KWA MUDA SASA BLOGU HII IMEKUWA KIMYA.HIYO NI KUTOKANA NA SAFARI YA KUJA HAPA NYUMBANI BONGO.LIBENEKE LITAENDELEA PINDI MAMBO YAKISHATULIA.WILL DO MY BEST TO KEEP YOU GUYS POSTED ABOUT WHAT'S HAPPENING KIPANDE HII
Wakati tunasherehekea sikukuu ya Pasaka ni vema tukifanya tafakuri ya mambo ambayo machoni yanaweza kuonekana madogo lakini yenye uzito mkubwa katika hali halisi.Ni muhimu kumshukuru Mungu kwa mengi au machache aliyo/anayotujalia.Hivi kuna zawadi kubwa kutoka kwa Mungu zaidi ya UHAI?Sambamba na uhai ni uzima/ukamili wa miili yetu.Tuliozaliwa tukiwa kamili (yaani bila ulemavu) tunaweza kujisahau kuuliza maswali magumu kama "ingekuwa vipi kama ningezaliwa nina mkono nusu,au pua iliyozama ndani,au hata jicho lililokaa kisogoni" hadi pale tunapowaona wenzetu kama huyu mtu-tembo (elephant man-sio yule wa dancehall),ambaye stori yake inapatikana HAPA
Jana nilishuhudia kituko cha mwaka.Mwanzoni nilidhani ni porojo tu lakini asubuhi hii nimeona tukio hilo limekuwa gumzo mtandaoni.Ilikuwa takriban saa 6 mchana za hapa (hapa saa zitabadilika mwishoni mwa mwezi huu),nikaamua kupoteza muda kwa kuangalia kipindi cha Fox&Friends.Nasema kupoteza muda kwa vile waendesha kipindi hicho huwa wananikera sana kutokana na kauli zao za upendeleo wa wazi kwa wahafidhina na upinzani wao mkubwa dhidi ya Democrats na liberals.Sikujutia uamuzi wa "kupoteza muda" kwani huku watangazaji Steve Doocy na Gretchen Carlson wakishikia bango kauli ya Obama kwamba grandmom wake ni like typical White person,mwenzao Brian Kilmeade aliamua kuondoka kwa muda studioni kutokana na kukerwa na namna wenzie walivyokuwa wakimsakama Obama.Kama hiyo haitoshi,muda mfupi baadaye,mtangazaji mwandamizi wa kituo hicho,Chris Wallace,alionekana hewani wakati Fox&Friends inaendelea ambapo alielezea waziwazi kwamba alikuwa akiangalia kipindi hicho na hakupendezwa na namna kauli ya Obama kuhusu bibi yake ilivyokuwa ikipotoshwa.Wallace alieleza wazi kwamba yeye si msemaji wa kambi ya Obama lakini angependa kuona kipindi hicho kinazungumzia suala hilo ndani ya context,na kwenda mbali zaidi kwa kuwashauri wana-Fox&Friends kuangalia pia habari nyingine za muhimu kuhusu Obama kama vile endorsement ya Bill Richardson na hotuba zake mbili kuhusu uchumi na vita ya Irak.

Kwa mujibu wa taarifa za kiuchunguzi za gazeti hilo,watu mbalimbali wamethibitisha tuhuma hizo ambazo zimekanushwa vikali na P.Diddy.Itakumbukwa kwamba kifo cha Tupac kinahusishwa pia na mauaji ya rapa mwingine maarufu Christopher Wallace a.k.a. Notorious B.IG. ambacho kinadhaniwa kuwa ni kisasi cha washirika wa Tupac.


Mmoja wa polisi wa ngazi za juu hapa Uingereza,Chifu Konstebo wa Greater Manchester Police,Michael Todd,amekutwa amekufa.Habari zaidi zinapatikana hapa
MAKALA HII YANGU ILITOKA KATIKA GAZETI LA MTANZANIA TAREHE 07 MACHI 2008

Mzimu wa uhuru wa Kosovo unaendelea kuisumbua Serbia na sasa serikali yake imesambaratika kutokana na tofauti za kimsimamo kati ya Waziri Mkuu,Vojislav Kostunica mwenye mtizamo wa kitaifa (nationalist) na Rais Boris Tadic mwenye mtizamo wa kimagharibi zaidi.Habari zaidi,soma HAPA.




MTANZANIA UGHAIBUNI
Nilikubaliana na Komando wakati huo,na nakubaliana nae sasa,kwamba madaraka ni mazuri na matamu,na ndio maana tunashuhudia hizi kelele zinazoendelea kutoka kwa waliokumbwa na zahma ya kisiasa baada ya skandali ya mkataba wa kampeni ya Richmond.Hakuna dhambi kwa madaraka kuwa matamu kwani hata njia ya kuyafikia sio nyepesi.Inahitaji jitihada na juhudi za kutosha kufikia hatua ya kuongoza watu wenye akili timamu.Na inatarajiwa kwamba mtu akishapata bahati ya kuwa kiongozi atatambua kwamba wengi,kama sio wote,wa aliokuwa akiwaongoza ni watu wenye akili timamu,uwezo wa kufanya maamuzi na wanaostahili heshima.

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)
Your email address is safe with us!
Wakati tunasherehekea sikukuu ya Pasaka ni vema tukifanya tafakuri ya mambo ambayo machoni yanaweza kuonekana madogo lakini yenye uzito mkubwa katika hali halisi.Ni muhimu kumshukuru Mungu kwa mengi au machache aliyo/anayotujalia.Hivi kuna zawadi kubwa kutoka kwa Mungu zaidi ya UHAI?Sambamba na uhai ni uzima/ukamili wa miili yetu.Tuliozaliwa tukiwa kamili (yaani bila ulemavu) tunaweza kujisahau kuuliza maswali magumu kama "ingekuwa vipi kama ningezaliwa nina mkono nusu,au pua iliyozama ndani,au hata jicho lililokaa kisogoni" hadi pale tunapowaona wenzetu kama huyu mtu-tembo (elephant man-sio yule wa dancehall),ambaye stori yake inapatikana HAPA
Jana nilishuhudia kituko cha mwaka.Mwanzoni nilidhani ni porojo tu lakini asubuhi hii nimeona tukio hilo limekuwa gumzo mtandaoni.Ilikuwa takriban saa 6 mchana za hapa (hapa saa zitabadilika mwishoni mwa mwezi huu),nikaamua kupoteza muda kwa kuangalia kipindi cha Fox&Friends.Nasema kupoteza muda kwa vile waendesha kipindi hicho huwa wananikera sana kutokana na kauli zao za upendeleo wa wazi kwa wahafidhina na upinzani wao mkubwa dhidi ya Democrats na liberals.Sikujutia uamuzi wa "kupoteza muda" kwani huku watangazaji Steve Doocy na Gretchen Carlson wakishikia bango kauli ya Obama kwamba grandmom wake ni like typical White person,mwenzao Brian Kilmeade aliamua kuondoka kwa muda studioni kutokana na kukerwa na namna wenzie walivyokuwa wakimsakama Obama.Kama hiyo haitoshi,muda mfupi baadaye,mtangazaji mwandamizi wa kituo hicho,Chris Wallace,alionekana hewani wakati Fox&Friends inaendelea ambapo alielezea waziwazi kwamba alikuwa akiangalia kipindi hicho na hakupendezwa na namna kauli ya Obama kuhusu bibi yake ilivyokuwa ikipotoshwa.Wallace alieleza wazi kwamba yeye si msemaji wa kambi ya Obama lakini angependa kuona kipindi hicho kinazungumzia suala hilo ndani ya context,na kwenda mbali zaidi kwa kuwashauri wana-Fox&Friends kuangalia pia habari nyingine za muhimu kuhusu Obama kama vile endorsement ya Bill Richardson na hotuba zake mbili kuhusu uchumi na vita ya Irak.

Kwa mujibu wa taarifa za kiuchunguzi za gazeti hilo,watu mbalimbali wamethibitisha tuhuma hizo ambazo zimekanushwa vikali na P.Diddy.Itakumbukwa kwamba kifo cha Tupac kinahusishwa pia na mauaji ya rapa mwingine maarufu Christopher Wallace a.k.a. Notorious B.IG. ambacho kinadhaniwa kuwa ni kisasi cha washirika wa Tupac.


Mmoja wa polisi wa ngazi za juu hapa Uingereza,Chifu Konstebo wa Greater Manchester Police,Michael Todd,amekutwa amekufa.Habari zaidi zinapatikana hapa
MAKALA HII YANGU ILITOKA KATIKA GAZETI LA MTANZANIA TAREHE 07 MACHI 2008

Mzimu wa uhuru wa Kosovo unaendelea kuisumbua Serbia na sasa serikali yake imesambaratika kutokana na tofauti za kimsimamo kati ya Waziri Mkuu,Vojislav Kostunica mwenye mtizamo wa kitaifa (nationalist) na Rais Boris Tadic mwenye mtizamo wa kimagharibi zaidi.Habari zaidi,soma HAPA.



Mambo hayo!Habari yenyewe iko HAPA
MTANZANIA UGHAIBUNI
Nilikubaliana na Komando wakati huo,na nakubaliana nae sasa,kwamba madaraka ni mazuri na matamu,na ndio maana tunashuhudia hizi kelele zinazoendelea kutoka kwa waliokumbwa na zahma ya kisiasa baada ya skandali ya mkataba wa kampeni ya Richmond.Hakuna dhambi kwa madaraka kuwa matamu kwani hata njia ya kuyafikia sio nyepesi.Inahitaji jitihada na juhudi za kutosha kufikia hatua ya kuongoza watu wenye akili timamu.Na inatarajiwa kwamba mtu akishapata bahati ya kuwa kiongozi atatambua kwamba wengi,kama sio wote,wa aliokuwa akiwaongoza ni watu wenye akili timamu,uwezo wa kufanya maamuzi na wanaostahili heshima.


