Featured Posts

Saturday, January 12, 2008

AKON,DIKEMBE....NOW FROM TANZANIA,IT'S TK (M-BONGO NDANI YA HOLLYWOOD)

Afrika imetoa mastaa kadhaa waliotamba na wanaotikisa nchini Marekani na duniani kwa ujumla."Zaire" ilitupatia Dikembe Mutombo na Senegal imetuzawadia Akon.Tanzania nayo inaelekea kupata kitu zaidi ya umaarufu wa Mlima Kilimanjaro au mbuga ya Selous.Hapa namzungumzia TK...TEDDY KALONGA,Mtanzania anayeleta matumaini ya kuliweka jina la nchi yetu kwenye ramani huko Hollywood.Mwenyewe anasema "kuna vipaji na taaluma,uzoefu na nia",nukuu ambayo imenivutia sana hadi nimeinakili kwenye msahafu wangu wa nukuu.Mwanadada huyu ambaye ndiye "covergirl" katika toleo la mwezi Desemba 2007 la jarida la MIMI,anaelezea kwamba kwake tafsiri ya neno "mafanikio" (success)ni kuwa na furaha,afya njema na jina linalojulikana duniani...na utajiri" (nani asiyependa kuwa tajiri?).Pia anadhamiria kuwa mfano wa kuigwa (role model) kwa wanawake wa Kiafrika.Inapendeza kuona tunazungumzia Mtanzania mwenzetu ambaye Hollywood,sehemu ngumu kabisa "kuitawala " sio tu mahala anapoishi bali pia ni eneo lake la kazi.Trust me,ni rahisi zaidi kuukamata udaktari wa falsafa kuliko kuikamata Hollywood,na kwa hilo dada yetu TK (ambaye blogu yake inapatikana hapa) anastahili kila anaina ya sapoti kutoka kwetu tunaopenda kuona Tanzania haiishii kutajwa kwenye media kwa habari za ufisadi kama ule wa BOT bali pia kwa mambo mazuri kama namna akina Mutombo na Akon walivyoweza kufanya kwa nchi zao na bara letu kwa ujumla.Big up,TK!!!!

For TK & all go-getter sistaz&brothers out there,here is an inspirational message from NAS....I Know I can





And who wouldn't fancy CRUISIN' when both ends meet?

And this is for all you having DREAMS (at least not in a gansta way)

0 comments:

Post a Comment

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Hot Sonakshi Sinha, Car Price in India