Featured Posts

Saturday, July 11, 2009

GLASGOW: MJI WA RANGI


Pamoja na sifa zake nyingi ikiwa ni pamoja na kuwa jiji la tatu kwa ukubwa (kwa idadi ya watu idadi ya watu,nyuma ya London na Birmingham) hapa UK,Glasgow,unabeba historia ya "Simba na Yanga" za Scotland,yaani klabu mbili za soka zenye upinzani wa kupindukia:Glasgow Rangers (almaaruf RANGERS) na Celtic.Tofauti na upinzani wa Simba na Yanga,au Manchester City na Manchester United,au kwingineko kwenye "mafahali wawili wanaopigania ubabe kwenye mji mmoja",upinzani kati ya Celtic na Rangers umevuka mipaka ya soka.Wakati Celtic ni,generally speaking,Wakatoliki,Rangers ni Waanglikana.Zamani hizi,ilikuwa jambo lisilowezekana kabisa kwa mchezaji Mkatoliki kusajiliwa na Rangers,au Muanglikana kusajiliwa na Celtic.

Sasa,moja ya tahadhari wanazopewa wageni katika jiji la Glasgow ni rangi za timu hizo mbili.Ukirogwa kuvaa "jezi" za Rangers kwenye maeneo ya wapenzi wa Celtic,au kutinga rangi za Celtic kwenye maeneo ya kujidai ya Rangers,tarajia yasiyotarajiwa.

0 comments:

Post a Comment

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Hot Sonakshi Sinha, Car Price in India