Featured Posts

Tuesday, June 30, 2009

SIJUI TUAMINI LIPI KUHUSU KIFO CHA MICHAEL JACKSON!





Kifo cha mtu maarufu huambatana na kila aina ya tetesi.Na kifo cha Michael Jackson is no exception.Ukisikiliza,kuona au kusoma kuhusu kifo cha mfalme huyo wa Pop,unaweza kumhukumu kirahisi tu kuwa alikuwa mithili ya mfu aliye hai (dead man walking).Baadhi ya vyombo vya habari vinadai Michael alikuwa akibwia madawa lukuki ya kumudu maumivu ya mwili.Mengine yanadai alikuwa amekongoroka kupita kiasi.Gazeti moja limekwenda mbali zaidi na kudai kwamba eti miezi michache iliyopita,ilibainika wazi kuwa Michael alikuwa na miezi si zaidi ya sita ya kuishi.Lakini picha hizi zilizopigwa wakati wa rehersal zake zilizopangwa kufanyika O2 Arena mwezi ujao,zinatoa taswira tofauti kabisa.

0 comments:

Post a Comment

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Hot Sonakshi Sinha, Car Price in India