Featured Posts

Tuesday, May 21, 2013

Msanii Mwenye Jina Kubwa Kabisa ktk Bongoflava, Profesa Jay, Aujiunga na Chadema

Click image for larger version.   Name: Prof Jay Ajiunga Na Chadema.jpg  Views: 0  Size: 47.5 KB  ID: 94612
 Profesa Jay akipokea kadi ya unachama wa Chadema kutoka kwa Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema) Mh. Joseph Mbilinyi (a.k.a Sugu)
Click image for larger version.   Name: Prof Jay Na Sugu Na Mnyika.jpg  Views: 0  Size: 40.8 KB  ID: 94613

Profesa Jay akiwa na Mh 'Sugu'  na Mbunge wa Ubungo (Chadema) Mh John Mnyika.

Ni Mtanzania gani kijana (na hata wazee wa kati) asiyemjua Profesa Jay, msanii mahiri wa Bongoflava ambaye jina lake halisi ni Joseph Haule (au Jay wa Mitulinga). Msanii huyo, pengine katika hali ambayo haikutarajiwa kabisa, leo amejiunga na chama cha upinzani cha Chadema.

Uamuzi wa Profesa Jay kujiunga na Chadema unaweza kuwa na manufaa makubwa sana kwa chama hicho hasa kwa vile mabadiliko ya kisiasa huko nyumbani yanategemea zaidi hamasa ya vijana.


Nitaandika zaidi baadaye kuhusu tukio hili muhimu kwa Chadema, muziki wa bongoflava na vijana kwa ujumla, lakini kwa sasa burudika na kibao hiki cha "Nikusaidiaje" cha Profesa Jay akimshirikisha Ferouz

0 comments:

Post a Comment

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Hot Sonakshi Sinha, Car Price in India