Featured Posts

Tuesday, July 31, 2012

Makala yangu ktk Raia Mwema Toleo la July 25: "Vipi Tuwe na Waheshimiwa Wasiojiheshimu?"



Mara nyingi kwa wenzetu huku nchi za Magharibi kila jambo linapotokea watu wa kada mbalimbali hujihangaisha kusaka maelezo yanayojitosheleza kuhusu chanzo cha tukio husika na jinsi linavyoweza kuzuiwa mbele ya safari.
Ukiangalia nchini Marekani, kwa mfano, mara baada ya mashambulizi ya kigaidi ya Septemba 11, 2001, taasisi mbalimbali zilikuna vichwa kusaka chanzo cha mashambulizi hayo na jinsi nchi hiyo itakavyoweza kuzuia uwezekano wa mashambulizi kama hayo kujirudia.
Ninaamini kwa wanaofuatilia siasa za kimataifa watakumbuka kazi iliyofanywa na Kamisheni ya Septemba 11 ambayo kwa kiasi kikubwa ilifukua kila eneo kuhakikisha inapata taarifa sahihi kuhusu mashambulizi hayo ya kigaidi na usalama wa nchi hiyo kwa ujumla.
Yayumkinika kuhitimisha kwamba jinsi Marekani ilivyoshughulikia ‘aftermath’ ya mashambulizi hayo imesaidia kwa kiasi kikubwa si tu kuuawa kwa mtuhumiwa nambari moja, Osama bin Laden, bali pia imesaidia kuepusha mashambulizi mengine.
Kwa hapa Uingereza, matukio ya vurugu za mwezi Agosti mwaka jana yaliyoanzia kitongoji cha Tottenham, jijini London, na kusambaa maeneo kadhaa yalisababisha taasisi na watu mbalimbali kuhangaika kusaka chanzo cha matukio hayo, zoezi ambalo hadi sasa linaendelea.
Na kutokana na umuhimu wa jiji la London-na Uingereza kwa ujumla-kwa dunia, vurugu hizo zilivuta hisia hadi nje ya mipaka ya nchi hii. Ripoti kuhusu vurugu hizo zilikamata vichwa vya habari kuanzia Zimbabwe hadi India, Amerika ya Kaskazini hadi Kusini, na kwingineko.
Lakini binafsi niliguswa zaidi na maelezo ya gazeti la mrengo wa kushoto la Ujerumani la Berliner Zeitung ambalo lilihitimisha ifuatavyo kuhusu vurugu hizo (ninanukuu)
The country has lost faith in every authority: the banks, politicians, the media, the police. The corruption has reached even the smallest unit - the family. There is a generation growing up without values of any kind.” (Tafsiri isiyo rasmi: nchi imepoteza imani kwa kila mamlaka: benki, wanasiasa, vyombo vya habari, polisi. Rushwa imetamalaki hadi kwenye eneo dogo la chini kabisa, yaani familia. Kuna kizazi kinachokua kisichokuzwa katika maadili ya aina yoyote ile)
Gazeti hilo likaendelea kueleza (ninanukuu tena) “In the economic crisis the financial establishment declared bankruptcy, and British politicians became mired in the expenses scandal of 2009. Then this year the media and politicians have been damaged by the Murdoch scandal...When the country's elites don't take the law seriously, why should we? No question is more dangerous for a society.” (Tafsiri isiyo rasmi: katika mtikisiko wa kiuchumi, taasisi za fedha ziliishia kutangaza kuwa zimefilisika, na wanasiasa wa Uingereza wakakumbwa na skandali ya posho mwaka 2009. Kisha, mwaka huu kashfa ya Murdoch imeathiri sana taswira ya vyombo vya habari na wanasiasa...Sasa kama wasomi wa nchi wanapuuza sheria, kwanini sie tuijali? Hakuna swali la hatari kwa jamii kama hili.”
Nukuu hizo mbili kuhusu vurugu za London zinaweza kabisa kutumika kuelezea mwenendo wa baadhi ya mambo huko nyumbani kwa sasa. Kimsingi, mwananchi wa kawaida anakumbana na matarajio makubwa kutoka kwa watawala wetu lakini licha ya Watanzania wengi kukidhi matarajio hayo ya tabaka tawala, wameendelea kushuhudia watawala na mamlaka za utawala zikishindwa kwa makusudi kuthamini matarajio na mahitaji ya wananchi.
Moja ya taasisi za utawala ambazo zimekuwa zikiwaangusha ambayo imekuwa ‘ikiwaangusha’ sana Watanzania ni Bunge, tunaloambiwa ni tukufu. Katika siku za hivi karibuni, Bunge letu limekuwa likifanya kila jitihada kujivunjia heshima na imani kubwa waliyonayo wananchi kwa taasisi hiyo.
Kimsingi, Bunge letu limegeuka zaidi ya kituko. Lakini baya zaidi, taasisi hiyo ya kutunga sheria imegeuka pia kuwa ‘utani mbaya’ (a bad joke), ambapo watu wanaotubebesha mzigo mkubwa kumudu maslahi yao ambayo kwa mwananchi wa kawaida ni ya kufikirika tu wameamua kuigeuza taasisi hiyo kuwa uwanja wa mipasho, vijembe, matusi na tabia nyingine unazoweza kuzikuta maeneo ya vijiweni tu.
Lakini tukirudi nyuma, Bunge ‘liliharibiwa’ tangu zamani, na tunachoshuhudia sasa ni mwendelezo tu wa uharibifu huo. Tukiangalia Bunge la mfumo wa chama kimoja tunabaini kuwa lilikuwa mkusanyiko wa watu waliopaswa kuwa na fikra za aina moja, kupitisha kila kinacholetwa na serikali ya chama kimoja kilichoshika hatamu, na mawazo yoyote yaliyokinzana na mtizamo wa watawala yalichukuliwa vibaya, lakini walau wakati huo zilikuwapo pia sauti zilizokuwa zikisema ukweli kwa jinsi ulivyokuwa.
Hatimaye tukapata Bunge la vyama vingi chini ya Spika Pius Msekwa. Kimsingi, Bunge hili liliendelea kuwa mithili ya lile la mfumo wa chama kimoja kwani wabunge wachache wa upinzani hawakupewa fursa yoyote ya maana kuipa changamoto serikali, na Bunge likaendelea kuwa kibaraka wa serikali kwa kutumia wingi wa wabunge wa chama tawala.
Lakini kama awamu zilizotangulia zilikuwa mbaya, basi zilizofuatia zilikuwa zaidi ya mbaya. Bunge lililokuwa chini ya Uspika wa Mheshimiwa Samuel Sitta lilizaa kile kinachofahamika sasa kama siasa za majitaka. Nisingependa kuingia kwa undani ni jinsi gani Sitta alifanikiwa kupata uspika lakini ninachoweza kusema pasi uoga ni kuwa Bunge hilo lililogubikwa na migongano lukuki ya kimaslahi, lilifanikiwa kupigia mstari hoja kuwa ni rahisi sana kuwaghilibu Watanzania.
Lakini ukidhani ‘Bunge la Sitta’ lilikuwa hivyo lilivyokuwa, na kama unakumbuka kituko kikubwa zaidi (tuhuma za ushirikina bungeni?) basi subiri tulichambue kidogo ‘Bunge la sasa la Spika Anne Makinda.’ Pengine hili litamkera Spika Makinda lakini moja ya maelezo mepesi ya utawala wake ni kuwa anaiendesha taasisi hiyo kidikteta ‘kupita maelezo.’
Kuna hoja moja ya kisiasa inayodai kuwa kuna nyakati udikteta ni muhimu. Kwamba kuna udikteta wa aina mbili: kwa ajili ya watu na dhidi ya watu. Udikteta mbaya ni huo wa aina ya pili (dhidi ya watu) kwani ni kwa ajili ya maslahi ya wachache. Lakini udikteta kwa ajili ya watu unaweza kuwa muhimu na lazima hususan pale maslahi ya wengi yanapoelekea kusipofaa.
Spika Makinda amekuwa ‘mungu-mtu’ wa Bunge letu, akitumia kila aina ya ubabe dhidi ya wabunge wa vyama vya upinzani, akiwatimua nje ya Bunge kadri apendavyo huku akiwaacha watu kama Mwigulu Nchemba kuigeuza taasisi hiyo kuwa mithili ya kituo cha mafunzo ya vijembe, mipasho, matusi na upuuzi mwingine.
Lakini tatizo si Makinda tu bali hata kiti cha Uspika. Yayumkinika kuhitimisha kuwa kiti hicho ni kama ‘kimerogwa’ kwani kila anayekikalia anajisikia mwenye nguvu zisizomithilika na kama ni lazima awathibitishie wabunge wa vyama vya upinzani kuwa wao ni sawa na kile Waingereza wanakiita ‘evil necessity’ (yaani jambo la kishetani ambalo inabidi liendelee kuwapo kwa vile tu ni muhimu, angalau kwa mujibu wa taratibu za kimaandishi na si kivitendo).
Kabla sijaandaa makala hii nimesoma habari katika gazeti moja inayomnukuu Waziri wa Makazi, Prof Anna Tibaijuka, akitoa wito kwa Watanzania kuwaombea viongozi wa ngazi zote wakiwamo wabunge ili wapate hekima na busara kutoka kwa Mungu.
Japo wazo la Waziri Tibaijuka lina maana laini sidhani kama Watanzania ambao tayari wanabebeshwa mzigo kumudu maslahi ya viongozi kama wabunge wapo tayari kujitwika ‘gunia jingine la misumari’ kufanyamaombi kwa ajili ya watu walioko bungeni kuendekeza mipasho na vijembe badala ya kuzungumzia kero za wananchi.’
Tuwaombee ili wapate busara za kusaka vina (verses) kali zaidi za mipasho yao ya kila siku? Tuwaombee ili waendelee kupigania kuboreshewa maslahi yao ambayo hayaendani kabisa na hali halisi ya uchumi wetu? Ninaamini kabisa kuwa hakuna Mtanzania mwenye ‘muda mchafu’ wa kuwaombea watu hawa. Wajiombee wenyewe ili wapatwe na akili ya kutambua kuwa ‘utoto’ wa vijembe, kashfa na matusi si tu unaisukuma taasisi hiyo kwenye lindi la ukosefu maadili bali pia unaweza kuzua mjadala kama kuna umuhimu wa kuwaita watu hawa waheshimiwa ilhali baadhi yao wana kauli chafu zaidi ya zile za vijiweni. Kwanini tuwe na waheshimiwa wasiojiheshimu?
Nimalizie makala hii kwa kukumbushia nukuu ya Berliner Zeitung kuwa kama ‘waheshimiwa’ hawajali sheria na taratibu kwanini basi wananchi waone umuhimu wa kuzijali? Kwa bahati mbaya, kufanya hivyo ni kukaribisha uvunjifu wa amani zaidi ya huo uliojiri hapa Uingereza mwaka jana.
Nihitimishe kwa kutoa wito kuwa kuna umuhimu mkubwa kwa marekebisho tarajiwa ya Katiba yetu kuangalia uwezekano wa wapigakura kuwadhibiti wabunge ‘wasio na heshima’ kutokana na kauli au/na vitendo vyao, sambamba na kutengeneza mazingira ya kudhibiti udikteta wa Spika na/au kiti cha uspika.

Wednesday, July 25, 2012

The Mabwepande Forest Effect: Kikundi cha utesaji chaibuka Moshi

KIKUNDI cha vijana wanaoendesha vitendo vya kihalifu unaoendana na mauaji kinachojiita ‘Kunguru Hafugiki’ kimeibuka na kuwa tishio kwa wakazi wa manispaa ya Moshi na vitongoji vyake.

Kikundi hicho hukodishwa na watu walioibiwa mali zao kwa kulipwa ujira mdogo na huwakamata washukiwa wanaodaiwa kuiba mali ya mtu husika na kuendesha vitendo vya utesaji kushinikiza watu hao kutaja walipoficha mali.

Katika tukio la juzi huko Pasua Manispaa ya Moshi, kikundi hicho kinadaiwa kukodiwa na mfanyabiashara mmoja jina limehifadhiwa, siku moja baada ya watu wasiojulikana kuvamia nyumba yake na kupora mali kadhaa.

Baada ya tukio hilo, mfanyabiashara huyo alimhisi jirani yake kuwa ndiye pengine alihusika na tukio hilo na ndipo alipomkamata yeye na nduguye na kuwapeleka kwenye kikundi hicho.

Baada ya kuwafikisha hapo aliwakabidhi kwa kikundi hicho ambacho kiliendesha mateso ya kila aina kikiwashinikiza wataje walikoficha mali za mfanyabiashara huyo bila mafanikio.

Katika tukio hilo, Sultan Mallya (28), alipigwa hadi akapoteza fahamu na kufariki katika Hospitali ya Mtakatifu Joseph iliyoko eneo la Soweto katika manispaa ya Moshi.

                                

Kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro, Robert Boaz, alidhibitisha jana kutokea kwa tukio hilo na kwamba watu wawili, Achibodi Maleko (52), pamoja na mfanyabiashara huyo wanashikiliwa na polisi kutokana na tukio hilo la mauaji.

Akifafanua juu ya tukio hilo, Boaz alisema Julai 22 usiku mfanyabiashara huyo alivunjiwa nyumba yake na alipata tetesi kwamba Michael Mallya na nduguye Sultan Mallya walihusika na kuvunja nyumba yake.

Alidai kuwa baada ya kupata tetesi hizo aliwakamata ndugu hao na kuwapeleka kwenye kikundi hicho na kuwapa mateso ya kila aina na hadi sasa Michael yuko mahututi katika hospitali ya rufaa ya KCMC baada ya kuumizwa vibaya.

Kufuatia tukio hilo, wananchi wenye hasira walizingira nyumba za watuhumiwa hao na kufanya uharibifu mkubwa wa mali kabla ya polisi hawajaingilia kati na kuwatia mbaroni watu wanane.
Wanaoshikiliwa kutokana na kufanya uharibifu wa mali kwenye nyumba za watuhumiwa hao ni Issa Haji, Issa Athuman, Juma Rajab, Issa Maulid, Bakari Kiduka, Bakari Evarist, Selestine Joseph na Hamis Mohamed.

Friday, July 20, 2012

Have you booked your tickets yet? 2nd Ugandan UK Convention 2012 15th September 2012


Email not displaying correctly? View it in your browser.

2nd Ugandan UK Convention 2012
Saturday, 15th September, 2012
Troxy, 490 Commercial Road, London E1 0HX London
Objectives - About us | To Exhibit | Register to Attend | Venue | Why Visit | VISA | Contact us
Respectively invite you to attend the 2nd Ugandan UK Convention
The theme of this year's convention is 'Aspiring for sustainable prosperity'.
Saturday, 15th September, 2012
Time: 9.30am - 2am
Venue: Troxy, 490 Commercial Rd, London E1 0HX United Kingdom

The event is now the largest Diaspora-led conference in Europe and will bring together the Diaspora, intellectuals, policy-makers and business leaders to confer on issues pertaining to the promotion and exchange of information, research and expertise in order to achieve sustainable prosperity for Ugandan Diasporans.

Unwind the day at the After Party featuring a live concert by Bobi Wine and Iryn Namubiru not to mention a cultural and fashion extravaganza.
Register here for free tickets.
Mobile: +447426 201 055 - Email: info@ugandanconventionuk.org
Uganda Convention
Attractions:
  • Business Expo
  • Fashion show
  • Top artists from Uganda
  • Cultural dance extravaganza

Among reasons to attend
  • Trade & Investment Opportunities in Uganda – Career and Employment in Uganda
  • Open up a £$ account in Uganda on the day
  • Mortgages in Uganda
  • Meet with senior business and government leaders to discuss the major developments, challenges and success stories in Uganda investment
  • Get first hand information on how to move back to Uganda
  • Discover various Investment Opportunities in Uganda.
Please call Mobile: +447426 201 055
Email: info@ugandanconventionuk.org.

Uganda: Mobile: +256-754-410-559 / +256-712-410-559
Website: www.ugandanconventionuk.org
Uganda Convention-UK
Mobile: +447426 201 055
Email: info@ugandanconventionuk.org
http://ugandanconventionuk.org
UCU2012register
Connect with us:Facebook Twitter LinkedIn Contact Us


Thursday, July 19, 2012

Makala yangu ktk RAIA MWEMA Toleo la Julai 18: "Naikumbuka Tabora Boys,Najivunia Uzalendo Wangu"


Wanafunzi wa Sekondari ya Wavulana Tabora wakiwa katika mafunzo ya kivita katika mapori ya Uchama,wilayani Nzega.Picha kwa hisani ya Tabora School Facebook Group

Naikumbuka Tabora Boys,Najivunia Uzalendo Wangu
NIANZE makala hii kwa kurejea barua-pepe niliyotumiwa na mmoja wa wasomaji wa gazeti hili. Msomaji huyo ambaye kwa bahati mbaya au makusudi hakuambatanisha jina lake alieleza kuwa aliguswa sana na makala yangu katika toleo lililopita iliyobeba kichwa cha habari “Ni Vigumu Kuiamini Serikali kwa Dkt Ulimboka.”
Na kuguswa kwa msomaji huyo ni kwa namna mbili; kwa upande mmoja alidai amevutiwa sana na changamoto niliyoitoa kwa Idara ya Usalama wa Taifa, ambayo kwa maelezo yake, anaiona kama taasisi pekee anayoitumainia kuiokoa Tanzania yetu inayoelekea kusikoeleweka.
Lakini kwa upande mwingine, msomaji huyo alionyesha wasiwasi wake kuhusu anachokiona kama uwezekano wa walioudhiwa na makala hiyo (na nyinginezo zinazowazungumzia) kutafuta namna ya kuninyamazisha.
Msomaji huyo aliniusia kuwa japo anatambua kuwa pengine ninachoandika kuhusu yasiyopendeza huko nyumbani kinatokana na uchungu tu kwa taifa langu lakini akanikumbusha yaliyowahi kutokea huko nyuma kwa wengi waliojaribu kukemea maovu katika jamii yetu.
Akanikumbusha kuhusu kiongozi aliyemuita ‘mtoto wa kweli wa Tanzania’ yaani aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Sokoine, ambaye kwa mujibu wa msomaji huyo, anaamini alifupishiwa maisha kutokana na kuingilia maslahi ya mafisadi wa zama hizo.
Kadhalika, aligusia kilichomkumba mmoja wa waandishi bora kabisa wa habari za uchunguzi Marehemu Stan Katabalo. Akadai, kilichompeleka kuzimu mwandishi huyo hakina tofauti na shambulio la kinyama la kumwagiwa tindikali mwandishi mwingine, Said Kubenea.
Pia akaniusia kuwa (namnukuu) “Kama kosa la Dk. (Steven) Ulimboka lilikuwa kutimiza tu wajibu wake kama kiongozi wa jumuiya ya madaktari na matokeo yake ametishia kutekwa na kuteswa, vipi wewe unayediriki kuikosoa taasisi nyeti kama Idara ya Usalama wa Taifa?”
Katika kuhitimisha, msomaji huyo aliniusia kwamba kwa maneno haya (namnukuu), “Kwa vile wewe upo huko Ulaya ambapo shida zake si kama huku kwetu, basi mie ninakushauri usijitafutie matatizo. Hii nchi yetu mtuachie sie wenyewe tuliokwishazoea mgawo wa umeme usioisha licha ya ahadi za kila kukicha, rasilimali zetu kutoroshwa kana kwamba tumezichoka, na mabilioni yetu kuletwa huko Ulaya kwenu kwenye akaunti za mafisadi huku wakituacha tunataabika na uchumi unaozidi kudidimia.”
Kwa hakika nimeguswa mno na barua-pepe hiyo ya msomaji huyu. Japo hakutaja jina lake lakini ninamshukuru kwa yote aliyoandika. Na kikubwa zaidi, angalau anatambua kwa nini 'ninajiingiza matatizoni' kwa kuzungumzia yale ambayo katika mazingira ya kawaida hayapaswi kuzungumzwa.
Ni kweli, nina uchungu na nchi yangu, na kama hilo ni ‘kosa’ litakaloweza kunigharimu huko mbeleni, basi na iwe hivyo. Naomba niweke rekodi vizuri: ninaposema nina uchungu kwa nchi yangu simaanishi kuwa mie ndiye mwenye uchungu (au mapenzi zaidi) kwa nchi yangu zaidi ya watu wengine. Hapana. Ninaamini huo ni wajibu wa asili wa kila Mtanzania mzalendo.
Lakini pengine ni vema nikieleza kwa nini ninaguswa sana na mwenendo wa mambo huko nyumbani, ukiachilia mbali Utanzania wangu. Pengine ni baadhi ya mazingira niliyopitia hadi kufika hapa nilipo. Kwa mfano, mwaka 1990 nilichaguliwa kujiunga na Shule ya Sekondari ya Wavulana ya Tabora (Tabora Boys High School). Shule hii yenye historia ya kipekee kwa nchi yetu imetoa mchango mkubwa sana wa ‘kuzalisha’ viongozi wa nchi yetu.
Wakati ninajiunga na shule hiyo ilikuwa na mchepuo wa kijeshi. Kama kuna faida kubwa niliyoipata kwa kuwa mwanafunzi hapo ni hiyo ‘bahati’ ya kuwa ‘nusu-mwanafunzi, nusu-mwanajeshi.’
Bahati nyingine niliyoipata nikiwa mwanafunzi shuleni hapo ni kuchaguliwa kuwa kiranja mkuu. Kwa vile shule ilikuwa ni ya mchepuo wa kijeshi, wadhifa wa kiranja mkuu ulikuwa ukijulikana kama Kamanda Mkuu wa Wanafunzi (kwa kimombo Students’ Chief Commander). Hadi leo, baadhi ya wanafunzi niliokuwa ninasoma nao wanaendelea kuniita ‘Chief.’
Kufupisha maelezo, mchepuo huo wa kijeshi sio tu ulitupatia wanafunzi ukakamavu na nidhamu ya hali ya juu bali pia ulitujaza uzalendo kwa nchi yetu kwa kiwango kikubwa. Huku tukiwa na sare zetu za ‘kijeshi’ (zilikuwa kombati za khaki kama za jeshi la mgambo), maafande wa Jeshi la Wananchi (JWTZ) waliokuwa wakiendesha ‘kitengo cha jeshi’ shuleni hapo walitupatia mwamko wa hali ya juu kuhusu kuitumikia na kuilinda nchi yetu.
Kabla ya kuanza masomo tulipewa kile kilichoitwa “karibu shuleni” iliyojumuisha kwata za kijeshi na hatua nyingine wanazopitia ‘makuruta’ wanapoingia kambini kwa mara ya kwanza. Ilipofika mwisho wa mwaka, wanafunzi wa kidato cha tatu na cha tano tulipelekwa msituni kwa mafunzo ya vita kwa vitendo.
Baada ya kutoka hapo nilijiunga na Jeshi la Kujenga Taifa ambapo kwa wakati huo ilikuwa ni lazima (kwa mujibu wa sheria). Kwa bahati nzuri, muda mfupi tu baada ya kujiunga na JKT nilichaguliwa kuingia kwenye kundi lililotarajiwa kutoa marubani na mainjinia wa ndege za jeshi.
Tukapelekwa kambi ya JWTZ Kunduchi (RTS). Tulipofika hapo, tukapewa jina la ‘wazalendo,’ yaani watu tuliojitolea kwa ajili ya nchi yetu. Well, sikufanikiwa kuwa rubani au injinia lakini ‘tuzo’ hiyo ya kuitwa mzalendo ilikuwa shani kubwa kwa kila mmoja wetu.
Miaka machache baadaye nilijiunga na taasisi moja ambayo sio tu ili kujiunga ilipaswa kuwa na uzalendo wa hali ya juu lakini pia ilinijaza ‘dozi zaidi’ za kuipenda na kuitumikia nchi yangu kwa nguvu zote.
Kama ilivyo kwa taaluma kama ualimu ambapo pindi ukiwa mwalimu unabaki kuwa na maadili ya kiualimu hadi uzeeni, mafunzo na uzoefu wa kazi niliopata kutoka katika taasisi hiyo unanifanya niendelee kuwa na wajibu ule ule: kutimukia nchi yangu kwa nguvu zote.
Sipendi kuandika makala inayonizungumzia mie, kwani lengo la safu hii ni kuzungumzia masuala muhimu yanayohusu nchi yetu. Lakini Nimelazimika kuandika haya ili kuondoa dhana potofu kuwa labda nina chuki na taasisi fulani au ‘kwa mujibu wa wahusika’ ninafanya uchochezi.
Kuna suala moja la msingi ambalo walafi wanaotafuna rasilimali zetu na mafisadi kwa ujumla wanajitahidi kulipuuza. Tanzania ni yetu sote, na kwa namna moja au nyingine sote ni kitu kimoja. Sasa fisadi anapokwapua fedha zilizopaswa kuleta maendeleo kwa nchi yetu anapaswa kutambua kuwa katika mlolongo wa wahanga wa ufisadi huo ni mtu au watu wanaohusiana naye.
Ni muhimu tufike mahala turuhusu maoni yanayokinzana na matendo au mtizamo wetu. Mara kadhaa tumeshuhudia wazalendo wanaojaribu kuwakumbusha watawala wetu wajibu wao wakiishia kuitwa majina mabaya na wengine kuhujumiwa. Mifano ni mingi lakini si vibaya kupigia mstari kauli za mtu kama Mzee Hans Kitine, Mkurugenzi wa zamani wa Idara ya Usalama wa Taifa, ambaye mara kadhaa amekuwa mstari wa mbele kujaribu kushauri kuhusu mwenendo wa CCM, serikali na taifa kwa ujumla. Lakini kila anayefuatilia vema matukio ya huko nyumbani, mzee huyo aliyelitumikia taifa kwa uadilifu (akiwa Mkurugenzi wa TISS, kabla ya kuingia kwenye siasa) ni mmoja wa wahanga wa fitna dhidi yake. Kosa lake kubwa ni kukemea maovu na kushauri njia mwafaka za kulinusuru taifa letu.
Sawa, kama alivyoandika msomaji aliyenitumia barua-pepe, sisi wengine tupo mbali na nyumbani, na ni kweli kuwa hatuguswi moja kwa moja na adha mbalimbali zinazoendelea huko. Lakini, uwepo wetu huku nje sio tu hautupunguzii Utanzania wetu bali pia ifahamike kuwa baadhi yetu tuna ndugu, jamaa na marafiki ambao ni wahanga wa kila siku wa mwenendo mbovu wa mambo huko nyumbani. Haihitaji busara kumaizi kuwa huwezi kuwa na raha ughaibuni huku watu wako wa karibu huko nyumbani ‘wanapigika.’
Kwa wanaodhani kuwa dawa na kudhibiti ‘kelele kama zetu’ ni ‘kutushughulikia sisi wapiga kelele’ ni vema wakatambua kuwa huwezi kuua wazo sahihi. Kama ambavyo vifo vya akina Katabalo havijazuia uzalendo wa kuwasemea walalahoi wasio na wasemaji (rejea timua-timua huko bungeni kwa baadhi ya wabunge wanaowasilisha vilio vya wapiga kura wao) ndivyo ambavyo baadhi yetu tutaendelea kukemea maovu yanayotishia kuipeleka Tanzania yetu kwenye korongo lenye kina kirefu.
Nimalizie makala hii kwa fundisho hili la historia: japo wabaguzi wa rangi walimuua Martin Luther King, Jr (mpigania haki za Weusi huko Marekani) lakini leo taifa hilo lina Rais Mweusi (Barack Obama). Na japo makaburu waliweza kumfunga Nelson Mandela kwa miaka kadhaa, leo hii Afrika Kusini ipo chini ya utawala wa weusi walio wengi.
Kutekwa na mateso kama vilivyomkumba Dk. Ulimboka, na matukio ya kihuni kwa watu kama Kubenea, na ‘sumu’ inayomwagwa kwa wazalendo kama Mzee Kitine, kamwe haviwezi kutuzui sisi wenye uchungu na nchi yetu kuendelea kukemea maovu na kudai kile Waingereza wanaita ‘value for money’ yaani ubora unaotokana na fedha (ya mlipakodi wa Tanzania).
Na kwa msomaji aliyenisihi niwe makini, licha ya kumshukuru ningependa kumhakikishia kuwa sijakurupuka katika harakati hizi za kuwasemea walalahoi. Mwanafalsafa wa Kichina wa sanaa ya vita (Art of War) Sun Tzu anaasa; “If you know the enemy and know yourself you need not fear the results of a hundred battles.”
Mungu Ibariki Tanzania (na umwangamizie kila fisadi na yule anayemlinda).

Monday, July 16, 2012

Makala yangu Ktk RAIA MWEMA Toleo la Julai 11: "Ni vigumu kuiamini Serikali kwa Dk. Ulimboka"



KWA mara nyingine, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetoa tuhuma nzito dhidi ya Idara ya Usalama wa Taifa (TISS), safari hii ikidaiwa kuwa baadhi ya viongozi wa taasisi hiyo nyeti wana mpango wa kuwaua baadhi ya viongozi wa CHADEMA.

Itakumbukwa kuwa wakati wa mchakato wa Uchaguzi Mkuu uliopita, CHADEMA kiliituhumu Idara hiyo kuwa ilikuwa inakihujumu chama hicho, tuhuma ambazo zilifanya Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TISS, Jack Zoka (pichani juu) , kuzikanusha vikali.

Tuhuma hizi za CHADEMA zimekuja siku chache baada ya tukio la kusikitisha na la kinyama lililomkuta kiongozi wa jumuiya ya madaktari Dk. Steven Ulimboka ambaye alitekwa na hatimaye kuteswa na watu 'wasiojulikana.'

Katika tukio la Dk. Ulimboka, Serikali imejikuta ikinyooshewa vidole kuwa inahusika, hali iliyomfanya Rais Jakaya Kikwete kulizungumzia suala hilo katika hotuba yake kwa Taifa hivi karibuni.

Lakini takriban kila anayefuatilia kwa ukaribu suala hilo anaweza kuungana nami kutanabahisha ya kuwa japo hotuba ya Rais Kikwete imesaidia kwa namna fulani kuonyesha kuwa Serikali yake imeguswa (kwa maana ya kusikitishwa) na tukio hilo, kwa kiwango kikubwa haijasaidia kuondoa fikra kuwa kuna mkono wa Serikali.

Binafsi, nimelichambua kwa kirefu tukio hilo la kutekwa na kuteswa kwa Dk. Ulimboka katika mfululizo wa makala zangu za sauti (podcasts). Makala husika yenye kichwa cha habari “Nani aliyemteka na kumtesa Dk. Ulimboka?”

Kwa kifupi, katika makala hiyo nimezungumzia dhana tatu kuhusiana na tukio la Dk. Ulimboka. Ya kwanza ni hiyo inayogusa hisia za wengi kuwa Serikali inahusika na tukio hilo. Katika makala hiyo, nimeungana kimtizamo na kauli ya Rais Kikwete kuwa “Serikali imteke na kumtesa Dk. Ulimboka ili iweje.”

Kadhalika, nimeeleza kuwa japo kuna nyakati Serikali kwa kutumia vyombo vya dola inaweza kutumia vitisho na hata nguvu ikibidi ili kuzima upinzani dhidi yake, katika mazingira ya kawaida ni vigumu kuamini kuwa Serikali ya Rais Kikwete ingekuwa tayari kujiingiza matatizoni kwa kumteka na kumtesa kiongozi wa madaktari ili tu iwatishe madaktari wanaogoma.

Nimebainisha hivyo kwa vile ninaamini kuwa Serikali inafahamu fika kuwa kumnyamazisha Dk. Ulimboka hakuwezi kuwanyamazisha madaktari wote nchini.

Dhana ya pili ni ile ya hujuma dhidi ya Serikali. Kimsingi dhana hiyo inabashiri kuwa pengine kuna ‘watu wenye nguvu na jeuri ya fedha’ ambao wamefanya unyama huo dhidi ya Dk. Ulimboka kwa minajili ya 'kuikoroga' Serikali. Takriban kila anayefuatilia mwenendo wa siasa ndani ya chama tawala CCM atakuwa anafahamu kuwa kuna mtifuano mkubwa (japo usiosikika sana waziwazi) unaoendelea ndani ya chama hicho, hususan kuhusiana na kinyang’anyiro cha urais mwaka 2015.

Kwamba kuna mafisadi wanaoweza kumwaga fedha aidha kwa ‘majasusi binafsi’ au ‘majasusi rasmi’ ni jambo linalowezekana. Kinachonifanya niipe uzito mdogo dhana hii ni uchambuzi wa hasara na faida za tendo husika (cost and benefit analysis).

Hivi, kama mafisadi wakimteka na kumtesa Dk. Ulimboka, kisha Serikali ya Kikwete ikaandamwa, mafisadi hao watanufaikaje (zaidi ya kufurahia kuona Serikali inabebeshwa lawama isizostahili)?

Dhana ya tatu, na ambayo binafsi ninaipa uzito mkubwa, ni uwepo wa kile kinachofahamika katika lugha ya Kiingereza kama ‘rogue elements of the state apparatus’ (yaani ‘watendaji katika taasisi za dola ambao wanatenda kazi zao kinyume na taratibu na sheria,’ kwa tafsiri isiyo rasmi).

Dhana hii ya mwisho inaweza kushabihiana na ya pili kwa maana ya hicho nilichoita ‘majasusi rasmi,’ yaani watumishi wa vyombo vya dola ambao wanatumia ujuzi wao kutekeleza matakwa, si ya mwajiri wao, bali ya mafisadi waliowapa fedha kwa ‘kazi maalumu.’

Katika makala hiyo ya sauti nimeeleza kuwa ni wazi vyombo vya dola vilikuwa vikimfuatilia Dk. Ulimboka na waratibu wengine wa mgomo wa madaktari. Hilo si la kuhoji kwani ni utaratibu ‘wa kawaida’ kwa wana usalama. Iwe ni taasisi ya mashushushu wa ndani wa Marekani (FBI), au wenzao wa Uingereza (MI5), au TISS huko nyumbani, kila mtu au kikundi kinachotazamwa kama tishio kiusalama hufuatiliwa kwa karibu.

Sasa basi, kwa kuzingatia dhana hiyo ya ‘rogue elements,’ inawezekana watendaji waliokabidhiwa jukumu hilo waliamua kutumia njia za ‘liwalo na liwe’ (hapana, si kama ile ya tamko la Waziri Mkuu Mizengo Pinda) baada ya ‘njia za kistaarabu’ kumlazimisha Dk. Ulimboka awaeleze ‘nani anayewachochea madaktari kugoma’ kutozaa matunda.

Yaani baada ya diplomasia kushindwa, wakaamua kutumia mateso ya hali ya juu (kwa lugha ya kisheria ‘third degree torture’ na kitaalamu ‘fifth degree torture’).

Kwa nini ninashawishika kuamini kuhusu rogue elements? Tumeshuhudia matukio kadhaa huko nyuma. Naamini wengi wa wasomaji mtakuwa bado mnakumbuka tukio la mwandishi wa habari mahiri na mhariri  wa gazeti la Mwanahalisi, Said Kubenea, kumwagiwa tindikali usoni. Kibaya zaidi katika tukio hilo, mmoja wa wahusika alitajwa kuwa ni mwajiriwa wa TISS.

Sijui kesi hiyo iliishaje lakini la msingi hapa ni kuwa iliacha doa la aina fulani kwa taasisi hiyo hasa kwa vile haikuwahi kumkana afisa huyo (kwa maana ya kusema hakutumwa kiofisi bali alikuwa ‘rogue officer’ tu).
Itakumbukwa pia kuwa Waziri wa Uchukuzi Dk. Harrison Mwakyembe aliwahi kueleza kuwa Idara ya Usalama wa Taifa ilikuwa na mpango wa kumuua. Kama ilivyokuwa kwa tukio la Kubenea lililomhusisha mtu aliyatajwa kuwa ni Afisa Usalama wa Taifa, Idara hiyo haikuwahi kukanusha tuhuma hizo.

Tukirejea kwenye tuhuma za CHADEMA dhidi ya TISS, binafsi nashawishika kuamini kuwa kama kuna ukweli katika tuhuma hizo basi itakuwa ni zilezile ‘rogue elements’ ambazo ninaamini zipo ndani ya taasisi hiyo nyeti.

Najua hili halitowapendeza wahusika, lakini kuna hisia kwamba ukiweka kando taasisi hiyo kuendeshwa kama kitengo cha usalama cha CCM moja ya sababu nyingine kubwa ya matatizo yanayoikabili taasisi hiyo ni ajira zilizotolewa pasipo kuzingatia ‘wito’ na ‘kipaji’ cha kuwa Afisa Usalama.

Popote duniani, maafisa usalama wanapaswa kuwa ‘watu zaidi ya watu wa kawaida’ kwa maana ya kuwa na upeo na uwezo wa hali ya juu katika takriban kila nyanja ya akili zao:  na huo ndio msingi wa neno INTELLIGENCE kwa kimombo.

Sasa tunaporuhusu watoto zetu, ndugu au jamaa zetu kuingizwa kwenye taasisi nyeti kama hiyo kwa vile tu ‘kuna maslahi manono’ tunaiweka rehani nchi yetu.

Naomba niwe mkweli. Madudu mengi yanayoendelea katika Tanzania yetu kwa sasa yanachangiwa na ubabaishaji unaoendelea ndani ya idara hiyo muhimu kwa ustawi na maendeleo ya taifa lolote lile duniani. Wao wanafahamu kanuni hii: uimara au kuyumba kwa nchi ni kielelezo cha uimara au udhaifu wa Idara ya Usalama ya nchi husika.

Sasa kama tuna maofisa usalama huko Benki Kuu (BoT) lakini bado ufisadi wa EPA ukafanikiwa, na kama TISS ipo kazini saa 24 lakini bado kuna majambazi wamemudu kutorosha mabilioni ya dola na kuzificha nchini Uswisi basi ni wazi Idara hiyo ni dhaifu.

Na kama tunakubaliana kuwa kuna udhaifu mkubwa katika taasisi hiyo, kwa nini basi CHADEMA wasiamini taarifa kuwa Idara hiyo ina mpango wa kuwadhuru? Sitaki kuamini kuwa, iwapo taarifa hizo ni kweli, basi ni za ki-Idara bali ninaendelea kuhisi kuwa ni matokeo ya kulea ‘rogue elements’ ndani ya chombo hicho muhimu.

Unajua, inapofika mahala Afisa Usalama wa Taifa anaona sifa kutangaza wadhifa wake baa ili vimwana watambue kuwa yeye ni shushushu, au kiongozi mwandamizi wa taasisi hiyo nyeti anapoweza kufanya ‘madudu’ hadi sisi tulio nje ya nchi tukafahamu, basi ni wazi kunahitajika kazi ya ziada kurekebisha mwenendo wa chombo hicho nyeti.

Ninatambua kuwa kuna watakaokerwa (na pengine kushauri hatua ‘mwafaka dhidi ya mtizamo wangu’) lakini ninaamini kuwa kila Afisa Usalama wa Taifa mzalendo na aliyekula kiapo cha utii kwa Taifa anakerwa kuona nchi yetu ikienda kwa mwendo wa bora liende huku rasilimali zetu zikiporwa kwa mtindo wa ‘bandika bandua.’

Pasipo mageuzi ya haraka ndani ya taasisi hiyo si tu itaendelea kutuhumiwa na CHADEMA lakini mwishowe walipa kodi wanaowezesha maslahi manono kwa wanausalama wetu watasema ‘imetosha.’
Watanzania wanaweza kufika mahala wakahoji umuhimu wa kuwa na taasisi ya ‘kufikirika’ ambayo licha ya kuogopwa na wengi (nikiamini bado kuna wanaoiogopa) inashindwa kudhibiti uharamia lukuki unaofanywa dhidi ya nchi yetu na Watanzania wenzetu kwa kutumia madaraka yao.

Nimalizie makala hii kwa kutoa tahadhari kwa Idara hiyo kwamba maswali magumu hayajibiwi kwa majibu mepesi. Mmoja wa viongozi wa ngazi za juu za taasisi hiyo amejibu tuhuma zilizotolewa na CHADEMA kwa namna ileile alivyojibu mwaka 2010 pale Idara hiyo ilipotuhumiwa kuihujumu CHADEMA kwenye kinyang’anyiro cha Uchaguzi Mkuu. Tatizo la kiongozi huyo, na pengine Idara hiyo kwa ujumla ni uzembe wa kusoma alama za nyakati.

Na kila mzalendo-awe ndani ya taasisi hiyo au mwananchi wa kawaida-anapaswa kupinga kwa nguvu zote dalili za kutaka kuigeuza nchi yetu kuwa ‘Mafia State’ (yaani dola ambayo kila Tom, Dick na Harry anaweza kuteka na kutesa au kupanga kuuwa wale  wanaopigania haki za wanyonge kama hao viongozi wa CHADEMA wanaodai kutishiwa kuuawa kwa ‘kosa la kuwakalia kooni wabaka uchumi wetu.’)

Biblia inasema mwenye haki ataanguka saba mara sabini lakini atasimama. Na kila mzalendo atakwazwa vya kutosha lakini, inshallah, Tanzania tunayoistahili itafikiwa.

MAKALA KAMILI INAPATIKANA HAPA http://raiamwema.co.tz/ni-vigumu-kuiamini-serikali-kwa-dk-ulimboka

Mchungaji Gwajima Azungumzia Sakata la Joshua the Kenyan (VIDEO)

 Sehemu ya kilichojiri Kanisani kwa mchungaji Gwajima, jumapili ya leo, pale mchungaji huyo mashuhuri nchini alipokuwa akikanusha kuwa kuna mtu mwenye asili ya Kenya ambaye alifika kanisani kwake kukiri na kutubu dhambi ya kuhusika kwake katika utekwaji na uteswaji wa Dr. Ulimboka, kama ambavyo jeshi la Polisi liliarifu hivi karibuni 

 Video na caption kwa hisani za Da Subi na Jukwaa Huru

Sunday, July 15, 2012

Mazishiya Mtanzania Aliyefariki ghafla huko Boston,Massachusetts, Marekani (PICHA)
































Marehemu Patrin Kibelloh aliefariki ghafla siku ya Jumanne July10,2012. alizikwa Ijumaa july13 huka kwenye makaburi ya Gardner, West Roxbury ,Massachusset. Nchini Marekani 



  
Baadhi ya ndugu na marafiki waliohudhuria katia msiba huko nyumbani kwake Saugus, Boston Massachusset.


Marehemu Patrin Kibelloh amepata mafunzo katika Institute proffesional & Restaurant mjini Boario nchini ITALY alizaliwa April 25,1963 huko Tanzania ameacha mke wa Watoto wawili akiwa na umri wa miaka 49. (Picha zote na swahilivilla.blogspot.com)

         Mwenyezi Mungu ailaze roho ya Marehemu Mahali Pema Peponi!

Dr Shaban Nzori on Joshua The Kenyan


Thanks for writing. Indeed, the attack on Dr. Ulimboko, the cover-up which followed thereafter and mumblings of the govt., the prime minister and the president over it paint a very pathetic picture of the country. If those who now claim it is a Kenyan criminal and his cohorts who carried out that horrendous crime, therefore, hardly should we accuse our own government of committing such a deplorable offense, I think they got it totally wrong as their small minds have now added an international dimension to the criminal act and I believe we will soon hear the Kenyan govt. and its citizenry demanding a thorough investigation be carried by an independent commission comprised by, among others, of officials from the Kenyan government and its security organs so as to ascertain the validity of the statement given by the Tanzanian police. Hence, a minor local problem involving the President and his govt. settling their scores with our doctors has been mishandled to such an extent that it has now spilled out of our borders to involve a neighbouring country while at the same we read of our doctors pleading to the international community through the UN office in Dar for help to fend off pressure, harassment and intimidation from their own government and its security organs including the police and intelligence services. And now we also learn that teachers are about to protest as well, read tc1, tc2.

The way our government treats cases of valid demands and concerns of its citizens as if such demands and concerns lack merit, with illegal methods used to harass, silence, maim and intimidate protestors leaves no space and amicable options to pursue this matter other than through international condemnation and other coercive measures to pressure our government and as you know there are quite a number of avenues the doctors, civil and human rights organizations in Tanzania can pursue to put pressure on the Tanzanian govt. One needn’t go far to find workable examples to follow. Take the example of the recent Magnitsky Bill in the US, named after Sergei Magnitsky, a Russian lawyer whose death in police custody generated international media attention and launched an investigation into allegations of abuse.[1] The Bill which is currently in the US Congress aims atpunishing Russian officials behind the death of Sergei Magnitsky (watch VIDEO and read Mg1Mg2Mg3Mg4Mg5) . People are now talking of making the bill have an international dimension by expanding its outreach to include all those in other parts of the world who are involved in human rights abuses in their countries – read (also read about human rights abuses in Russia here). Those government officials, people in the police force, intelligence services, prosecution, courts and other state organs in one way or the other involved in committing crimes like that on Dr. Ulimboko and similar atrocities, or those who have been involved in the poisoning of politicians like Dr. Harrison Mwakyembe, threats on the lives (read thr1thr2,thr3thr4thr5) of Zitto KabweSamuel SittaDr. SlaaJohn MnyikaGodbless Lema and many others in Tanzania could fall under the hammer of this bill which calls for the denial of visas to visit the US and other countries which have passed similar bills and restrictions on those accused – read! If President Kikwete will fail to take prompt and effective measures to arrest the problem of human rights abuses by the police, intelligence organs, prosecution and courts in Tanzania, and if it will be proven that he or his govt. are in one way or the other complicit in committing these crimes, don’t be surprised to hear one day that he himself has fallen victim to this bill, which calls for barring any state official including the president to visit the mentioned foreign countries. And taking into account how much our president and government officials like to travel, especially to the US, UK, Canada and other western countries which have passed or are about to pass similar bills, and also due to our country being too much dependent on foreign aid for budget support and other needs, this will mean the end of his presidency, that of his govt. and those in the police force, intelligence services, prosecution and the courts who commit human rights’ abuses. So, it is very important that our govt. and president solve the doctors’, teachers’ and workers’ problems expeditiously and in good faith without resorting to any illegal, moreover, thuggish methods like those employed onDr. Ulimboko.

Finally, I find it hard to understand how our president and his government intend to solve family planning in Tanzania as he declared at the recent summit in UK which he attended (read JK1JK2JK3) without having doctors, which he has sacked in hundreds (read dct1dct2dct3), and now more than a thousand of them are about to join demonstrations as noted in this article. We also see Zanzibari doctors on the verge of protesting like their counterparts on the Mainland – read! What is surprising, however, is that how is it that doctors are currently striking in Portugal, for example, protesting against govt. austerity measures which entail as well cuts in salaries and the health budget, the government has reduced overtime, increased prices for prescription medication and even closed certain services – read Pt1Pt2Pt3. Overworked doctors have denounced a "worrying and dramatic" fall in the quality of care in Portugal's health system - ranked 12th best in the world by the World Health Organization in 2000. The sector has also criticized the purchase of second-rate or obsolete equipment to cut costs and want the government to drop plans to use cheaper outside service providers instead of hiring additional staff, but one never hears that the Portuguese government is even contemplating sacking its worthy and highly-needed doctors while Tanzania with its few thousand doctors to cater for a population of over 44 mln people has sacked its valuable health personnel just for the mere sake of satisfying the ego and cocky arrogance of its shortsighted leadership – what low level of stupidity is this?

Winding up this letter, let me once again call on president Kikwete and his govt. to seize the opportunity, a God-sent one, however cynic this may sound, to clean-up the police force and intelligence services of corrupt and criminal elements in these structures and if it will be proven that indeed police and intelligence officials were involved in such horrendous crimes like the attack on Dr. Ulimboko, then Police Chiefs Saidi Mwema & Kova as well as the Chief of the Country’s Intelligence Service MUST resign. The Minister of Home Affairs should also go.
     

Best regards,

Shaaban
Moscow, Russia       



Friday, July 13, 2012

Chanzo cha Dkt Asha-Rose Migiro KUPOTEZA Unaibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa


Takriban wiki moja baada ya Naibu Katibu Mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa, Dkt Asha-Rose Migiro, kurejea nyumbani Tanzania baada a kukitumikia chombo hicho cha kimataifa kwa kipindi cha miaka mitano, vyanzo vya habari ndani ya Umoja huo vinadokeza kuwa utendaji kazi dhaifu na kushindwa ku-fit katika 'taasisi hiyo kubwa na ngumu' ndio sababu zilizopelekea Mtanzania huyo kunyimwa fursa ya kurefusha mkataba wake wa kazi.

"Wadhifa wa Naibu Katibu Mkuu ni mgumu na wenye mahitaji mengi; unahitaji mtu mwenye uzoefu wa kuongoza Sekretariaeti (ya Umoja huo).Changamoto kubwa kwake ilikuwa kutofahamu siasa za chombo hicho na kutengeneza 'marafiki' (alliances)," kilieleza chanzo kimoja kwa Vox Media kupitia maongezi ya simu.

Imefahamika kuwa Dkt Migiro alijaribu kulishawishi Kundi la Afrika (Africa Group),linalounda asilimia 28 ya wanachama wote wa Umoja wa Mataifa,kuomba limsaidie 'kumpigia debe' ateuliwe tena,ombi ambalo lilikataliwa.

"Hakuwa maarufu miongoni mwa wanadiplomasia, kwahiyo hakuna aliyemsikliza. Pia ukumbuke kuwa uteuzi wake ulipingwa sana," kilieleza chanzo hicho.

Jijini Dar es Salaam, mjumbe mwandamizi wa zamani wa Sekretarieti ya chama tawala CCM  aliyewahi kufanya kazi na Dkt Migiro kabla hajateuliwa kushika wadhifa huo wa Umoja wa Mataifa alieleza kuwa uteuzi huo katika chombo hicho cha kimataifa ulitokana na ukaribu wa Dkt Migiro na Rais Jakaya Kikwete.

Inafahamika kuwa Rais Kikwete na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon walijenga urafiki katika kipindi wote wawili walipokuwa mawaziri wa mambo ya nchi za nje wa mataifa yao.

Ilipofika wakati kwa Ban Ki-moon kuomba kura kushika wadhifa wake wa sasa, Tanzania ilikuwa mstari wa mbele kumsapoti,na kura ya Kikwete ilisaidia Migiro kuteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu.

Lakini Ki-moon alipoamua hivi karibuni kufanya mapitio ya timu yake nzima kwa minajili ya kukabiliana na upinzani mkubwa dhidi ya timu hiyo, ililazimika Dkt Migiro 'atoswe' kutokana na "utendaji kazi dhaifu na ukosefu wa uzoefu unaohitajika kwa watendaji wa ngazi za juu katika Umoja wa Mataifa."

CHANZO: Habari hii imetafsiriwa kutoka Vox Media.Shukrani za pekee kwa mdau @mactemba kwa kunitumia kiungo (link) cha habari hii.

Did You Check the Calendar? Today is Friday the 13th: Be Very Afraid

Monday, July 09, 2012

Chadema Yadai Kigogo wa Usalama wa Taifa Anataka Kuwaua Viongozi Wake Kadhaa

Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Jack Zoka


MBOWE ASEMA MPANGO HUO UNARATIBIWA NA KIGOGO WA USALAMA WA TAIFA, MKUCHIKA ASEMA NI TUHUMA NZITO, AZIVUTIA KASI

Geofrey Nyang’oro
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),kimetoa tuhuma nzito kikidai kigogo mmoja (jina tunalo) wa Idara ya Usalama wa Taifa anaratibu mpango wa kuwaua viongozi wake waandamizi akiwamo Katibu Mkuu, Dk Willbrod Slaa na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika.

Kwa sababu hiyo, chama hicho kimeitisha kikao cha Kamati Kuu (CC) leo kujadili mambo mbalimbali na Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe amesema ajenda kuu itakuwa kuzungumzia usalama wa viongozi wao kutokana na vitisho hivyo.

Kuhusu tuhuma hizo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), George Mkuchika amesema tuhuma hizo ni nzito na atazijibu kwa maandishi.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika Dar es Salaam jana, Mbowe alitaja majina ya baadhi ya maafisa idara hiyo (majina tunayahifadhi) na kudai kuwa mmoja kati yao ndiye anayeratibu shughuli hiyo na tayari yupo mjini Dodoma kwa ajili ya kuongoza  kundi linalotaka kumdhuru Mnyika.

Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, alisema mbali na viongozi hao wawili, mwingine aliyedai kuwa anafuatiliwa ni Mjumbe wa Kamati Kuu, Godbless Lema akidai kwamba, taarifa zinaonyesha kuwa wanafuatiliwa kwa saa 24.
Mbowe alidai kwamba idara hiyo ambayo haifanyi shughuli za siasa, inatumia ofisi yake vibaya kwa kufuatilia viongozi hao wakidhani chama hicho kina mambo ya siri kinayotaka kuyafanya katika nchi hii.

“Sisi Chadema hatuna mambo ya siri tunayotaka kufanya katika nchi hii. Matatizo ya Watanzania yapo wazi na yanajulikana na kila mmoja, Serikali ya CCM itekeleze sera na ahadi zao kwa wananchi na si vitisho,” alisema Mbowe na kuongeza:

“Tunaomba wananchi waelewe kuwa viongozi wao wako hatarini, lakini Chadema hatutarudi nyuma katika kutetea haki  za wanyonge hata kwa kufa na hatuwezi kupeleka malalamiko yetu polisi sababu nao ni sehemu ya tatizo.”

Alisema chama chake kimekuwa kikihusishwa na mambo mengi ukiwamo mgomo wa madaktari unaoendelea na kusema Chadema hakiko nyuma ya mgomo huo na hakijawahi kukutana na kufanya kikao na madaktari.

“Wametuhusisha na mambo mengi na sasa wanasema tuko nyuma ya mgomo wa madaktari, taarifa hizo siyo za kweli na wala hatujawahi kukaa nao kikao chochote kujadili masuala yao, madaktari wana madai ya haki zao. Hapa tunaingia kwenye utaratibu wa kutesana ili kupata taarifa, mmesikia Dk Ulimboka aliteswa ili aseme Chadema iko nyuma ya mgomo,” alidai Mbowe.

Hata hivyo, Mbowe alisema suala la kutokuwa nyuma ya mgomo huo haliwanyimi fursa ya kutetea makundi ya watu wanaodai haki zao wakimwamo madaktari na kusema anaunga mkono tamko la viongozi wa dini.
“Viongozi wa dini wametoa tamko lao jana (juzi), wakitaka Serikali kuwarudisha madaktari na kumalizia suala hilo kwa njia ya mazungumzo,” alisema.

Alisema Chadema kinaunga mkono tamko hilo akisema si busara kuwa fukuza kwa sababu Serikali imetumia gharama kuwaandaa.

Dk Slaa anena

Kwa upande wake, Dk Slaa alisema Chadema kimeamua kutotoa madai yake polisi akidai kuwa imepokea madai mengi kutoka kwa viongozi na wanachama ya kutendewa visivyo lakini hakuna hata moja lililowahi kufanyiwa kazi.

Kuhusu kitisho la kuuawa alidai kwamba alianza kutishiwa siku nyingi na kusisitiza kuwa hilo haliwezi kuwanyamazisha.

“Taarifa za sasa wanaanza na Mnyika na kufuatia mimi, ninachosema wafanye watakavyo hatutaacha kufanya kazi yetu, hata nilipoibua tuhuma za EPA niliwaambia watuhumiwa wengine wa sakata hilo ni Usalama wa Taifa,” alisema Dk Slaa.

Dk Slaa alitaja baadhi ya mambo ambayo alidai kuwa hayakushughulikiwa yalipowasilishwa polisi kuwa ni vinasa sauti alivyowekewa kwenye chumba alichokuwa amelala wakati wa vikao vya Bunge Mjini Dodoma.
Alisema vifaa hivyo vilichukuliwa na polisi kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi lakini hadi leo hakuna taarifa iliyotolewa hata kwake licha ya kuwa mhusika mkuu.

Mnyika: Namwachia Mungu

Akizungumzia madai hayo, Mnyika alisema anamuachia Mungu kwa kuwa ndiye aliyetoa uhai hata kwa hao wanaofikiria kutekeleza kitendo hicho.

Mnyika alidai kuwa baada ya kupata taarifa hizo ambazo alisema zimeandaliwa kwa ama kunyeshwa sumu au kuvamiwa na majambazi, alikutana na familia yake na uongozi wa chama chake ambao kwa pamoja wamemtaka aendelee na kazi ya kutetea rasilimali za taifa.

“Nilipopata taarifa hizi nimekutana na viongozi wangu wa chama na jana usiku (juzi), nilikutana na familia yangu, kwa pamoja wameniambia niendelee na kazi hii ninayoifanya kwani nimetumwa na wananchi na sauti ya wengi ni sauti ya Mungu, ”alisema Mnyika.

Kwa upande wake, Lema alisema  taarifa za kufuatiliwa na watu hao wanaodaiwa kuwa ni wa Usalama wa Taifa alizipata kwa mmoja wa vyanzo vyake kutoka serikalini.

“Nilipigiwa simu na mtu mmoja kutoka serikalini aliyeniambia kuna gari nyuma linanifuatilia, nilipogeuka niliona na kusimama kisha nikashuka na kubadili gari na lenyewe likaendelea kunifuatilia katika gari nililokuwa nimepanda,” alidai  Lema.

Lema alidai kwamba hata juzi asubuhi alikutana nalo katika nyumba aliyofikia na alipolikaribia watu hao walishusha vioo na kumsalimu wakimwita ni Mbunge wa Arusha aliyeko kwenye likizo.

CHANZO: Mwananchi

Mapitio (Review) Yasiyo Rasmi ya Video za SIHITAJI MARAFIKI (Fid-Q) na MISS TANZANIA (Solo Thang)




Naomba nivamie eneo ambalo ninaweza kujiita 'mgeni' (foreign territoty).Hili ni uchambuzi wa muziki,au kwa usahihi zaidi,uchambuzi wa video za muziki.

Nikurejeshe nyuma kidogo.Zamani hizooo,niliwahi 'kuota' kuwa mshiriki wa muziki.Well,sio kuwa mwanamuziki per se bali kujishughulisha na utengenezaji muziki.Nilipokuwa sekondari nilimudu kutunga nyimbo kadhaa kwa kwaya ya shule.Niliweza kutunga aya na sauti lakini tatizo lilikuwa kwenye namna ya uchezaji.Hadi leo,mie na kucheza ni kama kibaka na polisi.Kwa kifupi sijui ku-dance.

Ndoto za kuwa mtengeneza muziki (prodyuza) zilichangiwa zaidi na jinsi ninavyothamini 'michango isiyoonekana.' Hapa ninamaanisha kazi za watu kama watengeneza filamu, watengeneza muziki au hata mashushushu.Hawa ni watu wanaowezesha mengi na pengine laiti wangekuwa wanaonekana na 'products' zilizokwishakamilika basi sifa nyingi zingewaendea wao kuliko ilivyo sasa.

Tunapoona filamu nzuri,sifa nyingi huenda kwa actor au actress.Lakini kimsingi kazi kubwa inayoweza kupelekea filamu ikapata umaarufu hufanywa na mtengenezaji filamu.Kwenye filamu,uzuri wa filamu husika ni mkusanyiko wa jitihada za mwongozaji filamu (yaani director) na mtengenezaji filamu (yaani producer).

Nimeutaja ushushushu.Jamaa hawa ndio kila kitu.Ukiona nchi inakwenda vyema ujue wanafanya kazi yao kwa ufanisi.Ukiona mambo yanayumba basi ujue ndugu zetu hawa wana mushkeli mahala flani.Lakini kimsingi ni kuwa hawaonekani.Kama ilivyo kwa director au prodcuer wa filamu,sifa za kazi husika hulekezwa kwa wengine (kwenye filamu ni actors/actresses) na kwenye mwenendo wa nchi sifa huelekezwa kwa askari au taasisi nyingine za serikali.

Tofauti na filamu na ushushushu ambapo ni mara nyingi ni mkusanyiko wa wengi,kwenye muziki mara nyingi ni jithada za mtu mmoja au wawili. Mara nyingi producer wa muziki ndiye anayebuni ladha ya wimbo kwa maana ya kuunda beatsjapo jukumu la mwisho la ku-flow linabaki kwa msanii husika.Pia inawezekana wimbo ukawa umetungwa na mtu mwingine kisha kumpatia msanii au producer.La msingi hapa ni kuwa producer au mtunzi wa wimbo (kama si msanii mwenyewe) ni watu ambao hawapati sifa za kutosha ukilinganisha na msanii husika.

Kwahiyo moja ya ndoto zangu udogoni ilikuwa kuwa music producer...lakini kama tujuavyo katika maisha sio kila tutakacho ndio tupatacho.Ndoto hiyo 'ilikufa kifo cha asili' baada ya kuelekeza nguvu zangu kwenye  maeneo mengine ya maisha.Lakini hadi leo nina mapenzi ya dhati na muziki hususan wa kufokafoka.

Lengo la makala hii ni kuchambua kazi mbili za wasanii mahiri wa Bongoflava,Fid-Q na Solo Thang,ambao hivi karibuni wametambulisha video zao mpya.

Naomba nisisitize kuwa licha ya mapenzi yangu kwa muziki,mie si mtaalam (expert) wa eneo hilo.Uchambuzi wangu huu ni wa ki-layman (i.e. wa mtu asiye na upeo wa kutosha katika mada husika).

Jingine la kupigia mstari ni desturi iliyojengeka miongoni mwetu kuwa pindi ukionyesha mapungufu ya kitu flani basi wewe ni HATER.Binafsi,nimefika nilipofika kwa sababu siku zote nimekuwa nikipokea na kufanyia kazi maoni mbalimbali hata yale yanayokinzana na imani au mtazamo wangu.Kupewa sifa kuna tatizo moja: hakuwezi kukusaidia kutambua wapi umekwenda kombo.Ofkoz, kazi nzuri lazima isifiwe lakini pengine ili kumsaidia aliyefanya kazi hiyo ni vema kumfahamisha wapi arekebishe au penye mapungufu.Na hiki ndio nitakachofanya katika makala hii.

Video za muziki ninazozichambia ni ile ya SIHITAJI MARAFIKI ya FID-Q na MISS TANZANIA ya SOLO THANG.Kwa kifupi,video zote ni za ubora wa hali ya juu.Wasanii wote wawili wamechagua location za kuvutia wakati wanarekodi video zao.Kadhalika,ubora wa picha ni wa kiwango cha juu.


Wasanii hawa wana sifa moja inayolingana: ni mahiri mno katika uwasilishaji wa ujumbe uliomo kwenye wimbo husika.Wote wana uwezo wa hali ya juu wa kucheza na maneno, neno pekee la Kiingereza unaloweza kulitumia kuwaelezea ni LYRICAL ASSASSINS (Usitishwe na hiyo 'assassins' kwani ni neno tu linalotumiwa kutanabaisha namna msanii anavyoweza 'kucheza na maneno' kwenye tungo husika).

Wakati Solo Thang anamzungumzia Miss Tanzania,Fid-Q anazungumzia marafiki.Ujumbe katika tungo zote mbili haupo wazi sana na inambidi msikilizaji 'asome kati ya mistari' (reading between the lines) kuelewa kinachoongelewa.Usipokuwa makini unaweza kudhani Solo 'anawapaka' warembo lakini kimsingi MISS TANZANIA imebeba ujumbe mzito hususan kwa mabinti warembo wenye kuendekeza tabia zisizopendeza machoni kwa jamii.

Ujumbe wa Solo unapigia mstari mtizamo wa wengi kuhusu urembo kama fani (iwe u-Miss au uanamitindo).Yayumkinika kusema kuwa machoni wa wengi fani hizo mbili hutizamwa 'kwa jicho baya' hasa kutokana na tabia kama za huyo 'Miss Tanzania anayezungumziw na Solo.' Huu ni ukweli i.e. ni mtazamo wa wengi japo si kila Miss au mwanamitindo ana tabia zisizopendeza katika jamii.Inawezekana Solo anamzungumzia Miss Tanzania flani?Jibu la swali hili analo yeye mwenyewe lakini kwa vile ni mahiri mno wa 'kucheza na maneno' yayumkinika kuamini kuwa kuna ujumbe mpana pengine zaidi ya uelewa wetu.

Kwa upande wake Fid-Q, SITAKI MARAFIKI haimaanishi marafiki si muhimu bali kwa kutumia kipaji chake kikubwa cha kuwasilisha ujumbe kwa namna inayohitaji tafakuri,msanii huyo anaweka wazi mtazamo wake kuhusu mahusiano katika jamii,kwa kutumia mfano mwafaka wa marafiki.Nadhani ushaskia msemo  'MARAFIKI WA NINI KAMA MAADUI WANANISAIDIA.' Mara nyingi,marafiki zetu hupenda kututendea mazuri tu tunayotarajia kutoka kwao na pengine kuepuka kutueleza 'hapa umechemka.' Lakini maadui zetu huwa mahiri wa kuonyesha kasoro zetu (hata kama ni kwa uchache) japo kimsingi matarajio yao huwa ni kuonyesha mabaya yetu.Kwa hiyo pasipo kukusudia,maadui zetu wanaweza kuwa na mchango flani chanya katika maisha yetu kwa sababu hawana unafiki katika kunyooshe akidole mapungufu yetu.

Kwa anayezifahamu vema kazi za Fid-Q na Solo Thang ni wazi hatokuwa na wasiwasi kuhusu namna watakavyouwasilisha ujumbe kwenye tungo mpya.Kama nilivyoeleza hapo juu,wasanii hawa wana uwezo wa hali ya juu wa 'kucheza na lugha na maneno.' Uwezo huo unawasiaidia sana katika kuwasilisha ujumbe katika namna inayomwacha msikilizaji 'ameterazika' (ameridhika)

Sasa nigeukia eneo linaloweza kuniingiza matatizoni: mapungufu katika kazi hizo za wasanii hao.Kimsingi si mapungufu bali ni pungufu kwani ni moja tu,na si kubwa sana.Ukiangalia video zote mbili utabaini jambo hili: katika video ya Fid-Q,tangu mwanzo hadi mwisho wa video yake amevaa vazi lilelile.Kwa Solo,kwa kiwango kikubwa katika video hiyo yupo katika T-shirt ileile japo kuna vipande ambapo anaonekana amevaa shati.

Kama nilivyotanabaisha,hii ni kasoro ndogo inayoweza kabisa kufunikwa na ladha ( flavour) ya muziki, ujumbe uliomo katika wimbo,na kiwango cha video.Hata hivyo,kama inavyotanabaishwa kwenye na Andrew Goodwin kwenye Kanuni ya Video ya Muziki (Music Video Theory) vinavyoonekana katika video ya muziki (visuals) vinaweza kuwa na mchango mkubwa sio tu kuiboresha video husika bali pia kuiunganisha na hadhira.

Pengine ili uelewe ninachoelezea hapa nitolee mfano msanii kama Lady Gaga.Mavazi yake ni burudani tosha-japo sio aina ya mavazi unayoweza kumwambia fundi cherahani akutengenezee.Msanii kama Michael Jackson alifahamika sio tu kwa miziki yake bali pia mavazi yake.Kwa sanii wa hip-hop wa Marekani,mavazi ni moja ya vitu muhimu mno,na baadhi ya mapendezeo yao katika mavazi yamepelekea mwamko wa fasheni,kwa mfano mashati ya 'DOGI DOGI' yaliyokuwa yanapendelewa na wasanii wa rap/hiphop wa pwani ya magharibi ya Marekani (West Coast rappers) kwa mfano Snoop Dogg na Ice Cube



Nadhani sababu pekee iliyowafanya Fid-Q na Solo wasionekane katika mavazi tofaut tofauti katika video zao ni MUDA.Hapa ninabashiri kuwa hawakuwa na muda wa kutosha kurekodi video zao kwa muda mrefu ambao ungewapa nafasi za kubadili mavazi mara kadhaa.Naomba nisistize kuwa kasoro hiyo ndogo haijapoteza hata chembe ladha ya kazi zao bora kabisa.Nimeipigia mstari kasoro hii kwa minajili ya kuwasaidia wasanii hao huko mbeleni wajaribu kutumia muda zaidi katika kurekodi video zao.Kanuni nyepesi ya kurekodi kitu chochote kile ni hii: kadri unavyojipa muda wa kutosha ndivyo unavyomudu kurekodi vitu vingi zaidi ambavyo wakati wa kuhariri utaondoa vile usivyovitaka na kuacha vile unavyovitaka.

Lakini kasoro hiyo ndogo inarekebishika.Ninaamini tulichoshuhudia katika video ya SIHITAJI MARAFIKI na MISSI TANZANIA ni matoleo ya mwanzo tu (iwapo Fid na Solo wana mtizamo kama wangu).Si ajabu kwa msanii kutoa video ya mwanzo kisha kutoa video nyingine rasmi kwa ajili ya wimbo husika.Mfano mzuri ni huu wa kundi la TOK katika wimbo wao Footprints Hii ni version ya awali

Hii ni version rasmi

Pengine kitawachowarahisishia Solo na Fid-Q kutengeneza video 'r(kama wataona kuna haja ya kufanya hivyo) ni ukweli kwamba tayari wana video nzima ya asili,ambapo wakiamua kuongeza chochote inakuwa ni suala la kuongeza tu vipande vipya katika original version.Hili si lazima,as long as wao wameridhika na versions walizoweka hadharani.

Ukiweka kando kasoro hiyo ndogo,Solo Thang ameendelea kuwa mithili ya balozi wetu wa Bongoflava katika anga za kimataifa ambapo anafanyia kazi zake kutoka nchini Ireland.Lakini licha ya kuwa nguli (legend) wa bongoflava na 'wadhifa' huo wa ubalozi wa kimataifa,msanii huyu ni miongoni mwa wachache ambao ni down-to-earth sana na anayejali sana kuishirikisha hadhira,hususan kupitia Twitter na Facebook.Kadhalika,ana blogu yake anayotumia kuwafahamisha wapenzi wa muziki wake kuhusu kazi zake.

Kwa upande wa Fid-Q, mkongwe huyu wa muziki wa kufokafoka huko nyumbani amekuwa mahiri sana katika matumizi ya mitandao ya kijamii kutangaza kazi zake na kuishirikisha hadhira.Huko Twitter ana utaratibu wa kujibu maswali angalau mara moja kwa wiki kwa kutumia hashtag #AskFidQ. Hii inatoa fursa kwa wengi kumuuliza maswali mbalimbali.Kadhalika,anaendesha kitu kinachofahamika kama Hip-Hop Darasa,ambapo pamoja na mambo mengine anatoa elimu kwa kizazi kipya cha Hip-hop huko nyumbani.Taarifa za hivi karibuni zinaonyesha kuwa kipindi chake maarufu mtandaoni cha Fidstyle Friday kitaanza kuonyeshwa kwenye runinga katika kituo cha East Africa Television (EATV).Haya ni maendeleo makubwa.

Basi nimalizie kwa kuwapongeza Fid-Q na Solo Thang kwa kazi zao bora kabisa.Naomba wasitafsiri kasoro ndogo niliyobainisha hapo juu kuwa ni HATING. Sote tunapenda kuona wasanii wetu wakifanikiwa na kuteka anga sio huko nyumbani tu bali Afrika na duniani kwa ujumla.Natambua kuna wataosema "huyu nae,anajifanya anajua kila kitu" lakini lengo langu si kujifanya mjuaji bali kutoa mchango wangu kwa wasanii wetu.

Nimalizie makala hii na video zifuatazo za wasanii hao


 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Hot Sonakshi Sinha, Car Price in India