Featured Posts

Sunday, January 19, 2014

Baraza Jipya la Mawaziri: JK afanya utani mbaya, amteua Mwigulu Nchemba kuwa Naibu Waziri wa Fedha




UCHAMBUZI WA HARAKA:

Yaelekea matatizo ya uchumi wetu si miongoni mwa mambo yanayomnyima usingizi Rais Jakaya Kikwete, ndio maana amefanya kituko cha mwaka kumteua Mwigulu Nchemba kuwa Naibu Waziri katika Wizara hiyo nyeti. Ila mzaha huo ni wa kimkakati zaidi. CCM inahitaji fedha kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi mkuu mwaka 2015. Hadi hapo si tatizo, lakini tatizo lipo kwenye kupata fedha hizo kwa njia halali. Ninatafsiri uteuzi wa Mwigulu kwenda Wizara ya fedha kuwa ni sehehmu ya mkakati wa kuiwezesha CCM kupata fedha za uchaguzi mkuu ujao. Tutegemea EPA nyingine? Time will tell.

Adam Malima kupelekwa Wizara nyeti ya fedha si jambo la kushangaza, ikizingatiwa yyeye na JK wanatoka mkoa wa Pwani na ukaribu wao. Sijui nini kilichopeleka Juma Nkamia kupewa uwaziri wa Michezo, lakini majibu anayo JK mwenyewe.

BOTTOM LINE: Tatizo sio mawaziri bali Kikwete mwenyewe. Mbunge wa Ubungo aliwahi kuingia matatani alitamka bayana kuwa JK NI DHAIFU lakini ukweli unabaki kuwa ukweli, na alichosema Mnyika ndo ukweli wenyewe. Mawaziri wanaweza kubadilishwa kila wiki, lakini as long as kiongozi wao ni dhaifu, basi tuendelee kutarajia yaleyale yanayopelekea kabineti kubadilishwa mfululizo kama safari za JK nje ya nchi.

Na kwa waliodhani Pinda angeng'oka walikuwa wanaota ndoto za mchana. Pinda ni nyenzo muhimu kwa JK, ni mtu anayebeba lawama za bosi wake. Madudu yakifanywa na JK,lawama zinaelekezwa kwa Pinda.

Tuombe Mungu 2015 ifike mapema, JK amalize majaribio yake ya urais, labda nchi yetu itapata mwelekeo mpya.

MUNGU IBARIKI TANZANIA

MABADILIKO HUSIKA NI HAYA HAPA CHINI

- Hakuna Mabadiliko Ofisi ya Rais

- Ofisi ya Makamu Wa Rais - Naibu Waziri Kitwanga amehamishwa na nafasi yake imejazwa na Mhe. Ali Mwalimu

- Mwigulu Nchemba amekuwa Naibu Wizara ya Fedha (Sera). Aliyekuwa nafasi hiyo sasa ni Waziri Kamili
- Uchumi na Mapato sasa anatoka Janet Mbene na inajazwa na Adam Malima

- Asharose Migiro sasa ni Waziri wa Katiba na Sheria

- Ulinzi na Kujenga Taifa => Hussein Mwinyi

- Mambo ya Ndani - Mathias Chikawe

- Afya na Ustawi wa Jamii - Naibu wake sasa ni Waziri Kamili; naibu wa sasa ni Dr. Kebwe S. Kebwe

- Mulugo ameondoshwa rasmi serikalini. Nafasi yake imejazwa na Jenista Muhagama

- Pindi chana amejaza nafasi ya Ummi Mwalimu - Jinsia na watoto

- Mifugo na Maendeleo ya Mifugo - Titus Kamani atakuwa Waziri mpya. Naibu ni Telele na hivyo Wizara nzima imepata mawaziri wapya

- Ole Medeye OUT - Simbachawene kachukua nafasi yake (Naibu wa Prof. Tibaijuka)

- Naibu Kilimo - Zambi

- Habari - Naibu ni Juma Nkamia

- Nyalandu amekuwa Waziri Kamili. Naibu ni Mahmood Hassan Mgimwa

- Muhongo na Naibu wake wamebakizwa. Nishati atachukua Charles Kitwagwa akiichukua toka kwa Simbachawene


0 comments:

Post a Comment

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Hot Sonakshi Sinha, Car Price in India