Featured Posts

Sunday, March 18, 2012

Mdau Ahoji Kuhusu "Usiku wa Mabloga"


Nimetumiwa hii nami naiwasilisha kama ilivyo:




Ndugu Blogger, 
Husika na Kichwa cha Habari hapo juu, kwa masikitiko makubwa chanzo chetu cha ripoti kimepokea Habari ya kwamba kuna mchakato unafanyika wa kuweka usiku wa Bloggers Tanzania Lakini cha kushangaza sana usiku huo utakuwa ni usiku wa ubaguzi pia kwa maana watakao alikwa ni Bloggers wakubwa tuu wa Tanzania sasa tujiulize kwa umakini sana, Kwanza ni wakina nani hao ambao ndio wanazania kuwa ni bloggers wakubwa Tanzania, Pili tujiulize hao wanaojiita kuwa ni Mabloga wakubwa na maarufu tanzania wamechukua kigezo gani? 

Tufike mahali kwamba nyie mnao jiita bloggers wakubwa hapa nchini msiwadharau na kuwatenga hao mabloga wadogo, inasikitisha sana badala ya kuwasaidia nyie mnawakandamiza. kama mpo juu mpo juu tuu hakuna wa kuwashusha chini basi wasaidieni na hao mabloga wadogo wadogo.

Na mwisho kwa niaba ya Timu nzima inayo endelea kufuatilia kwa umakini mchakato mzima wa umoja wa bloggers Tanzania na kufuatilia kwa ukaribu na umakini vikao vya Siri na vya chini vinavyo endelea kwa ajili ya huo usiku wa bloggers, tunapenda kusema kwamba kama mpo hapa ni bora muwashirikishe na wengine email ndio hizi hizi za bloggers. Tusiwe na roho ya kwanini sote ni watanzania.

Imetolewa na 

Ripota wenu


0 comments:

Post a Comment

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Hot Sonakshi Sinha, Car Price in India