Featured Posts

Showing posts with label TANZANIA. Show all posts
Showing posts with label TANZANIA. Show all posts

Wednesday, August 14, 2013

Uchambuzi wa Mwanaharakati Yericko Nyerere kuhusu Rwanda, Kagame, Museveni na Uvamizi DRC

Default Ijue Rwanda, Kagame, Mseveni na Uvamizi wao katika Ardhi ya Kongo

Rwanda ilikuwa eneo penye utawala wa kifalme tangu karne ya 16 BK kabla ya kufika kwa ukoloni. Mwanzo wake ni katika eneo la Ziwa la Muhazi. Watawala wenye cheo cha "mwami" kutoka kikundi cha wafugaji (Watutsi) walitanua himaya zao tangu miaka ya karne ya 16 BK hadi kufika eneo la leo hii. Wafugaji wa ng'ombe Watutsi walikalia nchi pamoja na wakulima wa Kihutu na wawindaji Watwaa.

UKOLONI WA KIJERUMANI

Ukoloni ulichelewa kufika Rwanda, mwaka 1890 Ujerumani na Uingereza walipatana ya kuwa Rwanda na Burundi ziwe ni sehemu ya Afrika ya Mashariki ya Kijerumani. Lakini ilikuwa mwaka 1908 tu ya kwamba Wajerumani walimtuma afisa wa kudumu aliyekaa Rwanda kama mwakilishi wa serikali ya Ujerumani. Mwaka 1916 Ubelgiji na Uingereza walivamia Rwanda katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia. Baadae ikawa chini ya Ubelgiji pamoja na Burundi kama "Rwanda-Urundi" katika hali ya eneo la kudhaminiwa kutokana na azimio la Shirikisho la Mataifa (UNO).


Utawala wa Wabelgiji ulikuwa wa moja kwa moja na mkali zaidi kuliko wa Wajerumani. Wabelgiji walijaribu kutoa faida ya kiuchumi wakilazimisha wenyeji kupanda mikahawa na kutekeleza kazi za serikali ya kikoloni. Katika utawala wao Wabelgiji walitumia zaidi Watutsi wakiwapa nafasi za elimu na kuwatumia katika shughuli za serikali. Wataalamu wengine huamini ya kwamba siasa hii ilisababisha kukua kwa chuki dhidi ya Watutsi kwa upande wa wakulima Wahutu iliyoleta kumwaga kwa damu baadaye.

Katika miaka ya 1950 ilionekana na kudhihirika ya kwamba ukoloni unaelekea mwisho wake. Uhusiano kati ya Wahutu na Watutsi ukawa vigumu kwa sababu Wabelgiji walibadilisha siasa yao yakupendelea Watutsi wakidai haki zaidi kwa ajili ya Wahutu waliokuwa wengi. Ni hasa wamisionari wa katoliki Mapadre Weupe waliosimama upande wa Wahutu wakiona ndio wagandamizwa.

Mwami Mutara Rudahigwa aliyejiita pia Charles alijaribu kuleta upatanishi kati ya vikundi katika nchi. 1954 aligawa nchi ya kifalme kati ya Wahutu na Watutsi. Lakini alikuwa na wapinzani Watutsi waliomua mwaka 1959. Mtoto wake Mwami Kigeri V. alisimikwa kwenye kiti hicho. Hatua hii ilisababisha ghasia na vurugu nchini kwa sababu Wahutu walidai kuwa na neno katika mabadiliko ya serikali. Mwezi wa Novemba 1959 Mwami Kigeri V. alilazimishwa kuondoka nchini akikimbilia Uganda. Watutsi wenye siasa kali walijaribu kumwua kiongozi wa Mouvement Democratique Republicain (MDR) chama kikubwa cha Wahutu. Wahutu walijibu kwa kuwashambulia na kuua Watutsi. Wabelgiji walitumia wanajeshi wao kupoza hali hiyo nchini Rwanda. Katika uchaguzi wa kwanza wa halmashauri ya tarafa na miji kabla ya uhuru chama cha Parmehutu ndicho kilichopata kura nyingi. Viongozi wa Parmehutu walitangaza serikali mpya mwaka 1961. Uchaguzi wa Bunge ulileta kura ya 77% kwa ajili ya chama cha Parmehutu kilichomchagua kiongozi wake Grégoire Kayibanda kuwa Rais.

Tarehe 01.07.1962 Rwanda ilipata uhuru wake kamili. Wakati huo zaidi ya Watutsi 350,000 tayari walishakuwa wamekimbilia nchi za jirani. Mwaka uliofuata vikundi vya Watutsi kutoka nchi hizo za jirani walijaribu kufanya mapinduzi kwa kushambulia serikali mpya wakitokea uhamishoni. Kitendo hicho kilifuatiwa na uangamizaji wa kwanza wa Watutsi zaidi ya 100,000 waliouawa na Wahutu.
Hata katika miaka iliyofuata mauaji dhidi ya Watutsi iliendelea. Wanasiasa Wahutu walizoea kuita Watusi ndio "Wadudu". Kila kitu kilichokuwa si sawa kilielezwa ni kosa la Watutsi waliokuwa raia bila haki. Idadi kubwa ya Watutsi walikimbia Burundi, Uganda na Tanzania.

Mwaka 1973 Generali Habariyama alimpindua rais Kayibanda na kuanzisha serikali ya kijeshi akijaribu kupatanisha vikundi ndani ya taifa. Lakini hata mwaka uliofuata 1974 mauaji ya Watutsi yalitokea tena.

Mnamo 1990 ilikuwa wazi ya kwamba Rwanda ilikuwa na hali ngumu. Kwa upande moja nchi za mataifa zilisukuma serikali za Afrika kuruhusu kura huru za kisiasa.

Katika Rwanda ongezeko la wakazi lilileta msongamano mkubwa na uhaba wa ardhi ya kilimo na Ufugaji. Uchumi ulikuwa duni, Wakati huohuo wapinzani Wahutu walikusanyika nje ya nchi hiyo kudai demokrasia. Na katika makumi elfu ya watoto wa Watutsi waliokuwa nje ya nchi hiyo, sauti zikasikika zilizodai warudi tena kuijenga Rwanda.

Habyarimana alijaribu kutafuta suluhisho na ungamano wa kitaifa, akaanza kujadiliana na Watutsi wa nje lakini alikutana na upinzani kwa upande wa Wahutu wakali waliochukia uelewano na Watutsi.


Safari ya Kagame na RPF kurudu Rwanda kutoka Uganda.

Oktoba 1990 Watutsi waliokaa Uganda walianzisha chama cha RPF (Rwanda Patriotic Front) wakiwa na wafuasi wahutu wachache wakavamia Rwanda kwa silaha. Kiongozi wao alikuwa Paul Kagame aliyeondoka Rwanda akiwa mtoto wa miaka minne. Alikuwa amejiunga na jeshi la Yoweri Museveni na kupanda ngazi katika jeshi la Uganda hadi kuwa mkuu wa huduma ya usalama ya kijeshi ya Uganda. Walitaka kulazimisha serikali ibadilishe hali ya Watutsi kuwa raia bila haki. Lakini uvamizi huu ulisababisha kuongezeka kwa ukali wa Wahutu dhidi ya Watutsi ndani ya Rwanda na siasa kali kwa upande wa viongozi Wahutu. Kikundi cha kihutu cha Interahamwe kilipewa silaha kujibu mapigo dhidi ya uvamizi wa Kagame, Maelfu ya Watutsi Warwanda waliuawa. Vita kati ya wapinzani kutoka Uganda na jeshi la serikali iliendelea mpakani hadi pande zote mbili zilikutana hapa Arusha Tanzania na kupatana kukoma kwa vita 1992 chini ya uangalizi wa Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika.

Sehemu ya viongozi Warwanda walijiandaa kutafuta utaratibu mpya lakini wengine walifanya mipango ya kumaliza swali la Watutsi kabisa wakipanga kuua Watutsi wote nchini.

Tarehe. 06.04.1994 rais Habariyama akirudi nchini kutoka safari ya Tanzania, Ndege yake ilipigwa kombora kabla ya kutua ikaanguka chini akafariki. Uwezekano ni mkubwa ya kwamba ni Wahutu wenye msimamo mkali ndio waliomua, lakini wengine walisema ni Jenerali Paul Kagame na RPF yake.

Tendo hili ilikuwa mwanzo wa mauaji ambayo hayakuwahi kutokea Afrika. Viongozi wa Interahamwe, wa jeshi la kitaifa na vikundi vikali vya Kihutu walitekeleza mipango ya kukusanya Watutsi kila mahali na kuwaua. Haiwezekani kuwa na idadi kamili lakini makadirio ya chini yanataja Watutsi 750.000 na Wahutu wasio wakali zaidi ya 100.000 waliuawa na Interahamwe na wanajeshi wa serikali ya Kihutu. Watu walikimbilia na kutafuta hifadhi makanisani lakini hata huko walichinjwa bila neema. Wahutu waliokataa kushiriki katika mauaji waliuawa pia.

RPF chini ya uongozi wa Paul Kagame iliamua kutumia nguvu zote kusimamisha machinjo haya. Kwa miezi miwili mauaji na vita yalienda sambamba hadi RPF iliposhinda Julai 1994 na kuchukua madaraka ya serikali.

Jeshi, Waparmehutu na serikali ya Kihutu walikimbilia Kongo wakiwalazimisha wakazi wengi kuongozana nao hali iliyosababisha kutokea kwa makambi ya wakimbizi makubwa sana katika Kongo ya mashariki yaliyokuwa na idadi ya Wahutu milioni mbili. Walio wengi wamerudi baada ya kuimarika kwa serikali mpya.

Tangu ushindi wa kijeshi mwaka 1994, RPF walianzisha serikali ya umoja wa kitaifa. Rais alikuwa Pasteur Bizimungu mwanasiasa Mhutu aliyeshikamana na RPF Kagame akiwa makamu wake. Baada ya kupinduliwa kwa Bizimungu mwaka 2000 Kagame akawa Rais. 2003 palitokea uchaguzi wa kwanza wa kirai ambapo chama cha RPF chimi ya Jenerali Paul Kagame kilishinda.

Jeshi la Rwanda limeendelea kuwa na vita ndani ya Kongo likipigana na mabaki ya Interahamwe waliokuwa wanashambulia Rwanda mara kwa mara kutoka Kongo.

Kutokana na mauaji hayo ya 1994, mahakama ya kimataifa iliyopo nchini Uholanzi imeendesha hukumu nyingi kwa wahusika wake, vilevile mahaka ya kimataifa ya Arusha nchini Tanzania nayo imeendesha huku stahiki kwa wahusika,

Ndani ya Rwanda mahakama za vijijini zinazoitwa "gachacha" vilevile zimejaribu kutoa hukuma juu ya waliohusija na mauaji ya mwaka 1994.

Mapatano ndani ya Rwanda yamezidi kushamiri, huku Paul Kagame akionsha kuijenga vema Rwanda kwa mkono wa chuma, Mathalani: D.Gasangwa wa EACU arisisitiza kwamba "Sometime in April(2004)" movie, ilikuwa "ETHNIC CLEASING", si HOLOCOSTI!, kama ilivyoandikwa na Wazungu wa Magazeti ya Ulaya. Watu karibu 600,000 waliuawa Rwanda, na hapo Mkoa wa Kivu, Congo.

Afrika ina ujuzi sasa; kama ujuzi wa Kiarabu, Kiswahili, Kilingala, Kiwolof, Kiamharic. Utengamano wa siasa mpya rasima utatupa na fasi ya kujenga inchi mpya kama EACU na Rwanda Kazembe.

Lakini huku mapambazuko mema yakitamalaki Rwanda, Kiongozi wa utawala wa nchi hiyo ndogo, anatajwa kuwa ni miongozi mwa viongozi makupe barani Afrika, ukupe wake sio waufisadi bali ukwasi wenye chembe za kiyunani

Lakini leo yale mabaki ya vikundi vile vya Interahamwe vilivyokimbilia uhamishoni kaskazini mwa Kongo mji wa Goma na Kivu si vikundi vya uasi dhidi ya Rwanda tena bali ni vitendea kazi muhimu dhidi ya upanuzi wa miliki mpya ya Watusi,

Wale watusi waliokimbilia Uganda enzi za Mwami Kigeri V, Inatajwa na kuaminika kuwa Jenerali Paul Kagame, Yoweri Mseveni na Watutsi waliokimbilia Goma baada ya kushika dola zao, walikuja na malengo mujarabu yanayotekelezwa kwa hatua na kwa vipindi virefu sana,

Mpango huo ulikuwa ni kusimika dola imara la Watutsi barani Afrika hasa nchini Kongo katika Goma-Kivu ya Kasiskani mpango siri walioupa jina la "Nchi mpya ya ahadi ya Watutsi". Ni mpango endelevu ulio na lengo la kuwakusanya Watutsi duniani kote na kuwaweka pamoja wakimiliki ardhi na rasilimali zake!

Hili linathibitika katika kile walicho "Mkataba wa kuigawa Kongo" ulisainiwa na Yoweri Mseveni, Paul Kagame na Laurent Kabila akiomba msaada wa kuingia madarakani kwa mtutu wa bunduki,

Naam baada ya Laurent Kabila kuingia madarakani kwamsaada wa Kagame na Mseveni kupitia ule mkataba, Kabila alikataa kuheshimu mkataba ule nakusema yale yalikuwa ni maneno ya porini tu hivyo hawezi kuiuza nchi kwa karatasi za mstuni!

Hapo sasa ndipo tunapoingia kwenye madhila ya Kongo tuliyoyaona tangu mauaji ya L. Kabila na tunayoyashuhudia hii leo chini ya J. Kabila, M23, Kagame na Mseveni

.............................. ...........

MKATABA WA KUIGAWA na KUIUZA KONGO 






Kinachoitwa vita vya sasa nchini Kongo ni utekelezaji wa “Makubaliano ya Lemera” ya mwaka 1996 yenye shabaha ya kuigawa nchi hiyo kubwa kuliko yoyote ile Afrika Mashariki na Kati.

Makubaliano yalifanywa kati ya Laurent Desire Kabila, akiwa kiongozi wa chama cha “kuikomboa Kongo” kutoka utawala wa dikteta Mobutu Sese Seko, kwa upande mmoja; na wapiganaji wa Kinyarwanda kutoka Rwanda na Mashariki mwa Kongo.

Makubaliano ambayo yalifanyika kwenye vilima vya Lemera vilivyoko Kivu ya Kusini na kujulikana kwa jina hilo, yalitaka Kabila, baada ya kuwa rais wa Kongo, aruhusu mikoa miwili ya Kivu Kaskazini na Kusini kuwa makazi ya Wanyarwanda wa kabila la Kitutsi.

Taarifa zilizopo zinaonyesha makubaliano yaliandaliwa mapema mjini Kigali na pale Lemera yalikuwa yanazinduliwa tu. Ilikubaliwa wakati huo kwamba hiyo ndiyo ingekuwa “asante” kwa Rwanda “kwa ukombozi wa Kongo.”

Desire Kabila alikuwa tayari amechoka. Kwa takriban miaka 20 alikuwa akipambana na utawala wa Mobutu Sese Seko. Alikuwa amefikia hatua ya kukata tamaa na kutulia jijini Dar es Salaam.

Mwaka 1996, mjini Kigali, Rwanda kilikuwa kimeundwa kikundi cha wapiganaji waliojiita “wapinzani wa dikiteta Mobutu.” Hawa walikuwa Wakongomani na Wanyarwanda kutoka Rwanda na wengine waliokuwa wakiishi mkoa wa Kivu Kusini, Mashariki mwa Kongo.

Katika kundi hilo alikuwemo Mkongomani, Jenerali Andre Kisasi Ngando; askari mtaalam wa kusomea. Anadaiwa kupata mafunzo nchini Cuba, Ujerumani na Bulgaria. Alikuwa akiongoza Wakongomani wapatao 600 katika kikundi hicho.

Wakati kikundi hicho kinataka kuanza vita, kilitaka kuwa na msemaji. Mungu akupe nini! Hakuna uthibitisho wowote, lakini taarifa zinaeleza kiliomba ushauri wa Mwalimu Julius Nyerere “ambaye aliwapa Laurent Desire Kabila kuwa msemaji wa wapiganaji.”

Mwanzoni mwa vita ya kumg’oa Mobutu kikundi hiki kilijulikana kama cha Wanyamulenge. Dunia nzima ikaambiwa na kuaminishwa kuwa hayo yalikuwa “maasi ya Wanyamulenge.”

Wanyamulenge ni watu wanaodaiwa kutoka kwenye vilima vya Mulenge vilivyoko wilaya ya Uvira katika mkoa wa Kivu Kusini. Makabila ya asili ya hapa ni Wavira na Wafuliro. Wanaojiita Wanyamulenge ni Wanyarwanda wakuja.

Vita vilianza kwa propaganda kuu kwamba serikali ya Mobutu haitambui Wanyamulenge ambao walidai ni raia wa Kongo; inawanyanyasa na inawanyima uraia. Haya yalikuwa madai makubwa sana yaliyovuta hisia kali na huruma kwa wapiganaji.

Wapinzani, chini ya Jenerali Andre Kisasi Ngando, na msemaji mkuu wao Laurent Kabila waliteka, kama mchezo, mji mkuu wa Kivu Kaskazini, Goma. Wakavuka Ziwa Kivu na kuingia Kivu Kusini.

Ilikuwa baada ya kukamata mji wa Bukavu, makao makuu ya Kivu Kusini na sehemu nyingi za mkoa huo, wapiganaji wa Kinyarwanda waliingiza pendekezo la rais ajaye wa Kongo, kutoa Kivu Kaskazini na Kusini kwa Rwanda.

Lakini kabla suala hilo nyeti kupewa uzito unaostahili, wapiganaji wa Kinyarwanda, baada ya kuteka Bukavu, wanadaiwa kuanza kupora mali – magari, vifaa vya nyumbani, dawa katika maduka – hatua ambayo ilielezwa kuwa uhamishaji wa mali za wakazi wa Bukavu na maeneo mengine.

Alikuwa Jenerali Ngando anayeripotiwa kupinga uporaji usiomithilika, jambo ambalo lilimletea uhasama kwa baadhi ya wapiganaji. Kuona hivyo, Laurent Kabila akamwasi Ngando.

Ngando anasemekana kuuawa siku chache baada ya kutofautiana na wapiganaji juu ya uporaji. Inaelezwa kuwa alimiminiwa risasi na kuuawa na mwili wake kuchomwa moto katika mbuga ya wanyama ya Virunga.

Kabila aliulizwa mara nyingi juu ya Ngando. Alikuwa na majibu tofauti. Akiwa bado msituni alisema Jenerali Ngando amekamatwa na majeshi ya serikali na mara ametekwa na wanamgambo wa Mai Mai.

Baadaye Kabila alisema Ngando alijeruhiwa na kupelekwa Ujerumani kwa matibabu. Na wakati akiwa rais, aliwaambia waandishi wa habari mjini Kinshasa kuwa Ngando alikuwa askari kama askari wengine na kwamba alikufa kwenye mapambano.

Ilikuwa baada ya kifo cha Jenerali Ngando ndipo Kabila aliingizwa kwenye makubaliano ya kumega Kongo. Kwanza, kikundi cha wapiganaji kiligeuzwa kuwa chama – AFDL – Alliance de front Democratique pour la Liberation du Congo.

Kabila akapanda cheo na kuwa kiongozi wa chama cha ukombozi wa Kongo kutoka kuwa msemaji tu wa wapiganaji.

Baada ya kuundwa kwa AFDL, jina la Wanyamulenge likatoweka kabisa. Wapiganaji wakaitwa waasi wa Kongo. Taarifa zinasema kabla wapiganaji kutoka Bukavu na kuanza safari iliyomfikisha Kabila madarakani, waliingia katika mkataba ambao ndio umekuja kuitwa “Makubaliano ya Lemera.”

Kuna madai kwamba viongozi wakuu wa wakati huo wa baadhi ya nchi walipata nakala ya makubaliano hayo ya kumega Kongo. Miongoni mwa nchi hizo ni Namibia, Uganda, Burundi, Zambia, Ethiopia, Eritrea, Zimbabwe, Angola, Namibia, Sudan na baadhi ya nchi za Ulaya na Marekani.

Imeelezwa kuwa makubaliano ni pamoja na kufanya mikoa ya Kivu Kaskazini na Kusini kutawaliwa na Wanyarwanda wa Kitutsi kutoka mataifa ya Rwanda, Burundi na Uganda; na kwamba utawala huo ambao ungefanya kazi kwa ushirikiano na serikali ya Kabila, ungetekelezwa kwa awamu tatu katika kipindi cha miaka 10 kuanzia 1998.

Chini ya mpango huo, raia wa Kongo, wakazi wa Kivu Kaskazini wangehamishiwa Kivu Kusini, “taratibu na kwa utulivu huku makazi yao yakichukuliwa” na wavamizi.
Imeelezwa kuwa hatua ya kwanza isingekuwa ngumu kwani Rwanda ingedai kuwa inapambana na wanamgambo wa Kihutu walioitwa Interhamwe ambao itaelezwa kuwa wanatishia amani nchini Rwanda. Hivyo ndivyo imekuwa ikifanya hadi sasa.

Makubaliano yanadaiwa kueleza kuwa kuchukuliwa kwa miji ya Goma na Butembo mkoani Kivu Kaskazini, sharti iwe hatua ya kwanza kwa kuwa hayo ndiyo maeneo yenye upinzani mkubwa. Kufanikiwa kwa awamu ya pili, kungetegemea mafanikio ya awamu ya kwanza, makubaliano yanadaiwa kueleza.

Wafuatiliaji wa mahusiano ya Rwanda na Kongo wanasema ingawa mpango huo ulishindikana kutekelezwa kuanzia mwaka 1998, kuingia kwa majeshi ya Rwanda nchini humo hivi sasa, ni utekelezaji wa hatua ya kwanza ya Makubaliano ya Lemera; na tayari miji ya Goma na Butembo iko chini ya kile kinachoitwa “majeshi ya ushirikiano” ya Rwanda na Kongo.

Kwa mujibu wa masimulizi juu ya makubaliano hayo, awamu ya pili ingekuwa kujaza wakazi wa Kaskazini katika Kivu Kusini na kufanya uchaguzi wa serikali za mitaa ambapo wazawa wangeenguliwa, kukosa uongozi na hivyo kunyimwa sauti.

Hatua nyingine ilikuwa kuanzisha benki ya kusaidia wavamizi katika Kivu mbili, kujenga nyumba zipatazo 600,000 na kujiimarisha katika nchi ya kigeni – Kongo.

Imeelezwa kuwa Kabila alikubaliana na masharti ya makubaliano kwa kuwa lengo lake lilikuwa moja tu: Kuingia ikulu ya Kinshasa kwa msaada wowote kutoka kwa yeyote; Mungu au shetani.

Ilikuwa baada ya makubaliano hayo, Kabila alisonga mbele na hatimaye kushinda na kuingia ikulu ya Kinshasa akiwa na wapiganaji wa Rwanda, akiwemo mkuu wa sasa wa majeshi wa Rwanda, James Kabarebe.

Baada ya kuingia ikulu, Kabila anadaiwa kuwageuka wenzake. Ilikuwa baada ya miaka miwili ya urais, alitangaza, tena kwa jeuri, kuwa wageni wote waondoke nchini. Aliongeza kwa kufafanua, kwamba Wanyarwanda warudi kwao na kusema anawashukuru kwa kazi waliyofanya.

Kabila alikuwa tayari amesoma mwelekeo wa makubaliano yake na kuona kuwa yanatoa mwanya kwa kile kilichoitwa “Nchi ya Ahadi” ya Watutsi kutoka Rwanda, Burundi, Uganda, Somalia, Ethiopia, Eritrea na Tanzania.

Alitakiwa atangaze, akiwa rais, kuwa Kivu mbili zote ni makazi ya Watutsi; ili hata wananchi wa Kongo watakaobaki humo, wawe wanafahamu kwamba siyo kwao.

Kabila alinukuliwa akisema kuwa hayo (Makubaliano ya Lemera) ni “makubaliano ya porini” na kwamba yeye hakuwa na madaraka ya kuuza nchi. Alisema hakatai kuwepo mkataba, lakini akataka hilo “lipelekwe kwa wananchi – kupitia bungeni – ili wananchi wenyewe waamue.”

Kilichomshangaza zaidi Kabila, baada ya kutangaza kuwa Wanyarwanda warudi kwao, ni kwamba aliyekuwa wa kwanza kuondoka na kukimbilia Afrika Kusini, alikuwa waziri wake wa mambo ya nje aliyeitwa Bizima Karaha (Bizimana Karahamuheto).
Katika mshangao na labda kejeli, Kabila alisema, “Kumbe nchi ilikuwa imevamiwa! Hata waziri wangu wa mambo ya nje alikuwa Mnyarwanda?”

Hiyo ilifuatiwa na kufukuzwa kwa James Kabarebe aliyekuwa mkuu wa majeshi ya Kongo na sasa mkuu wa majeshi ya Rwanda. Hatua hizi na nyingine, ndizo zilisababisha kutotekelezwa kwa Makubaliano ya Lemera.

Lakini wachunguzi na wafuatiliaji wa mahusiano ya nchi hizi mbili wanasema, makubaliano yameandikwa na yapo; hayajafutika. Kilichofanyika ni “ukaidi wa Kabila” wa kutotaka kutimiza ahadi yake baada ya kuingia ikulu.

Kabila anasemekana alikuwa amesoma kitabu cha Raphael Ntibazokiza kikieleza mahusiano ya Watutsi na wabantu, kiitwacho Plan de la colonisation tutsi au Kivu et region centrale de l’Afrique – Mpango wa ukoloni wa Kitusi katika Kivu na eneo la Afrika ya Kati.

Raphael anaandika, “Mhutu ameumbwa kufanyia kazi watu wengine; hawezi hata kujaribu kupata uongozi. Chukua nafasi zote za mikoa na wilaya na atakayekuwa mtawala ahakikishe kuwa analinda maslahi yetu... Baadaye watakapokuja kustuka, watakuwa wamechelewa…”

Mmoja wa waliokuwa karibu na Laurent Kabila amenukuliwa akisema hakuna kitu kilichomsononesha Kabila kama kauli ifuatayo ndani ya kitabu cha Raphael:
“Tutumie ukarimu wao. Tujinyenyekeze kwao kama sisi ni watumishi wao.

Tukiishachukua nafasi zao tuwatelekeze na ‘kuwalipa ujira wa nyani’- payez-les en monnaie de singe pour montrer leur incapacite – ili kudhihirisha kuwa hawana uwezo.”

Kabila aliuawa kabla hajamaliza kunyukana na Rwanda. Aliuawa na mmoja wa “watoto” wake – vijana wadogo waliokuwa watu wa karibu sana na waliomlinda tangu akiwa msituni.

Kuna maelezo tatanishi juu ya kifo chake. Kuna wanaodai aliyemuua alitumwa na waliokuwa wakitaka atekeleze makubaliano ya Lemera; lakini wengine wanadai ni karata za nchi za Magharibi.

Kwa kuwa Jonas Savimbi aliuawa katika wiki moja tu baada ya kifo cha Kabila, inadaiwa kulikuwa na mkono wa mataifa makubwa; hili likitaka kuingia Kongo na hivyo kuomba msaada wa kuondoshwa kwa Kabila huku likiwezesha kukamatwa na kuuawa kwa Savimbi. Siasa hizi hazijafafanuliwa.

Kuingia kwa Joseph Kabila, anayedaiwa kuwa mtoto wa kufikia wa Laurent Kabila, kunaonekana kuleta mgeuko mwingine kuelekea kule ambako “baba” yake alikataa.
Kinachoitwa makubaliano kati ya serikali ya Rwanda na ile ya Kongo kinaonekana wazi kuwa utekelezaji wa mpango wa awali ambao Laurent Kabila alikataa.

Aidha, kukamatwa kwa Jenerali Laurent Nkundabatware na kuhifadhiwa nchini Rwanda kunaelezwa kuwa sura kamili ya “kuheshimu kazi ya maandalizi aliyokuwa akifanya nchini Kongo.”

Kuna madai kuwa Nkundabatware, Mnyarwanda kutoka Rwanda, lakini Rwanda inasema ni Mkongomani, hakuwa na jeshi lolote nchini Kongo. Aliongoza majeshi ya Rwanda hadi hapo ilipoonekana kuwa mazingira yamekuwa mazuri kwa Rwanda kuingilia kwa kisingizio cha “kufukuza Interhamwe na kuweka usalama mpakani.”

“Hata akipelekwa Kongo leo hii, Kabila atamlinda Jenerali Nkundabatware, labda kama wakuu wa Kongo na Rwanda watakuwa wamegundua kuwa amewasaliti,” kimeeleza chanzo cha habari hizi mjini Goma.

Rwanda imeingia Kongo. Nani ataiondoa? Baadhi ya nchi jirani zimekuwa watazamaji tu wakati nyingine zikiwa katika maandalizi ya kunufaika kutokana na mgogoro wa nchi hii.

Moses Byaruhanga, waziri katika ofisi ya rais (Siasa) nchini Uganda, amesema nchi yake inaunga mkono “shirikisho la Kivu na Kisangani” na kwamba wanasubiri kuona serikali ya Kinshasa inalionaje suala hilo.

Katika siku za karibuni kumekuwa na taarifa za kukamilisha kumegwa kwa mikoa miwili ya Kivu Kaskazini na Kusini kutoka Jamhuri ya Kongo na kuzifanya muungano wa Jamhuri ya Kivu.

Kauli ya msemaji wa ikulu Uganda inaongeza uwezekano wa kuimega Kongo pale inapohusisha jimbo jingine la Kisangani ambako majeshi ya Uganda yanadai kuwinda waasi wa Lord’s Resistance Army (LRA).

Kiongozi wa LRA, Joseph Kony amekuwa akipambana na majeshi ya serikali ya Yoweri Museveni kwa zaidi ya miaka 15. Uganda sasa inadai kuwa Kongo inatumika kama kichaka cha waasi hao.

Kauli ya Uganda haipishani na mipango inayodaiwa kufanywa na Rwanda ingawa Rwanda, kupitia balozi wake mjini Dar es Salaam ilikaririwa ikisema haina mpango wowote wa kuigawa Kongo.

Jumuiya ya kimataifa imetekwa kwa propaganda za Interhamwe, Wanyamulenge, waasi wa LRA na kumbukumbu za mauaji ya kimbari.

Isipokuwa Barrack Obama ambaye angalau amesema anataka Kongo tulivu na kwamba atasaidia kuleta hilo, mataifa mengine, pamoja na Ufaransa, yanataka kuimega Kongo.


Vielelezo:

Moabi KKK/BKK
Yunani
Wikipedia
Tutsi
Hutu
Twa
Paul Kagame
Laurant Kabila
Yoweri Mseveni
MwanaHalisi

Mimi Mwenyewe

Thursday, July 18, 2013

Monday, June 03, 2013

Saturday, June 01, 2013

Dar tells Kigali: "It's up to you to take or turn down our advice"

The Tanzanian Foreign Minister Bernard Membe wondered at Rwandan government strange attitude to overreact on a simple advise given in good faith to the country in full presence of the Rwadan Delegation in Ethiopia saying it is up to them accept or refuse the advise.

The Foreign Minister also stated categorically that the government will not move even an inch to apologize Rwanda since he still believed that engaging the enemies was the best option for Rwanda which he said has failed to to find amicable solution through wars for more than 15engage the rebels in the last 16 years.

Speaking before parliament in Dodoma yesterday, the visibly irked Minister wondered as to why was making lots of politics with a simple advise that a they either dumed to accept or refuse to.

Using the famous quotation used once by the Former Israel Prime Minister, Yizak Rabin Mr Membe said "We negotiate peace with our enemies not our friends" adding that" there is no need for Rwanda to sound an alarm for the advise given in the open table in Ethiopia."
Assah Andrew Mwambene
Po box 9000 Dar es Salaam
Mobile +255782-553737
+255756887880

RWANDA’S REACTION TO PRESIDENT KIKWETE’S STATEMENT IS SHOCKING TO SAY THE LEAST!


On 26 May 2013 in Addis Ababa the UN Secretary General, Mr. Ban Ki-moon and the Chairperson of the African Union Commission Dr. Nkosazana Dlamini Zuma, convened the first meeting of the Regional Oversight Mechanism of the Peace, Security and Cooperation Framework for the DRC and Region. It was at this important meeting where the President of the United Republic of Tanzania, H.E. Jakaya Mrisho Kikwete made what many level headed commentators have referred to as candid and commonsensical remarks about the protracted conflicts in the Great Lakes Region. President Kikwete - a seasoned and consummate diplomat who has helped broker many peace deals in Africa - remarked that it was high time Rwanda and Uganda gave serious attention to peace talks with FDLR and ADF rebels respectively. He said, and correctly so, that it was evident the barrel of the gun cannot bring about the ultimate answer as testified by the recurrence of fighting in our region. He never condoned the role that the FDLR rebels played in the 1994 genocide. He was being reasonable and pragmatic. 

Rwanda should know better than any other country that there is no way Tanzania would condone or sympathize with the perpetrators of genocide. To make such insinuations is, quite frankly, a demonstration of breathtaking ignorance about Tanzania’s enviable and unparalleled history - the history of speaking out against any forms of crimes and injustices. Moreover, for Rwanda to make such insinuations is to show just what a short memory span this country has.

Admittedly, genocide brought about painful and unforgettable misery to the people of Rwanda but its spillover effects were felt well beyond its borders. The effects of genocide were felt right inside Tanzania which had to shoulder the burden of providing for thousands of Rwandan refugees. By the way, Tanzania has a long history of taking good care of Rwandan refugees both before and after genocide. The sons and daughters of the Rwandan refugees benefitted from Tanzania’s generous education system by studying, for free, at the country’s Universities and many of them are now occupying high positions in the Government of their motherland.

So given the foregoing, I have to say that I have been taken aback by our neighbors’ over-reaction to what was a completely innocuous statement by President Kikwete. Indeed, what the President said could (and should) have been said by other leaders a long time ago. What he said is a no-brainer!  It is commonsensical!  Negotiations have a much better chance of resulting into durable peace than the use of force. Thus, I find the reactions from Rwanda not only disturbing but also objectionable and utterly impudent! What is even more shocking is the discourteous behavior shown by the Rwanda’s Foreign Minister.  She seems to be getting too much big for her boots as to suggest that President Kikwete’s statement was absurd! She even has the audacity to ask that he should retract it. If anything, I think it is our Foreign Ministry which should summon the Ambassador of Rwanda in Dar es Salaam and ask him to clarify his Minister’s inadvisable utterances.

For far too long now the international community has adopted a softly softly approach with respect to Rwanda and this has meant that this tiny country gets away with literally everything, even murder. Rwanda has become like a spoiled child - untouchable and overly sensitive to everything even the slightest suggestion of censure.  Rwanda has a tendency of not taking kindly any form of criticism whether from within or without. And its leadership comes across as snobbish and delusional. May be the western countries’ plaudits about its so called success story have finally got into the heads of Rwandan leaders so much that they think they know it all.

For Rwanda to say that they cannot engage in talks with FDLR rebels because of their role in 1994 genocide is to allow themselves to be the captives of the past. History is replete with numerous instances of former sworn enemies burying their hatchets and extending an olive branch to one another for the sake of peaceful coexistence and future prosperity. This happened in South Africa where ANC and other progressive movements sat down with the perpetrators of one of the most brutal and inhumane policies in the history of mankind (apartheid) and agreed to work together in an inclusive and democratic society. Similarly, after many decades of committing some of the most heinous crimes against the people of Angola, UNITA is now part of the democratic government of that country. And in 2011, US and its allies initiated direct talks with some elements of the Taliban in Doha (Qatar), if my memory serves me well.
Rwanda should wake up and smell the coffee! Being delusional has not worked and won’t work.  It is now close to 20 yrs since the 1994 genocide and during all that time Rwanda has not been able to achieve its objectives visa vis FDLR rebels through the use of force.  Any sane person in Kigali should see the wisdom of changing the tactic/strategy which is, for all purposes and intents, what our President said in the Statement. Rwanda should understand that by calling for direct talks, Tanzania does not suggest, by any stretch of imagination, that the architects and executors of genocide should go scot free. Not at all! Talks can, and indeed should, offer the mechanism of dealing with known perpetrators of genocide by isolating them from non-perpetrators such as those born after 1994. This is just one example of approaching talks. I am sure there are many others.

But talking of genocide, am I wrong in recalling that even President Kagame himself was once found to be complicit in this crime by a French Magistrate? I recall that Rwanda’s reaction to this finding was, as we have come to expect, fast and furious to the extent of severing its diplomatic relations with France. Again, this goes to show that this “spoiled child” can’t stand any sort of censure or straight talking. I also recall that as recent as last year a UN report revealed that Rwanda’s Kagame had committed or assisted in committing genocide in DRC!

Despite all this compelling evidence, neighbors of Rwanda are still ready to engage that country in talks. Why can’t Rwanda show the same attitude? And lest he forgets, Kagame himself and his RPF henchmen come from a background of rebellion. They were rebels operating from Ugandan forests before taking over power in 1994. However, despite their “rebels” status they were invited and took part in the Arusha peace process of the early 1990s. 

Finally, I have a gut feeling that Rwanda doesn’t want FDLR rebels to go away that’s is why it is vehemently opposing the suggestion of talks which is one sure way of ending this conflict once and for all. This because, the perpetual presence of FDLR rebels in DRC gives Rwanda a convenient excuse to interfere in the DRC’s affairs thereby making the country ungovernable for its own economic and geopolitical interests. I read somewhere that Rwanda’s army – which is one of the biggest for a country of that economy and size - is mainly sustained by the exploitation of DRC’s natural resources. So, Rwanda goes into the DRC on the pretext that it is in hot pursuit of the FDLR rebels but in actual fact what it does is to plunder the resources.

And Rwanda is particularly angry with Tanzania because by being part of MONUSCO in DRC, its misdeeds will be exposed and curtailed by our non-nonsense troops. So the over-reaction to our President’s innocuous statement should not be seen in isolation. It is part of the frustration born out of the uneasy situation which Rwanda finds itself in as a result of our troops being part of the UN/SADC intervention force in DRC.
I submit.
Concerned Citizen


Monday, August 01, 2011

The Biggest Spending Tanzanian Embassies - Budget 2011/12

The Biggest Spending Tanzanian Embassies 

- Budget 2011/12

A Rapid Analysis of the biggest spending Tanzanian Embassies - Budget 2011/12
Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation Budget 2011/12
  • UN Missions alone to spend 5,051,259,000/-
  • Missions in Europe and Moscow to spend 12,481,913,000/-
  • Embassies in four EA capitals allocated 3,746,956,000/- 
  • The Africa allocation is 10,945,095,000/-
  • Administration costs nearly half of ministerial vote
  • Salaries for London mission the highest (Pensionable posts & non-pensionable) at 868,142,918/- and Kigali the lowest at 80,201,559/-

Programme 20 - Diplomatic MissionsTshs
Permanent Mission to the UN - New York2,882,502,000
Permanent Mission to the UN - Geneva2,168,757,000
Embassy of Tanzania - Paris2,133,493,000
Embassy of Tanzania - London2,009,942,000
Embassy of Tanzania - Moscow1,907,166,000
Embassy of Tanzania - Rome1,891,547,000
Embassy of Tanzania - Berlin1,776,946,000
Embassy of Tanzania - Washington DC1,714,958,000
Embassy of Tanzania - Abu Dhabi1,710,597,000
Embassy of Tanzania - Tokyo1,662,626,000
Embassy of Tanzania - Nairobi1,625,277,000
Embassy of Tanzania - Brasilia1,532,748,000
Embassy of Tanzania - Brussels1,465,353,000
Embassy of Tanzania - Ottawa1,367,032,000
Embassy of Tanzania - Beijing1,352,422,000
Embassy of Tanzania - Stockholm1,297,466,000
Embassy of Tanzania - Pretoria1,269,178,000
Embassy of Tanzania - New Delhi1,215,144,000
Embassy of Tanzania - Kuala Lumpur1,160,872,000
Embassy of Tanzania - Riyadh1,156,879,000
Embassy of Tanzania - Addis Ababa892,277,000
Embassy of Tanzania - Maputo873,151,000
Embassy of Tanzania - Kampala822,513,000
Embassy of Tanzania - Kinshasa797,422,000
Embassy of Tanzania - Abuja778,726,000
Embassy of Tanzania - Muscat765,066,000
Embassy of Tanzania - Harare722,034,000
Embassy of Tanzania - Lusaka692,592,000
Embassy of Tanzania - Bujumbura659,258,000
Embassy of Tanzania - Kigali639,908,000
Embassy of Tanzania - Cairo595,191,000
Embassy of Tanzania - Lilongwe577,568,000
TOTAL Programme42,116,611,000
Administration Programme 1038,486,246,000
Total of Vote 34 80,602,857,000
Less Retention Scheme funds14,872,492,146
Net total of vote65,730,364,854
 

Friday, June 17, 2011

Tanzania Uses Wall Murals For Sex Education


Like subway posters or highway billboards, wall murals have long been popular as a form of cheap advertising in Tanzania for such products as Coca-Cola, Pepsi and Kilimanjaro beer. But as GlobalPost's Iva Skoch has found, the murals have taken on a new, albeit more provocative, role: promoting sex education throughout Dar Es Salaam, the country's largest city.
Little is considered taboo in the colorful new ads, which depict everything from general condom use and masturbation to more severe topics like teen pregnancy and female genital mutilation. While the murals may often be done in a tongue-in-cheek manner, Tanzania's statistics are considerably less so. The current HIV rate hovers at about 6 percent, while 40 percent of 18-year-old girls are already mothers or currently pregnant.
Officials say the occasionally racy murals are already proving effective, and many local schools are opting to follow suit with their own sex ed walls. "If you use a photograph, people don't identify with the person," said Alex Ngaiza, HIV program manager at the health communication organization PSI. "But with a mural, everyone can relate."


Read the full article, and view the amazing full gallery, here.
See photos of Tanzania's sex education murals, courtesy of GlobalPost, below:



Monday, January 03, 2011

British Doctor Denied NHS Cancer help lives out her African dream (in Tanzania)



Smiling happily as she teaches medicine in Africa, this is the young doctor who was ‘betrayed’ by Britain’s healthcare postcode lottery.
Becky Smith, 30, was told she could be dead within 18 months after her breast cancer was missed four times and health chiefs refused to fund a breakthrough treatment.
The Daily Mail told in May how her local NHS trust had denied funding for the £23,000 treatment, despite it being freely available from 40 other trusts across Britain.

Dr Smith won a funding U-turn after the Mail highlighted her case, and has now had the drug therapy, which she hopes will help to prolong her life. Together with months of chemotherapy and other treatment, it has stabilised her condition and left her well enough to realise her dream of teaching her skills to doctors in Africa.

Dr Smith flew to Tanzania within days of finishing her latest round of chemotherapy, and has just completed a two-week stint of voluntary work at a hospital there.

She said: ‘I am so grateful that I have had this chance – I have no symptoms at the moment, I’m not ill and I don’t feel ill.
‘For the first time in months, I don’t feel like a cancer patient. It goes to show what is possible, even with a terminal diagnosis.
‘But it’s only possible if you’re given the treatment you need to give you a fighting chance.’

Dr Smith found a pea-sized lump in her left breast in April 2008, when she was 28 and working at High Wycombe Hospital in Buckinghamshire.

She went to her GP but was told to wait a month because she was considered too young to have breast cancer and it was more likely to be a cyst.

She returned to her doctor in June and was referred to a specialist cancer clinic at the John Radcliffe Hospital in Oxford. She was given an ultrasound scan and examination but was told the lump was a benign cyst which posed no risk to her health.
But by December 2008 the lump had grown to the size of a golf ball and she returned to see a third GP at her local practice. Again, her fears were dismissed.

Dr Smith, a urologist, then asked a cancer care nurse at her own hospital for help. A scan revealed three lumps in her breast and she was diagnosed with cancer the day after her 29th birthday.

Worse still, further scans found it had spread to her liver and her spine, where it was inoperable.

She had a mastectomy to remove the breast cancer, and doctors believe she could live for ten to 20 years with the tumours in her spine, if they can treat her liver cancer. Specialists recommended she receive Selective Internal Radiation Therapy, but her local primary care trust in Ryde, on the Isle of Wight, refused to fund it.

It said there was not enough evidence that it was cost-effective, or that it would be successful.
Dr Smith was faced with having to cancel her wedding to childhood sweetheart Simon Morton to pay for the treatment, or allowing her retired parents to remortgage their house.

Within days of the Mail reporting her plight, generous readers had pledged more than £12,000 to help her. But she won an appeal against the funding decision, and completed her last round of treatment in November.

It is too early to know if it has successfully shrunk the tumours in her liver enough for them to be removed or destroyed, but preliminary scans have shown an improvement.

Meanwhile, Dr Smith married her fiance, a chartered engineer, in July and was able to carry out charity work on the Tanzanian island of Zanzibar, where average life expectancy is just 47.

Before her cancer diagnosis, she had been due to do a year’s voluntary work at the Makunduchi Hospital on the island, but was forced to cancel it while she had treatment.

Dr Smith said: ‘It’s been wonderful to be back in a hospital and working alongside doctors again.’

SOURCE: Daily Mail

Wednesday, November 17, 2010

Umaskini wa kutisha Tanzania

• RIPOTI MPYA YA UNDP YAANIKA KILA KITU

na Tutindaga Mwakalonge

SHIRIKA la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), limetoa ripoti yake ya hali ya maendeleo duniani inayoichambua Tanzania kuwa moja ya nchi zilizo nyuma sana kimaendeleo kwa kuwa na watu wengi wanaokabiliwa na umaskini.

Ripoti hiyo inayopima maendeleo ya nchi husika kwa kutazama maendeleo ya watu wake ilizinduliwa rasmi jijini Dar es Salaam jana na kuitaja Tanzania kuwa nchi ya 148 kati ya nchi 169.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, katika kila Watanzania mia moja, 36 wanaishi katika hali mbaya sana ya umaskini, sawa na asilimia 36 ya watu wote, milioni 41.3.

Pia ripoti hiyo ya kimataifa imeonyesha kuwa katika kila Watanzania mia moja, 97 wanaishi kwenye umaskini wa kipato wa chini ya dola 2 za Marekani kwa siku, sawa na chini ya takriban sh 2,000 za Kitanzania kwa siku.

Aidha, ripoti hiyo iliyobeba kauli ya ‘Utajiri halisi wa mataifa’, imeonyesha kuwa katika kila Watanzania mia moja, 89 wametajwa kuishi chini ya dola moja ya Marekani kwa siku.

“Kwa takwimu hizo, Watanzania wengi wako katika umaskini wa kutisha kwa sababu ya kuwa na uwezo duni wa kifedha wa kumudu maisha yao ya kila siku”, alifafanua mtaalamu mmoja aliyehudhuria uzinduzi huo.

Hata hivyo, pamoja na takwimu hizo, Wizara ya Fedha na Uchumi, kupitia kwa Katibu wake, Ramadhani Khijjah, iliendelea kusifia mwenendo wa ukuaji wa uchumi nchini huku ikidai kuwa sekta za elimu na afya zimekuwa zikichochea ukuaji wa uchumi.

Friday, August 27, 2010

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Hot Sonakshi Sinha, Car Price in India