Featured Posts

Tuesday, August 11, 2009

MGOGORO WA KIDIPLOMASIA KATIKA TAMASHA LA "FILIMBI"


Kuna tamasha kubwa la kimataifa linaloendelea jijini Glasgow.Wenyewe wanaliita World Pipe Band Championships.Ni mashindano ya bendi za kupuliza filimbi kama zile za brass band (pipes).Kumejitokeza mgogoro wa kiplomasia baada ya Wakala ya Mipaka ya Uingereza (UK Border Agency) kuwanyima viza wanabendi ya kupuliza filimbi kutoka Pakistan.Licha ya bendi hiyo inayojulikana kama Lahore Piping Band,msafara wa wafanyabiashara kutoka Pakistan nao umenyimwa viza.Kinachochochea zaidi songombingo hilo ni ukweli kwamba Glasgow na Lahore ni miji pacha (twin cities).

0 comments:

Post a Comment

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Hot Sonakshi Sinha, Car Price in India