Featured Posts

Wednesday, February 29, 2012

Kama JK alifanya Haya Akiwa Waziri,Ameshafanya Mangapi Zaidi Tangu Awe Rais?

Balozi Mahalu amlipua JK mahakamani 
Wednesday, 29 February 2012 07:31

Aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu
ANIKA ALIVYOSHIRIKI KATIKA MCHAKATO KIPINDI AKIWA WAZIRI MAMBO YA NJE, ASEMA ALIKUTANA NA MAMA MWENYE NYUMBA NA KUAGIZA ALIPWE DOLA MILIONI MOJA HARAKA, AKAMPA OFA KUJA MBUGA YA NGORONGORO 
Tausi Ally
ALIYEKUWA Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu ameiambia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa Rais Jakaya Kikwete wakati akiwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, alifahamu kuwepo kwa rasimu mbili za mikataba ya ununuzi wa jengo la Ubalozi wa Tanzania, Italia.

Profesa Mahalu alisema hayo jana mbele ya Hakimu Mfawidhi, Ilvin  Mgeta wakati akitoa utetezi wake dhidi ya kesi inayomkabili  ya uhujumu uchumi na kuisababishia Serikali hasara ya Euro 2,065,827.60 pamoja na aliyekuwa Ofisa Utawala wa ubalozi huo, Grace Martin.

Akiongozwa na wakili wake, Mabere Marando, Profesa Mahalu aliitambua barua ya Februari 20, 2002 ambayo ilikuwa ikieleza kuwa matayarisho yote ya ununuzi wa jengo la ubalozi huko Italia yamekamilika ikiwa ni pamoja na rasimu mbili za mikataba.

Mahalu alidai kuwa katika mchakato wa ununuzi wa jengo hilo wakati yeye akiwa Balozi chini ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, kulikuwa na rasimu mbili za mikataba na kwamba aliwahi kuwasiliana na wizara hiyo juu ya mikataba hiyo.

Alidai kuwa Desemba 2001, Kikwete wakati huo akiwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa alikwenda Rome, Italia kwenye Mkutano wa SADC na alipokuwa huko, ubalozi ulifanya mpango atembelee jengo hilo lililopendekezwa kununuliwa kwa ajili ya ofisi ya ubalozi.

“Wizara ya Mambo ya Nje ya Italia ilifanya mipango yote kwa kumpa utaratibu na usalama Kikwete ambapo alikwenda kutembelea jengo hilo na kukutana na mama mwenye jengo,” alidai Profesa Mahalu.

Alidai kuwa kabla ya mazungumzo na mwenye nyumba, mtoto wa mama huyo, Alberto alimtembeza Kikwete kwenye jengo hilo ndani na nje na baadaye mazungumzo hayo yaliendelea.

Balozi Mahalu alisema baadaye mazungumzo kati ya Kikwete na mama huyo yaliendelea na Alberto alikuwa akitafsiri, kwa sababu mama yake hakufahamu lugha ya Kiingereza.

Profesa Mahalu alidai kuwa katika mazungumzo hayo, Kikwete alimwuliza mama huyo: “Hivi ni kwa nini kunakuwa na mikataba miwili?” na mama huyo alimjibu kuwa hiyo ni kawaida kwa Italia ukitaka kununua jengo kwa bei nafuu.

Profesa Mahalu aliendelea kudai kuwa baada ya kupewa jibu hilo,  Kikwete hakuzungumza tena zaidi ya kucheka na kwamba mwenye jengo alimkumbusha kuhusu malipo ya awali ya dola milioni moja za Marekani ambapo aliafiki na kuahidi kuwa zingelipwa kabla ya mwisho wa mwaka 2001.
Profesa Mahalu alidai pia kwamba Kikwete alimweleza mama huyo kuwa atalishughulikia suala hilo baada ya kurejea Dar es Salaam na kumshukuru kwa kuwauzia jengo zuri.

Baada ya kutoa maelezo hayo, Profesa Mahalu alidai kuwa baada ya Kikwete kusema maneno hayo, alimgeukia na kumwambia: “Costa ni vizuri tupate hela tumlipe huyu mama watu wengine wasije wakachukua hili jengo.”

Profesa Mahalu alidai kuwa baada ya Kikwete kumshukuru mama huyo kwa ukarimu wake, alimkaribisha Tanzania awe mgeni wa Wizara ya Mambo ya Nje yeye na mumewe na kwamba watampeleka Ngorongoro.

“Tulipokuwa njiani tukirudi hotelini alipofikia Kikwete akiwa kwenye gari alimpigia simu Kibero akimuagiza afanye utaratibu wa kulipa Dola milioni moja kama malipo ya awali ya jengo hilo,” alidai Profesa Mahalu.

Alidai kuwa baadaye alimwagiza (Profesa Mahalu) aje Dar es Salaam kufuatilia mpango huo wa malipo ya awali ya ununuzi wa jengo hilo.

Awali, Profesa Mahalu akiongozwa na Wakili Alex Mgongolwa alidai kuwa anaitambua ripoti ya uthamini wa jengo hilo la ubalozi nchini Italia uliofanywa na Kimweri kutoka Wizara ya Ujenzi  aliyekwenda Rome Julai 15 hadi 26, 2001 kwamba jengo lilikuwa na gharama ya Sh6 bilioni.

Pia alizitambua ripoti za uthamini wa jengo hilo ambazo ni ile ya mama mwenye nyumba ambayo ilionyesha kuwa jengo hilo lilikuwa na thamani Sh5.500 bilioni na ripoti ya uthamini iliyofanywa na Serikali ya Italia iliyoonyesha kuwa jengo lilikuwa na thamani ya Sh11.117 bilioni.

Hakimu Mgeta aliiahirisha kesi hiyo hadi leo itakapoendelea kwa utetezi.

CHANZO: Mwananchi

Tuesday, February 28, 2012

Nigerian state governor funded international playboy lifestyle with £50m fraud

Nigerian state governor funded international playboy lifestyle with £50million fraud as he rose from humble roots working in London DIY store

  • James Ibori bought a portfolio of luxury London homes and a fleet of armoured Range Rovers
  • Fraudster may have stolen $250million from Nigerian coffers as he rose through the ranks
  • He spent £15,000 in two-day stay at London's The lanesborough hotel
  • He owned SEVEN properties in Britain
  • Ibori, 49, siphoned off millions by inflating state contracts
Last updated at 11:28 PM on 27th February 2012

His rise from DIY store worker to international playboy with a £250million fortune is the stuff of dreams.
A few years after quitting his £5,000-a-year job as a cashier for Wickes, James Ibori had become one of Nigeria's most influential and richest politicians.
He wasted no time spending his new-found wealth on luxury homes, top-of-the-range cars, five-star travel and fees at exclusive boarding schools.
Playboy lifestyle: James Ibori, 49, admitted a fraud totalling more than £50million. The former Nigerian state governor had a fleet of cars and six luxury properties in Britain
Playboy lifestyle: James Ibori, 49, admitted a fraud totalling more than £50million. The former Nigerian state governor had a fleet of cars and six luxury properties in Britain
But yesterday the 49-year-old stood shame-faced in the dock of London's Southwark Court as he admitted stealing tens of millions of pounds from the oil-rich state he governed in Nigeria. Scotland Yard detectives believe his fraud could exceed £250million.
He was on trial in the UK because much of the stolen money was laundered through his London office.
Ibori moved from Nigeria to West London in the late 1980s and was found guilty of stealing goods from the Wickes store he worked at in Ruislip in 1990.
 


A year later he was convicted of handling a stolen credit card. He moved back to Nigeria and worked for its president, Sani Abacha, as a policy consultant.
Rising quickly through the ranks of the ruling People's Democratic Party, he was voted governor of Delta State in 1999, winning re-election four years later.
In power, he systematically stole from the public purse, taking kickbacks and transferring state funds to his own bank accounts around the world.
Luxury: Property in Hampstead bought by Ibori for £2.2million in cash in 2001
Luxury: Exclusive home that Ibori bought in Hampstead, north London, with £2.2million in cash in 2001
He was helped by family members, including his wife Theresa, sister Christine Ibori-Ibie, his mistress Udoamaka Oniugbo, and Mayfair lawyer Bhadresh Gohil.
A massive police investigation into Ibori's activities revealed he had bought six properties in London, including a six-bedroom house with indoor pool in Hampstead for £2.2million and a flat opposite the nearby Abbey Road recording studios.
There was also a property in Dorset, a £3.2million mansion in South Africa and further real estate in Nigeria.
Extravagant: Ibori, 49, owned an apartment in this block on Abbey Road, London, opposite the famous music studios
Extravagant: Ibori, 49, owned an apartment in this block on Abbey Road, London, opposite the famous music studios
Fleet of cars: The former Nigerian state governor owned a number of cars including this Bentley Continental worth in the region of £150,000
Fleet of cars: The former Nigerian state governor owned a number of cars including this Bentley Continental worth in the region of £150,000
He owned a fleet of armoured Range Rovers costing £600,000 and a £120,000 Bentley. On one of his trips to London he bought a Mercedes Maybach for more than £300,000 at a dealer on Park Lane and immediately shipped it to South Africa.
He bought a private jet for £12million, spent £126,000 a month on his credit cards and ran up a £15,000 bill for a two-day stay at the Lanesborough hotel in London.
Prosecutor Sasha Wass told the court Ibori concealed his UK criminal record, which would have excluded him from office in Nigeria.
Extraordinary extravagance: James Ibori owned a fleet of armoured Range Rovers - including this one - bought with the proceeds of his £50million fraud
Extraordinary extravagance: James Ibori owned a fleet of armoured Range Rovers - including this one - bought with the proceeds of his £50million fraud
Large home: James Ibori's home in Abuja, Nigeria. Today he was facing a jail sentence after admitting a £50million fraud
Large home: James Ibori's home in Abuja, Nigeria. Today he was facing a jail sentence after admitting a £50million fraud
'He was never the legitimate governor and there was effectively a thief in government house,' Miss Wass said. 'As the pretender of that public office, he was able to plunder Delta State's wealth and hand out patronage.'
The court heard Ibori abused his position to award contracts to his associates including his sister and his mistress.
Scotland Yard began its investigation into Ibori after officers found two computer hard drives in his London office that revealed his criminality.
Fraudsters: Solicitor Bhadresh Gohil and James Ibori's wife Theresa who have already been convicted of money laundering
Fraudsters: Solicitor Bhadresh Gohil and James Ibori's wife Theresa who have already been convicted of money laundering
Guilty: Ibori's sister Christine Ibori-Idie and his mistress Udoamaka Okoronkwo who have both being found guilty of money laundering
Guilty: Ibori's sister Christine Ibori-Idie and his mistress Udoamaka Okoronkwo who have both being found guilty of money laundering
He was arrested by the Nigerian Economic and Financial Crimes Commission in December 2007, but two years later a court in his home town, Asaba, dismissed the charges saying there was not enough evidence.
When the case was reopened by Nigerian authorities in April 2010, Ibori fled to Dubai where he was detained at the request of the Metropolitan Police and extradited to the UK last April.
In a packed courtroom Ibori, dressed in a dark grey suit and black shirt, appeared in the dock to enter ten guilty pleas to fraud, money laundering and conspiracy on what was due to be the first day of a 12-week trial.
Luxury: Property in Lagos
Property: Kenton, north-west London
Luxury: Homes he owned in Lagos, Nigeria, and Kenton, north-west London
One of Christine Ibori-Ibie's London properties
One of Udoamaka Onuigbo's London properties
Homes: An apartment owned by Ibori's sister Christine Ibori-Ibie in Brent, north-west London (left) and a London property (right) owned by his mistress Udoamaka Onuigbo
His wife, his mistress and his sister were all jailed for five years each for money laundering offences following earlier trials.
Last March, Gohil, 46, and described as Ibori's London-based lawyer, was jailed for seven years for his role in the scam.
Attempts will be made to confiscate as much of Ibori's money and assets as possible so that they can be returned to Nigeria.
The Met's Detective Inspector Paul Whatmore said: 'It is always rewarding for anyone working on a proceeds of corruption case to know that the stolen funds they identify will eventually be returned to some of the poorest and most vulnerable people in the world.'
Ibori will be sentenced on April 16 and 17.
Luxury: One of Udoamaka Onuigbo's London properties
James Ibori's property in the West Country Bought in 2005 for £311,000
Fraud: A flat owned by Udoamaka Onuigbo, Ibori's mistress, in central London (left) and a property he bought in Shaftesbury, Dorset, for £311,000 in 2005 (right)


SOURCE: Daily Mail

Monday, February 27, 2012

Ize Komedi Shoo ya King Kinya (KATUNI)


kATUNI KWA HISANI YA kING kINYA NA gLOBAL PUBLISHERS.

Sunday, February 26, 2012

Kazi Mpya ya Msanii Jahson (AUDIO)




Song Push Dem
Artist:Jahson
Producer:Washingtone in Uganda

Wapende Au Wachukie Lakini Wapopo Wanazidi Kutuacha (Story and Videos))


Kwa Waafrika wengi,na pengine kwingineko ulimwenguni,Wanigeria wanatamba kwa sifa kuu mbili;moja mbaya  na nyingine nzuri.Mbaya ni tabia yao ya utapeli ambapo ni bora kulala na chatu mwinye njaa kuliko kumwamini Mpopo.Wenye uzoefu nao wanajua ninamaanisha nini.Sifa yao nzuri-hasa kwa wanaume ni kutamba katika soka takriban kila kona ya dunia.Inayoambatana na hiyo ni mfaniko makubwa waliyonayo wengi wao-hasa nje ya nchi (usiulize wameyapataje).

Katika hili la mafanikio,juzi juzi tu tumesikia wanamuziki kadhaa wa Kipopo wakivamia anga za muziki nchini Marekani ambapo tayari majina makubwa kama Snoop Dogg na Akon wameshafanya kazi nao.D'Banj kwa sasa anafanya kazi kwenye lebo ya G.O.O.D Music ya Kanye West



Kwa upande mwingine,wanamuziki maarufu wa Kinigeria P.Square, 2Face Idibia na Whizkid wamesaini kwenye lebo ya Konvict ya Akon.



Na wiki hii,gazeti maarufu la nchini Marekani la New York Times lina makala ndefu kuhusu kiwanda cha filamu za Nigeria kinachojulikana kama Nollywood.Unaweza kusoma makala hiyo ndefu HAPA.

Maendeleo haya ya wasanii wa kipopo yanaweza kuwa changamoto kubwa kwa wasanii wetu huko nyumbani.Japo kuna dalili kidogo za kutia matumaini baada ya wasanii AY na Jay Mo kushirikiana na wasanii wa kimataifa,kimsingi wengi wa wasanii wetu wanaendelea kutafsiri mafanikio kwa kigezo cha umaarufu ndani ya Tanzania (na kidogo kwa Afika Mashariki) na kuendekeza zaidi shoo za hapa na pale.



Tamko la Vinega Juu ya Makubaliano ya Sugu ya Ruge

Ifuatayo ni taarifa niliyotumiwa kutoka kundi la VINEGA kuhusu maafikiano yalifikiwa hivi karibuni kati ya Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi (a.k.a SUGU) na mmoja wa Wakurugenzi wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba.Ninaomba kuiwasilisha kama ilivyo:


Tamko La Vinega Juu Ya Makubaliano Ya Sugu Na Ruge

Saturday, February 25, 2012

Twitter 2012: The Freshest Statistics on the King of Microblogging Services

Friday, February 24, 2012

Aibu: Mume wa Rais wa Denmark Abambwa Akikodolea Macho "Eneo Nyeti" la Princess (VIDEO)

First Man of Finland caught gawping at Danish princess's breasts

The husband of Finland's president was caught on camera casting an admiring glance at the cleavage of Princess Mary of Denmark.






Pentti Arajarvi, Finland's "first gentleman", cast a glance as he sat next to the princess during a state dinner hosted by her mother-in-law, Queen Margrethe of Denmark.
As all eyes turned towards one of the evening's many speeches, Mr Arajavi's roamed down the neckline of the 43-year-old princess.
When she turned to face him, his gaze jerked upward and for a few awkward moments he pretended to be admiring the ceiling of the Amalienborg Palace in Copenhagen.
An alarmed Princess Mary raised a protective hand over her neckline as Mr Arajavi, 63, continued to squint upwards.
The incident provoked a scathing reaction in the Danish press and is unlikely to do much for the country's relationship with neighbouring Finland, which is governed by Mr Arajavi's wife, Tarja Halonen.
It carries echoes of the 2009 G8 summit in Italy when Nicolas Sarkozy was accused of leering at the figure of a shapely Brazilian woman.


SOURCE: Daily Telegraph

Thursday, February 23, 2012

Mheshimiwa John Mnyika aikalia kooni DAWASCO,Aituhumu Kukiuka Mikataba,Ataka Hatua za Haraka


Tamko la Mbunge wa Ubungo kupitia Chadema,Mheshimiwa John Mnyika kuhusu tatizo za upatikanaji wa maji jijini Dares Salaam na ubabaishaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka (Dawasco):


THURSDAY, FEBRUARY 23, 2012


DAWASCO imekiuka mikataba; hatua za haraka zinahitajika kuboresha upatikanaji wa maji DSM

Kampuni ya Maji Safi na Maji Taka (DAWASCO) imekiuka mikataba miwili muhimu inayoongoza kazi zake na kusababisha matatizo ya maji katika Jiji la Dar es Salaam ikiwemo maeneo mbalimbali ya Jimbo la Ubungo.


Imenibidi nitoe taarifa hii kwa umma kwa nilitumia taratibu za kawaida za kiofisi tarehe 14 Februari 2012 kuiandikia barua DAWASCO kuchukua hatua kuhusu tatizo la kutozingatiwa kwa ratiba ya mgawo wa maji katika Jiji la Dar es salaam hali ambayo imesababisha kero ya maji katika maeneo mbalimbali ya jimbo la Ubungo.


Hata hivyo DAWASCO haikujibu barua husika kueleza hatua ambazo imechukua, hivyo natoa mwito wa wazi wa siku tatu kwa DAWASCO kufanya ukaguzi wa mtandao wa maji na kurekebisha kasoro zilizopo na kutoa taarifa kwa umma kuhusu matitizo ya maji yanayoendelea katika maeneo mengi ya Jiji la Dar es salaam ikiwemo katika Jimbo la Ubungo. 


Kazi ya mbunge kwa mujibu wa katiba ni kuwawakilisha wananchi, kutunga sheria na kuisimamia serikali hivyo nakusudia kuchukua hatua zaidi za kibunge dhidi ya DAWASCO iwapo haitazingatia masharti ya mikataba husika na kushughulikia matatizo ya maji yanayoendelea hivi sasa katika jiji la Dar es salaam ikiwemo katika Jimbo la Ubungo.


Ikumbukwe kuwa DAWASCO ni shirika la umma lililoundwa kwa tangazo la Serikali nambari 139 la tarehe 20 Mei 2005 kwa mujibu wa Sheria ya Mashirika ya Umma ya mwaka 1992.


Tarehe 1 Julai 2005 DAWASCO ilipewa mkataba wa ukodishaji (lease agreement) na DAWASA ambao unaitaka DAWASCO kuendesha miundombinu ya maji na kuhakikisha matengenezo ya mtandao wa maji katika jiji la Dar es salaam.


Aidha, katika kutekeleza mkataba huo DAWASCO inapaswa kuzingatia mkataba wa huduma kwa wateja (Client Service Charter) ambao unaitaka DAWASCO kushughulikia kwa muda maalum malalamiko ya wateja na kutoa taarifa kwa umma kila panapokuwa na matatizo ya maji.


Kwa mujibu wa mkataba wa huduma kwa wateja DAWASCO inapaswa kushughulia malalamiko ya wateja na kuyajibu ndani ya siku tano na iwapo matatizo yaliyopo yanahitaji hatua za kiufundi; DAWASCO inatakiwa kushughulikia matatizo hayo ndani ya siku 30.


Kuanzia mwishoni mwa mwezi Disemba 2011 mara baada ya maafa ya mafuriko katika Mkoa wa Dar es salaam mpaka leo tarehe 22 Februari 2012 nimepokea malalamiko mbalimbali toka kwa wananchi kuwa hali ya upatikanaji wa maji katika kata mbalimbali za Jimbo la Ubungo sio nzuri kama ilivyokuwa baada ya hatua ambazo tulichukua kwa nyakati mbalimbali kuanzia Januari 2011 mpaka Septemba 2011.


Itakumbukwa kwamba tarehe 5 mwezi Septemba 2011 nilifanya maandamano ya kwenda DAWASCO nikiwa na wawakilishi wa wananchi wa kata mbalimbali za Jimbo la Ubungo ambapo tulifanya mkutano na Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASCO. 


Kufuatia mkutano huo DAWASCO ilichukua hatua mbalimbali ambazo ziliboresha mgawo wa maji katika maeneo kadhaa ya Jimbo la Ubungo kabla ya ratiba ya mgawo kuvurugika kufuatia mafuriko yaliyokumba mkoa wa Dar es salaam.


Hata hivyo, baada ya mafuriko hayo DAWASCO haikuchukua hatua zinazostahili kwa wakati na kuachia kurejea tena kwa mtandao haramu wa biashara ya maji wenye kuhujumu wananchi hususan wa kipato cha chini katika Jiji la Dar es salaam ikiwemo katika maeneo mbalimbali ya Jimbo la Ubungo.


Hivyo, bodi ya wakurugenzi ya DAWASCO chini ya uenyekiti wa Mhandisi Suleiman Said Suleiman na Mtendaji Mkuu wa kampuni Jackson Midala wanapaswa kurekebisha kwa haraka mfumo mzima wa ufuatiliaji wa DAWASCO kuwezesha ukaguzi wa ufanisi wa mtandao mzima wa maji.


Katika kipindi hiki cha matatizo makubwa ya maji katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es salaam ikiwemo katika kata mbalimbali za Jimbo la Ubungo DAWASCO iache kuwatumia wafanyakazi wanaohusika na ukaguzi kufanya kazi tofauti za kusoma mita na kugawa Ankara badala yake wafanyakazi tajwa wafanye ufuatiliaji wa dharura wa ufanisi wa mtandao mzima wa maji katika maeneo mbalimbali.


Baadhi ya maeneo ambayo yanapaswa kutembelewa ni kata za Makuburi, Kimara, Saranga, Mbezi Luis, Msigani, Kwembe, Goba, Kibamba, Sinza, Makurumla, Mabibo, Manzese, Ubungo na Mburahati. 


Kwa upande mwingine, kwa kuwa mkataba wa huduma kwa wateja unatoa haki kwa wateja wa DAWASCO lakini pia unaeleza wajibu; natoa mwito kwa wananchi katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es salaam kutimiza wajibu wa kuwaelekeza wakaguzi husika mitaa yenye matatizo katika mtandao wa maji ili hatua ziweze kuchukuliwa.


Mkataba huo unawataka wateja wa DAWASCO kutoa taarifa kuhusu uharibifu wa miundombinu, wizi wa maji na kuhusu matatizo ya maji hivyo wananchi watoe taarifa husika na kufuatilia wakaguzi kufika maeneo yao kwa kupiga nambari ya bure 0225500240 au 0762979627 za DAWASCO makao makuu.


Pia, wananchi wanaweza kuwasilisha kero za maji kwa ofisi ya DAWASCO zilizo katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es salaam na kupitia nambari zifuatazo: Temeke +255 775016184, Ilala +255 775048556, Magomeni +255 775016179, Boko/Tegeta +255 775048553, Tabata +255 775016181, Kawe +255 775016185, Kinondoni +255 775016180 na Kimara +255 775048554. 


Wananchi watumie pia nafasi hii kuwasilisha kwa DAWASCO maelezo na vielelezo kuhusu maeneo ambayo hakuna miundombinu ya maji kabisa au miundombinu iliyopo haijawahi kutoa maji kwa kipindi kirefu kwa ajili ya kutaka hatua za ziada. 


Matatizo ya maji katika maeneo mengi ya jiji la Dar es salaam ikiwemo katika Jimbo la Ubungo yamedumu kwa miaka mingi, wananchi wametupa wajibu wa kuwawakilisha kuisimamia serikali na mamlaka zake kupunguza kero husika kwa haraka hivyo wananchi watarajie vitendo zaidi vya kushinikiza uwajibikaji kwenye sekta ya maji katika kipindi cha karibuni.


Imetolewa tarehe 22 Februari 2011 na:


John Mnyika (Mb) 

Makala Yangu Katika RAIA MWEMA Wiki Hii : "DCI Manumba Amewasiliana na Wizara ya Afya ya Nchi Gani?"


DCI Manumba amewasiliana na Wizara ya Afya ya nchi gani?

Sumu ya Dk. Mwakyembe
Mwakyembe, Sitta wajiuzulu kutumikia Serikali wanayoituhumu
MIONGONI mwa matukio ya kukumbukwa ya Bunge lililokuwa chini ya Spika wa zamani, Samuel Sitta ni tuhuma kwamba mmoja wa wabunge alifanya vitendo vya ushirikina.
Japo suala hilo lilimalizwa kimya kimya, ukweli unabaki kuwa lilikuwa ni la kuaibisha na pengine kudhihirisha upungufu mkubwa kwa baadhi ya watu tuliowakabidhi jukumu la kutuongoza.
Na kama ilivyozoeleka kwenye masuala mengi yenye utata, Watanzania hawakuwa na jinsi ya kudai ukweli kuhusu suala hilo. Kwa upande mmoja huwezi kuwalaumu hasa ikizingatiwa kuwa, wengi wao wanahangaika tangu mawio hadi machweo kuhakikisha ‘mkono unakwenda kinywani.’ Kwa upande mwingine, watawala wetu wamejitengenezea mazingira ambayo mwananchi wa kawaida hawawezi kudadisi ‘upuuzi’ wao (kama huo wa madai ya ushirikina bungeni).
Lakini pengine kikubwa zaidi ni ukweli kwamba kama hadi leo hii watawala wetu wamegoma kabisa kutuambia kuhusu wahusika wakuu wa ujambazi wa mchana kweupe (daylight robbery) katika skandali za EPA (hasa nani anayemiliki kampuni iliyoiba fedha nyingi ya Kagoda), Richmond, Meremeta, Tangold na nyinginezo, basi ni dhahiri hawakuona haja ya kujihangaisha na ‘jambo dogo’ kama hilo la tuhuma za ushirikina bungeni .
Busara zinatukumbusha kuwa ‘usipoziba ufa utajenga ukuta.’ Tabia ya kuyapuuza masuala yanayopaswa kushughulikiwa ipasavyo sasa imeanza kuzua sokomoko mpya ambayo imeendelea kutawala vichwa vya habari kwa siku kadhaa sasa. Ninazungumzia sakata linalowahusu Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe, kwa upande mmoja, na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Robert Manumba, kwa upande mwingine.
Unaweza kulipanua sakata hilo na kumjumuisha Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta (ambaye amejitokeza kuwa mtetezi mkuu wa Mwakyembe) na Jeshi zima la Polisi chini ya uongozi wa IGP, Said Mwema.
Tuhuma kwamba Mwakyembe amenyweshwa sumu zilianza kama mzaha. Kadri siku zilivyozidi kwenda, suala hilo lilianza kupata uzito hasa baada ya tamko la wazi lililodai kwamba Idara ya Usalama wa Taifa ilikuwa na mpango wa kumuua.
Sijui nchi yetu imefika mahali gani kiasi naibu waziri na mbunge anaituhumu taasisi muhimu na nyeti ya dola kuwa ina njama za kuondoa uhai wake lakini wahusika waliipuzia. Lakini kama nilivyobainisha hapo awali kuwa, masuala mengi yenye kugusa hisia za umma yamekuwa yakimalizwa kienyeji, hazikufanyika jitihada zozote aidha kukanusha madai hayo ya Mwakyembe wala hatua madhubuti za kuyachunguza.
Mwananchi wa kawaida anaweza kujiuliza, “Hivi kama mashushushu wanaweza kupanga njama za kumuua kiongozi wa kitaifa anayetoka chama tawala CCM; je, hali ikoje kwa viongozi wa vyama vya upinzani? Na je, kama usalama wa vigogo unatishiwa na chombo kinachopaswa kulinda usalama wa nchi, hivi kuna usalama kweli kwa walalahoi?
Pengine suala hilo lilipuuzwa kwa matarajio lingekufa kifo cha asili na kusahaulika akilini mwa Watanzania. Hali ya Mwakyembe ikazidi kuwa mbaya na swahiba wake, Waziri Sitta, akapita huku na kule kuukumbusha umma kuwa mafisadi wakishirikiana na vyombo vya dola ndio waliomdhuru naibu waziri huyo ambaye pia ni mbunge wa Kyela (CCM).
Kama mchezo wa kuigiza vile, Waziri wa Mambo ya Ndani, Shamsi Vuai Nahodha, akaingizwa kwenye sakata hilo pale alipomtaka Waziri Sitta kuwasilisha ushahidi wa madai yake kuwa Mwakyembe amenyweshwa sumu.
Lakini katika kile kinachoweza kuashiria kuwa nchi yetu inaendeshwa kwa mtindo wa ‘bora liende,’ Nahodha pia alidai kuwa hajawahi kusikia suala hilo (japo yeye ndiye mwenye dhamana ya jeshi la polisi na usalama wa raia), na kuwataka waandishi wa habari wamuulize Sitta aliyetoa tuhuma hizo.
Hatimaye Sitta naye akamjibu Waziri mwenzake (Nahodha) kwa kubainisha kuwa hatapeleka ushahidi wa madai aliyotoa kuwa Mwakyembe alilishwa sumu kwa kuwa polisi tayari wanao ushahidi.
Awali, Nahodha alidai kuwa “...masuala yote yanayohusu uchunguzi hayawezi kuzungumzwa katika vyombo vya habari...ni mambo ambayo hufanyika kwa umakini mkubwa...” na hatimaye DCI Manumba akathibitisha kauli hiyo ya bosi wake (kufanya mambo kwa umakini) kwa kukurupuka na kudai Mwakyembe hajalishwa sumu. Pia, aliwataka wananchi kupuuza madai ya Sitta, akidai kuwa Jeshi la Polisi liliwasiliana na Wizara ya Afya ambayo ilithibitisha ilitoa taarifa kuwa Mwakyembe hakulishwa sumu.
Kauli hiyo ya Manumba ikawaibua Mwakyembe na Sitta ambao walishusha tuhuma nzito dhidi ya Manumba na Jeshi la Polisi kwa ujumla. Mwakyembe alikwenda mbali zaidi na kudai jeshi hilo lilimtuma ‘askari mtuhumiwa wa dawa za kulevya na ujambazi’ kufuatilia taarifa za (Mwakyembe) kutishiwa maisha yake.
Katika kile kinachoashiria kuwa ‘sinema’ hii inaweza kuendelea kwa muda mrefu, muda mfupi kabla sijaandika makala hii Waziri wa Afya, Dk. Hadji Mponda, ameikana kauli ya Manumba kuwa wizara hiyo ilitoa uthibitisho kwa polisi kuwa, Mwakyembe hajalishwa sumu.
Ni vigumu kuwasilisha sakata hili katika mtiririko unaoleta maana kwa sababu staili inayotumiwa na wahusika ni mithili ya ‘piga nikupige.’ Lakini kilicho wazi ni ombwe kubwa kabisa la uongozi kuanzia kwa Rais Jakaya Kikwete mwenyewe.
Kwa vyovyote vile Kikwete anashuhudia mtifuano huu unaoweza kabisa kupoteza imani ya wananchi kwa Serikali yake na taasisi kama Jeshi la Polisi na Idara ya Usalama wa Taifa, lakini amekaa kimya kana kwamba mambo hayo yanatokea Somalia na si Tanzania anayoiongoza.
Yeye ndiye aliyewateua Mwakyembe na Sitta, japo uteuzi huo ulionekana na baadhi ya wachambuzi wa siasa za nchi yetu kama mbinu ya ‘kuwadhibiti wanasiasa hao wanaotajwa kuwa ni makamanda wa vita dhidi ya ufisadi.’ Wanaodai hivyo wanapigia mstari kanuni ya uwajibikaji wa pamoja ambayo kama inazingatiwa, haitarajiwi mawaziri wanaotumikia ‘kabineti’ moja kupingana hadharani.
Kama Mwakyembe aliituhumu Idara ya Usalama wa Taifa kuwa ilikuwa na njama za kumuua, na kimsingi kiongozi mkuu wa taasisi hiyo nyeti (sponsor) ni Rais mwenyewe, hiyo inaweza kuzaa tafsiri kuwa Rais ni sehemu ya njama hizo. Kwa hiyo ni wazi kwamba laiti umakini ungetumika tangu mwanzoni mwa sakata hii, Rais Kikwete angeweza kuchukua hatua za aidha kumwajibisha Mwakyembe (kwa vile haiwezekani waziri anayeituhumu taasisi inayoongozwa na Rais kufanya kazi kwa ufanisi na Rais huyo) au kuitisha uchunguzi wa kina wa ili suala hilo kupatiwa majibu sahihi na hatimaye kulimaliza kabisa.
Lakini kwa upande mwingine, ninashindwa kabisa kuwaelewa Mwakyembe na Sitta. Japo ninaguswa na maradhi yanayomsibu Mwakyembe lakini sielewi kwa nini yeye na Sitta wanaendelea kuitumikia Serikali ambayo kimsingi wanaituhumu kuhusika na suala hilo la kulishwa sumu. Idara ya Usalama na Jeshi la Polisi si tu ni taasisi muhimu za Serikali bali pia zote zipo chini ya Rais ambaye ni Amiri Jeshi Mkuu.
Na kama Mwakyembe alikuwa na uhakika kwamba Idara ya Usalama ina mpango wa kumuua kwa nini hakumwomba Rais aingilie kati, hasa baada ya kubaini (kwa mujibu wa maelezo yake) kuwa Jeshi la Polisi lilikuwa linachukulia tuhuma zake kama mzaha?
Kwa upande wa Idara ya Usalama wa Taifa, ninaamini ukimya wao unachangia kulikuza suala hili. Tuhuma kutoka kwa naibu waziri kuwa taasisi hiyo ina njama za kumuua si ndogo. Sasa kama walidiriki kukana madai yaliyowahi kutolewa na aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA, Dk. Willbrod Slaa kuwa Idara hiyo ilishiriki kumhujumu katika Uchaguzi Mkuu uliopita, kwa nini ikalie kimya tuhuma kuwa inataka kumuua kiongozi asiye na hatia?
Ikumbukwe kuwa kuna nyakati taasisi za intelijensia katika nchi mbalimbali hulazimika ‘kummaliza mlengwa’ (termination) alimradi kufanya hivyo ni kwa maslahi ya nchi. Hilo lipo ndani ya mamlaka wanayokabidhiwa na taifa husika. Naomba ieleweke kuwa hapa simaanishi kuwa Idara yetu ya Usalama wa Taifa nayo inajihusisha na vitendo vya aina hiyo, lakini kwa vile mbinu hiyo ‘inakubalika katika mazingira ya utendaji kazi wa taasisi za aina hiyo,’ kunyamazia tuhuma za Mwakyembe kunaweza kusababisha hisia kuwa ni za kweli.
Jeshi la Polisi nalo lina maswali kadhaa ya kujibu. Kwanza, lini watatoa matokeo ya uchunguzi wao kuhusu tuhuma za Mwakyembe kuwa Idara ya Usalama ilikuwa na njama za kumuua? Pili, kama jeshi hilo limeshatamka bayana kuwa wananchi wapuuze madai ya Waziri Sitta kuwa Mwakyembe amelishwa sumu, kwa nini halijamchukulia hatua ‘kwa kutoa tuhuma nzito kama hizo’? Na tatu, DCI Manumba alipata taarifa kutoka ‘Wizara ya Afya ya nchi gani kuwa Mwakyembe hajalishwa sumu’ (kwani Waziri Mponda ameshang’aka wizara yake kuhusika na hilo)?
Nimalizie makala hii kwa kutoa hadhari kwamba hiki kinachoonekana kama ‘mchezo wa kuigiza’ kinaweza kuwa na madhara makubwa huko mbele.
Wanaozembea kwa kukaa kimya kwa matarajio kuwa suala hili litapotea tu kama masuala ya Kagoda, Meremeta na Tangold wanajidanganya na hatma yake inaweza kuwa mbaya na isiyoweza kurekebishika.

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Hot Sonakshi Sinha, Car Price in India