Featured Posts

Saturday, June 15, 2013

Habari na Picha za Mlipuko wa Bomu Arusha (TAHADHARI: Baadhi ya taswira ni graphic)




Habari zilizotufikia hivi punde bomu limelipuka katika eneo la Soweto mkoani Arusha kwenye mkutano wa Chadema leo, na kusababisha watu wanne  kufariki  Dunia.

Mlipuko huo umetokea majira ya saa 12:00 na  majeruhi ni zaidi ya 10 wamekimbizwa katika Hospitali ya Mount Meru STK 8493 kwa matibabu zaidi.

Bomu hilo ambalo lilikuwa limetegewa katika mkutano huo lilipuka na kusababisha mauti na kujeruhi watu zaidi 10.

Pia gari limevunjwa vioo na wananchi kwa madai ya kwamba limeshindwa kuokoa maisha ya majeruhi.
 
Inaonekana bomu lilitegwa karibu na gari la matangazo, Mtoto aliyelipukiwa na bomu amefariki uwanjani.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Abbas amesema kwamba watu wawili ndio wamepoteza maisha.



0 comments:

Post a Comment

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Hot Sonakshi Sinha, Car Price in India