
Awali pongezi nyingi zilikuwa zikielekezwa kwa rubani mkuu wa ndege hiyo,Kapteni Peter Burkill,lakini alipohojiwa kwenye mkutano na vyombo vya habari alieleza kwamba shujaa halisi alikuwa rubani msaidizi ambaye ndiye aliyekuwa kwenye "usukani" wakati ndege hiyo inahangaika kutua,na alitumia jitihada zake zote kuepusha maafa makubwa.Kichekesho ni kwamba kwa Kiswahili jina la shujaa huyo ni MSALITI,anaitwa John COWARD.Baadhi ya magazeti yakapata element ya kuchekesha katika habari hizo kwa vichwa vya habari kama hiki (kwenye gazeti la The Daily Mail):A Hero Called Coward (yaani "shujaa aitwaye msaliti")
Lakini kama hiyo haitoshi,moja ya magazeti ya udaku ya hapa,News of The World,leo limetoa picha za zamani za Kapteni Burkill akiwa nusu mtupu wakati anakula maraha kwenye likizo nchini Marekani.Katika baadhi ya picha hizo,rubani huyo anaonekana akiwa amemwagiwa chokoleti huku akinadada wawili wakijibidiisha kumlamba.Katika moja ya vimbwanga hivyo,rubani huyo ambaye wakati ho alikuwa mwajiriwa wa shirika la ndege la Caledonian,alilazwa sakafuni na chokoleti kumwagwa kwenye makali yake katika mchezo uliolenga kufananisha suala la kuendesha ndege.
Clip hii ya Ludacris ft Nate Dogg katika wimbo Area Codes inaweza kuwa mwafaka kwa stori hii ya ndege na airports (Caution: explicit lyrics)
No comments :
Post a Comment