East Afrika ni ya wazalendo na imeshalipa fidia kwa wakazi wa kijiji cha Kisesida lakini ile ya Wind East Africa haijafanya hivyo, badala yake inabebwa na kiongozi wa ngazi za juu mkoani ambaye amekuwa akiwakejeli wanakijiji wa Kisesida. Ndiyo maana kuna kuwa na malumbano kati ya Rostam Aziz na Dk Mwakyembe,” alisema Dk Mwakyembe.

Akizungumzia tatizo la mgawo wa umeme ambalo litangazwa na Tanesco hivi karibuni, Dk Slaa alisema,"Baada ya kubainika kwa kashfa ya Richmond, Rais Kiwete alitangaza kuwa suala la mgawo wa umeme litakuwa historia katika nchi hii, sasa mgawo huu unatoka wapi tena? nendeni mkamwulize,” alisema Dk Slaa.

Aidha alimshangaa Rais Kikwete kwa kuendelea kumwacha madarakani Mkurugenzi wa Tanesco, Idriss Rashid wakati anatuhumiwa kwa ufisadi.

"Dk Rashid (PICHANI JUU) alihusishwa na ufisadi alipokuwa Gavana wa Benki kuu. Tumeshatoa vilelezo vyote kuthibitisha jinsi alivyoshiriki kwenye ununuzi wa rada na ndiyo maana sasa hivi anashirkiana na Dowans ili kununua mitambo yake kiufisadi. Tunashangaa kwanini Rais Kikwete hamchunguzi, wala kumwajibisha. Eti wanasema Serikali ya Uingereza inachunguza, wakati si kweli. Uingereza wanachunguza ushiriki wa BAE system siyo watu wetu,” alisema Dk Slaa.



CHANZO: Mwananchi
IT MAKES A LOT OF SENSE,DOESN'T IT?UNAMKAMATA KIBAKA NA MALI YAKO,BADALA YA KUMKWINDA AKUREJESHEE NA HATIMAYE KUMFIKISHA POLISI ETI UNAKUBALI AKUUZIE ALICHOKUIBIA!IT COULD ONLY HAPPEN IN TANZANIA,I SUPPOSE!

Monday, March 23, 2009

NAPE: MAFISADI WAMEJIPANGA KUIFANYA NCHI ISITAWALIKE


KADA maarufu wa Chama cha Mapinduzi, Nape Nnauye, amesema malumbano yanayoendelea sasa nchini ni ishara kwamba mafisadi wamejipanga kuifanya nchi isitawalike.

Nape alitoa kauli hiyo jana alipotakiwa kutoa maoni yake kuhusu hali ya kisiasa nchini, hususani malumbano yanayoendelea sasa kati ya Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz na Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe.

Bila kutaja majina ya watu, Nape alisema chimbuko la malumbano hayo aliyoyaita ya kipuuzi ni kashfa nzima ya kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond, iliyosababisha aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi na aliyekuwa Waziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dk. Ibrahim Msabaha, kujiuzulu.

Huku akiwa makini kuchangua maneno ya kuzungumza, Nape alisema malumbano hayo yanaonyesha kuna baadhi ya watu hawakuridhika na taarifa ya Kamati Teule ya Bunge iliyoongozwa na Dk. Mwakyembe, hivyo kuna ulazima wa hoja hiyo kurudishwa tena bungeni ili kukata mzizi wa fitna.

“Kuna kila dalili kuwa mafisadi wamejipanga kuhakikisha nchi haitawaliki, ndiyo maana mijadala isiyo na kichwa wala miguu inaibuka kila kukicha hata kwa mambo ambayo yamekwishaamuliwa na chombo kikubwa kama Bunge,” alisema.

Katika kuthibitisha kauli yake, Nape alisema ana taarifa za siri kuwa kuna baadhi ya mafisadi wamekuwa wakifanya mikutano ya faragha ambapo pamoja na mambo mengine, wamepanga kuhakikisha nchi haitawaliki kwa kuibua hoja na mijadala kupitia baadhi ya vyombo vyao vya habari.

“Tunakoenda ni kubaya, ila naamini serikali iko imara na CCM kama chama tawala, tutaomba tulizungumze kwenye vikao vyetu kwa nia njema ya kuliokoa taifa linalovurugwa na watu wachache wenye fedha,” alisema Nape.

Nape alisema ili kuhakikisha Tanzania haiyumbishwi, aliwataka wananchi kupuuzia mjadala wa sasa kwa madai kuwa hauna tija na una lengo la kuhatarisha amani na utulivu uliopo nchini.

Kuhusu mjadala wa ununuzi wa mitambo ya kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans iliyorithi kutoka Kampuni ya Richmond, kada huyo wa CCM alisema anashangazwa na uamuzi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), kuomba kibali cha Bunge au kamati zake.

“Kwani TANESCO wanapoenda kununua transfoma na vifaa vingine, wanaomba kibali cha Bunge? Kama si hivyo, kwa nini wanataka kuhalalisha ununuzi wa mitambo ya Dowans kupitia kamati za Bunge? Hata hivyo, Bunge lilishatoa msimamo wake juu ya hilo, kama kuna mtu hakuridhika, alirudishe bungeni na si kuwagawa Watanzania kwa mijadala isiyoisha na vitisho,” alisema Nape.

Mwanasiasa huyo machachari aliwataka mafisadi kutambua kuwa hata wakiibua mijadala ya kuwagawa Watanzania kama ilivyo sasa, hakutabadili ukweli kwamba Richmond na hata mrithi wake Dowans, ndio waliolifikisha taifa hapa lilipo.

Kwa upande wake, Mbunge wa Maswa, John Shibuda, alisema malumbano yanayoendelea sasa kati ya Dk. Mwakyembe na Rostam kumetokana na upepo wa kisiasa ambao wakati mwingine huleta tija katika kukuza demokrasia.

Hata hivyo, Shibuda ambaye hupenda kuzungumza kwa mafumbo, alisema mjadala huo umejikita kwenye hila na visa vya kufunika mema na mazuri ya mtu.

“Mimi naona hayo ni mapepo ya kisiasa na mtenguko wa fikra ambao umeleta mng’atuko dhidi ya dhulma, lakini ni mjadala wa heri kwa maana kuwa unawafanya watu kutoa manung’uniko yao, bila hivyo hali ingekuwa mbaya siku moja, kwa hiyo naona mjadala uendelee,” alisema Shibuda.

Mbunge wa zamani wa Morogoro Vijijini, Semindu Pawa (CCM), aliiambia Tanzania Daima jana kuwa, mjadala huo sasa umechacha na kuwataka waandishi wa habari kuachana nao.

“Mimi sitaki kusema nani yuko sahihi, lakini nasema mjadala huo umechacha, umepitwa na wakati, wanahabari mkiacha tu, hautausikia tena, lakini naweza kusema wanahabari ndio mnaoukuza, waacheni,” alisema Semindu Pawa.

Mwishoni mwa wiki, Dk. Mwakyembe alijibu tuhuma zinazomhusisha na kumiliki kampuni binafsi ya kuzalisha umeme kuwa ni kazi mahususi inayofanywa na majeruhi wa vita ya ufisadi, ambao waliumizwa na matokeo ya kazi ya Kamati Teule ya Bunge ya kuchunguza mkataba wa Kampuni ya Richmond, ambayo yeye alikuwa mwenyekiti wake.


Hatua ya Mwakyembe kujibu tuhuma hizo, ilikuja baada ya magazeti mawili ya kila siku, (si Tanzania Daima) kuchapisha habari zinazomhusisha yeye na umiliki wa hisa 1,000,000 zenye thamani ya jumla ya sh bilioni 1.5 katika Kampuni ya Power Pool East Africa Ltd.

Mbali ya habari hizo kuandikwa katika magazeti hayo mawili; moja la binafsi na jingine la serikali, nyaraka kadhaa zinazomhusisha Mwakyembe na kampuni hiyo, zimesambazwa katika mtandao wa intaneti.

Taarifa hizo pia zinamtaja Mbunge wa Lupa, Victor Mwambalaswa ambaye ni Mjumbe wa Bodi ya TANESCO, kuwa miongoni mwa wanahisa wa kampuni hiyo binafsi ambayo wakati fulani Mwakyembe alipata kuwa mtendaji mkuu wake.

Taarifa hizo zinajaribu kujenga hoja zinazojaribu kumuondolea Mwakyembe uhalali wa kuendelea kudai kupambana na ufisadi ndani na nje ya Bunge ilhali yeye mwenyewe akionekana kuwa na ukwasi mkubwa unaotiliwa shaka.

Pia zinaonyesha kuwa, Mwakyembe licha ya kuwa na hisa nyingi katika kampuni hiyo, ameisaidia katika mambo mbalimbali ambayo hata hivyo hayakufafanuliwa, wakati akiwa katika wadhifa wa mtendaji mkuu.

Kwa mujibu wa uchunguzi wetu, lengo kuu la kusambaza nyaraka hizo ni kujaribu kumnyoshea kidole Mwakyembe na kujaribu kumuondolea uhalali wa kuendelea kupigania sekta ya nishati ilhali yeye mwenyewe akijua kuwa na maslahi.

Mwakyembe ambaye kitaaluma ni mwanasheria, alisema kuwa katika Kampuni ya Power Pool East Africa Ltd, hakuwezi kukamsababishia akaingia katika mgogoro wowote wa kimaslahi kutokana na ukweli kwamba, kampuni hiyo iliyosajiliwa kwa Wakala wa Usajili wa Makampuni (BRELA), bado ipo katika hatua ya awali ya mradi ambao bado haujaanza kuzalisha.

Alipotakiwa kueleza ni kwa nini wakati alipoteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge iliyoichunguza Richmond kuanzia Oktoba mwaka juzi na kuwasilisha ripoti yake mwaka jana, hakueleza lolote kuhusu kuwa na kampuni ya kuzalisha umeme, Mwakyembe alisema asingeweza kufanya hivyo wakati mkakati wao wa kikampuni ukiwa katika hatua ya mradi tu.

‘‘Kwa mujibu wa sheria ya makampuni, majina yanakuwapo mpaka hapo kampuni itakapoanza ‘ku-take off’ (kuanza kazi). Sikuweza kuitaja kuwa ni sehemu ya makampuni yangu, kwa kuwa bado ilikuwa katika hatua ya mradi,” alisema Mwakyembe.

Mwanasiasa huyo alikwenda mbele zaidi na kuwaeleza wanahabari hao ambao miongoni mwao walionekana dhahiri kukabiliana naye kwa njia ya malumbano kuwa, hata wakati akiandikisha mali anazomiliki chini ya sheria ya viongozi kutangaza mali wanazomiliki, hakuitaja kampuni hiyo ya Power Pool kwa sababu hizo hizo za kutoanza kwake kazi.

Akifafanua tuhuma hizo dhidi yake, alimgeukia mbunge mwenzake wa CCM, Rostam Aziz na kumtuhumu kuwa nyuma ya habari zote mbaya zinazoandikwa dhidi yake.

Huku akilitaja jina la Rostam mara kadhaa, Mwakyembe alisema ni jambo ambalo haliingii akilini kwa mtu ambaye amechafuka kuamua kutumia maji taka kujisafisha.


WALA TUSINGEFIKA HAPA TULIPO IWAPO SHERIA INGEFUATA MKONDO WAKE.VINARA WALIOTUINGIZA MKENGE KWENYE UTAPELI WA RICHMOND HAWAJACHUKULIWA HATUA BAADA YA KUJIUZULU,NA SASA WAMEPATA JEURI YA KUTAKA KUTULIZA MARA YA PILI KWA KUTUUZIA MITAMBO MITUMBA ILEILE ILE YA RICHMOND a.k.a DOWANS.HUU MTINDO WA KULINDANA UTALIPELEKA TAIFA MAHALA PABAYA.

HOWEVER,LET IT BE KNOW TO MAFISADI AND THOSE WHO SHIELD THEM THAT IF THEY TURN OUR BELOVED COUNTRY INTO ANOTHER MADAGASCAR THEY TOO WOULDNT BE SAFE!

Wednesday, September 10, 2008

NIMEJIHAMI VEMA DHIDI YA MAFISADI-HABARI NDANI YA GAZETI LA RAIA MWEMA

Pamoja na kuchukua sabbatical leave ya lazima katika uandishi wa makala katika gazeti la Raia Mwema,blogu hii itaendelea kuwaletea kinachojiri kila wiki katika jarida hilo mahiri huko nyumbani.Miongoni mwa habari zilizochukua uzito wa juu katika toleo la wiki hii ni pamoja na kauli ya Spika wa Bunge la Muungano,Samuel Sitta,kwamba amejiandaa vya kutosha kufuatia taarifa kwamba watuhumiwa wa ufisadi wameingiza sumu huko Bongo kwa lengo la kuwadhuru Sitta na Mbunge wa Kyela,Dr Harrison Mwakyembe.Sidhani kama inahitaji kujumlisha mbili na mbili kupata jawaba as to akina nani watakuwa the usual suspects wa unyama wa aina hii.Zaidi BONYEZA HAPA kusoma habari hiyo na nyingine motomoto.

Sunday, March 02, 2008

TANZANIA NI MUHIMU KULIKO MASLAHI YA MTU BINAFSI (MAKALA NDANI GAZETI LA MTANZANIA)

MTANZANIA UGHAIBUNI

Sakata la mkataba wa Kampuni ya Richmond linaelekea kuchukua mwelekeo mpya kila kukicha. Ni rahisi kutafsiri kwamba suala hili lisipopatiwa ufumbuzi wa kudumu linaweza kuwa na madhara makubwa kwa nchi na kwa chama tawala, CCM.

Tangu ripoti ya “Tume ya Mwakyembe” ilipowekwa hadharani katika kikao kilichopita cha Bunge la Jamhuri ya Muungano, kumejitokeza kauli kadhaa za utatanishi ambazo japo zinaweza kuwa ni za kawaida tu, tafsiri ya ndani inaashiria matatizo makubwa huko tuendako.

Naomba niwe muwazi zaidi katika makala hii, na ningependa kutamka bayana kwamba sina nia ya kumshushia heshima yeyote nitakayemtaja. Lengo kuu la makala hii ni kuikumbusha kila pande inayoguswa na sakata hilo kutambua kwamba taifa letu ni muhimu zaidi kuliko maslahi ya mtu mmoja.

Naikumbuka sana siku taifa lilipotangaziwa kifo cha Baba wa Taifa.Watanzania wengi walitokwa na machozi sio tu kwa vile hawangemwona tena Mwalimu bali pia ni ile hali ya kutokuwa na uhakika taifa letu lingekuwaje bila Nyerere.Naamini kwamba laiti Mwalimu angekuwepo, baadhi ya upuuzi kama huo wa mkataba wa Richmond wala usingetokea, lakini ndio hivyo tena, hatuko naye duniani.

Wanaoilaumu “Tume ya Mwakyembe” kuwa imewaonea wanasahau kwamba tume hiyo haikuundwa baada ya Mwakyembe na wenzake kutuma maombi ya kuwa kwenye tume hiyo.Inashangaza wanaolalamika sasa kwamba ripoti ya tume hiyo ilikuwa na ajenda za kumalizana kisiasa,ilhali hawakuipinga wakati inaundwa na pale ilipokuwa ikitimiza majukumu yake.Ina maana ajenda hizo za kisiasa zilianza baada ya akina Mwakyembe kuwa wajumbe wa tume au zilikuwapo kabla.Kama zilikuwapo kabla,kwanini basi waliotajwa kuhusika na kuliingiza taifa katika hasara kubwa kwa mkataba huo wa kizembe hawakulalamika?

Na iwapo ajenda hizo zilianza baada baada ya wajumbe hao kuingia kwenye tume,kwanini basi watajwa walikimbilia kujiuzulu (huku wengine wakigoma waziwazi kujiuzulu kwa kuendelea kung’ang’ania madaraka) badala ya kudai haki itendeke?Ni rahisi kuhitimisha kuwa kelele zinazoendelea hivi sasa ni za mfa maji.

Nakumbuka kwenye miaka ya tisini nilipokuwa mwanafunzi wa sekondari ya wavulana ya Tabora (Tabora Boys) tulibahatika kutembelewa na Komandoo Salmin Amour.Nayakumbuka baadhi ya maneno yake ambayo kimsingi yalikuwa na lengo la kutupa changamoto ya mafanikio ya kielimu na hatimaye kufanikiwa maishani (japo sio kila mara kufanikiwa kielimu ni tiketi ya moja kwa moja ya kufanikiwa kimaisha).Alitueleza kwamba madaraka ni mazuri na kutupa mifano ya namna yeye kama rais alivyokuwa na wasaidizi kibao wa kuhakikisha kila kitu kinakwenda vema.

Nilikubaliana na Komando wakati huo,na nakubaliana nae sasa,kwamba madaraka ni mazuri na matamu,na ndio maana tunashuhudia hizi kelele zinazoendelea kutoka kwa waliokumbwa na zahma ya kisiasa baada ya skandali ya mkataba wa kampeni ya Richmond.Hakuna dhambi kwa madaraka kuwa matamu kwani hata njia ya kuyafikia sio nyepesi.Inahitaji jitihada na juhudi za kutosha kufikia hatua ya kuongoza watu wenye akili timamu.Na inatarajiwa kwamba mtu akishapata bahati ya kuwa kiongozi atatambua kwamba wengi,kama sio wote,wa aliokuwa akiwaongoza ni watu wenye akili timamu,uwezo wa kufanya maamuzi na wanaostahili heshima.

Waziri Mkuu aliyepita,Edward Lowassa,ameendelea kuonyesha kwamba japo aliamua kubwaga manyanga kwa hiari yake,alifanya hivyo huku roho ikimuuma.Nasema hivyo kwa sababu kauli zake za hivi karibuni zinaashiria wazi kwamba bado ana kinyongo kikubwa na matokeo ya uchunguzi wa “Tume ya Mwakyembe.”

Lowassa anaamini kwamba atarejea tena kwenye ulingo wa juu wa kisiasa kama Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi ambaye alipokuwa Waziri alilazimika kujiuzulu kutokana na skandali iliyoikumba Wizara yake.Tofauti ya msingi kati ya Mwinyi na Lowassa ni ukweli kwamba wakati Mwinyi alijiuzulu kutokana na tukio lililotokea mbali kabisa na mahala alipokuwa akifanyia kazi (lilitokea Shinyanga wakati ofisi ya Mwinyi ilikuwa Dar es Salaam),Lowassa alijikuta akikumbwa na shutuma kuhusu mkataba huo kwa vile katika hatua flani ulipita machoni mwake na akaamua “kusikiliza maamuzi ya wataalamu.”

Uongozi ni pamoja na kuwa na maamuzi ya haraka na yanayoangalia athari zinazoweza kujitokeza mbeleni iwapo yatafanyika maamuzi potofu.Haiyumkiniki kwamba Waziri Mkuu mzima anaweza kusikiliza ushauri mbovu na kuafikiana nao pasipo kujiridhisha iwapo ushauri huo ni wa manufaa kwa taifa.Hilo pekee linamvua sifa ya uongozi mtu yeyote aliye katika nafasi ya juu kitaifa.

Hivi kama mkataba wa Richmond ungekuwa na madhara ya moja kwa moja kwa familia ya Lowassa,kiongozi huyo angeendelea kusikiliza ushauri asio na uhakika na matokeo yake au angetaka kujiridhisha kwamba kilichokuwa kikifanyika hakingekuwa na madhara kwa familia yake?

Tukimweka kando Lowassa kwa muda,tumeshuhudia vituko vingine kutoka kwa Mkurugenzi wa TIC Emmanuel Ole Naiko ambaye anadai kuna dalili za “mauaji ya halaiki” dhidi ya watu wenye asili ya wilaya ya Monduli.Hizi ni hoja mufilisi ambazo kama zitaachwa bila kudhibitiwa zinaweza kuliingiza taifa kwenye matatizo yasiyo na msingi.


Hivi Ole Naiko amefanya utafiti wa kutosha kiasi gani kuthibitisha kwamba kuna mpango wa “ethnic cleansing” dhidi ya watu wa Monduli?Kwa hakika serikali inapswa kumhoji kwa undani mtu huyu mwenye heshima kubwa ndani na nje ya nchi kutokana na matamshi hayo ambayo yanaweza kabisa kuathiri hata utendaji wa ofisi yake (hakuna mwekezaji aliye tayari kuwekeza kwenye nchi inayoelekea kwenye “ethnic cleansing.”)

Kuna tetesi kwamba upo mkakati mkubwa wa “kujibu mashambulizi” dhidi ya ripoti ya “Tume ya Mwakyembe.” CCM imekuwa ikituaminisha kila siku kwamba vikao nje ya chama ni majungu,sasa basi inapaswa kuhakikisha kwamba wote wenye kudhani hawakutendewa haki wawasilishe malalamiko yao kwa ngazi hsuika katika chama hicho au hata bungeni.

Kama taarifa tunazozisoma katika vyanzo mbalimbali kwamba kuna mgawanyiko mkubwa ndani ya CCM kutokana na skandali la Richmond zina ukweli, basi ni muhimu kwa uongozi wa juu wa chama hicho kuachana na itifaki zake za kawaida za kuwasifia hata wanaostahili kukemewa na badala yake kuwawekwa “kiti moto” waeleze malalamiko yao mbele ya vikao halali badala ya kuendeleza mbinu za chini chini ambazo zinaweza kabisa kuathiri hali ya usalama wa nchi yetu.

Tusirejee makosa yaliyojitokeza katika mkataba wa Richmond ambapo baadhi ya watu walitahadharisha mapema kuhusu uhalali wa kampuni hiyo lakini wakapuuzwa.Kuna watu wanataka urais kwa kutimia njia yoyote ile hata kama kwa kufanya hivyo wanahatarisha uhai wa chama.

Lakini wakati tunawalaumu wanaolalamika kwamba wameonewa na “Tume ya Mwakyembe” tunapaswa pia kujiuliza kama hawapati jeuri hiyo kutokana na uzembe unaendelea wa kutowachukulia hatua wahusika.Pengine jeuri waliyonayo inatokana na ukweli kwamba wanaamini kuwa hakuna mwenye jeuri ya kuwachukulia hatua hasa ikizingatiwa kuwa baadhi yao wameishia kupongezwa kwa “ushujaa wao” badala ya kushutumiwa kwa hasara waliyoisababisha kwa taifa.

Nadhani anachopaswa kufanya Lowassa,Ole Naiko na wengine wote waliohusishwa na mkataba wa Richmond ni kutafuta msaada wa kisheria kuona haki inatendeka upande wao iwapo wanaamini kuwa hawakutendewa haki,badala ya kuendeleza hizi porojo ambazo kwa hakika zinaweza kuua kabisa ndoto zao za kurejea kwenye ulingo wa juu wa siasa za nchi yetu.Mahakama zipo,vikao vya chama vipo,sasa kwanini kelele za kuonewa zisipelekwe huko?TANZANIA NI MUHIMU ZAIDI KULIKO MASLAHI YA MTU BINAFSI.

BAADA YA KUMALIZA KUSOMA MAKALA HII,UNAWEZA KUANGALIA VITUKO VYA SIASA ZA URUSI AMBAVYO VIMEZAA TERM MPYA YA NANO PRESIDENT (as in iPod Nano).BONYEZA HAPA

HALAFU KWA WALE AKINA DADA "WENYE ULIMI MZITO",CLIP IFUATAYO INAWEZA KUWA YA MSAADA WA INA FLANI


Wednesday, February 20, 2008

CHINA,MAREKANI: BERLIN CONFERENCE MPYA (MAKALA NDANI YA RAIA MWEMA)

Makala yangu katika toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema inazungumzia UHURU.Inaanza kwa kuhabarisha kuhusu tangazo la Uhuru wa Kosovo,kisha inachambua "urafiki mpya" wa Marekani na China kwa Bara la Afrika na kuhitimisha kwamba urafiki huo ni mithili ya Mkutano wa Berlin 1884-5 ulioligawa bara la Afrika miongoni mwa wakoloni.Makala hii inakumbushia pia kwamba kuna uwezekano ziara ya Bush barani Afrika ikabaki kumbukumbu muhimu kwake kutokana na namna alivyonyenyekewa katika kipindi ambacho ni mmoja ya marais wanaochukiwa sana katika sehemu mbalimbali duniani,na very unpopular nyumbani kwake US of A.Kadhalika makala inawashikia bango Mwanyika na Hosea kwamba wajiuzulu haraka sana,sambamba na wale wote waliotajwa kwenye ripoti ya Tume ya Mwakyembe.Pamoja na makala nyingine zilizokwenda shule ya hali ya juu,bingirika na makala hiyo kwa KUBONYEZA HAPA.

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Hot Sonakshi Sinha, Car Price in India