Featured Posts

Wednesday, January 29, 2014

PLUS SIZE CLOTHING SASA ZINAPATIKANA Zurii FASHION BOUTIQUE. KARIBUNI SANA

Wale wateja wetu wa Plus Size tumesikia kilio chenu na sasa Zurii Fashion & Beauty Boutique kuna Stock Mpya kwa ajili yenu Plus Size ladies (wale mlio jaliwa neema hahaha). Size 14-20 sasa zinaptikana ZuRii. Kuna Nguo nzuri sana na quality nzuri sana za kazini, kanisani na za mitoko.
Size ndogo 8-12 pia zipo.
 Tuko Sinza Legho, nyuma ya Rombo Green View Hotel, Dar Es Saalm. Whatsapp au tupigie +255659189769 kwa maelezo zaidi. Karibuni sana.
LOOK GOOD, FEEL GOOD with ZuRii.








Follow us on Instagram @zuriiboutique
Like our page on facebook Zurii Fashion Boutique

Sunday, January 26, 2014

Makala yangu ktk RAIA MWEMA Toleo la 22.01.13 "Uteuzi wa Mawaziri na Matumaini Hewa"


YAYUMKINIKA kuhitimisha kuwa Tanzania yetu ni moja ya nchi rahisi kuongozwa duniani. Japo wakati mwingine urahisi huo unachangiwa na sheria dhalimu au matumizi ya ubabe yanayofanywa na dola, kwa kiasi kikubwa Watanzania ni wapole kiasi kwamba hata wakitendwa visivyo kwa muda mrefu, kwa wengi wao si jambo la kuwaamsha kudai stahili zao.
Na pengine hakuna mfano rahisi wa urahisi wa kuingoza Tanzania kama katika adha ya mgawo wa umeme wa milele. Hapa nakiri ukweli kwamba moja ya mambo yanayonikera niwapo mtandaoni ni kukumbana na watu wanaolalamikia mgawo wa umeme (wengine kwa lugha isiyoandikika gazetini) kila kukicha.
Kulalamika si tatizo na wanaolalamika wana haki ya kufanya hivyo. Tatizo ni ukweli kwamba malalamiko yao ambayo nyakati nyingine huambatana na matusi mazito dhidi ya TANESCO hayajamsaidia kwa namna yoyote angalau kupunguza tatizo la mgawo wa umeme.
Kimsingi, atakayehitimisha kuwa Watanzania wameridhia kutopewa huduma ya uhakika ya umeme, hatakuwa amekosea. Nimewahi kutumia mfano huu wa hamasa mara kadhaa, kwamba mkoloni hakuamua tu kutupatia uhuru kwa vile hatukupenda uovu aliotufanyia, Nduli Idi Amin hakusalimu amri katika Vita ya Kagera kwa vile tulimwita kila aina ya jina baya, na makaburu huko Afrika Kusini hawakuamua tu kuacha mfumo wa ubaguzi kwa vile sio wa kibinadamu. Zilifanyika jitihada kubwa za kuwafikishia ujumbe wakoloni, Amin na makaburu kuwa ‘imetosha,’ sambamba na harakati za vitendo za kumaliza uovu wao.
Pengine mfano mwingine wa karibu ni malalamiko ya wananchi wengi kuhusu huduma zisizokidhi matakwa za baadhi ya kampuni za huduma huko nyumbani, hususan kampuni za simu. Utakutana na mtu anaitukana kampuni ya simu, ilhali hajashikiwa mtutu wa bunduki kuendelea kuwa mteja wa kampuni hiyo. Wengi wa watumiaji wa huduma ya simu huko nyumbani ni wa ‘malipo kabla’ (pre-payment) na hawabanwi na mikataba yenye masharti kama wale wa ‘malipo baada’ post-payment).
Binafsi, nipo katika mkataba wa miezi 24 wa huduma ya simu ya mkononi, na katika kipindi hicho, nikiamua kuachana na kampuni inayonipatia huduma nitalazimika kulipa fidia ‘kubwa tu.’ Lakini huko nyuma niliwahi kuwa mteja wa huduma za ‘pay as you go’ (lipa kadri unavyotumia) na kila nilipoona siridhishwi na huduma ya kampuni husika niliachana nayo.
Lengo la makala haya si kujadili tatizo la mgawo wa umeme, huduma mbovu za TANESCO na baadhi ya kampuni za huduma au hata upole wa Watanzania. Badala yake, wiki hii ninatupia jicho ‘matumaini hewa ya Watanzania wengi’ wakati walipokuwa wakisubiri mabadiliko ya Baraza la Mawaziri yaliyotangazwa Jumapili iliyopita.
Kama ilivyo kabla ya kila kikao cha Bunge ambapo vyombo mbalimbali vya habari hupambwa kwa vichwa vya habari kama ‘Bunge kuwaka moto’ au ‘Wabunge kuikalia kooni serikali,’ kisha vikao hivyo vya Bunge kuisha bila lolote la maana, kama ilivyotokea katika vikao vilivyotangulia, ndivyo vyombo vingi vya habari vilifanya bidii kubashiri ‘makubwa’ katika mabadiliko hayo ya Baraza la mawaziri.
Sijui matumaini hayo ‘hewa yalitoka wapi hasa ikizingatiwa kuwa taratibu za uteuzi ambazo huko nyuma zimeonekana kuzaa wateuliwa wabovu ni zilezile.
Nikiri kwamba nilikuwa ‘mhanga’ wa matumaini hayo  lakini angalau matumaini yangu hayakuwa ‘hewa’ kwani yametimia kwa kiasi fulani. Nilitaraji aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, awe Waziri kamili, na hilo limetokea. Niliandika katika makala yangu moja huko nyuma kwa nini ninamwona mwanasiasa huyo kama mwenye sifa kadhaa za kuigwa na wanasiasa wenzie, kubwa zaidi ikiwa ni uzalendo kwa mantiki ya kujiepusha na kasumba ya kutanguliza itikadi za kisiasa mbele ya maslahi ya taifa.
‘Kilichonitibua nyongo’ katika mabadiliko hayo yaliyotangazwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue (kuna wanaohoji kwa nini mabadiliko hayo hayakutangazwa na Rais Jakaya Kikwete kama ilivyozoeleka) ni uteuzi wa Mwigulu Nchemba kuwa Naibu Waziri wa Fedha. Pengine hisia zangu baada ya kusikia habari hizo zinaelezeka vizuri ‘andiko’ nililotundika katika blogu yangu kwamba uteuzi huo ni ‘utani mbaya’ (a bad joke).
Akiwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Tanzania Bara, Mwigulu alifanya kila aliloweza kujenga uhasama mkubwa miongoni mwa Watanzania kupitia kauli na matendo yake dhidi ya vyama vya upinzani na baadhi ya viongozi wake, hususan CHADEMA. Kuthibitisha upungufu wake wa busara, kuna wakati Mwigulu alionyeshwa katika pichani akiwa na mbwa aliyevishwa bendera ya CHADEMA. Kitendo hicho ni zaidi ya ‘utoto wa kisiasa’ (political immaturity).
Lakini pamoja na kushtushwa na kukerwa na uteuzi huo wa Mwigulu kuongoza Wizara hiyo nyeti,  binafsi nimeelewa mantiki ya Rais Kikwete (angalau kwa hisia zangu tu). Kwanza, sasa tunaelewa kuwa yale yote yaliyokuwa yanatukera wengi katika kauli na matendo ya Mwigulu yalikuwa na baraka za Mwenyekiti wake, yaani Rais Kikwete, na sasa amezawadiwa unaibu waziri kwa ‘kazi nzuri aliyofanya.’
Pili, sote tunafahamu kuwa moja ya changamoto zinazoikabili CCM kuelekea Uchaguzi Mkuu hapo mwakani ni upatikanaji wa fedha (kihalali au isivyo halali). Japo ninaweza kuwa sipo sahihi, ninashawishika kuhisi kuwa uteuzi wa Mwigulu kwenda Hazina una uhusiano na jitihada za chama hicho tawala kujitengenezea mazingira ya kupata fedha kwa ajili ya kampeni za uchaguzi huo. Je, tutarajie ‘EPA’ nyingine? Ni muda tu unaoweza kutupa jibu.
Tatu, uteuzi wa Mwigulu ni mwendelezo wa tatizo sugu la kuweka mbele itikadi badala ya maslahi ya taifa. Kila anayefuatilia siasa za nchi yetu anatambua kuwa mwanasiasa huyo ni nguli wa siasa za uadui, na japo katika utendaji wake wa kazi anapaswa kuzingatia taratibu na kanuni, ni wazi kuwa vyama vya upinzani vitaendelea kumwona kama adui yao.
Vinginevyo, vihoja lukuki alivyofanya dhidi ya wapinzani vilikuwa ni sehemu ya mkakati makusudi wa CCM, yayumkinika kujiuliza; “kama mtu alifanya madudu kwenye ulingo wa siasa, atawezaje kuleta ufanisi kwenye sekta nyeti ya uchumi (katika Wizara ya Fedha)? Tuwe wa kweli, wakati hata mimi ninaweza kubainisha kwa nini mtu kama Nyalandu alistahili kupanda ngazi, ni nani anayeweza kusimama hadharani kutueleza japo sababu moja tu ya Mwigulu kupewa wadhifa huo?
Kwa upande mwingine, ni muhimu kutambua kuwa ‘shangwe’ za kuona baadhi ya mawaziri wakipumzishwa baada ya mabadiliko hayo, kwa mfano aliyekuwa Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo, Philip Mulugo (atakayekumbukwa zaidi kwa ubabaishaji wake wa “Muungano wetu ni kati ya visiwa vya Pemba na Zimbabwe”) sio tu zinaambatana na gharama kubwa kifedha, lakini pia haitakuwa jambo la kushangaza kusikia waliopumzishwa wakipewa ukuu wa mikoa au ubalozi.
Nimalizie makala haya  kwa kurejea nilichotanabaisha mwanzoni kuwa nchi yetu ni rahisi sana kuongozwa, na pengine ndio maana tunashuhudia hata wanasiasa wenye vihoja kama Mwigulu wakipewa unaibu waziri katika wizara nyeti. Kwa nini mtawala achelee matokeo ilhali anatambua fika kuwa anaowaongoza sio tu ni wapole kupindukia lakini ni mahiri kwa mtizamo wa kwa nini tujali?

Sunday, January 19, 2014

Baraza Jipya la Mawaziri: JK afanya utani mbaya, amteua Mwigulu Nchemba kuwa Naibu Waziri wa Fedha




UCHAMBUZI WA HARAKA:

Yaelekea matatizo ya uchumi wetu si miongoni mwa mambo yanayomnyima usingizi Rais Jakaya Kikwete, ndio maana amefanya kituko cha mwaka kumteua Mwigulu Nchemba kuwa Naibu Waziri katika Wizara hiyo nyeti. Ila mzaha huo ni wa kimkakati zaidi. CCM inahitaji fedha kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi mkuu mwaka 2015. Hadi hapo si tatizo, lakini tatizo lipo kwenye kupata fedha hizo kwa njia halali. Ninatafsiri uteuzi wa Mwigulu kwenda Wizara ya fedha kuwa ni sehehmu ya mkakati wa kuiwezesha CCM kupata fedha za uchaguzi mkuu ujao. Tutegemea EPA nyingine? Time will tell.

Adam Malima kupelekwa Wizara nyeti ya fedha si jambo la kushangaza, ikizingatiwa yyeye na JK wanatoka mkoa wa Pwani na ukaribu wao. Sijui nini kilichopeleka Juma Nkamia kupewa uwaziri wa Michezo, lakini majibu anayo JK mwenyewe.

BOTTOM LINE: Tatizo sio mawaziri bali Kikwete mwenyewe. Mbunge wa Ubungo aliwahi kuingia matatani alitamka bayana kuwa JK NI DHAIFU lakini ukweli unabaki kuwa ukweli, na alichosema Mnyika ndo ukweli wenyewe. Mawaziri wanaweza kubadilishwa kila wiki, lakini as long as kiongozi wao ni dhaifu, basi tuendelee kutarajia yaleyale yanayopelekea kabineti kubadilishwa mfululizo kama safari za JK nje ya nchi.

Na kwa waliodhani Pinda angeng'oka walikuwa wanaota ndoto za mchana. Pinda ni nyenzo muhimu kwa JK, ni mtu anayebeba lawama za bosi wake. Madudu yakifanywa na JK,lawama zinaelekezwa kwa Pinda.

Tuombe Mungu 2015 ifike mapema, JK amalize majaribio yake ya urais, labda nchi yetu itapata mwelekeo mpya.

MUNGU IBARIKI TANZANIA

MABADILIKO HUSIKA NI HAYA HAPA CHINI

- Hakuna Mabadiliko Ofisi ya Rais

- Ofisi ya Makamu Wa Rais - Naibu Waziri Kitwanga amehamishwa na nafasi yake imejazwa na Mhe. Ali Mwalimu

- Mwigulu Nchemba amekuwa Naibu Wizara ya Fedha (Sera). Aliyekuwa nafasi hiyo sasa ni Waziri Kamili
- Uchumi na Mapato sasa anatoka Janet Mbene na inajazwa na Adam Malima

- Asharose Migiro sasa ni Waziri wa Katiba na Sheria

- Ulinzi na Kujenga Taifa => Hussein Mwinyi

- Mambo ya Ndani - Mathias Chikawe

- Afya na Ustawi wa Jamii - Naibu wake sasa ni Waziri Kamili; naibu wa sasa ni Dr. Kebwe S. Kebwe

- Mulugo ameondoshwa rasmi serikalini. Nafasi yake imejazwa na Jenista Muhagama

- Pindi chana amejaza nafasi ya Ummi Mwalimu - Jinsia na watoto

- Mifugo na Maendeleo ya Mifugo - Titus Kamani atakuwa Waziri mpya. Naibu ni Telele na hivyo Wizara nzima imepata mawaziri wapya

- Ole Medeye OUT - Simbachawene kachukua nafasi yake (Naibu wa Prof. Tibaijuka)

- Naibu Kilimo - Zambi

- Habari - Naibu ni Juma Nkamia

- Nyalandu amekuwa Waziri Kamili. Naibu ni Mahmood Hassan Mgimwa

- Muhongo na Naibu wake wamebakizwa. Nishati atachukua Charles Kitwagwa akiichukua toka kwa Simbachawene


Magazeti ya Tanzania Leo Jumapili 19.01.13: JK Kutangaza Baraza jipya la Mawaziri Leo?


.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

Saturday, January 18, 2014

Friday, January 17, 2014

Makala yangu Ktk RAIA MWEMA Toleo la 15.01.14: "Zitto na ushujaa wa kuonja sumu"

KATIKA hitimisho la makala yangu iliyochapishwa wiki mbili zilizopita, iliyobeba kichwa cha habari ‘Ni mwaka wa siasa za hovyo CCM, CHADEMA, niliahidi kuendeleza utabiri wa mwaka huu 2014, kwa kuangalia anga za kimataifa.
Kwa bahati nzuri, siku nne tu baada ya kuchapishwa makala hiyo, moja ya mambo niliyotabiri - kuendelea kwa mgogoro wa CHADEMA na uwezekano wa migogoro ndani ya vyama vya upinzani kuwa ya hadharani - limetokea.
Ninaomba niweke bayana kuwa masikitiko yangu kuhusu maendeleo mapya katika mgogoro wa CHADEMA ni makubwa zaidi ya furaha yangu kuona nilichotabiri wiki iliyopita kweli kimetokea. Nitakuwa mbinafsi na mnafiki ‘kusherehekea usahihi wa utabiri wangu’ katika jambo lisilopendeza. Laiti ingekuwa ni chaguo langu basi ningetamani mabaya yote niliyotabiri yasitokee, lakini kwa bahati mbaya hali halisi haikwepeki.
Takriban wiki mbili zilizopita, Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA) Zitto Kabwe alirusha ‘bomu zito’ ambapo alitoa tuhuma kubwa na hatari dhidi ya Mwenyekiti wake taifa wa chama hicho, Freeman Mbowe, na chama hicho kwa ujumla. Pengine ili kuleta ladha halisi ya alichosema Zitto ni vema nikanuu ‘waraka’ mzima kama ifuatavyo:
"Lissu anasema nimepewa magari 2 na Mzee Mkono. Anasema kaambiwa na Mkono. Naamini Mkono alimwambia pia mwaka 2005 alimpa Freeman Aikaeli Mbowe tshs 40m ili Mbowe asifanye kampeni Musoma Vijijini.
“Nadhani alimwambia pia mwaka 2008 (baada ya orodha ya mafisadi kutangazwa 2007) Mkono alimpa Freeman tshs 20m za uchaguzi wa Tarime na Freeman akasema kwenye chama ametoa mkopo na akalipwa. Nadhani alimwambia pia kuwa mwaka 2010 Mkono alimpa Mbowe tshs 200m za kampeni ya Slaa.
“Pia hakusahau kumwambia kuwa Rostam Aziz alimpa Mbowe tshs 100m za kampeni. Lissu anajua kuwa gazeti la Tanzania Daima limeanzishwa na fedha za chama kutoka Conservative Party?
“Nimefanya internship yangu kwa Mkono and Company Advocates kuhusu masuala ya mikataba. Mzee Mkono ni Mzee wangu na alisaini petition ya kumtoa Waziri Mkuu Pinda. Lissu awaambie waliyemtuma wamwambie ukweli wote. Lissu ajue yeye ni kifaranga tu, Mimi namtaka mama wa kifaranga ajitokeze. Aeleze aliingia deal gani na Kinana na Sumaye mwaka 2005 kufuatia deni lake NSSF. Aweke wazi mkataba kati yake na NHC kuhusu nyumba ya umma ilipo Club Bilicanas.
“They must know I am not a push over. Chacha died, I won't. Mtu ambaye hawezi kuheshimu mke wake aliyemzalia watoto hawezi kunyooshea mtu kidole kuhusu maadili."
Zitto alibandika waraka huo katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Facebook, lakini kwa sababu anazojua yeye pekee, baadaye aliuhariri na kutojumuisha tuhuma hizo. Aidha kwa kutofahamu au makusudi, uhariri uliofanywa na mwanasiasa huyo katika waraka huo haukuzuia kusambaa kwa kasi mtandaoni.
Niliposoma waraka huo nilipatwa na mshtuko mkubwa, nikabaki ninajiuliza iwapo Zitto alikuwa ‘mzima’ wakati anaandika alichoandika.  Japo inawezekana alifanya hivyo kwa kuzingatia kile kinachofahamika mtaani kama ‘umemwaga ugali na mie namwaga mboga...bora tukose wote,” ukweli ni kwamba bandiko hilo lina madhara makubwa, kwa Zitto binafsi na kwa pengine ustawi wa CHADEMA kwa ujumla.
Madhara kwa Zitto ni ya kisheria zaidi. Tayari Mbowe ameonyesha nia ya kumburuza Zitto mahakamani kuthibitisha tuhuma hizo nzito. Bila kujali kuwa tuhuma hizo zina ukweli au la, mtu yeyote mwenye uelewa wa ‘dili za siri’ atafahamu kuwa ni vigumu kuzithibitisha kisheria, yayumkinika kuhisi kuwa Zitto atakuwa na kazi ya ziada katika ‘kesi’ hiyo (iwapo itafunguliwa).
Iwe ni tuhuma za Nimrod Mkono kumpa Mbowe shilingi milioni 260 katika mazingira ambayo si tatanishi tu bali pia kwa namna fulani ni hujuma dhidi ya CHADEMA, au Rostam Aziz kumpatia Mbowe shilingi milioni 100, au ‘dili’ kati ya Mbowe na Waziri Mkuu wa zamani, Frederick Sumaye na Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana, sidhani kama Zitto anaweza kuthibitisha tuhuma hizo iwapo Mbowe atatimiza azma yake ya kufungua kesi. 
Je, inawezekana kuwa kwa kutambua ‘kosa hilo la kisheria’ ndio maana muda mfupi baadaye Zitto alihariri ‘post’ hiyo? Wakati jibu analo Zitto mwenyewe, ukweli unabaki kuwa tuhuma hizo ni nzito mno, na iwapo ni za kweli basi zinapoteza kabisa hadhi ya CHADEMA.
Ikumbukwe kuwa katika waraka uliopelekea Zitto kuvuliwa nyadhifa zake mbalimbali ndani ya CHADEMA, walioandika waraka huo waligusia walichokiita ‘udhaifu wa wanayemtaka’ (wakimaanisha Zitto), na kudai, “Maneno yake mara nyingine hayazingatii anayazungumza katika mazingira gani na hivyo kuwasha masikio ya wanataasisi jambo linalompunguzia kukubalika kwake taratibu.” 
Kadhalika, walieleza kuwa; “Kuna wakati tunayemtaka (Zitto) hujibu kwa taharuki kubwa dhidi ya mashambulizi yanayoelekezwa kwake jambo linalomfanya achukue maamuzi yasiyo sahihi kwa wakati huo. Kwa kifupi kuna wakati tunayemtaka (Zitto) huonekana kufanya maamuzi kwa hisia zaidi badala ya kutulia kwanza na kutafakari kwa kina ikiwa ni pamoja na kutafuta ushauri kwa wenzake kabla ya kujibu.”
Ndugu msomaji, huhitaji kuwa mwanasaikolojia kuhisi kuwa huenda kilichomsukuma Zitto kuandika ‘waraka’ huo kwenye ukurasa wake wa Facebook ni kile Waingereza wanakiita “putting emotions in front of common sense”, yaani kwa tafsiri isiyo rasmi, kuweka mbele jazba badala ya busara.
Kwa kujaribu kuonyesha kuwa Mbowe si mwadilifu (kwa maana ya kupokea misaada kutoka kwa ‘wanasiasa kama Mkono na Rostam waliowahi kutajwa na CHADEMA kuwa ni mafisadi’), linakuja swali la msingi, kwanini Zitto alikalia kimya tuhuma hizo nzito kwa takriban miaka minane hadi sasa baada ya kuvuliwa madaraka? Hivi kuna neno stahili kuelezea hali hiyo zaidi ya unafiki?
Tukiamini tuhuma hizo za Zitto, je naye si sehemu ya ‘uhuni wa CHADEMA’ wa kukemea mafisadi hadharani ilhali pembeni wanapokea misaada ya watu hao hao wanaowatuhumu? Ninasema hivyo kwa sababu Zitto hakuwa katibu wa shina bali Naibu Katibu Mkuu (taifa)  wa chama hicho, na mbunge, na kwa vyovyote vile naye ni mnufaika wa fedha hizo ‘za mafisadi.’
Laiti angekuwa haridhii vitendo hivyo basi aidha angejitoa mhanga na kuweka ukweli hadharani wakati huo (na hiyo ingeweza kuzuia kurejea kwa vitendo kama hivyo) au angeweza kujiuzulu kwa kuona ‘chama chake kinashirikiana na watuhumiwa wa ufisadi. Kwa nini hakufanya hivyo? Jibu jepesi ni hilo nililoandika hapo juu: alikuwa mnufaika wa vitendo hivyo (iwapo kweli vilitokea, maana tayari baadhi ya aliowataja wamekanusha ‘kumpa msaada’ Mbowe).
Binafsi, ninadhani moja ya matatizo yanayomkabili Zitto ni wanaojiita au kujitambulisha kama wafuasi wake. Wengi kati yao ni wenye mapenzi na CCM, na ushabiki wao kwa Zitto ni wa kirafiki (kimaslahi?) zaidi. Ndio, tofauti za kiitikadi hazimaanishi uadui, lakini wengi wetu tunaufahamu msemo ‘nionyeshe marafiki zako na nitakwambia wewe ni nani,’ yaani mara nyingi watu wanaotuzunguka hutoa picha fulani kuhusu sisi wenyewe.
Lakini tatizo jingine kuhusu ‘wafuasi na marafiki hao wa Zitto’ ni kutokuwa washauri wazuri kwake. Ukisoma mengi ya wanayoandika, hususan huko kwenye mitandao ya twitter, utabaini kuwa kimsingi wanachofanya ni ‘kumvimbisha kichwa Zitto’ bila kutoa ushauri unaoweza kusaidia ustawi wa kisiasa wa mwanasiasa huyo kijana.
Na mfano wa hivi karibuni ni baada ya Zitto kubandika waraka huo wenye tuhuma nzito huko Facebook. Wengi wa wafuasi wake walionekana kuchekelea ‘Mbowe alivyoumbuka’ bila kujali athari za kisheria kwa Zitto na ustawi wa CHADEMA kwa ujumla (kwanini wajali ilhali wengi wao ni wanaCCM)?
Kwa wafuasi wa Zitto, mwanasiasa huyo ni majeruhi wa siasa za chuki na mizengwe ndani ya CHADEMA. Lakini kwa wengine, Zitto anaonekana kama mtu anayeendeshwa na ‘ego’ kubwa inayomfanya kujiona yeye ndiye-au zaidi ya- CHADEMA.
Ni vigumu kubashiri hatma ya maisha ya kisiasa ya Zitto lakini kwa hali ilivyo ni vigumu mno kuona mustakabali wake ndani ya chama hicho. Ninakumbuka mwanasafu mmoja wa gazeti hili alimshauri mwanasiasa huyo hivi karibuni kuwa suluhisho la busara kwake kwa sasa ni kutosubiri kuvuliwa uanachama, ajiondoe mwenyewe huko CHADEMA, na kuitaka Mahakama isiingilie kazi ya chama.
Mwisho, bado ninaamini kuwa Zitto ni mwanasiasa mzuri lakini pengine kwa upungufu wa kibinadamu au makusudi, washauri wabovu au sababu nyinginezo, hazingatii umuhimu wa busara hizi tatu katika medani ya siasa: moja, waweke marafiki zako karibu lakini waweke maadui zako karibu zaidi, na pili, hakuna marafiki au maadui wa kudumu katika siasa, na tatu, hakuna mwanasiasa anayeweza kuwa mbadala wa chama (hasa katika mazingira ya siasa zetu ambapo kwa kiasi kikubwa chombo pekee cha uongozi wa kisiasa ni chama cha siasa. Bila chama, mwanasiasa hata awe maarufu kiasi gani anabaki kuwa raia wa kawaida tu).
Katika waraka wake, Zitto aliandika, “They must know I am not a push over. Chacha died, I won't” (lazima wafahamu mie sio mtu wa ‘kupelekeshwa.’ Chacha (Wangwe?) alikufa, mimi sitokufa). Hiki ni kiburi, utoto au? Ni mwanadamu mwenye uhakika wa kutokufa? Nihitimishe kwa kumshauri kwamba labda kweli ana uhakika wa kuishi milele lakini kwa kutanguliza hisia badala ya busara, yayumkinika kubashiri kuwa anaweza kuwa anajiua mwenyewe kisiasa (committing political suicide).


Wednesday, January 15, 2014

Ligi Kuu England: Gazeti Maarufu Latabiri Matokeo Mechi zilizosalia...na Bingwa wa Ligi Hiyo


Gazeti maarufu la Daily Mail la hapa Uingereza limetabiri matokeo ya mechi zilizosalia katika Ligi Kuu ya England, na hatimaye bingwa wa ligi hiyo maarufu duniani.

Round 30
Aston Villa 1 Chelsea 2
Everton 1 Cardiff 0
Hull City 2 Man City 2
Man Utd 1 Liverpool 1
Spurs 1 Arsenal 2
 
Round 31
Cardiff 2 Liverpool 2
Chelsea 1 Arsenal 1
Everton 1 Swansea 1
Man City 5 Fulham 0
Spurs 2 Southampton 2
West Ham 2 Man Utd 1
 
Round 32
Arsenal 2 Man City 1
Crystal Palace 0 Chelsea 1
Fulham 1 Everton 1
Liverpool 2 Spurs 0
Man Utd 2 Aston Villa 0
 
Round 33
Chelsea 3 Stoke 1
Everton 1 Arsenal 1
Man City 2 Southampton 0
Newcastle 1 Man Utd 2
Spurs 1 Sunderland 1
West Ham 2 Liverpool 2 
So close: Olivier Giroud is denied during Arsenal and Chelsea's stalemate in December
So close: Olivier Giroud is denied during Arsenal and Chelsea's stalemate in December
Crisis: Manchester United were beaten 1-0 by Newcastle United in November, can they exact their revenge on Tyneside?
Crisis: Manchester United were beaten 1-0 by Newcastle United in November, can they exact their revenge on Tyneside?
Round 34
Arsenal 3 West Ham 1
Liverpool 3 Man City 2
Man Utd 1 Hull City 0
Sunderland 0 Everton 1
Swansea 0 Chelsea 0
West Brom 1 Spurs 2
 
Round 35
Chelsea 2 Sunderland 0
Everton 2 Man Utd 1
Hull 1 Arsenal 1
Man City 3 West Brom 0
Norwich 1 Liverpool 4
Spurs 1 Fulham 0
 

Round 36
Arsenal 3 Newcastle 0
Crystal Palace 1 Man City 3
Liverpool 2 Chelsea 1
Man Utd 3 Norwich 0
Southampton 1 Everton 1
Stoke 1 Spurs 1 
Round 37
Arsenal 3 West Brom 0
Chelsea 4 Norwich 0
Crystal Palace 1 Liverpool 1
Everton 1 Man City 0
Man Utd 1 Sunderland 0
West Ham 1 Spurs 2 
Two good: Mesut Ozil was among the goals as Arsenal enjoyed a 2-0 victory over Hull City in December
Two good: Mesut Ozil was among the goals as Arsenal enjoyed a 2-0 victory over Hull City in December

THE LAST DAY OF THE SEASON  

Standings going into the final day
Manchester City 84 points
Chelsea 82
Liverpool 79
Arsenal 78
Tottenham 67
Everton 65
Manchester United 65
 
Round 38
Cardiff 1 Chelsea 3
Liverpool 3 Newcastle 0
Hull 2 Everton 2
Man City 3 West Ham 1
Norwich 1 Arsenal 2
Southampton 1 Man Utd 2
Spurs 2 Aston Villa 0
 

Scroll down for the predicted final top seven
Champions: Our calculations have Manchester City winning the trophy they lifted in 2012
Champions: Our calculations have Manchester City winning the trophy they lifted in 2012
Good Kompany: City skipper Vincent Kompany could be set for another bus-top parade with the Premier League trophy
Good Kompany: City skipper Vincent Kompany could be set for another bus-top parade with the Premier League trophy
Ed boys: We believe that Manchester City and Edin Dzeko will be celebrating a title win come May
Ed boys: We believe that Manchester City and Edin Dzeko will be celebrating a title win come May
Final table (top seven)
1st Man City..........87pts
City's formidable home form proves the difference as they reclaim the title and Manuel Pellegrini celebrates his first season with the championship crown. They see out the season with a perfect home record, Chelsea the only one of their top-seven rivals still to visit the Etihad. Back-to-back away losses at Arsenal and Liverpool trigger fears of a late stutter, but they recover to confirm their title with a final-day victory over West Ham.
2nd Chelsea.........85pts
The Chelsea of old under Jose Mourinho shines through as the season draws to its close and they finish the campaign just two points shy of the champions. February's defeat at the Etihad proves costly, as does a late-season reverse at Liverpool, but they still take the race to the wire. 
3rd Liverpool........82pts
The return of Daniel Sturridge, allied to Luis Suarez's unrelenting brilliance, sees the Reds win the next six, including victory in the Merseyside derby. A string of away draws curtails their title challenge but still they finish just five points adrift of the winners and claim third position ahead of Arsenal.
4th Arsenal...........81pts
With their squad stretched as the season gathers pace and European football returns, the Gunners' title aspirations fade. They do enjoy a home victory over Man City and are beaten just twice - at Liverpool and Stoke - between now and the end of the season, but Arsene Wenger's wait for a fourth title is extended to at least 11 years.
5th Spurs..............70pts
The top four prove too strong for the other challengers and crucial defeats against rivals Man City, Arsenal and Liverpool do for their Champions League ambitions. Still, though, Tim Sherwood's boys do enough to hold off Man Utd and Everton to take fifth position and Europa League qualification - they're sure to be thrilled with that...
6th Man Utd..........68pts
Inconsistency continues to plague United's title defence and the now customary defeat by their city adversaries sparks yet more talk of crisis for David Moyes. They do win the last three to take sixth position ahead of Everton, but will that be enough to earn Moyes another season at Old Trafford?
7th Everton...........66pts
Draws prove the Toffees' undoing as their failure to turn one point into three sees their Champions League hopes slip away. It's still a respectable return for Roberto Martinez in his first season at Goodison Park, although they are pipped to sixth by former boss Moyes.
 


Tuesday, January 14, 2014

TANZANIA JOINS FORCES WITH BRITAIN'S NO. 1 SCHOOL TO UNEARTH FOOTBALL TALENTS

By Jestina George,
“Tanzania has taken the first step towards producing their first Premier League player – thanks to Eton College, England’s premier public school.
Eton Coach, Glen Pierce speaking at the press conference on Friday 10 Jan 2014 at Tanzania House London. 
Together with Safarihub and charity organisation ACE Africa, Eton are sending Glen Pierce, head of sports, plus Ali Lyon, 19, Nicholas Zafirios, 18,  and Tom Pearson,18, who are on a gap year before starting university, to Tanzania to teach local children the finer arts of football.
Ali has already passed his  Level 1 Football Association coaching badge and the quartet cannot wait for the challenge ahead of them.
Coach Glen Pierce with Eton students who will be travelling to Tanzania, Nicolas Zafiriou, Ali Lyon and Tom Pearson
Pierce said: “We are about to embark on a wonderful trip. I have taught at Eton for 27 years and was offered the opportunity to take a sabbatical. This is an chance to see a new country with boys I tutored. We shall be going into schools to coach and to encourage kids to attend school through football. If they do not go to school they will not have this opportunity. We want to attract them to go to school and football is the icing on the cake. I hope the boys will be an encouragement to local kids.”
Eton was founded in 1440 and among the college’s more recent famous old boys are Prime Minister David Cameron, Mayor of London Boris Johnson, the Archbishop of Canterbury plus Prince Harry and Prince William, who Pierce taught.
Minister Counsellor  Amos Msanjila speaking Freddy Macha & Urban Pulse
Amos Msanjila, Minister Counselor of the High Commission, did not hide his pride about the venture. He said: “We are honoured to have the boys going because Eton is not a normal school. In Tanzania we do not have a culture of different schools, but I have been in England long enough to know which school you attend matters. Eton has produced 19 Prime Ministers so, as I said, it is not a normal school. The boys could have gone to any country in Africa, indeed in the world, and we have so much pleasure that they chose Tanzania.” 
Director of  Safari Hub, Dilip Navapurkar  speaking at the press conference on Friday 10 Jan 2014 at Tanzania House London.
Dilip Navapurkar from Safarihub said: “I recently formed the company and one aim is to set up a pilot scheme to play football. We hope to see Tanzania qualify for the World Cup for the first time and produce some top-class Premier League footballers, but it will not happen overnight.
"Tanzania has the raw talent, it is our belief that we will one day produce players who will perform on the world's biggest stage."
John Collenette, chairman of ACE Africa and Future Stars Academy, said: “I have been in Tanzania for five years and I am particularly excited about this venture. Children have different problems to confront in their daily lives and we are committed to help them.”
High Commissioner Peter Kallaghe speaking at the press conference on Friday 10 Jan 2014 at Tanzania House London.
Peter Kallaghe, the High Commissioner, hosted a reception in London on Friday to announce the collaboration with Eton College and sent the football party away with his best wishes. He said:“We are greatly honoured by this initiative. We are fully behind a wonderful plan. Eton has produced 19 British Prime Ministers, maybe we have the 20th travelling to Tanzania this weekend."
High Commissioner Pete Kallaghe poses with guests after the press conference.
Images by Urban Pulse
-- Regards, Jestina George 
Mobile +44 7404 332 910/+44 7557 304 940 
Email: jestinageorge@gmail.com            info@jestina-george.com 
website: www.jestina-george.com 

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Hot Sonakshi Sinha, Car Price in India