Featured Posts

Showing posts with label UNAFIKI. Show all posts
Showing posts with label UNAFIKI. Show all posts

Thursday, May 30, 2013

Mnafiki SITTA Aendelea Kuumbuka: Baada ya WASSIRA Kumwashia Moto, MAGUFULI mkana hadharani

Magufuli amkana Sitta, asema hana ubia naye urais 2015


Siku chache baada ya Waziri wa Afrika Mashariki Samuel Sitta kumhusisha Dk John Magufuli na kundi la urais la mwaka 2015, Waziri huyo wa Ujenzi, ameibuka na kupinga kauli hiyo, akisisitiza hafikirii kuwania nafasi hiyo.
Waziri Sitta alinukuliwa na gazeti hili juzi akieleza kuwa wakati ukifika, yeye na rafiki zake Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, Waziri wa Ujenzi, Dk Magufuli na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe, watachagua mmoja wao watakayeona anafaa kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015. Alisema hayo juzi kwenye Kongamano la Mawasiliano katika Nyanja za Digitali la wanafunzi wa Idara ya Uhusiano na Masoko, Chuo Kikuu cha St. Augustine (SAUT), Mwanza.
Kabla ya hapo alikuwa amewataja rafiki zake hao wakati wa hafla ya kuchangia Kanisa Katoliki, Josephine Bakita, Parokia ya Igoma, Mwanza, Jumapili iliyopita.
Alisema hatagombea tena ubunge mwaka 2015, baada ya kuwa katika ulingo wa siasa kwa miaka 35 na badala yake ataangalia namna nyingine ya kuwatumikia wananchi huku akigusia mchakato wa kuwania urais ambao alieleza anamwachia Mungu.
“Kwa ubunge nimekwishawaeleza inatosha, sitagombea tena kwani miaka 35 inatosha, … lakini hatima yangu ni nini siwezi kujua lakini nina afya nzuri na mmoja wa wanasiasa wakongwe, wenye afya nzuri, mnaona ninavyopendeza... kwa urais namwachia Mungu tutaona,” alisema Sitta.
Kauli ya Magufuli
Akizungumza na gazeti hili nje ya ukumbi wa Bunge jana, Dk Magufuli alisema haelewi msingi wa kauli ya waziri mwenzake huyo, kwani hajui chochote katika mtandao wa urais alioutaja.
Magufuli alisisitiza kusema hana kundi, hakuwahi kuzungumza wala kuhudhuria vikao vya kundi lolote, na kwamba kundi lake ni CCM na Mwenyekiti wake ni Jakaya Kikwete.
“Sina kundi. Sijawahi kuwa na kundi na sitarajii kuwa na kundi lolote. Ninachojua kundi langu ni CCM na kiongozi wake ni mwenyekiti wake, Rais Kikwete,” alisema Dk Magufuli.
Hata hivyo, Dk Magufuli pia alipuuza taarifa kuwa alichangia harambee hiyo akisema, “Si kweli, Mwanza sijatoa hata senti na hata siku ilipofanyika hafla hiyo, nilikuwa Dar es Salaam katika mkutano na makandarasi.” Licha ya kutajwa kuwa miongoni mwa vinara wa urais 2015, Magufuli alieleza kuwa hakuwahi kuzungumza na Sitta suala hilo linalohusu makundi ya urais mwaka 2015.
CHANZO: Mwananchi
WAKATI HAYO YAKITOKEA, JANA PIA ILIKUWA SIKU CHUNGU  KWA SITTA,KAMA INAVYOONYESHA HABARI HII HAPA CHINI
Wassira amvaa Sitta
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Mahusiano na Uratibu, Stephen Wassira, amemtaka waziri wa ushirikiano wa Afrika Mashariki Samwel Sitta, aweke wazi njia anazotumia kupambana na ufisadi nchini ambazo mawaziri wengine wa serikali ya CCM hawawezi kuzitumia.

Wakati Wassira akitaka ufafanuzi huo, Waziri wa Katiba na Sheria Mathias Chikawe kwa upande wake alikataa kuzungumzia mbinu anazotumia Samwel Sitta kwa kile alichoeleza kuwa hawezi kuongelea masuala ya serikali na mtu asiyemjua.

Wassira na Chikawe walitoa kauli hiyo jana wakati gazeti hili lilipotaka maoni yao juu ya kauli ya Sitta iliyonukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari akisema kuwa katika serikali nzima ni mawaziri wanne waliojipambanua kupambana na ufasadi na kutetea wanyonge.

Wassira alisema kwa sasa hawezi kuchangia jambo lolote juu ya kauli hiyo ya Sitta kwa kuwa hajaliona katika vyombo vya habari au kumsikia waziri huyo akisema hadharani.

Alisema kama kauli hiyo imetolewa na Sitta ni vema angefafanua mbinu anazotumia ili wengine waige.
“Mimi siwezi kuzungumzia hayo; mmeyasema nyie pia ingekuwa ni vema kama angeulizwa Sitta mwenyewe na atueleze mbinu zake tuone na wengine wanafanya nini,” alisema Wassira.

Alipoulizwa kama majina yaliyotajwa ni miongoni mwa makundi yanayodaiwa kujipanga ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM), kwa ajili ya urais wa 2015; Wassira alisisitiza jambo hilo aulizwe Sitta.

Kwa upande wake Waziri wa Katiba na Sheria Mathias Chikawe, alipopigiwa simu kwa ajili ya ufafanuzi wa kauli hiyo, alikataa kuzungumzia jambo lolote kwa madai kuwa alishajeruhiwa kwa kutoa habari kwa njia ya simu.

“Sitaki na sizungumzi mambo ya serikali na mtu nisiyemjua tena katika simu…siku moja alinipigia mtu akasema anatoka Daily News nilipompa habari akaandika anavyojua na ikaniletea matatizo, kwanza kwa sasa niko Arusha,” alisema Chikawe na kukata simu.

Juzi wakati Waziri Sitta, akishiriki harambee ya kuchangia ujenzi wa Kanisa la Mtakatifu Joseph katika Parokia ya Igoma jijini Mwanza, aliwataka Watanzania kujihadhari na watu wasio waadilifu katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka 2015.

Alisema watuhumiwa wa kashfa ya ufisadi wa kampuni ya kufua umeme ya Richmond na Dowans ni hatari na hawastahili kuungwa mkono katika uongozi.

Alisema kutokana na hali hiyo ya ufisadi yeye pamoja na mawaziri wengine watatu wako pamoja katika fikra za kupambana na vitendo vya kifisadi, uonevu na mikataba tata.

Aliwataja mawaziri hao kuwa ni Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe, pamoja na Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli.

Monday, April 06, 2009

MOTO ALIOUANZISHA MALECELA WAENDELEA KUSHIKA KASI NDANI YA CCM

MIMI SI MWANASIASA JAPO MALENGO YANGU YA BAADAYE NI KUWA MCHAMBUZI WA SIASA (POLITICAL ANALYST).BINAFSI SIICHUKII CCM ILA NAKERWA NA BAADHI YA KASUMBA ZILIZOOTA MIZIZI NDANI YA CHAMA HICHO KIKONGWE.NA KASUMBA KUU INAYONITATIZA KUHUSIANA NA CHAMA HICHO NI UNAFIKI.

JUZI JUZI TUMESIKIA KAULI ZA MMOJA WA WAKONGWE WA CCM,MZEE JOHN MALECELA,AMBAPO PAMOJA NA MAMBO MENGINE ALIAMUA "KUSIGINA DEMOKRASIA" KWA KUWATAKA BAADHI YA VIONGOZI WA CHAMA HICHO WANAOLUMBANA WAKOME MARA MOJA.>
SWALI LA MSINGI HAPA NI JE KWA KUKOMESHA MALUMBANO HAYO NDIO UFUMBUZI WA "KINACHOLUMBANIWA" UTAKUWA UMEPATIKANA?BUSARA NDOGO TU INAWEZA KUTUELEZA KWAMBA MTOTO ANAPOLIA INAWEZA KUASHIRIA KUWA ANA TATIZO (NJAA,KIU,ANAUMWA,NK).KUMFINYA MTOTO HUYO ANYAMAZE BADALA YA KUCHUNGUZA KINACHOMLIZA HAIWEZI KUWA SOLUTION YA TATIZO.

HUHITAJI KUWA MCHAMBUZI WA SIASA KUBAINI KUWA MALUMBANO YANAOENDELEA NDANI YA CCM NI MKINZANO WA WATETEZI WA UFISADI vs WAPINZANI WA UFISADI,WABINAFSI vs WANAOJUA JUKUMU LAO KWA TANZANIA,WANAFIKI vs WASEMA KWELI,NA MAKUNDI KAMA HAYO.KITU PEKEE KINACHOWEZA KUYAPATANISHA MAKUNDI HAYO NI KWA CCM KUWA WAZI-SI KWA MANENO PEKEE BALI KWA VITENDO-INASIMAMIA UPANDE UPI KATIKA MIKINZANO HIYO.IWAPO CCM IKISEMA INAPINGANA NA UFISADI HALAFU IKACHUKUA HATUA ZINAZOSTAHILI DHIDI YA BAADHI YA VIONGOZI WAKE WANAOTUHUMIWA KWA UFISADINI DHAHIRI BASI MALUMBANO YANAYOENDELEA YATAKOMA.LAKINI TUSITEGEMEE "UKIMYA" KWA HALI ILIVYO SASA AMBAPO,KWA MFANO, MTU KAMA MZEE WA VIJISENTI PAMOJA NA TUHUMA ALIZONAZO ANAENDELEA KUWA MJUMBE WA KAMATI YA MAADILI NDANI YA CHAMA HICHO.

KAULI YA MZEE MALECELA IMEANZA KUPATA SAPOTI KUTOKA KONA MBALIMBALI NDANI YA CHAMA HICHO.JANA,WAKONGWE FLANI WA CCM WAMEITISHA MKUTANO NA WAANDISHI WA HABARI AMBAPO PAMOJA NA MAMBO MENGINE WAMEKEMEA MALUMBANO HUKU WAKIONEKANA KUKEMEA BAADHI YA VIONGOZI WA CCM WALIOSHIKILIA BANGO VITA DHIDI YA UFISADI.KWA BUSARA ZA WAZEE HAWA,WANATAKA SUALA HILO LIACHWE MIKONONI MWA CCM.HIVI LAITI CCM INGEKUWA IMEMUDU KUFANYA HIVYO,AKINA MWAKYEMBE,KILANGO NA SELELII (KWA MFANO) WANGEKUWA WANAPIGA KELELE KUHUSU UFISADI?

WANACHOJARIBU KUFANYA WAZEE HAWA (PAMOJA NA MALECELA) NI KUJIAMINISHA KUWA HAKUNA TATIZO NDANI YA CHAMA HICHO,NA KELELE ZINAZOPIGWA NA BAADHI YA VIONGOZI WAKE NI SAWA TU NA UTOVU WA NIDHAMU.YALEYALE YA KUMFINYA MTOTO ANYAMAZE PASIPO KUFANYA JITIHADA ZA KUJUA KINACHOMLIZA.

KUNA WENZETU AMBAO KWA MTIZAMO WAO UKIZUNGUMZIA MABAYA YA CCM BASI UMETENDA KOSA LA JINAI.TATIZO LA WATU WA AINA HII NI KUPUUZA NAFASI YA CCM KATIKA ULINZI WA AMANI NA HATMA YA TAIFA LETU KWA UJUMLA.DHAMANA YA NCHI IKO MIKONONI MWA CHAMA HICHO KWA VILE NDICHO KILICHO MADARAKANI KWA SASA.SOTE TUNAWEZA KUBASHIRI KILICHO MBELE YETU IWAPO TUKIIRUHUSU CCM IENDESHE MAMBO INAVYOTAKA-HATA KAMA INATUPELEKA PABAYA-NA SIE TUENDELEE KUKAA KIMYA!

ANYWAY,HEBU SOMA BUSARA ZA WAZEE WETU HAWA HAPO CHINI:

Wenyeviti wastaafu wa CCM waonya

Wenyeviti wastaafu wa mikoa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamevunja ukimya na kuwataka viongozi wa chama hicho wanaotaka kuyatumia mapambano dhidi ya rushwa kama mtaji wa kisiasa na kujipatia umaarufu, kuacha mara moja. Sambamba na hilo, wazee hao wametaka mapambano dhidi ya rushwa yasiwe kichaka cha kuficha ubovu wa uongozi na kushindwa kuwajibika. Akizungumza kwa niaba ya wenyeviti wastaafu wa chama hicho Dar es Salaam jana, Mwenyekiti mstaafu wa Mkoa wa Dodoma, Pancras Ndejembi alisema mapambano dhidi ya rushwa ni ya CCM na si mwanachama binafsi au kikundi cha wanachama wachache.

“Tunashuhudia baadhi ya viongozi wa CCM kurushiana maneno wenyewe kwa wenyewe kwa kutaka kuonyeshana nani zaidi na nani ni vinara kuliko wengine katika mapambano dhidi ya rushwa, hii si sawa,” alisema Ndejembi aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa CCM Tanzania. “Tusingependa kuona mapambano haya yanatumiwa kama njia ya kujipatia umaarufu binafsi, mwenyekiti wetu Rais Kikwete ambaye ndiye jemedari wa mapambano haya humsikii anafanya hivyo na sisi wengine tusifanye hivyo…. kama wewe ni kiongozi na hutekelezi wajibu wako kwa wapiga kura wako wakikuuliza uko wapi, usisingizie kupigwa vita na mafisadi,” walionya.

Ndejembi aliyeambatana na wenyeviti wastaafu Hemed Mkali (Dar es Salaam), Tasil Mgoda (Iringa) na Jumanne Mangara (Pwani), alisema wazee hao wamesikitishwa na malumbano ya hadharani baina ya viongozi wa CCM ambao wengine wa ngazi ya juu ya uongozi ndani ya chama. Alisema tabia inayoonyeshwa na viongozi hao ya kushutumiana, kunyoosheana vidole, kuwekeana visasi, kuonyeshana ubabe na kuwekeana nadhiri ya kupambana baina ya viongozi, kunadhoofisha na kukipunguzia heshima chama hicho.

“Lakini pia kufanya hivyo hadharani, kwa nia ya kutaka kuungwa mkono katika shutuma na visasi hivyo kunajenga chuki, uhasama na migawanyiko katika jamii, viongozi hatupaswi kuwajaza watu chuki na uhasama ndani ya mioyo yao,” alisema Ndejembi kwa niaba ya wenzake na kutaka neno ufisadi lisitumiwe kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwakani. Alisema kumuita mtu fisadi kwenye vyombo vya habari haitoshi katika kushinda mapambano dhidi ya rushwa, bali watu waipigie kelele serikali iimarishe taasisi na vyombo vya kupambana na rushwa kama Polisi, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na Mahakama ambako watuhumiwa wanafikishwa.

Licha ya kuwapo malumbano baina ya viongozi hao wa CCM, wastaafu hao walisema kuhitilafiana ni kitu cha kawaida na kamwe watu wasitarajie chama hicho kitameguka. Wastaafu hao walieleza kumuunga mkono Rais Jakaya Kikwete iwapo atagombea tena urais mwakani na kutaka watu wengine wamuunge mkono, kwa maelezo kuwa anafaa kuongoza nchi. Walitoa sababu za kumuunga mkono kuwa ni kukubalika na anaowaongoza, anawapenda watu wote, mvumilivu, mkereketwa wa maendeleo ya wananchi na hana jazba.

Wazee hao walisema wameamua kuzungumza na waandishi wa habari kuhusu mambo hayo ili ujumbe uwafikie viongozi, wanachama na mashabiki wa CCM, lakini yote hayo waliyoyaeleza wameshayawasilisha kwenye vikao wanavyoshiriki vya matawi na mashina na wamezungumza na viongozi wa sasa wa chamahicho. Ingawa wastaafu hao hawakuwataja kwa majina viongozi wa CCM waliolumbana hadharani, lakini hivi karibuni Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe ambaye ni mwanahisa wa Kampuni ya kuzalisha umeme wa upepo ya East Africa Power Pool, amelumbana na Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz.

Dk. Mwakyembe anadai Rostam anatumia vyombo vyake vya habari kumchafua huku Rostam akitaka mbunge huyo ambaye kitaaluma ni mwanasheria na mwandishi wa habari, kuelezea mgongano wa maslahi wakati alipochaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini. Mbali na wazee hao, pia Makamu Mwenyekiti mstaafu wa CCM Tanzania Bara ambaye ni Mbunge wa Mtera, John Malecela alitaka malumbano hayo yakome, kwani hayana faida kwa mwananchi na wahusika watumie vyombo husika vya chama kufikisha malalamiko yao.
CHANZO:
HabariLeo

WITH ALL DUE RESPECT,BAADHI YA HAWA WAZEE NDIO WAMETUFIKISHA HAPA TULIPO KUTOKANA NA ITIKADI HIZIHIZI ZA "KUJENGA UMOJA NA MSHIKAMANO NDANI YA CHAMA" PASIPO KUANGALIA ATHARI ZAKE KWA JAMII KWA UJUMLA (AFTERALL,SIO KILA MTANZANIA NI MWANA-CCM).

HATUJACHELEWA.INAWEZEKANA IWAPO UZALENDO NA MASLAHI YA TAIFA YATAWEKWA MBELE YA (in front of) KUJIPENDEKEZA NA UNAFIKI.

Wednesday, February 27, 2008

UNAFIKI WA AKINA MWANDOSYA (MAKALA NDANI YA GAZETI LA RAIA MWEMA)

Makala yangu ndani ya toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema inazungumzia UNAFIKI: Ule wa Profesa Mwandosya kuitaka Dawasco isiwataje hadharani mawaziri wanaodaiwa maji na Mamlaka hiyo;ule wa Askofu Thomas Laizer wa KKKT Dayosisi ya Arusha kutumia neno la Bwana kuwapiga vijembe wanamwandama Lowassa,na ule wa "mabilioni ya EPA yanayorejeshwa kwa kasi."Makala hiyo imeanza kwa stori za hapa na pale,mambo ya muziki wa kufokafoka na albamu ya Jay-Z ya American Gangster ilivyosahau matatizo ya Black Americans.Stori hizo ni zinaunganishwa katika namna ile ile ya conversational style,napenda sana makala iwe mithili ya kupiga stori na msomaji,iwe kijiweni,kwenye pub,au hata barazani.Pamoja na habari na makala zilizokwenda shule,bingirika na makala hiyo kwa KUBONYEZA HAPA

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Hot Sonakshi Sinha, Car Price in India