Featured Posts

Wednesday, January 30, 2008

ZIARA YA BUSH ITUSAIDIE DHIDI YA UFISADI (MAKALA NDANI YA RAIA MWEMA)

Pamoja na mambo mengine,makala yangu katika toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema inatoa changamoto kwa vyombo vya habari vya Tanzania kutumia ipasavyo teknolojia ya habari kwa kuwezesha habari zao kupatikana mtandaoni.Pia nimegusia kwa kifupi "tangazo" la Balozi Ali Karume kuhusu dhamira yake ya kugombea urais wa Zanzibar mwaka 2010.Vilevile nimetumia sehemu kubwa kuelezea namna ziara ya Rais Bush nchini Tanzania inavyoweza kusaidia mapambano dhidi ya ufisadi,hasa kama "tukimwaminisha" kuwa fedha zinazoibiwa na mafisadi hao zinaweza kuishia mikononi mwa akina Osama bin Laden (well,pengine mafisadi hawana uhusiano na magaidi wa kimataifa lakini wengi tunajua kwamba neno UGAIDI likihusishwa na kitu chochote kile/mtu yeyote yule lazima itamsukuma Bush kufanya kitu flani).Bingirika na makala hiyo na nyinginezo zilizokwenda shule kwenye gazeti mwanana la Raia Mwema kwa KUBONYEZA HAPA

0 comments:

Post a Comment

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Hot Sonakshi Sinha, Car Price in India